Ushauri, Maoni na Msaada: Kwa wanaotaka kujilipua nje ya nchi kusaka maisha, kusoma na kuwekeza

Ushauri, Maoni na Msaada: Kwa wanaotaka kujilipua nje ya nchi kusaka maisha, kusoma na kuwekeza

Kuna nchi inaitwa lithuania naona wa Nigeria wana recommend sana kwenda maana hawana longo longo hasa kwa wale wanao enda kusoma Degree na kuendelea. Maana nchi nyingi wanataka ufanye test zao zile za Teofel so hawana kuna kozi kibao nzuri. Mimi ndio nataka nipitie Huko. Hapa na jichanga kwanza mpk October nitajua mbivu na mbichi.
Mkuu hebu niambie process zake na mimi nijaribu hiyo nafasi.
 
Mzee huko hakuna kazi kabisa,labda kama unataka kuuza drugs.

Sijawahi kufika Italy na nilidhani ni kiwanja poa kazi na fursa Za kumwaga
Umenitisha sana mkuu kuwa huko ni drugs mbele kwa mbele
 
N
Nimesaidia sana watu kuingia huku ulaya, na nimesaidia sana watu kupata wanza wao huku. ni vizuri kiasi furani kutoa wazo au kutoa mianya ya watu kuingia nchi za ulaya. Lakini kitu kimoja tu kimenitia doa hata sasa nimeamua kutokukubali tena kumwalika mtu ni hiki, unawaleta watu kwa mwaliko wako na kujicommet kwa chochote atakaa kwako kwa kipindi chote anatanachotafuta njia ya yeye kubaki, huku najitoa kwa gharama zote mfano chakula na huduma muhimu za nyumbani na hata pesa ya mizunguko yake, au wageni wake anaowaalika kwa ajiri ya kufanikisha lengo lake. sasa basi pale anapofanikiwa, tayari kishakusoma kila kitu juu ya life yako, kibinadamu kila mtu ana mapungufu yake, mimi nikiwa kwangu nina sheria zangu au mume wangu anasheria zake ambazo mtu lazima azifuate. mtu anaondoka na kuanza kukuongelea vibaya mno. Hapo haesabu mazuri hata moja uliyomfanyia, na pale unapofanikiwa kuleta mtu mwingine tena kwa ajiri la kumsaidia anaanza kutafuta mbinu ya kumuingia huyo mtu mpya tena na kutete, na yule mpya anapofanikiwa naye anakugeuka kama vile mimi ni adui na ni mnyama mbaya sana. kusambaza siri za ndani ya nyumba yangu nchi au kwa watu wanaonijui. imefikia hatua nimeona bora tu kutomwalika mtu, nitampa mbinu tu huko huko Tz basi, ila nimlipie au kuandika mwaliko tena siwezi tena
Mkuu inasikitisha na kukasirisha unampo msaidia mtu halafu akakulipa ubaya.. Nisaidie hizo mbinu mkuu za kufika huko..
 
Si kweli nchi zote zina ubalozi bongo isipokua visa handling ndo hufanywa na ubalozi mmoja... Ila Sweden... Norway.. Denmark wote wana ubalozi mkuu...

Ok ndio maana yangu kuwa visa handling inafanya na ubolozi mmoja,na ndio maana ukuinvite mtu huku Europe wanapa shengen visa.
 
Ndugu zangu Watanganyika mm nawambia nchi za Ulaya kila sehemu wamebana kuhusu wahamiaji hata zile ndoa zetu za usanii ni ngumu sana na hii inatokana na kuwa Raia wenyewe hawataki wageni tofauti na zamani ambavyo serikali ndio ilikuwa inakataa wageni wa magendo sasa inapofikia raia wenyewe hawataki wageni linakuwa ni tatizo kwa raia ndio wakukuficha dhidi ya serikali


Nakumbuka mwaka jana nilikuwa airport nchi flani nikakutana na mtu mmoja tukawa tunapiga story za hapa na pale si unajua wasafiri wakati tunapiga story kwenye TV wakawa wanaonyesha wahamiaji wale wa kutoka Libya kwenda Italy jamaa akanambia dah wanahatarisha maisha sana waafrica nikawambia na mm ni mwafrica kwani watu weusi wengi wa Ulaya au US ktendo cha kuitwa wanaasili ya Africa kwao wanaona kama ni kashifa wanataka waitwe blacks tu wanataka watambulike kwa race si Asili kitu ambacho kinatufanya watu weusi tuonekane tunamatatizo makubwa sana ya akili na ufahamu nimetembea sana nimekutana na watu wengi sana Ukmkuta mchina hata kama China hajawai fika anapenda kwanza atambulike kwa Asili yake kwanza watu wote weupe wanapenda kutambulika na Asili zao kwanza mm nawapenda sana wazanzibar wanajitambulisha kwa Asili zao mfano popote alipo mzanzibar anapenda atambulike kama Mzanzibar japo duniani hakuna nchi inayoitwa Zanzibar kuna Tanzania

Sasa katika mazungumzo yetu na yule dada tulitekutana nae Airport akanambia mm nimetokea Malta ni mfanyakazi wa serikalini akanionyesha passport yake ilikuwa ni Diplomatic pass kwa wenzetu weupe kupata Dip pass si kitu rahisi kama kwetu tu so akanambia kuhusu Malta kwamba wao ndio wenye Sheria rahisi sana kuliko nchi zote za ulaya na ukikaa Malta mwaka mmoja ukiomba uraia si RP wanakupa hasa kwa nchi zilizotawaliwa na waingereza nikashangaa sana akanambia hii ndio njia nyepesi ya Kuingia Ulaya na pia ndani ya kisiwa cha Malta wanataka sana wafanyakazi kutoka nchi zilizokuwa koloni la Uingereza nchi ina watu wachache sana so nguvu kazi ni ndogo sana Malta ina watu laki 4 na nusu tu sasa wanaitaji sana watu sasa njia hii ambayo watu wengi hawaijui kwani ni siri na watu wakijua wataingia kwa wingi na madhumuni yao yatakuwa ni kuingia ulaya baada ya kupata uraia na hii itapelekea Umoja wa Ulaya watawazingua so tukapiga story nying tu


Siku zote wanasema aiwezekani kwenda jela bila ya kupitia mahabusu kwanza mahabusu ni kama katikati ya Uraiani na jela so watu wengi wanataka kwenda Ulaya lakini Mm ningependekeza kabla ya kwenda Ulaya ni vizuri ukapitia nchi yeyote wanayoishi watu wa jamii ya Ulaya ili kupata uzoefu wa kuishi Ulaya moja wapo ni Malta

Faida ya Malta kwanza wanaongea kingereza na Lugha yao jeshini hawaamini ktk namba 3 Uraiani namba 3 ni kama namba ya kuruhusu kufanyika kwa kitu na namba tatu imekuwa namba kipenzi kwa Raia lakini namba tatu ni adui kwa watu au vyombo vya usalama na ulinzi kwa nini nimetumia mfano wa namba tatu kwanza ni ngumu sana kwa Ulaya kupata kazi bila kujua Lugha vizuri ya mwenyeji wenzetu kingereza ukijua au kuto kujua hakiwezi kukuletea mafanikio au kukupunguzia kitu kuanzia maendeleo au kijamii


Sasa unapokwenda nchi ambazo hawaongei kingereza inakuwa ni ngumu sana kumbuka nchi zote zinazoongea kingereza zina sheria kali ya uhamiaji kwa vile wahamiaji wamejaa kwani robo tatu ya dunia wanajifunza au kuongea kingereza na target yao ni kwenda nchi zinazoongea kingereza mfano UK,US ,Canada,Australia ,NZ ni nchi ambazo zimejaa wahamiaji na kufanya hata ajira kuwa ni ngumu sana kwa watu wanaokwenda huko


Tanganyika wanaojua kingereza vizuri ni wachache sana so unataji kwenda kwenye nchi inayoongea kingereza kwanza ukijue vizuri then ndio unahamia nchi ambayo hawaongei kingereza ndio maana nikasema Malta kwni kutafasiri Lugha kwa njia tatu ni Tatizo kwani ukienda Ujerumani kwanza utakitoa kijerumani kukiwekwa kwa kiswahili then ukipeleke kingereza kwanza utajikuta unapoteza maana ya neno husika kwanza ni vyepesi sana kutafasiri Lugha yeyote kutoka kwenye kingereza lakini ukishazidisha Lugha ya tatu ni Tatizo Ukiwa Malta mwaka mmoja utakijua kingereza na kiswahili kitaondoka kwa vile hakuna mtu wa kuongea nae so kingereza ndio kitachukua nafasi ya Kiswahili ktk ubongo wako so kutoa kingereza kwenda Lugha unayotaka ni vyepesi tu kwanza pale Malta wanafundisha Lugha za mataifa mengine so unaweza kuanza kusoma hapo hapo kabla ujaenda kwenye nchi husika


Kwa nini nimechagua Jeshi kwanza ndio njia nyepesi ya kupata uraia nchi nying kupata uraia ni lazima ufanye mtihani ambao unatakiwa upate 70% kwenda juu wengi wanafeli sana mtihani huu lakini ukipitia Jeshini hufanyi mtihani huu ww unapata tu uraia kama ukitaka pia jeshini kwa huku Unasoma chochote gharama ni za jeshi kumbuka wazungu hawaamini Elimu ya Africa so kama umesoma shahada yako utaongezea masters kama ujasoma utatafuta cha kusoma kwani mkataba ni miaka mitano mitano

Nchi nying sana za dunia ya kwanza wanachukua Raia kutoka nchi nyingne lazima uwe ni mkazi halali wa nchi hyo yani upate RP kitu ambacho ni kigumu sana kwa wahamiaji wa kutoka nchi masikini vigezo ni vigumu sana lakini kwa raia wa Ulaya na US wanayo haki ya kufanya kazi au kuishi ndani ya nchi yeyote ya Ulaya au US au Canada na Austaralia
hv mnajua Russia wanatoa uraia kwa mtu yeyote anayetaka kuingia jeshini tena kutoka sehemu yeyote duniani? Russia unapata uraia kwanza ndio unaingia jeshini

Pia faida ya Jeshi kwanza unalipwa mshahara so maisha yako yatayatakuwa ni mazuri pia unapata elimu bure pia jeshi ndio taasisi inayoheshimika dunian so kama utamaliza trust me huwezi maliza mtaa kabla ujapata kazi tena kwa fani uliyoisomea kwa sababu ukipita jeshini vyeti vyako vitaonyesha so mzungu akiona ulikuwa jeshini dah unajua wenzetu wana uzalendo sana so utapata kazi na watakuheshimu sana kazini

Yapo mengi ya kuonge bt mwenye swali ushauri au kuhusu nchi yeyote lakini si Africa coz sina uzoefu na nchi za Africa

Note Katika Wajerumani kumi ukimwambia ww umetoka Tanganyika nane watataka wawe rafiki yako wajerumani wanawapenda sana watanganyika ( Tanzania) Sema serikali yetu imeshindwa kutumia fulsa hii lakini kama watakaa chini na wajerumani wakongea vizuri wanaweza kutusaidia sana kuanzia kimasomo kwa vijana wetu kwenda kusoma huko kuliko hata mwingereza mwingereza hana mapenzi na sisi sana kwani anaona sisi si kama koloni lake kivile yeye anamapenzi na Kenya

Kingine ninachowashauri ndugu zangu kama unakuja huku na kufanikiwa kosa kubwa wanalofanya watu kutoka Africa ni kuoa au kuolewa na watu wa huku ni kosa la kiufundi sana kufanya hvyo hii imepelekea watu wengi kukaa miaka mingi bila ya kwenda Africa kwani ni ukweli usiofichika wazungu ni wabinafsi yani swala la ndugu au jamaa kama sisi kwao hakuna so unajikuta unaiga tabia hyo na kujikuta unashindwa kuwekeza kwenu au kuwasaidia ndugu zako wa Africa

Pia hata watoto mtakao wapata nataka kusema ukweli na nimefanya utafiti juu ya hili kuwa watoto ambao mtu mweusi anazaa kwa kuchangaya damu na watu wa jamii nyingine wanakuwa na roho mbaya sana dhidi ya jamii ya watu weusi wanatamani kuonekana wazungu lakini jamii ya wazungu inawakataa wanajikuta njia panda so wanakuja kwa jamii ya watu weusi lakini wanakuwa na chuki kubwa sana kwa watu weusi lawama zao ni kwa mzazi mweusi kuwa bila ya ww mm nisinge tengwa au kutukanwa so watoto hawa kujua au kusaidia ndugu zao waliopo Africa ni ngumu sana ww fanya uchunguzi tu kwani wanajiona wao si waafrica wanajiona ni wazungu lakini jamii ya wazungu inawakataa

Lakini ukioa mtanzania mwenzio kwani hapo lazima kuja nyumbani Africa mtakuja na kitendo cha nyinyi kuja kinawafanya na watoto wenu wajue umuhimu wa ndugu zenu na kuwasaidia kwani kunakuwa na connection kati ya nyinyi na ndugu na watoto kupitia nyinyi

NO PM (chumbani ) kwani siku zote mazungumzo yanafanyikia Sitting room au sehemu ya wazi chumbani(PM) yanafanyika mazungumzo ya wapenzi tu


Dumelang jme Tembo2 impongo kui Tombstone Piledrive Prishaz wembeee pius1021 cognition


Mrike mwandende impelle Chakochangu Agogo Jr

Richard chotera lusungo Sky Eclat Mfikilwa
Hon Nkundwe 365 bigmind MANCNOO
dah, ngoja nikusanye air fare niibuke malta, hivi kinywaji cha malta asili yake ni malta mkuu?
 
Lithuania uchumi wao ni mbaya saana,hata wao wanapambana kukimbilia nchi nyingine,chuo utapata lkn kazi hazipo,nisawa na Spain choka mbaya huko .au Italy,romania bora ya Tanzania

Ni njia mkuu, kabla hujafika Botswana unapitia Zambia kwanza.
 
Njia rahisi ni kupitia Nairobi Kenya coz Dar hawana embacy Ila visa yao ni very easy kuipata.
Nipo tayali nitoke inje ya Africa maana nimeenda Inchi zote za east Africa na Central Africa na baadhi katika inchi za kusini mwa Africa sioni jipya,
 
Dah mkuu embu nielekeze hayo maujanja yako ili kesho morning tu nitie maguu migration coz nasafari ya kenya halafu migration wanizingua tu.
Kama ni kenya si wakupe ndogo ile karatasi na picha juu. Ila ndo hivyo kaka tafuta namna ujianfikie hiyo invitation letter mwenyewe, ingia net sample kibao,
 
Aisee hakuna kitu kinasumbua Kama reference letter hapa kwetu. Yaani lecturers hawana muda kabisa wa kukuandikia barua. Akikuonea huruma sana anakwambia umpelekee draft then yeye arekebishe na kusaini
Mm niliamua kuchonga muhuri pale congo street sipati tena shida, zipo permanent nikurekebisha title tu
 
Mwaka juzi nikapata admission Coventry University - MSc Oil and Gas Management, scholarship zinapitia wizara ya elimu, natimba mjengoni wananiuliza wewe umejuaje kama kuna scholarahip, nikawafungulia pc nikawaonyesha tangazo kwenye website yao. Daaaa nilijua tu hapa sina changu. Nilikosa scholarship ile.


Kwenye nyekundu hapo, ushapata admission tayari sasa wizarani ulifuata nini mkuu? Fafanua kidogo hapo.
 
Back
Top Bottom