Ushauri, Maoni na Msaada: Kwa wanaotaka kujilipua nje ya nchi kusaka maisha, kusoma na kuwekeza

visa on arrival means that you will need to pay a small fee to purchase a visa sticker when you are entering the respective country
Asante mkuu, kumbe muda mwingine neno halimaanishi kama lilivyoandikwa[emoji3] [emoji3] [emoji3]
 
Mikakati bado inaendelea Jana baada ya kupata taarifa za mkuu Izzo kujitoa, roho iliniuma lakini haina jinsi as nilikuwa nategemea ntampata mtu wa kuhost kutoka kwake


Sasa usiku kucha nikaumiza kichwa yaani sikupata usingizi kabisa, asubuhi na mapema nikachana kibubu changu laki moja ya kitanzania hivi then nikabeba vyeti vyangu, vya mshua na bibi mkubwa mpaka ofisi za uhamiaji Arusha kupata passports ya kusafiria, yaani pale maswali niliyopigwa mzee acha tyu.....sasa naulizwa passport ya nini kijana mdogo kama wewe embu rudi huko.....asee nilipata moto balaaa, nikawaambia nasafar ya kwenda China kuchukua mzigo next week......Mara nkasikia mbona haujaweka leseni ya biashara yako.....dah yaan nkabembeleza pale ila nachoshukuru kuna form ya mwanzo ile nishajaza, nkapeleka kwa mwenyekiti wa mtaa, nasubir maamuzi yao.

WAKUU HABARI NZURI NI KWAMBA NIMEJIUNGA coachsurfing.com yaani Leo Leo nikampata mdada mmoja wa Canada anaitwa Maya, tuko kwenye discussion naye mwezi April au June mwanzoni anataka kuja ila ameniambia tuendelee wasiliana kwanza atanipa info sijafahamu hili ni kwanini, ila alichoniomba nimrushie picha za
1: Room (muhimu hapa nimemwambia shared bed)
2: sitting room
3: bathroom
4:Garden ( kwetu hamna ni sehem tu ya kuanika nguo na bomba la maji)
5: neighborhood ( uswahilini ila nimemwambia hill)

Yaani hapa bado tunafanya mawasiliano naye na nilikuwa namwambia vipi Mimi nikija kwako, sijui if she will think am too rush.


cc
Dr Adam
Stunner
Lukizo
Daby
Kirikou
Na wakuu wenzangu wote.......



AFU LILE DUBWASHA LILODONDOKA HAPA NAONA JANA NA LEO NLLINAJIPONGEZA SANA.
 
Hongera sana mkuu money9. Kazana mungu atakusaidia pass utapata tuu,
 
Kwa wale mnaonitumia PM mniwie radhi napata PMs nyingi mno kwa sasa na wiki hii yote nakosa nafasi hata ya kushiriki vizuri hapa... nitajaribu kuwajibu wote kwa kadiri nipatavyo nafasi... nitajaribu kujumuisha pia aina ya misaada ili nije niijibu hapa yote kwa pamoja.

Kila la kheri.
 

Mkuu money9 Hongera sanaaaaa tu.
Kila la kheri Na kuombea upate Mafanikio mema.
 
nimepoteza passport nikiwa Namibia je ni taratibu zipi za kufuata niipate nyingine uzuri nina electronic copy yenye particulars ya pass iliyopotea? Je uhamiaji wana database labda ya kudumu haitanihitaji kusubmit viambatanishi vya awali?
Fanya upate POLICE REPORT ya huko ulipopotezea alafu utangaze kwenye gazeti uambatanishe copy ya gazeti wakati unaenda kuomba. Otherwise sio rahisi update maana kesi za LOST PASSPORT huwa hawa-handle wale maofisa wadogo wadogo, lazima zipelekwe kwa MKURUGENZI yule kama sikosei.
 
Kujiripua kumesha pitwa na Wakati kwamika hii wazungu wameshastuka ukijifanya wewe ni Msomali umejilipua mzungu anakuitia msomali mwenzako mupate kuzungumza kwenye mahojiano. Kisha huyo Msomali anakutoa nishai anamwambia mzungu kuw awewe sio msomali. Hao Wa-Tanzania waliojiripua mika ya nyuma kwa kutumia Utaifa wa Kisomali katika nchi hzi hapa (USA, UK, NORDIC COUNTRIES, NA WESTERN EUROPE COUNTRIES.) kwa hivi sasa wazungu wameshastuka huwezi tena kujiripua.Tanzania nchi yetu ni nzuri sana kama una pesa za kufanya biashara yoyote inalipa ili mradi ufanye kazi ndipo utakapo pata pesa ukiwa mvivu hutoweza kupata pesa na ukiangalia ukiwa ugenini ni sawa sawa na mtumwa wa watu weupe utatumika kwa wazungu na kila mwisho wa mwezi pesa unayoipata utaishia kulipa kodi ya kuangalia TV kodi ya Mama malkia wa uingereza kila kitu nchi za nje ni kodi hata ukitaka kwenda (Toilet) unalipa kodi aka (tax pay) utaishia kila mwisho wa mwezi huna pesa na madeni mengi yana kuandama matokeo yake, hata ukiamuwa kurudi nyumbani huna kitu.Asikwambie mtu nyumbani ni kuzuri kuna kila njia ya kuweza kupata pesa ili mradi usivunje sheria za nchi ninaishia hapo kwa leo.
 
Nasikia hii thread ni ya kitapeli
Umechanganya madawa. Ujinga mwingine wa watu wengi wanaochangia kwenye uzi huu hawataki kisoma kuanzia post namba moja, mtu anakuja na kurusha makamasi yake tu, hajali nguvu na muda watu waliochukua kujadili mambo ya maana.

Aliyekwambia ni mjinga kama wajinga wengine wanaoharibu mambo mema ya wavujajasho wenzao
 
Sasa mbona wewe hutaki kuishi Tanzania? Kipi kilichokusibu
 
Mgogoone mimi nimesafiri na kukaa nchi nyingi sana, sisi watanzania tuna roho mbaya sana, wenzetu waliyoko majuu ukifika kwao ukawambia kuwa wewe umetoka nchini kwao watakukaribisha na kukusaidia kupata kazi, work permit, hata ikiwezekena uraia ndio maana wao ni wengi nje ya nchi mfano wakenya, waganda, wanageria..... ila njo wabongo mpigie tu binamu yako kuwa akutumie visting card utamsikia mambo kibao; maisha magumu, usalama, kazi hamna, elimu huna, ninataka kurudi bongo hapa hapalipi. au nenda kichwa kichwa huko nakuambia ataongea na wewe kijapani wala hatakujua, ila fanikiwa uone kila siku anataka mkutane dinner.

Watanzania ni ndugu, wakarimu mdomoni sio kivitendo. nchi ambayo inaongoza kuwa na watu waliyoko nje ni bongo ila sasa tafuta stastics uone kama utazipata. tunavyoishi kinafiki nafiki hapa bongo ndio kinatokea huko nje.
 


Hata hapa wako. Wao kazi yao kukatisha watu tamaa na kutoa sababu kedekede. Muulize mbona wewe hurudi na kuishi huku hakuna jibu zaidi ya kusema maneno ya kipuuzi
 
nimepoteza passport nikiwa Namibia je ni taratibu zipi za kufuata niipate nyingine uzuri nina electronic copy yenye particulars ya pass iliyopotea? Je uhamiaji wana database labda ya kudumu haitanihitaji kusubmit viambatanishi vya awali?
Mkuu wao ndio wanakumbukumbu za kwako hasa zile za awali wakati unaomba pass na hapa kama ulitoa za uogo inabidi kichwa chako kisiwe na byte kiwe na angalau GB ili kiweze kukumbuka pale utakapo ulizwa maswali mawili matatu kwa wao kujilizisha wasije wakaona walitoa pass kwa mtu asiye wa jamhuri ya muungano... walichukua picha, alama za vidole, na kumbukumbu muhimu hivyo suala lako ni rahisi kama utaanza na kureport polisi kwa upotevu wa mali ya jamhuri ili hiyo taarifa ikusaidie kama reference ya kupata msaada uhamiaji na ubalozo huko ulipo...
 
umeeeleza vizuri sanaa mkuuu....
 
Mkuu South Sudan kuna vita vya wenyewe Kwa wenyewe.Fursa ziko Ila NI hatari Kwa wageni.
Unaweza kwenda Uganda Halafu unatafuta njia ya kuingilia S.Sudan.
kwenye migogoro ndipo watu wanatoboa risk kubwa faida kibao... hata pesa zao thamani yake nikubwa karibu kwa nchi zote zinazotuzunguka kasoro uganda tu na hapa ukijumlisha migogoro yao... Mf. Kenya, somalia, Ethiopia, Sudan zote, Burundi, Rwanda, DRC, Jamhuri ya Kati, Zambia, Malawi, Msumbiji, Na nchi zilizopo Bahari ya Hindi.... hapa Uganda ndio tunawaweza....

Pesa ikiwa kubwa kwangu binafsi ndio nashawishika kwenda katika hiyo nchi maana hata pato nitakaro lipata ni nafaida kiuwekezaji nikilirudisha nyumbani kwa maana litaongezeka maradufu kama nimeweka akiba bank ya muda fulani (Fixd)
 
Kama huwezi Basi huo ni unafiki na umbea. Ikiwa Umekuwa kuusema hapa na umeshindwa kuwataja huo ni zaidi ya ushambenga. Mambo yote yalikuwa yanafanyika hadharani
Hachana nae mkuu... tupige umbea wetu wenye faida wa kuangalia faida nje ya boksi hacha yeye ajifungie chumbani...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…