USHAURI WA VIFAA VINAVYOHITAJIKA
Vifaa vinavyohitajika kwa kuanzia ni Pressure Washer hii bei yake inategemeana na ukubwa wa mashine yenyewe lakini niliwahi kuona moja Jengo la NHC posta Bei ikiwa ni laki sita kama miaka mitatu nyuma.
Kifaa kingine ni Vacuum hiki ni kwaajili ya kuvuta uchafu ndani nayo bei yake inategemea. Tatu MAJI unafikiria kazi au biashara hii basi ufikirie maji ya uhakika kama hakuna maji ya Dawasco basi kwa Dar kuna wale wanaouza kwenye Makenta.
Eneo ambapo biashara hii utaifanya hapa bei inategemea na eneo na mwenye eneo. Lakini pia kingine ni Sabuni maalumu za kuoshea magari hizi sifahamu wapo zinapatikana na bei zake sifahamu.
Vijana wa kufanya nao kazi ambao watakuwa wanaosha malipo mtakubaliana
Vitambaa vya kuoshea na kufutia magari
Polish na Airfresh
Baada ya hapo bei nadhani zinajulikana japokuwa zinatofautiana sehemu na sehemu lakini bei nayofahamu mimi ni Shilingi Elfu 10 kwa gari ndogo hizi Sedan, SUV hatchback nk.
Mengi nadhani wapo wanaoweza kuongezea kila la heri katika kulifanikisha hili