Ushauri, Maoni na Msaada: Kwa wanaotaka kujilipua nje ya nchi kusaka maisha, kusoma na kuwekeza

Mtu muoga hatakiwi hata kuwa rafiki yako
 
Scholarship nyingi hua zina mashart ya lazima kurudi nchini kwenyu baada ya kumaliza ili utoe mchango kwa ile elimu waliyokupa, so ukitaka kusepa majuu lazima uamue kweli kweli sio kubeep beep tu
Ukiishi ng'ambo zaidi ya miaka miwili harafu uwe hujajipanga kupotelea huko basi amini utakuwa na mtindio wa ubongo
 
Bro Kama Unaye mtu wa kukutumia invitation later ya nchi kama marekani ili kuepuka kufeli kwenye visa interview ni documents gani mtu anatakiwa kua nazo, Or You If You Can Hook Me Up With Someone Who Can Help Also Will Appreciate
Plan kwanza kuingia nchi za Kusini mwa Afrika chaka lingine naloona ukitaka kuanzia maisha ni Namibia. Kuna nchi hapa Africa unaweza zitumia kama daraja tu ili kufika mamtoni
 
Australia na Belgium ni ngumu sana kwa first degree unahitaji fedha nyingi kuanzia ada, malazi na fedha za kujikimu.

India na China, nenda wizara ya sayansi na teknolojia utafute zile nafasi za kufadhiliwa hasa China kwa first degree.
Mtu yoyote anayetaka kuzamia kwa ajili ya kwenda kusoma mimi huwa sina ushauri nae
 
Wakuu Mimi nimepata manzi kutoka USA, Bahati nzuri katika kuchati na kuongea kaniambia anakuja Tanzania kutalii na anataka kujifunza Kiswahili pia anapenda Africa. Yeye Ni Black Amerika.Mpaka sasa tupo kwenye mahusiano.
Sasa naomba mnipe abcd na mawazo kupitia yeye niweze kuingia US.




Sent using Jamii Forums mobile app
 

KInachoangaliwa na watu wa Homeland Security watakapokuuliza masuali ni "genuine relationship" yaani uhusiano wa kweli katika kupima kama unastahiki kupata visa ya kuingia USA.

Hivyo kama una nia kweli ya kwenda USA kuishi na huyo mwanamke, basi vuta subira na chukulia kama hauko na wala usimwonyeshe upo "desperate".

Pia itabidi yeye akirudi USA basi anakualika na wewe unaenda huko kisha baadae kijana unatoa sera zako imara.

Haya mambo haitaji haraka yanakwenda kwa mtindo twaite "chronological order" mpaka kufikia lengo lako.

Kila la kheri.
 
Nitakuelezea kwa uelewa wangu na mwisho nitavaa uhusika wako.

Kwanza, Tu-assume sio tapeli ni mdada mwema kabisa. Lengo lake yeye ni kuja kutembea Afrika ajifunze kiswahili na kukuona wewe boyfriend wake.

Ila wewe lengo lako ni kumtumia kuingia USA.

Nitajitoa ufahamu hapa.
Sio wewe wa kwanza kuwatumia hawa watu kuingia nchi zao ni watu wengi tu wamefanikiwa kwa hili.

Kikubwa akupende wewe na asiwe choka mbaya, hapa utafanikiwa. Kupendwa naye ni pagumu kueleza...maana kila mmoja anapenda kivyake. Ila kikubwa hawa watu mwonekano na uwazi.

Black sio wazungu ni waafrika wanaoishi ulaya hivyo uzungu kwao sio kivile. Kwa hiyo usitarajie mengi kutoka kwake...ila kama angekuwa mzungu ungetarajia mengi.

ok...

Utamtumia kuingia hasa hasa kwa kutembea. hapa kuna mawili utapewa visa au usipewe.

Bahati nzuri Ukipewa.
Utaenda kumtembelea kama alivyokuja kukutembelea. Kama una roho ngumu Utamtoroka unakuwa umeshachora ramani huku. Hapa lazima uwe na mtu huko uendako maana huwezi ukamtoroka demu ukaingia mtaani pasipo na sehemu ya kwenda. [Sishauri ufanye au usifanye]

Upande wa pili

Mahusiano yenu yanaweza kuwa mazuri mkapanga kuoana. Hapa uwanja ni mpana maana utafuata sheria na utaishi kwa kujitawanja. Tatizo la hapa patachukua muda mrefu na mnaweza kuachana hata kabla ya kuprocess chochote.

-Njia zingine ni ndogo ndogo kama kumtumia akutafutie scholarship. n.k
 
Asante mkuu, hata Mimi mwanzo nilianza pupa lakini baadae nikaona sijioneshe nipo after something.

Je issue Ni kwenda kwa mwaliko tuu au mpaka tufunge ndoa ndio naweza kukaa USA nakusaka life.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu Daby umeongea point Muhimu sana, kwa Sasa yeye Ni Lecturer chuo flani huko na yupo 30s age. Kwa kweli process za ndoa naona zitachukua mda mrefu, la msingi namsubiri aje kwanza niweze kumjua impression yake ipo vipi. Nashukuru Sana Mkuu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kawià ufike, hiyo njia ya ndoa ndio ya uhakika 100% percent, American woman hawezi kukubali kutenganishwa na spouse wake.

Achana na issue zote fuata process za ndoa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu nazidi kupokea maarifa nashukuru kwa hilo, una experience na hizi process kidogo.

Sent using Jamii Forums mobile app
Njia zingine ziko rafiki kwa waajiliwa wa serikali, safari za kidini lakini lazima uwe na strong ties Tanzania na MTU yeyote anayefanyakazi kampuni kubwa kubwa hapa Tanzania zenye majina hata wale wazungu pale ubalozini wanazijuwa hawana shida wanakupa viza bila shida yoyote.

Mdogo wangu alikuwa anafanyakazi Swiss air ilikuwa akifika ubalozini anaingiza tu passport take zamu ya kuitwa na councillor ikifika kwenye interview swali lao walikuwa wanamuuliza tu unaenda kukaa muda gani?

Mara ya tatu aliondoka na demu kama mke wake hats makaratasi ya ndoa hawakuuliza na ndio ikawa kimoja mpaka Leo na ni American citizen na anatumia American passport, na amepiga Public health kule yuko mtamu sasa hivi kupita maelezo na ameshawavuta karibu vijana 7 mpaka sasa na ana health center yake analipwa na Federal government, ukifika unaanzia maisha hapo kabla hujapata kazi sehemu nyingine.

Tatizo kubwa wanaotaka viza ya Marekani wengi ni majobless au watu wasio na shughuli maalum za kueleweka na hawana hata kampuni za kuzitumia kama bonye, huu ndio ukweli.

Lakini MTU yeyote anayetoka taasisi ya kueleweka ni lazima wakupe viza.

Note: Watanzania ni wachache sana Marekani ukilinganisha na wahamiaji kutoka nchi zingine za Africa, Waethiopia wanaongoza wamejaa tele.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Asante mkuu, hata Mimi mwanzo nilianza pupa lakini baadae nikaona sijioneshe nipo after something.

Je issue Ni kwenda kwa mwaliko tuu au mpaka tufunge ndoa ndio naweza kukaa USA nakusaka life.

Sent using Jamii Forums mobile app

Daby amekueleza kuhusu mwaliko hapo juu.

Ila hakikisha huyo mchumba ana kazi ya maana na ataweza kukusaidia kipindi chote unapokuwa upo kule.

Wewe pia uwe na kazi inayoeleweka au hata ya kutumia ili ikusaidie pale utakapoomba viza.

Lakini unapokuwa kule unakuwa unajijenga kidogokidogo kwa kusoma mji anaoishi, kazi zinapatikana vipi, vyuo na kadhalika.

Katika mambo mengi ambayo yatakusadia wewe ni huyo mchumba kuwa anafanya kazi na sio kuja kuwa mtegemezi wako wewe ambae bado ni mgeni huko.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…