Ushauri kwa Serikali na Huduma za Jamii Tanzania

Ushauri kwa Serikali na Huduma za Jamii Tanzania

Nalitupia hili hapa.

Hivi hao wawekezaji tunaoambiwa wanawekeza na kuongezeka bwelele, wananchangia nini kwenye huu Uchumi wetu?

Ninavyofikiri kuwa, uchumi unavyo kua na Huduma za Jamii ndivyo zinavyo kua, au?
Nisaidieni.
Uwekezaji siyo muujiza, haulipi leo na kesho. Soma kuhusu ROI katika uwekezaji.

Kikiubwa tunachofaidika kuanzia mwanzo wa uwekezaji ni ajira. Faida zingine huja baada ya wawekezaji kurudisha gharama zao.
 
KWANINI KIPINDI HIKI CHA MAMA RUSHWA IMEZIDI NA UZEMBE KAZINI KULIKO KIPINDI CHA MAGUFULI? huduma zilipiwe hasa ya kipolisi.polisi ofisi za serikal za vijiji na mtaa ndyo maeneo yanayoongoza kwa rushwa.hata na hvyo bila uongoz imara hata km unalipia huduma mambo bdo n yaleyale
Hata sahivi unalipia, si una lipa kodi na wao wanalipwa mishahara? tatizo ni mfumo mbovu wa CCM
 
Suala la rushwa ni kwa serikali karibu zote za Afrika. Lazima tutibu kwanza mzizi wa tatizo.

Mishahara mingi ya wafanyakazi wa serikali ipo chini haikidhi uhalisia wa maisha.Hivyo wanajiongeza kwa kuomba rushwa.
Tatizo la rushwa Tanzania linaanzia juu kushuka chini, utachukuaje rushwa kama boss wako siyo mla rushwa? Waziri kituo chake cha kazi kipo Dodoma analipwa perdiem 470,000 na yupo Dodoma(Bungeni) na wakati kuna VEO anadai nauli yake ya likizo 30,000 anazungushwa kila siku na ni halali yake, why asichukue rushwa kwa mnyonge wake ambaye ni mwananchi? Katibu Mkuu wa Wizara anajilipa per diem 250,000 siku 20 kuzunguka mikoani matokeo yake anaenda siku 3 anarudi ofisini hiyo siyo rushwa? mfumo wa kijinga uliopo umeletwa na CCM
 
Kwani Tanzania kuna huduma ya Bure? Kodi mnalipa za Nini kumbe?

Hata hivyo, sidhani hicho ulichoshauri ni suluhisho. Hata TANESCO kuna mashtaka ya rushwa, mteja analipia gharama za kuunganishwa umeme na Bado anatozwa rushwa.

Rushwa ni malipo yasiyo Halali Ili kufanya Mtu kutoa favor isiyo Halali, au kupewa favor isiyo Halali. Ndio maana katika Sheria ya rushwa mtoaji na mpokeaji wanachkuliwa ni wakosaji.
Nilienda siku moja kupata huduma kwa VEO hana karatasi wala printer ikabidi nitoe pesa akachapishe pamoja na kutoa copy, nilipiga naye story akasema tangu ameajiriwa 2019 amewahi kupewa ream paper moja tu kutoka kwa DED, unategemea huyo mtu afanyeje kuwahudumia wananchi? nami nilimhurumia nikampa elf 5 ya vocha, tuna mfumo wa kijinga sn, pesa za kulipana posho nono wanazo lakini siyo za kutoa huduma kwa wananchi
 
Mfano mzuri ni jana kariakoo, moto uliotokea, hakuna huduma ya zima moto.

Sasa kwanini kujna vituo vya zimamoto kama hawana hata ubunifu wa kuwa na na malori kumi au kumi na tano ya maji wakati wote?

Au kuwa na ubunifu wa kuweka matank ya reserve -, mfano kariako ulipotokea moto karibia majumba yote yana visima vya maji.

Ubunifu unatushinda Watanzania, akili zetu zimelala sana, tunachowaza ni kulewa, ngoma, uasherati, kujionesha kwa watu na mambo ya kijingajinga tu.
Eh hujazoea tu matukio + uzembe wa fire
Hivi tuwalaumu fire au ilaumiwe serikali

Ova
 
Zaidi ya miaka 60 ya uhuru mnaongoza nchi ambayo bado ni maskini wa kutupwa.

Hamna mnachoweza.

Nini kimewashinda kuifanya nchi iwe na trillion dollar economy?
Kuna kaa laana fulani

Homeboy

Ova
 
KWANINI KIPINDI HIKI CHA MAMA RUSHWA IMEZIDI NA UZEMBE KAZINI KULIKO KIPINDI CHA MAGUFULI? huduma zilipiwe hasa ya kipolisi.polisi ofisi za serikal za vijiji na mtaa ndyo maeneo yanayoongoza kwa rushwa.hata na hvyo bila uongoz imara hata km unalipia huduma mambo bdo n yaleyale
Baada ya wiki Moja tu jembe JPM kulala mavumbini kila kitu kilirudi kama awali.niloshangaa sana hili ni kasema hii nchi ya ajabu sana
 
hiyo kawaida ya uongozi wote duniani, lazima muwepo mnaolalamika bila kuleta njia kifanyike nini.

Mapapai yaliyovunda hayajifichi.
Kama wananchi kinachotakiwa nikubadili chama ndio suruhisho. Kumbuka huwezi kutatua tatizo kwakutumia njia ileile uliokosea na utegemee kupata matokeo tofauti lakini ulivyo sikio lakufa huwezi kuamini.
 
Baada ya wiki Moja tu jembe JPM kulala mavumbini kila kitu kilirudi kama awali.niloshangaa sana hili ni kasema hii nchi ya ajabu sana
Kwani ilikwisha, sisi yeye ndiye aliwapa "go ahead" mapolisi kwa " za kupigia polish viatu?
 
"Platinum Member" umewaaaazaa na kuwazua ukaja na hii.. ujinga mtupu. Yaani CCM imeshindwa kuthibiti rushwa mkaona hio iwe fursa kwenu na kuwapa mzigo tena wananchi. Na hio huduma ikiwa ya kulipia hizo hela zikienda kwenye miradi n.k mwende mzipigee tenaa.. ujinga mtupuu
 
Uwekezaji siyo muujiza, haulipi leo na kesho. Soma kuhusu ROI katika uwekezaji.
Kwa msingi huo, kwanini unaona miaka miwili ya Samia haitoshelezi kurejesha uwekezaji/faida kwa Wananchi?
Kikiubwa tunachofaidika kuanzia mwanzo wa uwekezaji ni ajira. Faida zingine huja baada ya wawekezaji kurudisha gharama zao.
Sawa, hayo hata Darasa la Saba anaweza kudadavua.

Turudi kwenye hoja yako ya msingi kwamba Serikali haikusikilizi, kwamba Rushwa imekithiri, kwamba huduma za kijamii au za kiserikali zianze kulipiwa.

Ni dhahiri umekerwa wakati ukitafuta huduma katika hayo maeneo uliyoyataja-Mahakamani, Polisi n.k Lakini kikubwa ni Rushwa na kukosekana kwa Sheria au sera madhubuti za kupambana nayo.

Je, unafikiri Wawekezaji wataweza kuja kutatua masuala/kero hizo? Badala ya Serikali kusimamia Huduma hizo? How?
 
Nilileta wazo huduma za Kipolisi ziwe "private", Sasa nimeboresha wazo "privatization" ianzie serikalini wapate ujuzi.

Hizo idara zote zinazotowa huduma za bure ziwe ni vyanzo vya pesa na watu walipwe vizuri rasmi, badala ya kuteswa raia.
KUNA KITU HAPA unakumbuka vyoo vya uma awali ilikuwa bure na huduma ilikuwa mbya na chafu baada ya kulipia ikawa nzuri.huduma zilipiwe kwa garama ndogo
 
Binafsi ni mwana CCM kindakindaki tokea ilipobuniwa 1977, kabla ya hapo nilikuwa TANU Youth League.

Ingawa ni mwana CCM lakini si kila jambo la serikali linaniridhisha, kuna ambayo tukipata nafasi tunayafikisha vikaoni lakini hivi sasa imekuwa ngumu sana kufikisha ujumbe kwenye ngazi za maamuzi, sifahamu kwanini wakati sasa hivi tunaishi kwenye dunia inayopitia kwenye miongo ya mawasiliano habari (IT).

Kwanza naishauri CCM iboreshe namna ya kuwasiliana na ngazi za uongozi pili naishauri serikali kuu, mawaziri wote mpaka Rais wa Tanzania waige mfumo wa Zanzibar wa "sema na Rais".

Kwa kukosa njia za kufikisha ujumbe kwa haraka nimeona bora ushauri wangu niutowe hapa JF, nafahamu utawafikia walengwa wote.

1) Nashauri huduma zinazotelewa bure na serikali ziwe za kulipia rasmi, kwa zote namaanisha zote. Kuanzia huduma zinazotolewa Polisi, iwe mtu ukitaka huduma yoyote ya kipolisi ulipie, kama siyo siku hiyo hiyo basi uandikiwe una deni kwa kupewa huduma hiyo na utailipa kupitia control numbers.

Rushwa imezidi serikalini, kama haujaombwa waziwazi basi utazungushwa kupatiwa huduma mpaka utie akili utowe rushwa au atokee "kishoka" wa hapo akusomeshe utowe rushwa, ndipo huduma yako ishughulikiwe.

Kwa mambo kama hayo, iwekwe wazi tu, kuwa ukienda kushitaki polisi unapewa control number unalipia unapewa huduma, na afisa ataekuhudumia atalipwa mgao wake hukohuko official kabisa.

Ili kupigana na rushwa, kama tumeshindwa kuweka sheria kali ni vyema tukaihalalisha tu malipo kwa kila huduma.

Au kama ilivyofanywa kwenye matibabu, iwekwe bima ya lazima kwa kila raia awe analipia hizo huduma, na pesa zitazotokana na hiyo bima waongezewe mishara na posho watowa huduma badala ya kuzungusha watu ili wale rushwa serikalini. Hii ni kwa wizara na idara zote zinazotowa huduma za bure kwa jamii, ambako ndiko kunakonuka uozo wa rushwa.

Kauli za viongozi kama zile za "za polish ya viatu", "kila mmoja ale kwa urefu wa kamba yake" zimekuwa zikihalalisha rushwa kiaina, sasa iwe ni wazi kabisa ihalalishwe kwa kuzilipia hizo huduma.

Polisi, mahakama, uhamiaji, ardhi, huduma zote za bure za manispaa. Ongezea na wewe kwengine.

Tunataka tuwe ni wateja rasmi wenye kuweza kudai haki zetu tunaponyimwa huduma kwa wakati.
Leo siju umesoma suratu kursiyu akili imechangamka vibaya sana
 
TANESCO wananchi wanalipia kila huduma... Nguzo, Meter, n.k.

Mwananchi anakamilisha kila kitu, lakini hawaendi kumfungia huo umeme unless ametoa rushwa!

Ukikaza kwamba hutoi rushwa, then utazungushwa sana... "Nguzo za eneo lenu bado hazijafika. Meter zimeisha subiri batch ijayo" n.k n.k.

Nchi hii ujinga ujinga rushwa na dharau kwenye ofisi za umma bado ni doa sugu!

-Kaveli-
 
Mfano mzuri ni jana kariakoo, moto uliotokea, hakuna huduma ya zima moto.

Sasa kwanini kujna vituo vya zimamoto kama hawana hata ubunifu wa kuwa na na malori kumi au kumi na tano ya maji wakati wote?

Au kuwa na ubunifu wa kuweka matank ya reserve -, mfano kariako ulipotokea moto karibia majumba yote yana visima vya maji.

Ubunifu unatushinda Watanzania, akili zetu zimelala sana, tunachowaza ni kulewa, ngoma, uasherati, kujionesha kwa watu na mambo ya kijingajinga tu.
Hayo ndio matunda ya chama chetu.
Na kwenye paragraph ya mwisho kinachoongezeka ni uchawa na bila connection hupati kitu.
 
Back
Top Bottom