Ukitaka kufanikiwa/kutoka katika maisha lazima uwe na tabia ya kufanya yafuatayo:
1)Usipende kufuata mfumo(social system),fanya kile ambacho wewe unaona ni sahihi na moyo wako umekipenda ila mradi usivunje sheria, kanuni na norms
2)Fanya zile kazi/shughuli ambazo ukifanya zinakupa rahaa na furahaa licha ya kupata na kipato juu
3)Unapotaka kufanya kazi/shughuli fulani usitangulize hela au faida mbele bali tanguliza kupata furahaa, utu,e.t.c
4)Kuwa jasiri wa kujaribu na ukishindwa usikate tamaa bali rudia tena na tena hadi uweze ila mradi kitu hicho unakipenda
5)Usipende kufanya biashara bali fanya ujasiriamali
6)Penda sana ku-take risk na rafiki yako mkuu awe risk
7)Kuwa na marafiki wenye mawazo ya kimapinduzi achana na marafiki wanaowaza kufungua duka, kuanzisha traditional farming e.t.c
8)Penda sana kufuatilia vipindi vya elimu ya dunia hii kwa njia mbalimbali kama vile kusoma vitabu, kusikiliza radio, kuangalia tv, kusoma magazeti, kusoma majaridi, kuperuzi internet
9)Fuatilia na kuwa na marafiki na watu waliofanikiwa
10)Jali sana mda
11)Ogopa na kimbia umbea
12)Usipende kusingizia kuwa huna mtaji, kumbuka mtaji wako mkubwa ni ubunifu wako wa namna ya kuweza kufanikisha jambo lako
13)Usipende kuona kuwa huna mda tena na mda umeshakutupa mkono.Kumbuka unaweza kufanya kitu hata kama una miaka mia ila mradi una uhai na akili inafanya kazi
14)Acha kuwa muoga wa kuanzisha na kufanya jambo
15)Amini ya kuwa mambo yote ambayo unaona watu wanafanya katika jamii bado hawajaweza kufanya vya kutosha na uamini kuwa wewe unaweza kufanya mapinduzi zaidi
16)Lazima ujue na kuamini kuwa hakuna uhusiano wowote kati ya jinsia yako na kuweza kufanya na kufanikisha jambo fulani
17)Penda kushirikisha watu wenye mawazo ya kimapinduzi katika maisha yako ya kila siku
18)Changua kitu kimoja unachikipenda na kufa nacho hadi kifanikiwe badala ya kutangatanga mara leo hichi mara leo kile
19)Penda kufanya zile kazi/shughuli/jambo ambalo watu wengi hulikimbia na kuona halifai labda kwa sababu ni jambo gumu, au ni jambo lenye risk kubwa sababu shughuli kama hizo huwa na returns/faida kubwa
20)Heshimu na kuwapenda wanadamu wote
21)Jali afya yako