Ushauri, Maoni na Msaada: Kwa wanaotaka kujilipua nje ya nchi kusaka maisha, kusoma na kuwekeza

Ushauri, Maoni na Msaada: Kwa wanaotaka kujilipua nje ya nchi kusaka maisha, kusoma na kuwekeza

Dah lini sijui ndg zangu
Kwa sasa ukitaka kwenda UK basi uende kama mwanafunzi.

Sasa hivi wamerudisha viza ya miaka miwili baada ya kumaliza masomo, yaani first degree.

Hiyo yaitwa graduate visa na baada ya hapo ukitaka kuendelea kuishi na kufanya kazi basi utahitaji kuomba viza ingine iitwayo Skilled Worker Visa.

Hii Skilled Worker visa ni ya miaka 5
 
Huu uzi ni mzuri maana utasaidia wenzetu pia kimawazo na kifikra pia,mtu anaweza kujua wapi pa kuanzia Kama akitaka kusafiri,sema me naanza na hapo kwenye faida ulizopata,ni kweli faida ni nyingi sana ukitofautisha na bongo,lakin kaka sijaelewa kitu,umesema umeishi miaka 8 na umeweza kujenga ghorofa bongo na mashine,sasa me najiuliza mbona miaka 8 midogo sana??uliwezaje??au ulikuwa hauli vizuri??ulikuwa unajibana sana au ulikuwa unaishi nje ya mji(maana huko ndo kila kitu kinakuwaga poa,tofauti capital city au capital ya uchumi)???
Swali langu la 2,Kujilipua,sijaelewa kidogo hapo,unazungumzia kujilipua kWa aina gani??maana zipo nyingi sana,mfano kuna kujilipua kwa kujipa uraia wa nchi zenye vita ili kuomba hifadhi(mfano wa nchi,Somalia(watoto wa kinzanzibar wanajilipua sana na kujipa uraia wa kisomali,Eritrea,Africa ya Kati,Sudan n.k),au kujilipua pia kWa kuchana passport kWa ajili ya kuomba hifadhi Kama mtu ambaye hana uraia wa nchi yeyote ile,hiyo ni mifano tu na kuna wengine wanaweza ongezea,sasa kaka wewe unazungumzia ipi hapo??maana kutafuta mke mzungu kuoa na kupata karatasi,hiyo siyo kujilipua(mawazo yangu).
Kingine kwenye changamoto,naweza ongezea hali ya hewa maana sisi wengi tushazoea joto au jua kWa mwaka mzima lakin wenzetu kuna baridi sana baadhi ya miezi na kuna joto kWa miezi 4 tu katika mwaka,changamoto nyingine inaweza ikawa karatasi mfano Europe kila unachokifanya inabidi ufanye photocopy,unabaki na original unatoa copy na katika kila kitu utakachofanya na wakati kwetu siyo hivyo,wengine wanaweza ongezea.
La mwisho naweza ongezea pia hapo jinsi ya kwenda,unaweza pia kwenda nchi yeyote ya Europe kWa kisingizio cha kutaka kusoma lugha yao,kWa mfano ujeruman,unaweza ukatafuta chuo au center yoyote ambayo hipo ujeruman ambayo inajulikana na serikali ya ujeruman na ambayo inaweza kukualika kWa ajili ya masomo ya lugha yao ya Dutch,hao jamaa wakishakubali uwa wanakutumia barua ambayo inaonyesha ushajiandikisha katika chuo chao kWa ajili ya kwenda kusomea lugha,hiyo barua wanatuma pia ubalozi wa ujeruman Dar,so ukienda pale wanaweza kukupa visa ya kusoma,inaweza ikawa ya mwaka na ukawa unaruhusiwa kufanya kazi labda kWa masaa 20 kwa week(kihalali)na kuweza pia kufanya kazi masaa mengi zaidi ya hayo,ukapata sana mpunga lakini isiwe kazi ya kihalali,nikimaanisha black work(watu walioishi Ulaya na USA wanaelewa naongelea nini),baada ya hiyo visa unaweza omba card ya kuendelea kusoma kWa mwaka wa pili au unaweza mpata mtu mwenye uraia au resident permit akakuoa na maisha yakaendelea au ukapata kazi ya kudumu na ukaweza badilisha status kutoka kwenye uwanafunzi na kuwa na status Kama mfanyakaz,hapa wanaweza kukupa kabisa resident permit ukaweza kuvuta na ndugu zako wengine kupitia mgongo wako.
Jingine unaweza tafuta mtu mwenye uraia wa Ulaya au USA ukaongea naye,ukampa pesa mnafunga ndoa ya uongo,yeye anasimamia kila kitu mpaka unapata permit yako halafu anafanya divorce lakin anakuacha na permit yako,nafikiri wengine watakuja kuongezea,sema kaka naomba unijibu hilo swali langu hapo juu kuhusu kujilipua.
Shukrani sana[emoji1317]
Kaka nimekuelewa Kaka nimekupenda hiyo
 
Ujermani pako Poa mkuu, na huduma za kijamii wapo vizur.... ukishapata Residence permit selikali inakulipia asilimia flan kwaajir ya kusoma Lugha , nauli, na pesa ya makazi. Pia wanazo ofisi zibaitwa Job-center ni kwaajili ya kuwatadutia wageni kazi... Pia kazi zisizo rasmi ni nyingi kama kusambaza magazet, upishi migahawani, usafi nk. Na unapata pesa nzuri tu mwisho wa siku... ubaguzi umebaki kwa wachache sana.. na kumbuka hali ya Usalama ni kubwa sana... wenzetu walishtuka kitambo mfano Hamburg na Berlin hadi kuna makanisa ya Waghana... ebu tuamkeni na tujiamini tusiogope simulizi za uongo na kukatishana tamaa....
This is true
 
Kijilipua kama refugee. ( unatafuta nchi inayokubalika)Ukiwasilisha maombi yako, unakuwa na one year mpaka wakujibu, hivyo mda huo unaweza tafuta mwenza
 
Jiwe moja ndege wawili mkuu naona wadau wengi walinishauri ninyooke mojakwamoja ughaibuni lakini pia njia ya kufika botswana ndo ilikuwa lengo la kuweza kufika ughaibuni kiufupi nacheza kotekote ili mradi tu njia ifunguke.
Kwahiyo mkuu ukisha fika Botswana unauhakika gani Kama pale njia unaweza kuwa simple mzee ufafanuzi kidogo kaka
 
Mkuu usiuchukie uzi mzima kwa makosa ya "wahuni wachache".

Kuna watu tumesaidiwa hapa na uzi umekua ukitoa mwangaza mwanana kwa wadau mbalimbali.

Ila pole kwa yaliyokukuta.

Umesaidiwaje kwenye siredi hii? share your story.

Hakuna lolote lilonikuta humu la kuhitaji 'pole'. Nililetaga feedback kamili ya kilichojili. Soma post #3,190.

Ni thread ambayo motive yake kuu ilikuwa ni ya kitapeli, na ilikuwa iko well organized na kagroup ka watu kadhaa humu maarufu. Tuna full evidence.

Of course wachangiaji wengine waliifanya thread kuwa informative on some issues.

Basically, ilikuwa ni siredi ya 'koneksheni' hewa za kwenda ughaibuni. Bongo nyoso!! 😎

-Kaveli-
 
Umesaidiwaje kwenye siredi hii? share your story.

Hakuna lolote lilonikuta humu la kuhitaji 'pole'. Nililetaga feedback kamili ya kilichojili. Soma post #3,190.

Ni thread ambayo motive yake kuu ilikuwa ni ya kitapeli, na ilikuwa iko well organized na kagroup ka watu kadhaa humu maarufu. Tuna full evidence.

Of course wachangiaji wengine waliifanya thread kuwa informative on some issues.

Basically, ilikuwa ni siredi ya 'koneksheni' hewa za kwenda ughaibuni. Bongo nyoso!! 😎

-Kaveli-
"Of course wachangiaji wengine waliifanya thread kuwa informative on some issues."

Hapo ndio tuliposaidiwa wengine.
Ahsante.
 
Tuwe makini na kujilipua wakuu, waweza ukakosa maji na chakula jangwani😢😢
1491906_IMG_20170312_230723.jpeg
 
Pole sana mkuu. Tupe story yako kama hutojali, wadau waweza saidia kumnyoosha huyo tapeli.

Cc: Mwanamaji

-Kaveli-
anaitwa Patrick Emmanuel meagie, ni mkazi wa Arusha
namba zake za simu +255758354393 na 0622596982
tulikutana ktk huu uzi alitoa wazo la kuanzisha wasup group ili tuweze kupeana fursa za kazi nje ya nchi
ilikuwa 2020 mwanzoni ktk majadiliano kupitia wasup akasema yeye ana fursa ya kazi ktk nchi ya poland inahitajika kulipia agent fees mil 2.5
nikaonana nae dar kwakuwa sikumuamini sana nilienda kwa mwanasheria tukaandikishana
2020 janga la Corona akadai mipaka imefungwa ,nikamwambia ikifika 2021 Sept sijaondoka nirudishie pesa zangu
ilipofika huo mwezi nikaanza kumdai pesa zangu alichoamua ni kuni block japo namba zake zipo hewani
nikaenda polisi kushtaki wakasema nikachukue Rb ktk mkoa niliojaza nae mkataba ambao ni dar mimi nipo mwanza.hadi sasa sijapata nafasi ya kwenda dar kuchukua Rb
 
Back
Top Bottom