Ushauri kwa Serikali: Mtu anayepinga tozo na kodi kwa maendeleo ya Taifa akamatwe

Ushauri kwa Serikali: Mtu anayepinga tozo na kodi kwa maendeleo ya Taifa akamatwe

Tatizo ni wenye nyumba, watakubali kupokea kiasi kinachobaki baada ya kulipa tozo?

Mimi nafikiri, Serikali iwe serious kidogo, kabla ya kuanzisha hizi tozo na kuzizindua waweke mazingira mazuri kwa mlaji wa mwisho.

Leo hii unataka 10% ya pango, mwenye nyumba nae anasema nataka unipe kodi yangu kama ilivyo bila kukatwa TRA utajuana nao wewe, au anaongeza kidogo badala ya sh 200 anapangisha kwa 250, hivi hapa nani anateseka?

DHIBITI BEI YA KUPANGISHA NYUMBA KWANZA. Kama haiwezekani tuondolee huu mzigo.
Bandiko hili naona limekuja na mawazo mazuri ya wachangiaji.

Bila shaka wadau huko serikalini mnafatilia maoni ya wananchi wenu.👍👍👍
 
UJINGA ,MARADHI NA UMASKINI BADO NI TATIZO.KAMA UNGEWEZA KUNAMBIA VAT NA TOZO NANI ANACHUKUA KWENYE MUAMALA NA UKANAMBIA MAANA YA DOUBLE TAXATION NINGEUNGA MKONO HOJA.
Swali lako watakuja kulijibu wataalam maana humu naimani wamo
 
Tatizo rasilimali zipo nying hazisimamiw ipasavyo kukusanya kod kwa faida ya taifa Bali mwananchi ndiy anabeba mzigo wote wa tozo hali yakua Kuna inflation kubwa ya bidhaa,lakin pia hakuna usimamiz mzr wa fedha zitolewazo kweny mirad mbali mbali Kuna inch wanahitaji hat wangekua n bandari mija to kuisimamia ipasavyo kwa manufaa ya taifa,tunapotoka tuna pajua lakin tunakoenda hatupajui Kwan giza linatanda na usingizi hakuna....
TANZANIA WE ARE POOR BECAUSE WE CHOOSE TO BE POOR.
Umeongea point muhimu sana mkuu.

Bila shaka wadau katika serikali ya Mh Rais Samia wanachukua notes na nina imani watalifanyia kazi
 
Kamua tu hadi watoe damu. Kamshahara kamepitia bank unataka kumtumia kijana ada ya shule. Unatoa ada bank TOZO,unaweka kwenye simu unatuma TOZO, anatoa kwa agent TOZO-je tutafika?
Hahahaa hili nalo watalitazama
 
Ingekua vizuri kama ungeshauri wanaobainika kufuja mali za umma na mafisadi wafilisiwe mali zao ingekua vizuri zaidi. Kuliko kupambania kulipa tozo alafu wakazifaidi wachache.
Lakinj sheria za kudhibiti uhujumu uchumi na ufisadi zipo na zinafanya kazi.
 
Hakuna mtu anaeunga mkono swala la tozo kwahali hiyo mtakamata wengi na nagereza yatakuwa machache.
Wanaendelea kuelimishwa nadhani bado hawajajua umuhimu wa jambo hili. Kwa mujibu wa tafiti za Twaweza jana waliripoti kuwa acceptance ni 60%.

Hii ndogo iliyobaki ya 40 wataendelea kuelimika kidogo kidogo.
 
Back
Top Bottom