Bandiko hili naona limekuja na mawazo mazuri ya wachangiaji.Tatizo ni wenye nyumba, watakubali kupokea kiasi kinachobaki baada ya kulipa tozo?
Mimi nafikiri, Serikali iwe serious kidogo, kabla ya kuanzisha hizi tozo na kuzizindua waweke mazingira mazuri kwa mlaji wa mwisho.
Leo hii unataka 10% ya pango, mwenye nyumba nae anasema nataka unipe kodi yangu kama ilivyo bila kukatwa TRA utajuana nao wewe, au anaongeza kidogo badala ya sh 200 anapangisha kwa 250, hivi hapa nani anateseka?
DHIBITI BEI YA KUPANGISHA NYUMBA KWANZA. Kama haiwezekani tuondolee huu mzigo.
Swali lako watakuja kulijibu wataalam maana humu naimani wamoUJINGA ,MARADHI NA UMASKINI BADO NI TATIZO.KAMA UNGEWEZA KUNAMBIA VAT NA TOZO NANI ANACHUKUA KWENYE MUAMALA NA UKANAMBIA MAANA YA DOUBLE TAXATION NINGEUNGA MKONO HOJA.
🤣🤣🤣🤣we jamaaUmesahau hii:
"Unapipinga Tozo unawakosesha usingizi walamba asali jambo ambalo halikubaliki."
Kwani utakuwa unataka walambe nini sasa?
Umeongea point muhimu sana mkuu.Tatizo rasilimali zipo nying hazisimamiw ipasavyo kukusanya kod kwa faida ya taifa Bali mwananchi ndiy anabeba mzigo wote wa tozo hali yakua Kuna inflation kubwa ya bidhaa,lakin pia hakuna usimamiz mzr wa fedha zitolewazo kweny mirad mbali mbali Kuna inch wanahitaji hat wangekua n bandari mija to kuisimamia ipasavyo kwa manufaa ya taifa,tunapotoka tuna pajua lakin tunakoenda hatupajui Kwan giza linatanda na usingizi hakuna....
TANZANIA WE ARE POOR BECAUSE WE CHOOSE TO BE POOR.
Hahahaa hili nalo watalitazamaKamua tu hadi watoe damu. Kamshahara kamepitia bank unataka kumtumia kijana ada ya shule. Unatoa ada bank TOZO,unaweka kwenye simu unatuma TOZO, anatoa kwa agent TOZO-je tutafika?
Lakinj sheria za kudhibiti uhujumu uchumi na ufisadi zipo na zinafanya kazi.Ingekua vizuri kama ungeshauri wanaobainika kufuja mali za umma na mafisadi wafilisiwe mali zao ingekua vizuri zaidi. Kuliko kupambania kulipa tozo alafu wakazifaidi wachache.
Wanaendelea kuelimishwa nadhani bado hawajajua umuhimu wa jambo hili. Kwa mujibu wa tafiti za Twaweza jana waliripoti kuwa acceptance ni 60%.Hakuna mtu anaeunga mkono swala la tozo kwahali hiyo mtakamata wengi na nagereza yatakuwa machache.
Huko siko