Ushauri, Maoni na Msaada: Kwa wanaotaka kujilipua nje ya nchi kusaka maisha, kusoma na kuwekeza

Mkuu umesema upo tayari kuwa host if I'm not mistaken!
 
Canada kupata kazi ni rahisi mno mno... Sasa sijajua requirements za hiyo form ni nini but kikubwa kuliko vyote ni valid passport tuuu yenye uhai....
ubarikiwe aisee...unajua mi.mwenyewe wakati natafuta schengen visa ya.uholanzi nilikua natishwa sana sijui lazima bank ststement ishibe...huwezi amini booking nilifanya booking.com zile za kucancel baada ya wiki na statement ilikua na laki 2 mbili tu ila kuna jamaa kama wewe alinifariji...thanks boss ubarikiwe
 
Du mkuu kumbe ni muda sana nafikiri ilikuwa kipindi hayati mwalimu nyerere yu hai.
Je wewe ulipataje fursa ya kufika ughaibuni na ninafikiri mpaka sasa upo huko njia ipi ulitumia kuta viza mpaka kupata PR huko uliko?

Mkuu,

Mimi niko hapa hapa nyumbani Tanzania, nina familia na nafanya shughuli zangu hapa hapa. Nimewahi kutembelea nje lakini ni kwa mwaliko/kikazi na kwa kufuata utaratibu ambao wenzangu wameuelezea vizuri tu humu. Umri haujanitupa mkono kutoka kwa sasa lakini ninahitaji kujipanga haswa. Ila ukiwa na dhamira ya kweli kabisa utafanikiwa na nawashukuru sana wote wanaochangia hoja/mawazo/maoni elekezi (constructive ideas) kwa wanaohitaji kusafiri nje ya mchi kutafuta maisha.

Shukrani tena wote. Msiache moyo huu!

Kaka ...
 
Asante kwa kutuwekea fulsa hii
Tena km mimi nipo pande za kaskazini mwa Tanzania kuwatembeza tuu it will be so simple,tuunganishe mkuu kwa upande wangu sitakuangusha mkuu.
 
 
Amen... Karibu sana... Hizo bank statement kwanza unaweza hata ku edit.... Wengi hufanya hivyo... Unapeleka statement ina 20M kumbe uongo na wala hawafuatilii unapewa visa kiulainiii [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Kikubwa kupambana!!
 
ps chengine unajua wabongo tukiona wazungu tunajishtukia sana kuwaongelesha labda ngozi ila mi last month natoka gomz nmepanda na wajeruman wawili madem na mmoja boyfriend wa dem mmoja ndo katokea ujeruman..sikushobokea madem ila kupiga stori.na jamaa yuko peace sana uzuri sikuhizi mambo ya whats app sijui instagram..amekua bonge la mshkaji yaani na ukimtoa out usimdondokee sana hadi ajishtukie sometimes simamia game akuone independent
 
Sawa sawa mkuu... Mungu akubariki sana.... Naamini tutafanya kitu hapa watu waamke.
kweli aisee
Mkuu hyo ya Canada ni Option number 3 kuna jimbo linaitwa Quebec Mission na Project yetu itakijita ndani ya Quebec
boss naomba muwe mnanitag kukiwa na.madini maana vibarua vya wakenya kama wahindi na watoto lazima wale aisee..mbarikiwe
 
Mimi nataka kwenda Denmark. Naomba jinsi ya kuingia na fursa zilizopo huko zisizohitaji elimu.yaani nguvu kazi.
Nilikaa Denmark mwaka, ni nchi ya watu wastaarabu Europe nzima, ni wapole na wenye upendo. Kazi za mikono kibao.

Kama alivyosema Lusungo kwamba kuna njia mbalimbali na sababu zaw kukupeleka huko ikiwa ni pamoja na Kuomba kwenda kusoma, kualikwa na rafiki/ndugu/mwenza au masuala ya utamaduni....

Omba Mungu upate Denmark ni pazuri sana......
 
nakubali hoja
 
Ni kweli, Denmark imeshika namba moja kwa nchi zenye furaha zaidi duniani.
 
Ok kujibu maswali yako kwa ufupi

AGENT
Nimeshazungumzia aina za maagent na kazi au usaidizi wao katika mipango ya safari ambapo kuna aina 3 za maagent

So kama umesoma bandiko langu kuhusu Maagent na kazi zao ktk kufanikisha safari nadhani nilikuwa nakujibu ww
katika post ile

Mm najua maagent wengi lakini Option ya kupitia kwa Agent hasa wa Africa ni ngumu sana kutokana na siasa za uhamiaji kwa zile nchi zilizo kwenye A list

Pia unatakiwa kujua Agent ni Biashara kama zilivyo biashara zingine so siku zote mfanyabiashara wana vitu vitatu
1 kufanya biashara
hii aijalishi mazingira au athari ya biashara yake kwa jamii au mazingira

2 Ni kutengeneza faida
hii ndio option pendwa na wafanya biashara karibu wote duniani

3 Service (Huduma)
Hii ni option ya mwisho kwa mfanya biashara kwn kuna biashara zingine ni zahuduma kwanza ndio biashara kama biz ya kuuza majeneza au duka la madawa hyo kwanza ni huduma then ndio biashara lakn fedha kwanza ndio huduma wakt inatakiwa huduma kwanza ndio fedha


So kwa mifano hyo unaweza kuona wafanya biashara wanavyopenda fedha kuliko huduma so Agent wengi wa Africa anakufanyia mpango anajua kabisa kuwa ww ni lazima utarudishwa airport tu hata nje utapaona so unarudi wakat yy ameshapata fedha


Swali lako la pili VISA
Visa ukienda na tourist visa ni miezi 3-6 uwezi kufanya kazi ww ni wakukaa tu bhasi Malta wana aina 18 za visa ikiwamo visa ya uchumba

Raia yeyote wa Malta anayonafasi wa kuwa na mwenza hata nje ya nchi pia malta wanakubali uraia pacha so kama mkazi wa Malta amepata mchumba nje ya Malta anachotakiwa kufanya ni kwenda uhamiaji ya kwao na kueleza au kutoa taarifa zako na Uhamiaji wanapeleka taarifa hzo ubalozi ambao ww umeombea visa kumbuka mdhamini wako ni yule mchumba wako ambae yuko Malta na yeye ndio anakudhamini juu ya visa hii madhumuni ya visa hii ni kumpa nafasi shemeji au wifi kutoka taifa jingine kuja kujitambulisha ukweni so ukishafika Malta mambo mengine yanaweza kuendelea ikiwamo ndoa muda wa visa hii ni miaka 2 ambapo unatakiwa kubadilsha status ya visa kwenda kwenye RP kumbuka visa hii unaruhusiwa kufanya kazi ndani ya Malta



kirikou1 kweupee Hary Jay Ndata Prishaz WiseLady Mrike wembeee talentboy Dr.adams faida Daby Tombstone Piledrive Padri Mcharo Shyshii lucley kui tagamwa binti kiziwi dangadunguri Tembo2 lusungo kweupee pius1021 Prof cognition Agogo Jr Chakochangu soul provider Mrike
 
Hivi malta kwa utalii ipoje?
 
Asante mkuu....

Nilink na katoto ka kimalta basi mkuu...sitakuangusha nipate hiyo RP nikaangalie watu wanavyokula raha DL au sweden.
 
Du mkuu kumbe ni muda sana nafikiri ilikuwa kipindi hayati mwalimu nyerere yu hai.

Hiyo ni kitambo kidogo, nilipata mwanga (namaanisha "exposure") nilipojiunga na skauti nikiwa bado mdogo (darasa la 4 hivi). Nyerere hai tena na nguvu zake kabisa.

Je wewe ulipataje fursa ya kufika ughaibuni na ninafikiri mpaka sasa upo huko njia ipi ulitumia kupata viza mpaka kupata PR huko uliko?

Japo nimewahi kutoka nje ya Afrika na kuzuru nchi kadhaa duniani, nimetumia utaratibu wa kawaida kwa safari hizo, ni kupata mwaliko kisha safari ila sijawahi weka makazi huko kote na kwa sasa mimi nipo hapa hapa kwa JPM empire mkuu, nina familia na naendesha shughuli zangu pia. Haja ya kutoka bado ipo lakini inabidi kujiandaa haswa. Nawahamasisha wote wenye dhamira ya kweli ya kutoka kusaka ugali huko nje waende tena makumi kwa mamia.

Kaka ...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…