Pre GE2025 Ushauri: Mbowe ajiuzulu mara moja kama Mwenyekiti wa CHADEMA

Pre GE2025 Ushauri: Mbowe ajiuzulu mara moja kama Mwenyekiti wa CHADEMA

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Ni chama kipi kisichokuwa na changamoto? Vyama vipo vingi na pia kuna ruhusa ya kuanzisha vingine vipya. Kwa yeyote anaeona Chadema ya Mbowe ina changamoto ni ruksa kutimukia chamaa kisicho na changamoto au kuanzisha chama chake.

Kwa wenye weredi kipindi hiki cha karibu na uchaguzi ni kukaa pamoja na kutatua changamoto kwa pamoja kuliko kuhubiri mifarakano yenye lango la kukigawa chama.

Moja ya njia za kutatua mgogoro ni Kuondoa uongozi mbovu. Ndio maana ninamuomba Mbowe astaafu.
 
Wewe una lako jambo, Mbowe kama mwenyekiti alikuwa na haki ya kuwa na misimamo kama hiyo uliyoisema akiamini kukivusha chama kwa njia ya maridhiano. Aliyeshidwa kutekeleza hayo maridhiano siyo Mbowe wala Chadema hisipokuwa Samia kwa shinikizo la waafidhina ndani ya CCM. Kwanini Mbowe aachie ngazi kwa kosa ambalo hakulitenda yeye? Kama kuna sababu nyingine zielezeni lakini si hizi za maridhiano.

Ni muda mrefu tangu vyama vingi vianzishwe na njia nyingi zimekuwa zikitumika kukabiliana na wizi, sheria kandamizi za uchaguzi na mambo mengine. Njia zote hizi kwa muda wote hazijawai kuzaa matunda. Iweje hii ya maridhiano ndilo liwe kosa la kumfanya aachie ngazi?

Sina Jambo lolote. Msimamo wangu ni kwamba Mbowe kajuta kumwamini Samiah, na alionywa Sana. Fuatilia hotuba ya Diaspora aliyoitoa. Sasa leo atasemaje kwamba aliingizwa kingi na Samiah?. Huo ni ujinga. Unalazimisha Jambo ukifeli inaanza kulalamika.
 
Usiweke imani yako kwa mwanasiasa kwa sababu hoja zozote unazokuwa unazisikia huwa scripted...

Huwa wanaongea au kutenda vitu fulani wakiwa na lengo fulani kwa manufaa yao kisiasa...

Hizo kauli za Mbowe zina "huenda" nyingi mno...
 
Unachekesha, kwamba amekiri kuzidiwa maarifa na mama Samia? Ni lini Chadema ilishaizidi maarifa CCM? Kosa lake ni kusema ukweli au kukaidi lile mlilolitaka nyie? Mara ngapi nguvu imetumika kuikabili CCM ikashindikana? Leo hili la maridhiano imekuwa jinai

Wewe ndio unachekesha. Unaniuliza ni lini CHADEMA imeizidi CCM akili halafu unataka Mbowe aendelee kuwa Mwenyekiti. Yani unakubali CHADEMA haijawahi kuizidi CCM akili na unataka huyo kiongozi aliyezidiwa akili Miaka yote na CCM aendelee kuwa Mwenyekiti.

Ndio maana nikasema kwasababu Mbowe kaonekana kuzidiwa akili na CCM muda wote, aakae pembeni tafadhali.
 
Kukosea hata kama alionywa na kina Lissu ndiyo siasa yenyewe, sasa kajisahihisha baada ya kuona yaliyotokea. Chama kaaeni pamoja na kuandaa mikakati mipya.

Ukiniambia una mahaba na Lissu awe m/kiti, Heche Katibu na Ruge makamo nitakuelewa maana hiyo ndiyo demokrasia. Lakini fuateni utaratibu ndani ya chama na kama wengi watakuwa na mtizamo kama wako sawa, lakini kama wengi bado wako kwa Mbowe basi sanduku la kura litaongea.

Tatizo lako unakwepa ukweli. Akina Lissu walimuonya mapema akawakatalia na hata kuwananga kwenye mkutano wake wa Diaspora, Leo baada ya kufeli ndio anakiri aliingizwa mtegoni. Yani angekubali ule ushauri kipindi kile Cha Mwanzo hakuna ambaye angemlaumu, ila kitendo Cha kukataa ushauri na Kuja kufeli baadae kina discredit Mbowe mazima.

Angesikiliza ushauri wa akina Lissu asingekuwa anatulilia kijinga. Ni kwamba Mbowe alikataa ushauri, Sasa Leo anamlilia nani? Aende huko.
 
Aisee! Watu walimtaka Mbowe aweke wazi anaongea nn ktk maridhiano, lkn yeye akafanya siri. Sasa inamtafuna.

Kwa maoni yangu Mbowe akubali kuwajibikq kwasabb plan yake hii imefeli.

Na hii ndio point yangu. Unajifanya busy na Jambo kana kwamba ipo serious, ukiulizwa unafanya Siri. Ikija kufeli unaanza kulilia watu. Mbowe must go.
 
Habari Wana JF.

Kwanza nielezee masikitiko yangu kwa kauli ya Jana ya Mwenyekiti wa CHADEMA Mheshimiwa Mbowe kwamba anajuta kumwamini Rais Samia

Mheshimiwa Mbowe alipigiwa kelele sana kuhusu kuingia maridhiano na CCM hakusikia kabisa. Nakumbuka kwenye mkutano wa CHADEMA Mwanza, tarehe 21/1/2023, Mbowe alidai hatamsema vibaya mama Samia. Leo inakuwaje ndio anashtuka muda umeenda? na kudai anajuta kumwamini Mama Samiah?.

Pia nakumbuka kwenye mkutano wake na diaspora wa Marekani tarehe 11/12/2022, Mh Mbowe alidai kuwa hatarudi nyuma kwenye mazungumzo, na kudai anaweka maslahi ya nchi mbele na sio CHADEMA, Leo inakuwaje anajutia kumwamini Rais Samiah.

Mbowe anajua yaliyotokea Zanzibar na alitakiwa kuchukua Kama fundisho. Kwamba pamoja na maridhiano, CCM wakaiweka CUF ya maalim kwenye mtego mpaka leo imekuwa historia. Mwishoni maalim ikabidi akimbilie ACT baada ya Msajili kutumika kumfustrate. Hii ilitosha kumfundisha Mbowe aache kujikomba kwa Mh Samiah na CCM yake. Ilitakiwa ajifunze kutoka kwa Maalim. Kwamba pamoja na Maalim kujishusha na kukubali maridhiano , CCM wakakivunja chama chake Cha CUF na pia kumfanyia unyama 2020.

Sasa Kutokana na kauli ya Mbowe ya Jana, Naomba nishauri yafuatayo:

1. Kwakuwa Mbowe alilazimisha Maridhiano na yeye kujiweka mbele Kama kiongozi wa maridhiano, basi kwa kuwa maridhiano yameshindikana, nashauri aachie ngazi mara moja. Maana kashindwa kutimiza hayo maridhiano aliyo lazimisha.

2. Kwa kuwa Mh. Mbowe alidharau sauti za wanachama wa CHADEMA kumkataza kuendelea na hayo maridhiano, na kwa kuwa hakufanikiwa na hayo maridhiano aombe Radhi wanachama kwa maamuzi hayo ambayo hayakufanikiwa na yaliyoiweka CHADEMA rehani.

3. Kwa kuwa Mh. Mbowe ameshindwa kutimiza approach yake ya diplomacy , itakuwa ujinga akiendelea kuongoza approach nyingine dhidi ya serikali au CCM maana haaminiki Tena. Hivyo ajiuzulu kupisha uchaguzi wa mwenyekiti mpya ambaye atatumia approach nyingine kabisa kuliko ya Mbowe.

4. Kwamba, kwakuwa imeonekana maridhiano sio njia sahihi ya kutatua malalamiko ya CHADEMA kutokana na kiburi Cha CCM na serikali yake, nashauri CHADEMA waachane na approach ya maridhiano watafute approach nyingine.

5. Kwa kuwa inaonekana maoni ya CHADEMA kwenye mswada ya sheria yamekataliwa na Kamati ya kudumu ya bunge ya Katiba na Sheria, nashauri CHADEMA watangaze rasmi kutoshiriki chaguzi za serikali za mitaa na uchaguzi mkuu.

Naomba kuwasilisha.
Una hoja usikilizwe
 
Aisee! Watu walimtaka Mbowe aweke wazi anaongea nn ktk maridhiano, lkn yeye akafanya siri. Sasa inamtafuna.

Kwa maoni yangu Mbowe akubali kuwajibikq kwasabb plan yake hii imefeli.
Nadhani kuweka siri ilikuwa ni sharti la maridhiano. Hakuna Reconciliation inaanz ana uwazi kwa sababu kuna mambo mazito yanaongelewa humo.
 
Kwani umelazimishwa kuwa mwanachama wa CHADEMA? Anzisha chama, kikuze upate uzoefu wa vyama vya siasa kisha uje na hizi kelele za Mbowe jiuzulu.

CCM kazi yao ni kumtoa Mbowe kwenye uwenyekiti wa CHADEMA miaka yote. Mbowe mlimuweka jela muda mrefu tu, kwanini hamkummaliza huko huko?

Mbona hamsemi Lipumba ajiuzulu au Hasim Lungwe ajiuzulu? Kuna vyama tangu vimesajiriwa na msajiri wa vyama havijawahi kufanya mkutano au jumuiko lolote, na viongozi ni wale wale lakini sijawahi kusikia mkiwataka wajiuzulu, kwanini iwe ni Mbowe kila siku?

IFUTENI CHADEMA Kama inawakera sana.

Naona umerukia juu bila kusoma nilichokiandika. Kasome Historia yangu, sijawahi kuwa mwanacc na sitawahi. Nachokushauri Usipende kuzima mawazo ya watu kisa wanamkosoa Mbowe. Huyo Mbowe alituaminisha kwenye mkutano wa Diaspora marekani kwamba atahakikisha maridhiano yanafanikiwa na akawapinga waliokuwa wanamkataza kuhusu hayo maridhiano na hata alipoulizwa wanajadili Nini akadai ni Siri. Leo inakuwaje Tena anarudi kwa wanachama na kulia ametapeliwa?

Nyie endeleeni kumlamba miguu Mbowe mkidhanu mnamsaidia, ngoja akipeleke chama shimoni ndio mtaelewa. Amekifanya chama kisiwe na msimamo. Leo maridhiano, kesho maandamano, keshokutwa maridhiano etc. Tuwe na msimamo Kama chama la sivyo tutakuwa predictable kwa CCM kama Sasa hivi mama kashapata alichokitaka.
 
Usiweke imani yako kwa mwanasiasa kwa sababu hoja zozote unazokuwa unazisikia huwa scripted...

Huwa wanaongea au kutenda vitu fulani wakiwa na lengo fulani kwa manufaa yao kisiasa...

Hizo kauli za Mbowe zina "huenda" nyingi mno...

Sijawahi kuweka imani kwa kiongozi Bali imani yangu ipo kwenye Chama Cha CHADEMA
 
Huu ndio wakati wa Mbowe kujenga heshima yake isije kupotea Kama akina Mrema na Lipumba. Astaafu kwa heshima. Pia ni wakati wa CHADEMA kuleta fresh minds na fresh approach ya kuikabili CCM. Ila tukiendelea kuleta ujinga mwisho hautakuwa mzuri.
 
Huu ndio wakati wa Mbowe kujenga heshima yake isije kupotea Kama akina Mrema na Lipumba. Astaafu kwa heshima. Pia ni wakati wa CHADEMA kuleta fresh minds na fresh approach ya kuikabili CCM. Ila tukiendelea kuleta ujinga mwisho hautakuwa mzuri.
acha upotoshaji yaani chadema kuna fresh mind 🤣 tsaaatsaahhhaaa....🐒
 
Sijawahi kuweka imani kwa kiongozi Bali imani yangu ipo kwenye Chama Cha CHADEMA
kumbe ndio maana una imani haba, potofu na mtazamo hasi sana kwa kila jambo iwe limefanywa chadema au CCM? 🐒
 
Naona umerukia juu bila kusoma nilichokiandika. Kasome Historia yangu, sijawahi kuwa mwanacc na sitawahi. Nachokushauri Usipende kuzima mawazo ya watu kisa wanamkosoa Mbowe. Huyo Mbowe alituaminisha kwenye mkutano wa Diaspora marekani kwamba atahakikisha maridhiano yanafanikiwa na akawapinga waliokuwa wanamkataza kuhusu hayo maridhiano na hata alipoulizwa wanajadili Nini akadai ni Siri. Leo inakuwaje Tena anarudi kwa wanachama na kulia ametapeliwa?

Nyie endeleeni kumlamba miguu Mbowe mkidhanu mnamsaidia, ngoja akipeleke chama shimoni ndio mtaelewa. Amekifanya chama kisiwe na msimamo. Leo maridhiano, kesho maandamano, keshokutwa maridhiano etc. Tuwe na msimamo Kama chama la sivyo tutakuwa predictable kwa CCM kama Sasa hivi mama kashapata alichokitaka.
unavyomlamba miguu Lusu atakupeleka wap, nothing new at all 🐒
 
Moja ya njia za kutatua mgogoro ni Kuondoa uongozi mbovu. Ndio maana ninamuomba Mbowe astaafu.
mawazo yako ni mazuri na huru, lakini hayatekelezeki kutokana na historia yako binafsi ya nyuma na historia ya unaowalamba miguu eti ndio watake over chadema 🐒

never ever 🐒
 
Huu ndio wakati wa Mbowe kujenga heshima yake isije kupotea Kama akina Mrema na Lipumba. Astaafu kwa heshima. Pia ni wakati wa CHADEMA kuleta fresh minds na fresh approach ya kuikabili CCM. Ila tukiendelea kuleta ujinga mwisho hautakuwa mzuri.

1. Ikumbukwe kina Putin, Medvedev na sasa Trump (yuko njia moja) waliwahi kushika hatamu wakatoka na baadaye kurudi.

2. Mtu unaweza ukatoka ukarudi ukipenda ukiwa fresh na mawazo mapya. Ndiyo maana kuna likizo, rest and recuperation, sabbatical leave, nk.

3. Kukaa kiti kile kile muda mrefu inaweza kumpa mtu chronic fatigue na bila kujitambua akabweteka.

4. Leo chadema ina chawa na vijana wa hovyo kama wale wengine.

5. Hapo #4 hata nidhamu na heshima imekuwa changamoto.

6. Hapo #5 si ajabu illiterates na hata vijiweni na mitandaoni kuwakuta wanamzodoa Shivji, Nyerere, Mandela, Tutu, Lissu nk kiboya boya, kwa uchawa wao tu bila kujali jitihada, michango au mafanikio ya watu kama hao duniani, kwa jina la chama.

7. Kina Nanye Go na wenzao wengi ni mfano wa watu hao ambao bila ya uhalali wowote, si nadra kuwaona na kujinadi kwa kudhani wao ni wanachama zaidi kuliko wengine, wakiwaitisha hata kama vipi kuondoka isipokuwa wao!

8. Kwamba hapo #7, vijana wa hovyo hawa, chama kimeshindwa hata kuwakemea hadharani? Ukiwa ni mwendelezo wa mapungufu ya yasiyo na afya ya yatokanayo na haya tunayoyaoigia kelele Kila leo kwa maslahi ya chama:

"Mbowe, Lissu wafundeni wafuasi Falsafa ya Chama"

9. Hapo #8, ni hali isiyoweza kuwavutia wenye kujitambua au akili zao chamani. Kwa hakika ni ujasiri wa kutokuwa tayari kuwasusia fisi bucha kuendelea kukomaa nao.

10. Hatuwezi kuendekeza ujinga, wajinga au kuwAendekeza watu wasiojua wanataka au hawataki nini kwenye mapambano yasiyohitaji ajizi kuwatia CCM madarakani.

11. Wanasema mjini kwa mwendo huu hatuwezi kutoboa!

12. Siyo siri, tunahitaji mwanzo mpya wa mawazo. Tulipo tumegonga mwamba.

13. Waungwana wanasema, "retreat is no surrender."
 
Kwani umelazimishwa kuwa mwanachama wa CHADEMA? Anzisha chama, kikuze upate uzoefu wa vyama vya siasa kisha uje na hizi kelele za Mbowe jiuzulu.

CCM kazi yao ni kumtoa Mbowe kwenye uwenyekiti wa CHADEMA miaka yote. Mbowe mlimuweka jela muda mrefu tu, kwanini hamkummaliza huko huko?

Mbona hamsemi Lipumba ajiuzulu au Hasim Lungwe ajiuzulu? Kuna vyama tangu vimesajiriwa na msajiri wa vyama havijawahi kufanya mkutano au jumuiko lolote, na viongozi ni wale wale lakini sijawahi kusikia mkiwataka wajiuzulu, kwanini iwe ni Mbowe kila siku?

IFUTENI CHADEMA Kama inawakera sana.

Nilipanga kukupuuza lakini nikadhani sitakuwa nimekutendea haki:

1. Kwamba "umelazimiswa kuwapo chamani?!" Maneno magumu haya kutoka kwa mwanachama mmoja kwenda kwa mwingine.

2. Kwani wewe nani? Au wewe ndiye uliyelazimishwa kuwapo?

3. Kwani wewe una haki zaidi kuliko nani?

4. Au ni busara zako tu ndugu kwenda likizo bila taarifa au bila ya weye kujua?

5. Hao CCM mtawalaumu sana kama dobi tu, wakati kaniki ni rangi yake. Wengine wakisema mtamaliza bucha zote, nyama ni ile ile.

6. Tuwaseme Lipumba, Lungwe, au wengine unsowataja, kwani hao wanatuhusu sisi nini?

7. Hapo #6 tunawasema na tutaendelea kuwasema nyote kwa muktadha huu:

Tutambuane: Wenye ujasiri au sababu za kuikabili CCM

8. Kulikoni kututaka kumsema awaye yote kwa muktadha wako? Kwa muktadha wako si unamsema mwenyewe ndugu?

9. Hapo #7 ni nia yetu ya dhati kumfurusha CCM madarakani. Tunamfurusha huyo na majasiri na waliodhamiria kwenye hilo.

10. Hapo #7 tunajua mpo mlio CCM bila ya wenyewe kujitambua kwa maana bila mnadhani CCM ni rangi na siasa ni ushabiki tu kama wa mpira.

11. Hapo #10, wapo walio CCM hadi viongozi upinzani bila ya wao kujitambua. Hili halijali hata nyadhifa walizo nazo.

12. Hapo #11, misahafu inasema, "si wote waniitao bwana bwana, wataurithi ufalme wa mbinguni."
 
Tatizo unataka kunilazimisha kuukataa ukweli. Naomba nikuelimishe kidogo tu, mikutano ya siasa ni haki ya kila raia, haikutakiwa maridhiano kujirudisha Bali kauli ya kisiasa tu kutoka kwa Rais.

Naomba nikupe ushahidi wa mambo mawili kwamba Mbowe alituhakikishia kwamba mambo yataenda vizuri. Kwa mfano Kwenye mkutano wa kwanza wa CHADEMA 2022, pale Mwanza Mbowe alisema wazi kwamba yeye hatamsema vibaya Mama Samiah. Ile kauli ilisababisha CCM kudai Mbowe anampigia kampeni mama Samiah na kuonesha kwamba CHADEMA inamuunga mkono mama Samia, pamoja na dhihaka zote Mbowe akiendelea na hiyo kauli. Leo utasemaje kwamba ilikuwa bahati mbaya?. Mbowe kakiingiza chama kwenye Jambo ambalo chama kingeweza kuepuka.

Pia baada ya hapo Akina Lissu wakapinga maridhiano na CCM ikiwemo na Mimi, Mbowe akashupaza shingo na kudai ameweka taifa mbele kuliko chama. Sasa leo utadai ni bahati mbaya au makosa ya kibinadamu?. Yani mtu anashauriwa hataki, halafu Leo analeta stori za kujuta wakati amekiingiza chama kwenye shida?.

Msimamo wangu ni kwamba pamoja na Mbowe kujuta, aachie madaraka kuonesha kweli anajutia.
Hauna hoja nakwambia ukweli, ndio maana nimekuuliza maswali madogo umeshindwa kujibu.

Hiyo haki ya kila raia kwanini hamkupewa wakati ule wa Magufuli na mkanyamaza? au kwa Magufuli haikuwa haki ya raia!

- Kwanini hiyo "haki ya raia na kauli ya Rais" vikaja baada ya maridhiano?

Nakwambia tena, hauna hoja, kwa hiki ulichoandika hapa umekurupuka.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
1. Kama kesi umetoa kwenye maneno yangu umeninukuu sivyo. Hakuna popote nimesema hayo!

2. Kama kutofautiana kimawazo ni tatizo kwako si tatizo kwetu. Tatizo ni misimamo, imani na falsafa kuparaganyika.

3. Kwenda sawa ni jambo la msingi. Kama ni nia yako kujadili tukubaliane kwenda na hoja moja moja. Kumbuka nilijibu na kuuliza tokea kwenye lukuki uliyokuwa umeandika.

4. Kuondoka ni jambo la afya. Hakuna wa kukaa milele, kumtaka au kutokumtaka Hilo ni jambo la kidemokrasia na kiutendaji.

5. #4 ukikiuka misingi tutakosa uvumilivu.

6. Kukivuruga chama ni kukiuka haki za wengine. Kuziita hoja za wengine wenye mawazo tofauti kupiga kelele ni mfano wa vurugu hizo za wazi.

7. Umoja ni nguvu hapo #6 sijui ni harakati zipi za chama zitafanikiwa kwenye utengano.

8. Hapo #3 yapo maoni ya wazi ya namna ya kuendelea mbele. Uchaguzi ni wako.

9. Ukipenda angalia mdau hapa na umuhimu wa imani thabiti:

"Imani ni kuwa na uhakika."

10. Bila kusahau, hakuna popote nimesema demokrasia ni kile tu tunachosema sisi, labda wewe kama unadhani demokrasia ni kile tu mnachosema ninyi.
Nimekwambia "kesi" nimetumia kama msemo, soma uelewe.

Habari ha kutofautiana mawazo kwangu sio tatizo, nachotaka taratibu zifuatwe.

Niko simple sana, sioni sababu ya kubishana, tatizo hunisomi vizuri unielewe, unaonekana unakimbilia kujibu tu.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom