Ushauri, Maoni na Msaada: Kwa wanaotaka kujilipua nje ya nchi kusaka maisha, kusoma na kuwekeza

Ushauri, Maoni na Msaada: Kwa wanaotaka kujilipua nje ya nchi kusaka maisha, kusoma na kuwekeza

Njoo basi inbox tuongee.

Kuna jamaa yupo korea. Alichukua mkopo ofisini kwake akapotea ila alipofika ikabidi ajirudi aombe msamaha akaulipa
Ilikuwaje tena akarudi tena mkuu alihali mambo yalikuwa yamenyooka vile au alikuta korea pamenuna?
 
Ilikuwaje tena akarudi tena mkuu alihali mambo yalikuwa yamenyooka vile au alikuta korea pamenuna?
Hakurudi...yaani alijirudi ofisini kwake akaomba msamaha akawatumia pesa aliyokopa. Hadi leo yupo huko
 
Mkuu Lusungo naona bado Tokyo 40 na Copenhagen hawajatia timu hapa.
 
Isanga family mkuu hiyo fursa ya vietnum wanafaidi sana Waganda ndio siku hizi wanafuata sana pure leather shoe huko na wanauza sana DRC na unaambiwa ni bei rahisi sana.

Mkuu sisi ni waoga but kama unaijua vizuri tuelimishane ili mwenye uthubutu aanze. Mwenye macho haambiwi tazama.
 
Bibi mzaa mama yupo.sasa nikifika kurasini nisemeje.
Kama yupo basi wewe ni kuandika Ile hati then anaweka sahihi na Jina lake...ila mimi nilifanyia mkoa kuna Brother angu mmoja alikuwa mwanasheria so aniliandikia akaniambia niende mahakamani nikapige muhuri. Kwa wewe kaulizie kwanza utaratibu upo vipi wa kuipata affidavit then utajua pa kuanzia ikizingua wewe andaa mwenyewe tuu...cha msingi muhuri wa mahakama na statement ya kiapo ya bibi basi.
 
Miaka ya nyuma kuna wakenya wengi na watanzania baadhi walitumia ile fursa ya wakimbizi wa kutoka burundi walioishi kambi za mtabila na nyarugusu pale kigoma kupelekwa nchi ya pili ya ukimbizi zaidi ilikua canada na marekani hivyo ikawa nao wanajichanganya humo humo kama refugees wanaenda nje kilaini sana.
 
huu uzi ni mzuri sana...shida kubwa ya wa tz ni ubinafsi.....yes tumeumbwa hivyo wanadamu ila utaifa wetu hua hatuuweki mbele...mimi nimetembelea baadhi ya nchi ukikuta wenzetu wa nchi zingine wanaishi kindugu ila sisi mkiisha salamiana basi kila mtu kivyake.. niliokua nao karibu walikua wakenya, Ghana, pili ukienda kwenye hizo nchi unatakiwa uwe na malengo kabisa kabla hata ya kuondoka hio itakusaidia kwakua unakua unajua unatafuta nini.

Hapana mkuu.

Tatizo ni kwamba kila mtu amepitia njia nyingi na mbalimbali ambazo huwa ni vigumu sana kukukaribisha uwe karibu nae.

Kwa mfano watu wengi hawapendi kutoa barua za mwaliko kwa sababu nchi kama Uingereza wao wameweka dhaman ya pauni 1000 ambayo yule anaetoa mwaliko anaweka kiasi hicho kama dhamana ya wewe kwamba utarudi ulikotoka wakati wewe una mawazo mengine ya kujilipua.

Na kama atakukaribisha kuna wengine wanakuwa hawahami pale au hata kujitahidi kuchakarika na pengine kama una mke/mme ndani kijana anaanza ubaradhuli wake humo ndani wewe ukiwa kazini.

Hivyo watu wengi wanaogopa hiyo kitu ni hatari sana.
 
Australia wana mfumo mgumu sana wa uhamiaji na unaigwa na Uingereza na Marekani wanaiga sasa hivi.
Kuna nchi inaitwa lithuania naona wa Nigeria wana recommend sana kwenda maana hawana longo longo hasa kwa wale wanao enda kusoma Degree na kuendelea. Maana nchi nyingi wanataka ufanye test zao zile za Teofel so hawana kuna kozi kibao nzuri. Mimi ndio nataka nipitie Huko. Hapa na jichanga kwanza mpk October nitajua mbivu na mbichi.
 
Kwa hiyo huwa wanaendaga bila kupenda bali ni kwa kulazimishwa au?

Na una uhakika gani kama isingekuwa huyo JPM watu wasingetamani kwenda nje?
Kama maisha Congo au Naija yangekuwa bien kama ulaya wangeenda ulaya kufanya nini?ulishawahi kuwaona wanamibia ama wabotswana wengi ulaya /marekani?Yes before awamu ya tano majorities hawakupenda kwenda kuishi nje as waliona life in bongo is better than anywhere.
 
  • Thanks
Reactions: Qj_
Ni ajabu na kweli!!
Leo hii kubeba boksi kunatafutwa hivi wakati muda sio mrefu wabeba maboksi walikuwa wanatukanwa na kukejeliwa?
Holy mother!!
Jambo kubwa unalopaswa kufahamu ni kwamba MAISHA YANABADILIKA hata Yahya Jammeh aliyesababisha watu wakimbie nchi hakuwahi waza siku moja naye atakuwa mkimbizi....
 
Kuna nchi inaitwa lithuania naona wa Nigeria wana recommend sana kwenda maana hawana longo longo hasa kwa wale wanao enda kusoma Degree na kuendelea. Maana nchi nyingi wanataka ufanye test zao zile za Teofel so hawana kuna kozi kibao nzuri. Mimi ndio nataka nipitie Huko. Hapa na jichanga kwanza mpk October nitajua mbivu na mbichi.

Bado I recommend nchi za Ulaya Mshariki , Lithuania, Bulgaria, Romania, Hungary, Estonia na Czech.

Hawa wana ada ndogo sana za vyuo.
 
Miaka ya nyuma kuna wakenya wengi na watanzania baadhi walitumia ile fursa ya wakimbizi wa kutoka burundi walioishi kambi za mtabila na nyarugusu pale kigoma kupelekwa nchi ya pili ya ukimbizi zaidi ilikua canada na marekani hivyo ikawa nao wanajichanganya humo humo kama refugees wanaenda nje kilaini sana.

Sasa hivi hamna kitu kama hiyo.
 
Ahaa ahaa dah umenichekesha kweli wanasema never say never. Mara ohoo tunawaogesha mababu na mabibi Mara oh mabox Mara majina kibao but take it easy bro .

Halafu bongo kwenyewe kulivyokuwa kunasifiwa ni tambarare utadhani kila mtanzania anamiliki Vogue!
Nyadhifa nzuri lazima ufoji vyeti au utumie jina la mtu mwingine
Boksi hoyeeeeeee
 
Back
Top Bottom