Pre GE2025 Ushauri: Mbowe ajiuzulu mara moja kama Mwenyekiti wa CHADEMA

Pre GE2025 Ushauri: Mbowe ajiuzulu mara moja kama Mwenyekiti wa CHADEMA

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
1. Wapi unapoisoma unayoiita kesi? Kulikoni kutokujikita kujibu hoja kwa hoja?

2. Wanaohusika ni kina nani ndugu? Aghalabu na sisi unaothubutu kutuita tusiohusika labda nasi pia ni nani?

3. Kwanini neno demokrasia kwenu ni shida? Kwanini mnaotaka kuleta vurugu msiwe ni ninyi?

4. Kwanini hudhani tuliompigia kura Mbowe ni sisi? Na pia kwanini mnataka kujimilikisha chama? Kwanini mnadhani mna haki zaidi kuliko wengine?

5. Kwanini hamdhani chamani tuna haki sawa? Kwanini hamuoni kuwa mnahangaika kupinga demokrasia tunayoipigania nchini na vyamani?

6. Umeandika mengi ambayo kwa hakika hayana msingi wowote!

7. Hakuna tunapolazimisha lolote wala popote, zaidi ya kuwa tunaona mnataka kutulazimisha misimamo yenu mipya isiyokuwapo. Kilichokuwa chama cha haki, uhuru na demokrasia leo kimekuwa na siasa za tombola.

8. Ustaarabu ni kuwa, kukitokea kukengeuka, demokrasia huchukua mkondo wake. Ni Hilo tu tunalolitaka kurejelewa sasa.

9. Tumesema huyu bwana ana uchaguzi mmoja, ku retreat kwenye misimamo ya chama inayoeleweka au kupumzika?

10. Kulikoni #9, ni chungu mno kwenu? Kwamba mnataka kutulazimisha na siasa za ku bet? Hiki chama ni cha umma, si mali binafsi.

11. Kulikoni ninyi kutaka kuleta vurugu hivi? Ni watu wa namna gani ninyi msioweza kuona wanachama wanataka nini?

12. Waziwazi siasa hizi za kulamba sumu hatuzitaki.

CHADEMA, ACT, CUF na wengine, na hofu ya kuonja sumu

13. Ninakazia:

hiyo #12 hatutaki
"Kesi" nimetumia kama msemo tu, nikiwa na maana kutofautiana mawazo.

Maswali yako mengine kuyajibu naona kuchoshana, kama una hoja iweke kwa mtindo huo twende sawa, lakini sio maswali juu ya maswali...

Ajabu unasema nimeandika mengi yasiyo eleweka halafu unasema kwangu neno "demokrasia ni shida", wakati kwenye hayo maelezo yangu nimekuonesha na wenzako demokrasia ikoje kwa vitendo, na sio maneno kama haya unayoandika hapa.

- Hapo demokrasia ni shida kwangu au kwenu? au kwenu demokrasia simply mnamaanisha mnachokitaka nyie ndio lazima kiwe tofauti na wengine walivyoamua?! kutaka Mbowe aondoke mna maana ipi? ndio demokrasia yenu hiyo?! hata siwalewi na ndio maana hata mleta mada nae amepotea!.

All in all, muda wa Mbowe ukifika ataondoka, simple, kama hamumtaki muandaneni yule mumtakaye, lakini kupiga kelele zenu wakati huu ni kukivuruga chama kikiwa kwenye harakati zake nyingine.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Kesi nimetumia kama msemo tu, nikiwa na maana kutofautiana mawazo.

Maswali yako mengine kuyajibu naona kuchoshana, kama una hoja iweke kwa mtindo huo twende sawa, lakini sio maswali juu ya maswali...

All in all, muda wa Mbowe ukifika ataondoka, simple, kama hamumtaki muandaneni yule mumtakaye, lakini kupiga kelele zenu wakati huu ni kukivuruga chama kikiwa kwenye harakati zake nyingine.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app

1. Kama kesi umetoa kwenye maneno yangu umeninukuu sivyo. Hakuna popote nimesema hayo!

2. Kama kutofautiana kimawazo ni tatizo kwako si tatizo kwetu. Tatizo ni misimamo, imani na falsafa kuparaganyika.

3. Kwenda sawa ni jambo la msingi. Kama ni nia yako kujadili tukubaliane kwenda na hoja moja moja. Kumbuka nilijibu na kuuliza tokea kwenye lukuki uliyokuwa umeandika.

4. Kuondoka ni jambo la afya. Hakuna wa kukaa milele, kumtaka au kutokumtaka Hilo ni jambo la kidemokrasia na kiutendaji.

5. #4 ukikiuka misingi tutakosa uvumilivu.

6. Kukivuruga chama ni kukiuka haki za wengine. Kuziita hoja za wengine wenye mawazo tofauti kupiga kelele ni mfano wa vurugu hizo za wazi.

7. Umoja ni nguvu hapo #6 sijui ni harakati zipi za chama zitafanikiwa kwenye utengano.

8. Hapo #3 yapo maoni ya wazi ya namna ya kuendelea mbele. Uchaguzi ni wako.

9. Ukipenda angalia mdau hapa na umuhimu wa imani thabiti:

"Imani ni kuwa na uhakika."

10. Bila kusahau, hakuna popote nimesema demokrasia ni kile tu tunachosema sisi, labda wewe kama unadhani demokrasia ni kile tu mnachosema ninyi.
 
- Kwanini Mbowe amseme vibaya Samia wakati walikuwa wote kwenye meza ya maridhiano? unataka wakati anajenga, awe tena anabomoa hapo hapo?! haiingii akilini.

- Ukisema maridhiano hayajazaa matunda, utakuwa na tatizo la kupoteza kumbukumbu, hukumbuki hata hii mikutano ya siasa inayofanywa na Heche maeneo tofauti kwa sasa nchini ni matunda ya maridhiano.

• Labda wewe usiyetaka maridhiano utuambie, njia ipi unayoipenda iliyowahi kufanikisha jambo lolote kisiasa ambayo ulitaka Mbowe aifuate? sio kelele tu.

- Mbowe kujuta kumuamini Samia hilo sio kosa kwake, ni ubinadamu; yule sio jini aijue dhamira ya Samia kuanzia mwanzo, hoja zako nyingi hazina mantiki.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app

Tatizo unataka kunilazimisha kuukataa ukweli. Naomba nikuelimishe kidogo tu, mikutano ya siasa ni haki ya kila raia, haikutakiwa maridhiano kujirudisha Bali kauli ya kisiasa tu kutoka kwa Rais.

Naomba nikupe ushahidi wa mambo mawili kwamba Mbowe alituhakikishia kwamba mambo yataenda vizuri. Kwa mfano Kwenye mkutano wa kwanza wa CHADEMA 2022, pale Mwanza Mbowe alisema wazi kwamba yeye hatamsema vibaya Mama Samiah. Ile kauli ilisababisha CCM kudai Mbowe anampigia kampeni mama Samiah na kuonesha kwamba CHADEMA inamuunga mkono mama Samia, pamoja na dhihaka zote Mbowe akiendelea na hiyo kauli. Leo utasemaje kwamba ilikuwa bahati mbaya?. Mbowe kakiingiza chama kwenye Jambo ambalo chama kingeweza kuepuka.

Pia baada ya hapo Akina Lissu wakapinga maridhiano na CCM ikiwemo na Mimi, Mbowe akashupaza shingo na kudai ameweka taifa mbele kuliko chama. Sasa leo utadai ni bahati mbaya au makosa ya kibinadamu?. Yani mtu anashauriwa hataki, halafu Leo analeta stori za kujuta wakati amekiingiza chama kwenye shida?.

Msimamo wangu ni kwamba pamoja na Mbowe kujuta, aachie madaraka kuonesha kweli anajutia.
 
Kumbe unakiri ule ulikuwa uwanja wa vita, ajabu unataka Mbowe aende kwenye uwanja wa vita bila silaha, wake up dude!.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app

Nikuulize swali, Mbowe ameenda kwenye vita gani? Na Silaha gani?. Kwa hivyo kujirahisisha kwa Samiah ndio Silaha. Wewe ndio uamke usingizini.

Mbowe must go, maana approach yake imeshindwa ameleta dharau kwa CHADEMA. Yani kukiri kuzidiwa maarifa na mama Samiah ni upuuzi mkubwa.
 
Sijakuwekea maneno, nimeupanua ubongo wako, umezoea kufikiria ndani ya box kuamini njia moja tu kisiasa ndio sahihi miaka yote!.

Sio tu timu ikikosa mafanikio kocha huondoka, hata na wachezaji nao wapo wanaoondoshwa, think outside the box.

Ukishapata jibu mtuambie jina la huyo malaika wenu atakayekuja kuiongoza Chadema asikosee...



Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app


Wewe ndio unatakiwa kupanua ubongo. Nimeeleza kwenye mada yangu, issue sio kukosa, issue ni kuendelea na makosa hayo kila siku. Mbowe amekifanya chama kuwa bila msimamo. Leo maridhiano, kesho maandamano, kesho kutwa maridhiano etc. Sasa huu ni ujinga, CCM wanachukia advantage, ni heri kuwa na msimamo mmoja mpaka mwisho.

Sio unashupaza shingo hutaki kuambiwa, siku Samiah amekuingiza mjini inaanza kulia najuta kumwamini Samiah, that is a shame. Mbowe astaafu, tujenge image mpya ya chama.
 
Sijakuwekea maneno, nimeupanua ubongo wako, umezoea kufikiria ndani ya box kuamini njia moja tu kisiasa ndio sahihi miaka yote!.

Sio tu timu ikikosa mafanikio kocha huondoka, hata na wachezaji nao wapo wanaoondoshwa, think outside the box.

Ukishapata jibu mtuambie jina la huyo malaika wenu atakayekuja kuiongoza Chadema asikosee...



Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app

Napropose Lissu Mwenyekiti na Heche Katibu Mkuu, Makamu Mwenyekiti tumpe Catherine Ruge.
 
Habari Wana JF. Kwanza nielezee masikitiko yangu kwa kauli ya Jana ya Mwenyekiti wa CHADEMA Mheshimiwa Mbowe kwamba anajuta kumwamini Rais Samiah.

Mheshimiwa Mbowe alipigiwa kelele sana kuhusu kuingia maridhiano na CCM hakusikia kabisa. Nakumbuka kwenye mkutano wa CHADEMA Mwanza, tarehe 21/1/2023, Mbowe alidai hatamsema vibaya mama Samiah , Leo inakuwaje ndio anashtuka muda umeenda? na kudai anajuta kumwamini Mama Samiah?.

Pia nakumbuka kwenye mkutano wake na diaspora wa Marekani tarehe 11/12/2022, Mh Mbowe alidai kuwa hatarudi nyuma kwenye mazungumzo, na kudai anaweka maslahi ya nchi mbele na sio CHADEMA, Leo inakuwaje anajutia kumwamini Rais Samiah.

Mh. Mbowe anajua yaliyotokea Zanzibar na alitakiwa kuchukua Kama fundisho. Kwamba pamoja na maridhiano, CCM wakaiweka CUF ya maalim kwenye mtego mpaka leo imekuwa historia. Mwishoni maalim ikabidi akimbilie ACT baada ya Msajili kutumika kumfustrate. Hii ilitosha kumfundisha Mbowe aache kujikomba kwa Mh Samiah na CCM yake. Ilitakiwa ajifunze kutoka kwa Maalim. Kwamba pamoja na Maalim kujishusha na kukubali maridhiano , CCM wakakivunja chama chake Cha CUF na pia kumfanyia unyama 2020.

Sasa Kutokana na kauli ya Mh Mbowe ya Jana, Naomba nishauri yafuatayo:

1. Kwakuwa Mh. Mbowe alilazimisha Maridhiano na yeye kujiweka mbele Kama kiongozi wa maridhiano, basi kwa kuwa maridhiano yameshindikana, nashauri aachie ngazi mara moja. Maana kashindwa kutimiza hayo maridhiano aliyo lazimisha.

2. Kwa kuwa Mh. Mbowe alidharau sauti za wanachama wa CHADEMA kumkataza kuendelea na hayo maridhiano, na kwa kuwa hakufanikiwa na hayo maridhiano aombe Radhi wanachama kwa maamuzi hayo ambayo hayakufanikiwa na yaliyoiweka CHADEMA rehani.

3. Kwa kuwa Mh. Mbowe ameshindwa kutimiza approach yake ya diplomacy , itakuwa ujinga akiendelea kuongoza approach nyingine dhidi ya serikali au CCM maana haaminiki Tena. Hivyo ajiuzulu kupisha uchaguzi wa mwenyekiti mpya ambaye atatumia approach nyingine kabisa kuliko ya Mbowe.

4. Kwamba, kwakuwa imeonekana maridhiano sio njia sahihi ya kutatua malalamiko ya CHADEMA kutokana na kiburi Cha CCM na serikali yake, nashauri CHADEMA waachane na approach ya maridhiano watafute approach nyingine.

5. Kwa kuwa inaonekana maoni ya CHADEMA kwenye mswada ya sheria yamekataliwa na Kamati ya kudumu ya bunge ya Katiba na Sheria, nashauri CHADEMA watangaze rasmi kutoshiriki chaguzi za serikali za mitaa na uchaguzi mkuu.

Naomba kuwasilisha.
Wewe ni Nani kwenye hii Taasisi!
Kwaki kutomuamini ni dhambi!
Fuatilia yanayiendelea Amerika na kwengineko acha uchawa.
 
Umeshasahau misukosuko mliyopitia miaka kadhaa nyuma na jinsi Mbowe alivyosimama kidete kuiokoa Chadema dhidi ya anguko baya kabisa la kutengenezwa na watawala au unajitoa ufahamu ?

Hata mkimtoa mtampa nani kwa sasa huo Uenyekiti?

JokaKuu Nguruvi3 Pascal Mayalla zitto junior

Nani hatambui mchango wa Mbowe? Nani hatambui Mbowe alivyojitoa kwaajili ya chama?. Ninachosema approach anayotumia haitatufikisha popote, CCM watakuwa wanatuchezea kila siku.

Halafu unaweza kufanya mengi mazuri ukayaharibu yote kwa siku moja. Pia unaweza kuwa hero uakaishia zero. Kasome hadithi ya Mugabe alivyoishia Kama zero. You can do good but spoil all the good in one day.

Mbowe kafanya mazuri mengi sana, ila ili akumbukwe Kama kiongozi Bora ajiuzulu kwa kukiingiza chama kwenye mtego wa CCM , na mwishowe kukiri CCM walimrubuni. Hatuwezi kuendelea na kiongozi anaendelea kurubuniwa na CCM kila siku. Akae pembeni.
 
Sasa kama ametambua hilo na kusahihisha, shida iko wapi? Admitting weaknesses/failures is a positive attribute.

Kukubali amekosea sio vibaya, shida ni kwamba wakati anakosea akaonywa ila akakaza shingo na kuwaona akina Lissu ndio wenye shida. Leo anarudi kulalamika amaechezewa na CCM. Sasa anamlalamikia nani?.

Ili kunielewa vizuri, kaangalie video ya mkutano wa Mbowe Marekani kwa diaspora alivyoongea na Leo anavyoongea. CHADEMA haiotaji kiongozi kinyonga never.
 
Suala la kuachiana vijiti sio kesi, lakini tukubaliane hivyo vijiti vya kuachiana kuna taratibu zake, sasa kama wale wanaohusika wako tayari kuendelea kuongozwa na yule msiyemtaka mnakuwa na maana na nia gani? hamjioni kama nyie ndio mnataka kuleta vurugu huko chamani?

Kwa nini hamtaki kuheshimu maamuzi ya wale wanaompigia kura Mbowe? kwanini mnajiona nyie ndio wenye hati miliki ya kuamua nani awe mwenyekiti wa Chadema? kwanini hamtaki kufuata taratibu?

Kama mna mtu wenu mnaamini ni mzuri zaidi ya Mbowe, huwa mnakuwa wapi kumwambia akachukue form ya kugombea, ili nanyi mkamfanyie kampeni apate ushindi dhidi ya Mbowe?

Hapa zisiwepo sababu za uchaguzi huwa sio huru, hizi ni sababu za waliokata tamaa na kile wanachotaka wasio na lakujitetea, huwezi kusema uchaguzi sio huru ikiwa kura hupigwa kwa uwazi, kuhesabiwa kwa uwazi, na matokeo kutangazwa wazi, pasiwepo mjumbe yeyote anayelalamikia zoezi isipokuwa wajumbe nyie wa JF!.

Kama issue ni kukaa sana, wenye uamuzi wa kumuondoa ni wapiga kura wakiona kuna haja ya kufanya hivyo, lakini msitake kulazimisha mawazo yenu na matakwa yenu ndio yawe juu ya wengine, huu ni udikteta, mnaleta vurugu, nyie ni kama vile mnaandaa mapinduzi part 2 ya kina Zitto, Mwigamba, na Kitilla yaliyofeli, sijui kama mnaiona hiyo tafsiri yenu kwa nje!.

- Msijiite wafuasi wa chama cha demokrasia huku mkitaka kumuondoa Mbowe kwa mawazo yenu binafsi.

Chadema ina taratibu zake, ziheshimiwe na kufuatwa, sio kulazimisha mambo kama vile kile ni chama cha barabarani, msikishushie heshima yake, mmekipenda kwa sababu hiyo, na muendelee kuishi hivyo, muda ukifika pelekeni mgombea wenu mfanyieni kampeni ashinde, asiposhinda; mjue hiyo ndio demokrasia, sio kulazimisha mambo yawe vile mtakavyo nje ya taratibu.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app

Mbowe astaafu kwa heshima, asilazimiahe awe Kama mrema au Lipumba. Miaka 22 ni mingi Sana. Ndio maana anafanya makosa ya wazi kabisa.
 
Ndio mkimtafuta huyo malaika wenu sasa muwe na sababu za msingi kumkataa Mbowe, sio kila mmoja anakuja na lake mnasahau Mbowe hakuwa malaika, kama hamumtaki nendeni straight Mbowe ondoka, tena muwe na hayo mabango siku hiyo ya maandamano, sioni sababu kwenu ya kulia lia kila siku kama vile Mbowe ndie anaizuia Chadema kwenda ikulu, mkijitia upofu msizione sababu nyingine.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app

CHADEMA haitaki malaika Bali inataka kiongozi asiyeyumba. Akisema hapana ni hapana. Sio inaitwa ikulu unageuza msimamo haraka.
 
Sijui kwann watu huwa wakali na hawapendi kuukubali huu ukwel.

Sikatai, mbadala wa Mbowe hata mimi naona itachukua muda kumpata ila kwa sasa Freeman hana jipya tena. Ndio yale yale ya Mrema na lipumba yanaenda kumpata wakat angeweza kuacha kwa heshima.

Mbowe hana jipya kwasasa na ameanza kuonekana kama mjanja janja tu..Nothing more

Mbowe amefanya mengi, Sasa ni wakati wakuwaachia vijana aliowatengeneza kushika haramu. Kwa Sasa Hana ushawishi, maana hachelewi kugeuza msimamo.
 
Economist, Chadema ikifuata maoni na mawazo ya aina hii itaangamia. Nilipi kosa la Mbowe kufanya maridhiano? Kwa nini hasilaumiwe Samia na CCM yake walioeshidwa kutekeleza maridhiano badala yake unamlaumu Mbowe, je, ulitaka Mbowe achukue bunduki aingie msituni badala ya kukaa meza moja kutafuta muafaka wa kisiasa?

Tatizo mkuu umesoma mada yangu kwa juu juu bila kuipitia vizuri. Nimesema Mbowe ajiuzulu Kama Mwenyekiti wa CHADEMA. Hoja yangu ipo objective kwenye uongozi na sio Mbowe.

Nasema hivi kwa Sasa tulipofikia, Mbowe ameonesha kutokuwa na msimamo. Alitetewa maridhiano wanachama wa CHADEMA wakapinga ila Mbowe akadai anapamabania nchi, leo anawarudia wenzake waliomkataza na kuwalilia kuwa anajuta muwaamini CCM.

Mbowe Hana msimamo na hivyo kujifanya CHADEMA kiyumbe. Leo maridhiano, kesho maandamano etc. Kama umeamua maridhiano endelea na maridhiano , Kama umeamua confrontational uwe confrontational, sio unakuwa vuguvugu mpaka CCM wanajua jinsi ya kukuhadaa maana wanajua huna msimamo.

Kuhusu CCM nani awalalmikie wakati wanajulikana ni matapeli?. Kwenye madam nimetoa mfano wa maalim seif jinsi walivyomtapeli akaingia kwenye mtego wa CCM na pamoja na kujishusha kwake CCM walimlima marungu 2020. So CCM ni waovu tangiepo.
 
Habari Wana JF. Kwanza nielezee masikitiko yangu kwa kauli ya Jana ya Mwenyekiti wa CHADEMA Mheshimiwa Mbowe kwamba anajuta kumwamini Rais Samiah.

Mheshimiwa Mbowe alipigiwa kelele sana kuhusu kuingia maridhiano na CCM hakusikia kabisa. Nakumbuka kwenye mkutano wa CHADEMA Mwanza, tarehe 21/1/2023, Mbowe alidai hatamsema vibaya mama Samiah , Leo inakuwaje ndio anashtuka muda umeenda? na kudai anajuta kumwamini Mama Samiah?.

Pia nakumbuka kwenye mkutano wake na diaspora wa Marekani tarehe 11/12/2022, Mh Mbowe alidai kuwa hatarudi nyuma kwenye mazungumzo, na kudai anaweka maslahi ya nchi mbele na sio CHADEMA, Leo inakuwaje anajutia kumwamini Rais Samiah.

Mh. Mbowe anajua yaliyotokea Zanzibar na alitakiwa kuchukua Kama fundisho. Kwamba pamoja na maridhiano, CCM wakaiweka CUF ya maalim kwenye mtego mpaka leo imekuwa historia. Mwishoni maalim ikabidi akimbilie ACT baada ya Msajili kutumika kumfustrate. Hii ilitosha kumfundisha Mbowe aache kujikomba kwa Mh Samiah na CCM yake. Ilitakiwa ajifunze kutoka kwa Maalim. Kwamba pamoja na Maalim kujishusha na kukubali maridhiano , CCM wakakivunja chama chake Cha CUF na pia kumfanyia unyama 2020.

Sasa Kutokana na kauli ya Mh Mbowe ya Jana, Naomba nishauri yafuatayo:

1. Kwakuwa Mh. Mbowe alilazimisha Maridhiano na yeye kujiweka mbele Kama kiongozi wa maridhiano, basi kwa kuwa maridhiano yameshindikana, nashauri aachie ngazi mara moja. Maana kashindwa kutimiza hayo maridhiano aliyo lazimisha.

2. Kwa kuwa Mh. Mbowe alidharau sauti za wanachama wa CHADEMA kumkataza kuendelea na hayo maridhiano, na kwa kuwa hakufanikiwa na hayo maridhiano aombe Radhi wanachama kwa maamuzi hayo ambayo hayakufanikiwa na yaliyoiweka CHADEMA rehani.

3. Kwa kuwa Mh. Mbowe ameshindwa kutimiza approach yake ya diplomacy , itakuwa ujinga akiendelea kuongoza approach nyingine dhidi ya serikali au CCM maana haaminiki Tena. Hivyo ajiuzulu kupisha uchaguzi wa mwenyekiti mpya ambaye atatumia approach nyingine kabisa kuliko ya Mbowe.

4. Kwamba, kwakuwa imeonekana maridhiano sio njia sahihi ya kutatua malalamiko ya CHADEMA kutokana na kiburi Cha CCM na serikali yake, nashauri CHADEMA waachane na approach ya maridhiano watafute approach nyingine.

5. Kwa kuwa inaonekana maoni ya CHADEMA kwenye mswada ya sheria yamekataliwa na Kamati ya kudumu ya bunge ya Katiba na Sheria, nashauri CHADEMA watangaze rasmi kutoshiriki chaguzi za serikali za mitaa na uchaguzi mkuu.

Naomba kuwasilisha.

Kiongozi angekuwa Lisu au mwingine yoyote sidhani kama angekubali kwenda ikulu baada ya kutolewa jela na mtu aliyemfunga, kuacha kupigania katiba mpya, kuingia maridhiano yao wawili binafsi, kukubali 150mn binafsi kwa niaba ya kanisa, kutetea maridhiano ya kificho.

Ni wao wawili tu walikuwa wanajua wanaridhiana nini?
 
Hii ndio mindset ya hawa jamaa, wanataka Chadema wasio na silaha wakashindane na CCM yenye silaha physically, na wameikariri hii njia moja miaka yote!.

Swali dogo tu nimewauliza; kama maridhiano hawayataki wao walitaka itumike njia gani mbadala? ajabu hakuna hata mmoja wao aliyenijibu!

Simply wanataka kitu wasichokijua.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app

Acha kujiona unajua zaidi ya wengine, huo ni udhaifu. Halafu usipende kuconclude mambo Kama unavyotaka. Nimetoa sababu kwanini nimesema hivyo. CCM hawaaminika na ndio maana Mbowe ameenda kwenye Maridhiano wamegeuka.

Mbinu ambayo wanaotakiwa kunitumia ni passive Confrontational politics. Siasa za msimamo mkali zisizokuwa na vurugu ndani yake.

Kwa mfano tulikuwa tunapenda vizuri. Tulikataa uchaguzi, tuliwafukuza kina halima, tulikataa Ruzuku, tulikataa kwenda kwenya mabaraza ya kinafiki etc. Hiyo ndio passive Confrontational politics, siku mambo yakienda vibaya tutaendea mbali zaidi.
 
Wewe ni Nani kwenye hii Taasisi!
Kwaki kutomuamini ni dhambi!
Fuatilia yanayiendelea Amerika na kwengineko acha uchawa.

Wewe ni nani wa kuniuliza Hilo swali? Halafu usinipangie Cha kusema.
Huwezi kujua Mimi ni nani ndani ya CHADEMA, ila nikuhakikishie nimekuwa mwanachama wa CHADEMA kabla Mbowe hajawa mwenyekiti wa CHADEMA. Sisi ni wale tutafia CHADEMA.

Halafu Kama wewe ni chawa Baki nao huko mwenyewe. Mimi siyumbishwi na watu Kama wewe wakuja na kupitia. Sisi tunajua CHADEMA imetoka wapi na inaenda wapi. Hivyo punguza ujuaji. Mimi naita koleo ni koleo sio Kijiko kikubwa.
 
Primary target ya ujasusi was Tanzania ilikua katiba mpya!na chadema ilipaswa kuwa sauti hiyo!

Wao wakazimishwa na nusu mkate yaani wakafika bei hii ikaleta hasira kali na kutokuaminika Kwa mbowe Toka Kwa wale jamaa wanaopigania katiba!!

Nadhani plan ya katiba kabla ya uchaguzi imefeli coz mwenyekiti was CCM ame was outsmart wale jamaa wa Dola!Sasa nadhani wata execute plan B:-

1.Uchaguzi 2025 uvurugike mabaka wakachukua Dola!

2.Damage ya kisiasa Kwa mtia Nia was urais mapema ambae no mwenyekiti was ccm,nadhani wamefanikiwa coz hakuna mwananchi was kawaida kabisa anaemkubali kihivyo has Hulu bara tumebaki sisi chawa wa mchongo tukiziimba nyimbo zake Ili kufurahia ugali na teuzi zake!!

Lengo ni kumuingiza mgombea mwingine 2025 na sie huyu !

3.Hii mbaya sana!I have a feeling ni kuwindana Hadi viwanja vya ndege ili apewe mwingine!!

Watumishi wanaomba mungu haha yasitokee!

Hoi inachagizwa na Ile "original plan in and out""!!!

Ngoja tuone!!!

Mbowe kafeli coz hajui no Dola ilishinikiza atolewe mahabusu Kwa kesi ile Ili apiganie katiba Sasa yeye kalamba asali plus nusu mkate!!!
Pia inawezekana no plan ya mbowe kurudisha Imani ya wanachama kwake baada ya kuvurunda,Kwa kuitisha maandamano!!


Ngoja nisubiri!!!
Mbowe kajenga nyumba kali sana
 
Habari Wana JF. Kwanza nielezee masikitiko yangu kwa kauli ya Jana ya Mwenyekiti wa CHADEMA Mheshimiwa Mbowe kwamba anajuta kumwamini Rais Samiah.

Mheshimiwa Mbowe alipigiwa kelele sana kuhusu kuingia maridhiano na CCM hakusikia kabisa. Nakumbuka kwenye mkutano wa CHADEMA Mwanza, tarehe 21/1/2023, Mbowe alidai hatamsema vibaya mama Samiah , Leo inakuwaje ndio anashtuka muda umeenda? na kudai anajuta kumwamini Mama Samiah?.

Pia nakumbuka kwenye mkutano wake na diaspora wa Marekani tarehe 11/12/2022, Mh Mbowe alidai kuwa hatarudi nyuma kwenye mazungumzo, na kudai anaweka maslahi ya nchi mbele na sio CHADEMA, Leo inakuwaje anajutia kumwamini Rais Samiah.

Mh. Mbowe anajua yaliyotokea Zanzibar na alitakiwa kuchukua Kama fundisho. Kwamba pamoja na maridhiano, CCM wakaiweka CUF ya maalim kwenye mtego mpaka leo imekuwa historia. Mwishoni maalim ikabidi akimbilie ACT baada ya Msajili kutumika kumfustrate. Hii ilitosha kumfundisha Mbowe aache kujikomba kwa Mh Samiah na CCM yake. Ilitakiwa ajifunze kutoka kwa Maalim. Kwamba pamoja na Maalim kujishusha na kukubali maridhiano , CCM wakakivunja chama chake Cha CUF na pia kumfanyia unyama 2020.

Sasa Kutokana na kauli ya Mh Mbowe ya Jana, Naomba nishauri yafuatayo:

1. Kwakuwa Mh. Mbowe alilazimisha Maridhiano na yeye kujiweka mbele Kama kiongozi wa maridhiano, basi kwa kuwa maridhiano yameshindikana, nashauri aachie ngazi mara moja. Maana kashindwa kutimiza hayo maridhiano aliyo lazimisha.

2. Kwa kuwa Mh. Mbowe alidharau sauti za wanachama wa CHADEMA kumkataza kuendelea na hayo maridhiano, na kwa kuwa hakufanikiwa na hayo maridhiano aombe Radhi wanachama kwa maamuzi hayo ambayo hayakufanikiwa na yaliyoiweka CHADEMA rehani.

3. Kwa kuwa Mh. Mbowe ameshindwa kutimiza approach yake ya diplomacy , itakuwa ujinga akiendelea kuongoza approach nyingine dhidi ya serikali au CCM maana haaminiki Tena. Hivyo ajiuzulu kupisha uchaguzi wa mwenyekiti mpya ambaye atatumia approach nyingine kabisa kuliko ya Mbowe.

4. Kwamba, kwakuwa imeonekana maridhiano sio njia sahihi ya kutatua malalamiko ya CHADEMA kutokana na kiburi Cha CCM na serikali yake, nashauri CHADEMA waachane na approach ya maridhiano watafute approach nyingine.

5. Kwa kuwa inaonekana maoni ya CHADEMA kwenye mswada ya sheria yamekataliwa na Kamati ya kudumu ya bunge ya Katiba na Sheria, nashauri CHADEMA watangaze rasmi kutoshiriki chaguzi za serikali za mitaa na uchaguzi mkuu.

Naomba kuwasilisha.
Mbowe ni chawa wa CCM, mnajuwa leo...!?
 
Habari Wana JF. Kwanza nielezee masikitiko yangu kwa kauli ya Jana ya Mwenyekiti wa CHADEMA Mheshimiwa Mbowe kwamba anajuta kumwamini Rais Samiah.

Mheshimiwa Mbowe alipigiwa kelele sana kuhusu kuingia maridhiano na CCM hakusikia kabisa. Nakumbuka kwenye mkutano wa CHADEMA Mwanza, tarehe 21/1/2023, Mbowe alidai hatamsema vibaya mama Samiah , Leo inakuwaje ndio anashtuka muda umeenda? na kudai anajuta kumwamini Mama Samiah?.

Pia nakumbuka kwenye mkutano wake na diaspora wa Marekani tarehe 11/12/2022, Mh Mbowe alidai kuwa hatarudi nyuma kwenye mazungumzo, na kudai anaweka maslahi ya nchi mbele na sio CHADEMA, Leo inakuwaje anajutia kumwamini Rais Samiah.

Mh. Mbowe anajua yaliyotokea Zanzibar na alitakiwa kuchukua Kama fundisho. Kwamba pamoja na maridhiano, CCM wakaiweka CUF ya maalim kwenye mtego mpaka leo imekuwa historia. Mwishoni maalim ikabidi akimbilie ACT baada ya Msajili kutumika kumfustrate. Hii ilitosha kumfundisha Mbowe aache kujikomba kwa Mh Samiah na CCM yake. Ilitakiwa ajifunze kutoka kwa Maalim. Kwamba pamoja na Maalim kujishusha na kukubali maridhiano , CCM wakakivunja chama chake Cha CUF na pia kumfanyia unyama 2020.

Sasa Kutokana na kauli ya Mh Mbowe ya Jana, Naomba nishauri yafuatayo:

1. Kwakuwa Mh. Mbowe alilazimisha Maridhiano na yeye kujiweka mbele Kama kiongozi wa maridhiano, basi kwa kuwa maridhiano yameshindikana, nashauri aachie ngazi mara moja. Maana kashindwa kutimiza hayo maridhiano aliyo lazimisha.

2. Kwa kuwa Mh. Mbowe alidharau sauti za wanachama wa CHADEMA kumkataza kuendelea na hayo maridhiano, na kwa kuwa hakufanikiwa na hayo maridhiano aombe Radhi wanachama kwa maamuzi hayo ambayo hayakufanikiwa na yaliyoiweka CHADEMA rehani.

3. Kwa kuwa Mh. Mbowe ameshindwa kutimiza approach yake ya diplomacy , itakuwa ujinga akiendelea kuongoza approach nyingine dhidi ya serikali au CCM maana haaminiki Tena. Hivyo ajiuzulu kupisha uchaguzi wa mwenyekiti mpya ambaye atatumia approach nyingine kabisa kuliko ya Mbowe.

4. Kwamba, kwakuwa imeonekana maridhiano sio njia sahihi ya kutatua malalamiko ya CHADEMA kutokana na kiburi Cha CCM na serikali yake, nashauri CHADEMA waachane na approach ya maridhiano watafute approach nyingine.

5. Kwa kuwa inaonekana maoni ya CHADEMA kwenye mswada ya sheria yamekataliwa na Kamati ya kudumu ya bunge ya Katiba na Sheria, nashauri CHADEMA watangaze rasmi kutoshiriki chaguzi za serikali za mitaa na uchaguzi mkuu.

Naomba kuwasilisha.
Kama kuna kitu kinajuwa kuwapotezea Watz muda na kuwatia umaskini, ujinga na kuhasimiana ni VYAMA VYA SIASA.
 
Chama ni chama mbowe alichorithishwa na mkwe wake,.kwa hiyo ni mali yake binafsi na siyo mali ya chama.kama unataka wewe ondoka muachie mbowe kitega uchumi chake.
Jinga wewe, Mwinyi (baba) alikuwa Rais Zanzibar na baadae Jamuhuri ya Muungano, kwanini hukumzuia mtoto awe Rais? Sijuhi wewe jamaa ni punguani
 
Back
Top Bottom