Uwekezaji siyo muujiza, haulipi leo na kesho. Soma kuhusu ROI katika uwekezaji.Nalitupia hili hapa.
Hivi hao wawekezaji tunaoambiwa wanawekeza na kuongezeka bwelele, wananchangia nini kwenye huu Uchumi wetu?
Ninavyofikiri kuwa, uchumi unavyo kua na Huduma za Jamii ndivyo zinavyo kua, au?
Nisaidieni.
Hata sahivi unalipia, si una lipa kodi na wao wanalipwa mishahara? tatizo ni mfumo mbovu wa CCMKWANINI KIPINDI HIKI CHA MAMA RUSHWA IMEZIDI NA UZEMBE KAZINI KULIKO KIPINDI CHA MAGUFULI? huduma zilipiwe hasa ya kipolisi.polisi ofisi za serikal za vijiji na mtaa ndyo maeneo yanayoongoza kwa rushwa.hata na hvyo bila uongoz imara hata km unalipia huduma mambo bdo n yaleyale
Tatizo la rushwa Tanzania linaanzia juu kushuka chini, utachukuaje rushwa kama boss wako siyo mla rushwa? Waziri kituo chake cha kazi kipo Dodoma analipwa perdiem 470,000 na yupo Dodoma(Bungeni) na wakati kuna VEO anadai nauli yake ya likizo 30,000 anazungushwa kila siku na ni halali yake, why asichukue rushwa kwa mnyonge wake ambaye ni mwananchi? Katibu Mkuu wa Wizara anajilipa per diem 250,000 siku 20 kuzunguka mikoani matokeo yake anaenda siku 3 anarudi ofisini hiyo siyo rushwa? mfumo wa kijinga uliopo umeletwa na CCMSuala la rushwa ni kwa serikali karibu zote za Afrika. Lazima tutibu kwanza mzizi wa tatizo.
Mishahara mingi ya wafanyakazi wa serikali ipo chini haikidhi uhalisia wa maisha.Hivyo wanajiongeza kwa kuomba rushwa.
Nilienda siku moja kupata huduma kwa VEO hana karatasi wala printer ikabidi nitoe pesa akachapishe pamoja na kutoa copy, nilipiga naye story akasema tangu ameajiriwa 2019 amewahi kupewa ream paper moja tu kutoka kwa DED, unategemea huyo mtu afanyeje kuwahudumia wananchi? nami nilimhurumia nikampa elf 5 ya vocha, tuna mfumo wa kijinga sn, pesa za kulipana posho nono wanazo lakini siyo za kutoa huduma kwa wananchiKwani Tanzania kuna huduma ya Bure? Kodi mnalipa za Nini kumbe?
Hata hivyo, sidhani hicho ulichoshauri ni suluhisho. Hata TANESCO kuna mashtaka ya rushwa, mteja analipia gharama za kuunganishwa umeme na Bado anatozwa rushwa.
Rushwa ni malipo yasiyo Halali Ili kufanya Mtu kutoa favor isiyo Halali, au kupewa favor isiyo Halali. Ndio maana katika Sheria ya rushwa mtoaji na mpokeaji wanachkuliwa ni wakosaji.
Ndiyo rushwa hizo hizoWatanzania unafiki utatuua!
Kutwa tunailaumu ccm na madudu wanayofanya kila siku
Ila ikifika kipindi cha uchaguzi tunajifuga vibwebwe kuipigia kampeni bila hata aibu!
Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
Eh hujazoea tu matukio + uzembe wa fireMfano mzuri ni jana kariakoo, moto uliotokea, hakuna huduma ya zima moto.
Sasa kwanini kujna vituo vya zimamoto kama hawana hata ubunifu wa kuwa na na malori kumi au kumi na tano ya maji wakati wote?
Au kuwa na ubunifu wa kuweka matank ya reserve -, mfano kariako ulipotokea moto karibia majumba yote yana visima vya maji.
Ubunifu unatushinda Watanzania, akili zetu zimelala sana, tunachowaza ni kulewa, ngoma, uasherati, kujionesha kwa watu na mambo ya kijingajinga tu.
Kuna kaa laana fulaniZaidi ya miaka 60 ya uhuru mnaongoza nchi ambayo bado ni maskini wa kutupwa.
Hamna mnachoweza.
Nini kimewashinda kuifanya nchi iwe na trillion dollar economy?
Baada ya wiki Moja tu jembe JPM kulala mavumbini kila kitu kilirudi kama awali.niloshangaa sana hili ni kasema hii nchi ya ajabu sanaKWANINI KIPINDI HIKI CHA MAMA RUSHWA IMEZIDI NA UZEMBE KAZINI KULIKO KIPINDI CHA MAGUFULI? huduma zilipiwe hasa ya kipolisi.polisi ofisi za serikal za vijiji na mtaa ndyo maeneo yanayoongoza kwa rushwa.hata na hvyo bila uongoz imara hata km unalipia huduma mambo bdo n yaleyale
Kama wananchi kinachotakiwa nikubadili chama ndio suruhisho. Kumbuka huwezi kutatua tatizo kwakutumia njia ileile uliokosea na utegemee kupata matokeo tofauti lakini ulivyo sikio lakufa huwezi kuamini.hiyo kawaida ya uongozi wote duniani, lazima muwepo mnaolalamika bila kuleta njia kifanyike nini.
Mapapai yaliyovunda hayajifichi.
Kwa msingi huo, kwanini unaona miaka miwili ya Samia haitoshelezi kurejesha uwekezaji/faida kwa Wananchi?Uwekezaji siyo muujiza, haulipi leo na kesho. Soma kuhusu ROI katika uwekezaji.
Sawa, hayo hata Darasa la Saba anaweza kudadavua.Kikiubwa tunachofaidika kuanzia mwanzo wa uwekezaji ni ajira. Faida zingine huja baada ya wawekezaji kurudisha gharama zao.
KUNA KITU HAPA unakumbuka vyoo vya uma awali ilikuwa bure na huduma ilikuwa mbya na chafu baada ya kulipia ikawa nzuri.huduma zilipiwe kwa garama ndogoNilileta wazo huduma za Kipolisi ziwe "private", Sasa nimeboresha wazo "privatization" ianzie serikalini wapate ujuzi.
Hizo idara zote zinazotowa huduma za bure ziwe ni vyanzo vya pesa na watu walipwe vizuri rasmi, badala ya kuteswa raia.
Leo siju umesoma suratu kursiyu akili imechangamka vibaya sanaBinafsi ni mwana CCM kindakindaki tokea ilipobuniwa 1977, kabla ya hapo nilikuwa TANU Youth League.
Ingawa ni mwana CCM lakini si kila jambo la serikali linaniridhisha, kuna ambayo tukipata nafasi tunayafikisha vikaoni lakini hivi sasa imekuwa ngumu sana kufikisha ujumbe kwenye ngazi za maamuzi, sifahamu kwanini wakati sasa hivi tunaishi kwenye dunia inayopitia kwenye miongo ya mawasiliano habari (IT).
Kwanza naishauri CCM iboreshe namna ya kuwasiliana na ngazi za uongozi pili naishauri serikali kuu, mawaziri wote mpaka Rais wa Tanzania waige mfumo wa Zanzibar wa "sema na Rais".
Kwa kukosa njia za kufikisha ujumbe kwa haraka nimeona bora ushauri wangu niutowe hapa JF, nafahamu utawafikia walengwa wote.
1) Nashauri huduma zinazotelewa bure na serikali ziwe za kulipia rasmi, kwa zote namaanisha zote. Kuanzia huduma zinazotolewa Polisi, iwe mtu ukitaka huduma yoyote ya kipolisi ulipie, kama siyo siku hiyo hiyo basi uandikiwe una deni kwa kupewa huduma hiyo na utailipa kupitia control numbers.
Rushwa imezidi serikalini, kama haujaombwa waziwazi basi utazungushwa kupatiwa huduma mpaka utie akili utowe rushwa au atokee "kishoka" wa hapo akusomeshe utowe rushwa, ndipo huduma yako ishughulikiwe.
Kwa mambo kama hayo, iwekwe wazi tu, kuwa ukienda kushitaki polisi unapewa control number unalipia unapewa huduma, na afisa ataekuhudumia atalipwa mgao wake hukohuko official kabisa.
Ili kupigana na rushwa, kama tumeshindwa kuweka sheria kali ni vyema tukaihalalisha tu malipo kwa kila huduma.
Au kama ilivyofanywa kwenye matibabu, iwekwe bima ya lazima kwa kila raia awe analipia hizo huduma, na pesa zitazotokana na hiyo bima waongezewe mishara na posho watowa huduma badala ya kuzungusha watu ili wale rushwa serikalini. Hii ni kwa wizara na idara zote zinazotowa huduma za bure kwa jamii, ambako ndiko kunakonuka uozo wa rushwa.
Kauli za viongozi kama zile za "za polish ya viatu", "kila mmoja ale kwa urefu wa kamba yake" zimekuwa zikihalalisha rushwa kiaina, sasa iwe ni wazi kabisa ihalalishwe kwa kuzilipia hizo huduma.
Polisi, mahakama, uhamiaji, ardhi, huduma zote za bure za manispaa. Ongezea na wewe kwengine.
Tunataka tuwe ni wateja rasmi wenye kuweza kudai haki zetu tunaponyimwa huduma kwa wakati.
Hayo ndio matunda ya chama chetu.Mfano mzuri ni jana kariakoo, moto uliotokea, hakuna huduma ya zima moto.
Sasa kwanini kujna vituo vya zimamoto kama hawana hata ubunifu wa kuwa na na malori kumi au kumi na tano ya maji wakati wote?
Au kuwa na ubunifu wa kuweka matank ya reserve -, mfano kariako ulipotokea moto karibia majumba yote yana visima vya maji.
Ubunifu unatushinda Watanzania, akili zetu zimelala sana, tunachowaza ni kulewa, ngoma, uasherati, kujionesha kwa watu na mambo ya kijingajinga tu.