Ushauri: Nataka kuacha kula wanga kwa mwaka mzima

Ushauri: Nataka kuacha kula wanga kwa mwaka mzima

Una Kilo ngapi Kwanza?
Acha Hizo,Mi nina zaidi ya miaka 40,Ninakula Vyote wali,Kuku,Samaki,Ugali,Dagaa,
Nilikuwa Nina Kilo 74kg Mwaka jana,Leo Nina 66kg!
Fanya Mazoezi tuu Kaka,
Mi nafanya Kukumbia tuu na Kunywa Maji Mengi!
Cha Msingi Punguza Kidogo wanga Ila Usiache Mkuu Mimi Siachi Ng’oo nakuka wanga Kama Kawa na Nimepungua 8kg for One year.
Kimbia 5km daily, 3/4Pwr week.
Nna kilo 75, na uzito huu sijazidi wala kupungua kwa miaka karibia 3 sasa.
 
Vyakula vya wanga ndio source ya energy kwenye mwili wako .

How are u going to survive without carbs?
Mi sili wanga napata nguvu kutoka kwenye vyakula vya mafuta kama nyama ,mayai ,maziwa na mazoezini walaji wa wanga nawashinda
 
Asije kuwa kama mtoto wa willy smith baada ya kuamua kuwa vegetarian akapata utapi wa mlo mpala wazazi kuingilia kati kumuokoa
Vegetarian sio mfumo sahihi unakosa virutubisho vingi hasa protein
 
Nani kakukaririsha hayo matango Pori mkuu? Kwa hiyo Kwa uelewa wako uadhani sukari haihitajiki mwilini?
Mwili unazalisha sukari wenyewe inayotoshekeza mahitaji ya mwili, mimi sili sukari kabisa
 
Haya niambie ni chakula gani hicho?
Mimi si wa kwanza kuacha kula wanga. Na nimekuita hapa unishauri. Kama unaona nakosea unasema nipunguze. Sio kuleta kashfa mkuu. Tuheshimiane.
Mi niko na wewe siumwi lakini sili wanga, sijasubiri nipate kisukari ndio nibague vyakula hata profesa janabi wa jk cardiac institute hali wanga na anashauri watu waache
 
Kuna huyu jamaa wa apple aliamua kuishi maisha yake yote akiwa anakula matunda tu, alikufa.

Ishu ni kwamba kila aina ya kirutubisho mwili unakihitaji so kuamua kustick na aina fulani tu ya virutubisho hapo ni kujiandalia kifo.
Kama alikula matunda tu hakua sahihi sababu hayaleti enegi yoyote lakini kuacha wanga ni idea nzuri sababu kazi ya wanga ni kuleta energy ambayo utaipata kwenye mafuta
 
Huwezi pungua kupitia kuacha kula peke yake.

Naona wadau wengi wanasema wameacha wanga na mwili umepungua.

Mwili unapungua kwa mawili ama ufanyiwe operation au ufanye mazoezi. Intentional starvation itabackfire na ulcers na magonjwa mengine.

Halafu mazoezi ni ishu ndogo sana. Yaani wewe unayeruka kichura chura mara tano kila siku you are better off kuliko mimi ninayekesha nacheza PS.
Sio kweli kuna mtumishi mwenzetu ni mtu mzima mama wa 50 hivi kafuata lishe ya dr boaz mkumbo bila kufanya zoezi lolote na amepungua kilo 23
 
Ni kweli asiache sukari kabisa, atumie kidogo kwenye chai na matunda ya sukari ale tu Wala hayana shida, ila soda ndo anaweza kuacha Ili kuzuia kujaza mwili sukari ya ziada angekuwa bonge ndo ningemshauri ale nini na hiyo kufunga Ili apungue ila kutokula wanga kabisa simshauli kuacha ila kula kidogo sana na upande wa vegetables ndo uwe sana pamoja na matunda, niliacha sukari kwa muda wa miaka miwili madhara niliyopata bila kujua mpaka Leo najuta hivyo Kila kitu kwenye mwili ni muhimu ila kwa vipimo sahihi na kuzidi au kupungua ndo kunakoleta matatizo kiafya.
Hahaaa ukiacha sukari unapata madhara? Hii kali nadhani ulikua na shida nyingine mi nimeacha sukari 2018 na afya yangu inazidi kuimarika
 
Hongera sana kwa hatua hiyo, wanga ni JANGA la afya kwa walio wengi, ukijitahidi na ukiwa na dhamira ya kweli HUTAJUTIA uamuzi wako. Wakati unaendelea na mkakati huo tafuta kitabu kinaitwa 'Sayansi ya Mapishi, kimeandikwa na Dr Boaz Mkumbo (MD)

https://www.facebook.com/drboazmkum...apotaka-kujitibu-magonjwa-y/2069771126628541/

Dr boaz amesaidia wengi sana nikiwemo mimi, nimepata elimu kubwa kupitia yeye mwanzo nilikua sijui kua wanga na sukari inaweza kuleta ugumba
 
Mchana ukiwa kazini unewezaje kupata parachichi, mchemsho wa mboga mboga unavichemshia wapi?

Nataka nipungue kidogo, ila mazingira ya kazini najikuta ni wali na chips. Usiku nilikuwa nimeweza kula mboga mboga na matunda na maziwa ila nikaja pata dalili za amoeba, nikajua ni ma mboga.

Nimeacha kula usiku ila bado sijapungua. Mimi sio mnene nina mwili wa kawaida ila naona kama kuna ka kitambi kanakuja kwa mbali.

Kuna rafiki yangu mchana ugali anaokula mkubwa nusu sahani jion bonge la sahani ya wali, cha ajabu hana tumbo hata kidogo haya maisha.

Kufanya diet yataka moyo, najikalia zangu ndani najilia nyanya chungu parachichi na ka ugali kadogo mara shoga yangu anaingia na kitimoto, najisemea moyoni sili, mara naonja moja, mara mbili kweli yataka moyo.
Kitimoto hakina shida mi nakula sana, mfollow dr boaz mkumbo atakusaidia sana
 
Mimi hapa nilikua na uzani wa 126kg na kitambi chote nje nje, ila leo hii mara yangu ya mwisho kupima nilikua na 82kgs, maana kwamba nimepunguza sana, yote hii kwa jitihada za kama miaka mitatu.
Kwanza kabisa aliyekuambia uepuke wanga alikupotosha, ni muhimu sana mwili ukapata carbs, kimsingi ni ujue aina gani za carbs ambazo zinaweza kusaidia, kwa mfano epuka mikate mikate maana yenyewe ni simple carbs, inakua digested upesi na kusababisha njaa mapema.
Kula complex carbs kama magimbi, yanakushibisha na kukupea nguvu wala hutamani chakula haraka.
Kula mboga mboga kwa wingi na pia matango na maji mengi.
Ukiepuka wanga kabisa mwili utakua mnyonge mnyonge na mzembe hadi hata kufanya kazi ndogo unapata shida, hata mazoezi yatakushinda.
Kingine, usitegemee matokeo ya haraka, itachukua muda kabla uone au kuhisi chochote, ila komalia humo humo.
Sio kweli mi nimeacha wanga na nina nguvu za kutosha na mazoezini walaji wa wanga mbona nawazidi msome dr boaz mkumbo amesaidia wengi kwa elimu yake ya kuacha wanga na sukari, by the way kila mtu atachagua mfumo anaoona unafaa sababu miili inatofautiana mimi nikila wanga hata kidogo matokeo yanachukua muda mrefu na baadae nanenepa sana, na baada ya kuacha wanga sipati njaa za mara kwa mara kama mwanzo
 
Kama una mke utasaidiwa kula mzigo,punguza wanga lakini usiache kabisa.
 
Eti tuache kutumia Mafuta ya Karanga,Soya au korosho,halafu sababu hatoii kisa tu ni mbeguu. Hapana aisee...

Tutatumia mafuta ya mimea Kwa wingi ya wanyamaa tutatumia kidogo.
Mafuta ya mbegu mengi hayahimili moto mkali yanazalisha sumu zinazoitwa free radicals na pi mengi yana omega 6 fatty acids nyingi kuliko omega 3,mazuri ni siagi, samli, nazi, olive oil
 
kitakacho kudhuru sio wanga ni mafuta wanayopikia mitaani ni yapi?na yamepikiwa mara ngapi ? na rangi yake ikoje ? wengi watu huumia bila kujijua wanapokula nje.huwezi kuepuka kula chakula cha wanga kula ila punguza. mchele uoshe pia pikia maji mengi kisha ikichemka mwaga maji itakuwa umeiondoa wanga
Mbona mi nimeepuka wanga
 
United States wanaongoza kulima mahindi karibu acres 90+M wanalima tu mahindi lakin ugali unaongoza kuliwa sana huko usukumani hamna hata maeneo ya kulima hayo mahindi ndo ujue kuwa ugali siyo kitu kizuri
Hujaeleweka. Fafanua
 
Principally, wanga huongeza nguvu katika mwili na ikiwa nyingi mwilini, mwili hubadili wanga kuwa mafuta/fats/lipids for storage purposes. Kwa hiyo kula wanga kulingana na uhitaji wa mwili wako. Km unafanya kazi za nzito wanga lazima ule wanga wa mwingi ili mwili uweze kuzalisha nishati ya kutosha kuwezesha kumudu kufanya kazi nzito. Ila km shughuli zako ni laini huhitahi kula wanga mwingi. Mlo/diet hutegemea sana na shughuli ya mtu afanyayo. Ila hitimisho wanga hauepukiki by anyhow.
 
Back
Top Bottom