Ushauri: Nimekuta 'urine pregnancy test' kwenye kimkoba cha binti yangu

Ushauri: Nimekuta 'urine pregnancy test' kwenye kimkoba cha binti yangu

Ushauri Wangu ni huu

Elewa umri aliyopo binti yako kitaalamu unaitwa adolescent kwa tafsiri nyepesi anahama kutoka utoto kwenda utu uzima kukiambatana na mabadiliko ya kimwili na kihisia…….Vitu vingine siwezi viweka wazi sana vinaweza tumiwa forum kwa manufaa ya sexual predator au ma-pedophilia (Watu wenye kuvutiwa kingono na watoto wadogo).

Katika umri huo kuna kuwa na udadisi sana wa kujitambua “Yeye ni nani” na lazima hawe na msimamizi au guider hadi atakapopita umri huo kufikia 20s.

Binti yako kwa sasa ana umri wa miaka 14 na haushi na mama yake lakini nilitaka kujua baada ya kutengana na mama yake mahusiano yenu au ugomvi wenu umewaathiri watoto kina namna gani? Je unawaruhusu kuonana na mama yao hasa hao wa kike? (Samahani si lengo la kuingilia familia yako) ila ningefurahi kujua to what extent there some impact to her.

Elewa kingine ingawa hujachelewa sana barehe hasa binti hao huanzia miaka 11 muhimu sana “BABA NDIYO MPENZI WA KWANZA WA BINTI YAKE” (simaanishi sexual contact HAPANA) Je umeitumia nafasi hiyo kwa namna gani?

Tangia akiwa mdogo. Pengine kinamsumbua bintiyo ni self-image yaani anaonekana vipi mbele za wenzake na yeye ni somebody mbele ya teens wenzake muhimu sana kama hakuipata hiyo taswira kutoka kwa Mwanaume wa Kwanza tangia anazaliwa (Baba YaKE) sasa pasipokujua yaani “libido” inampeleka kwa other man au teens wenzake.

Jitahidi sana kujenga mahusiano na mwalimu wakike shuleni anaposoma au ungemtumia mama yake kwa hilo hasa wa darasani kutakuwa na good monitoring ya bintiyo anapokuwa shuleni.

Halafu weka mazingira ya kuanza wajua rafiki zake mtaani na hata shuleni huwafahamu wao na wazazi wao na si vibaya na mahali wanapoishi. Hiyo ni mission muhimu kwa kila mzazi hata kama unabanwa na shughuli gani hao ni watoto wako si wa house girl au wapangaji wenzako

Jitahidi na ni nani wa kumpa Elimu kwa karibu sana na very serious kuhusu Reproductive health ni vizuri mama yake akachukua nafasi hiyo.

Makosa Makubwa wanayofanya wazazi wanadhania labda kwa kuwa mtoto anakula basi ndiyo kumlea hii chart fupi sana kuhusu malezi ya mtoto

Mwili: Chakula Mavazi na Malazi mazuri

Nafsi: Maneno Chanya na kumtia nguvu ya kujiamini wakati wote “yeye ni nani” na discipline ya maisha na adhabu juu ya matendo mabaya nb kuchapwa anapokosea hasa wakati hajafikia Barehe

Roho:Hamjue Muumba wake na awe committed anapokuwa na rafikize au mbali na wazazi basi Mungu Yupo na anamuona hata katika vile anavificha kwa siri….

(Ukali wa baba unamfanya mtoto afanyie maovu mbali ambapo baba hawezi kuona lakini hukimsaidia hawe na hofu ya Mungu mahali popote Mungu anamuona hatajitenga na maovu)



Sitaweza funguka kwa sana sababu kwa maelezo niliyoyaokota katika threads hii yamenipa maswali ya namna hiyo vingine nikiviweka sana public kama nilivyoomba radhi kuna hatari ya Sexual Predator na Pedophilia wakachukulia advantage kwa Maangamizi ya Binti zetu ambapo kwa sasa wakipata Mimba “NO MORE SCHOOL”

Shukrani sana mkuu kwa elimu uliyonipa.Nitaufanyia kazi ushauri wako.
Again thank you sana sana


Najisikia fahari kuwa MTANZANIA
 
Wakuu wa JF.
Nawashukuru sana sana kwa ushauri wenu mzuri,wengi sana mlionesha kuguswa na tukio lililofanywa na bint yangu kiasi ambacho nadhani mlihisi kama bint yenu.nawashukuru sana sana ijapokuwa wachache walinidhihaki na kunifanyia masihara.labda hawajakuwa wazazi bado lakini watakapokuwa wazazi wataelewa.
Nitaleta mrejesho baadae kidogo hatua niliyofikia na bint yangu kutokana na ushauri.nitaleta huu mrejesho ili wale ambao ni wazazi kama mimi waone ni changamoto gani zipo kwenye malezi ya watoto hasa wa kike.
Lakini nina ushauri kidogo kwa wale ambao wako ndani ya NDOA na wana watoto.
Fanya kila linalowezekana kuilea,kudumisha na kuienzi ndoa yenu.kuna athari kubwa sana sana kwa malezi ya watoto kama mtakubali kuvunja ndoa yenu.inawezekana kukawa na kero na karaha tupu ktk ndoa yenu lakini ni bora'funika kombe mwanaharamu apite' ili muweze kulea watoto wenu kwa ushirikiano wa baba na mama ,kwa mahaba na mapenzi makubwa juu ya watoto wenu.
ASANTENI SANA


NITALETA MREJESHO BAADAE KIDOGO


Najisikia fahari kuwa MTANZANIA
 
Na kama imeshindikana wao kuishi wawili kama mke na mume, amruhusu mama kuwa karibu na watoto wake wote wawili. Lazima kuwe na maamuzi ya hekima; unless aseme huyo mwanamke hafai kuwa mke na hata mama kwa watoto wake
vizuri sana
wenngi tumekuwa wabinafsi na tunafikiri kuwa ndoa ni ya watu wawili kumbe sio.
tendo la ndoa ndio la watu wawili lakini kuna watu wengi wenye maslahi mapana yandoazetu ikiwemo matokeo ya tendo la ndoa yaani mimba na watoto.
kwa kifupi ndoa ni taasisi. hivyo tuangalie madhara yakuachana kwa wengine tusiwe wabinafsi rudisha mke unaweza vunja uhusiano wa tendo la ndoa.
amua kiume
 
Mkuu kwanza pole sana kwa ulezi. Mtoto bila wazazi /familia iliyo tulia ni kazi sana kuwalea katika maadili. Vinginevyo Kudra za Mwenyezi Mungu zinahitajika. Numbisa Kasha maliza Mwite mama yao attete nae maana hapo kama una hasira unaweza anda jera sasa hivi.

Mwisho Hakikisha unamzawadia mvua 30 huyo anaye mrubuni. Hakikisha binti anamtaja na mnamuweka mtegoni umnase kama kunguru mwizi.

Baba mwenye nyumba kashakataza wazazi kurudi shule anataka kuharibu future ya binti yako.
 
Habari zenu wana JF,

Niingie kwenye mada, binti yangu yupo kidato cha pili sasa hivi na ana miaka 14. Leo asubuhi hii ameenda shule. Mimi na mama yake tumeachana kwa hiyo watoto nakaa nao mimi mwenyewe na sina mke kwa sasa.

Leo hii asubuhi naingia chumbani kwake nakuta kimkoba kidogo kitandani kwake na nashawishika kukifungua. Napata mshtuko wa mwaka nakuta kikaratasi cha (URINE PREGNANCY TEST) kilichotumika.

Nimechanganyikiwa sijui niongee nae nini.

Naombeni ushauri wana jamii na wazazi wenzangu, 14yrs?
e88bf85a623157bfa9b5e80d09c881e5.jpg



Najisikia fahari kuwa MTANZANIA

Hongera kwa mjukuu [emoji23]
 
washatoa bikira tayar

Sent from my GT-I9300 using JamiiForums mobile app
 
Kwanza +ve?

Sent from my SM-G903F using JamiiForums mobile app
 
Atakuwa alitumwa na mwalimu wa biology kwa practical

Sent from my TECNO-J8 using JamiiForums mobile app
 
yani kwa kifupi huyo ameshakuwa ni muhenga kwenye sita kwa sita,ata ukute anajua kila aina ya vodonge,mbinu na doctor mzuri wakukurupusha mimba ingawa ni 14 pole sana ndugu kwani hajawai kukuomba kiasi kikubwa cha hela?

lazima tulipe kodi
 
Miaka 14 kiruu mi nlikua cjui ata kitu

Post sent using JamiiForums mobile app
 
hapo hakuna namna mkuu ww sasa jaribu kumwambia aanze kutumia kondom tu wakati wa kuchakachuana kwa kuwa kashaonja tunda kumzuia tena ni atakudanganya tu we kaa naye chini mhusie kuhusu ngono zembe madhara yake na mimba za utotoni ila mwambie akiwa katika 6*6 na mupinziwe atumie ndom tu hakuna namna nyingine
 
Nimesikitika sana, ni hatari!
Muite umuulize mwenyewe kwamba hicho ni cha nini na umueleze hatari inayomkabili.
 
Je ungekuta condoms ama pedi ilio tumika ingekuaje....[emoji15] [emoji15]
Hii kwahakika haipendezi sisi wababa kukagua vitu vya mabinti zetu.... Haya sasa, anza kutafuta mke ili akusaidie kukulelea binti yako na kumuelimisha kuhusu usichana wake.
Ukiona ngumu, mrudishe akalelewe na mama yake
Kupekua ndio kumemsaidia kujua, kupekua mabegi ya watoto ni muhimu kuliko unavyofikiri. Yeye ndie baba yake ulitakiwa apekuliwe na nani wakati hakai na mama yake? kwani baba hajui kwamba bintiye huwa na mp?
 
Asante sana mkuu.Dua zako naomba MUNGU azipokee.
Mimi sitamuuliza chochote,nina hofu nisimuulize alafu akanijibu sivyo alafu nikamtia mkononi.
Nimeongea na mama yake labda wanaweza ongea lugha yenye kufanana lakini sitamuuliza chochote


Najisikia fahari kuwa MTANZANIA
Unakosea sana, baba lazima uonyeshe ubaba kama kweli umechukizwa. Unajuaje kama huyo mama yake atapamba naye ipasavyo na je kama wanaongea lugha moja!?
 
Shukrani mkuu.
mimi nimeanza kukaa nao mwezi wa sita mwaka huu.kabla ya hapo walikuwa wakikaa na mama yao.sasa sijui mama yao kama aliwapa uhuru wa kupita kiasi na inaonekana kama ilikuwa hivyo.
Nitafuata ushauri wako mkuu

Najisikia fahari kuwa MTANZANIA
Haya ndiyo madhara ya wazazi kuachana. Watoto wanalelewa kwa changamoto na mbaya zaidi ni pale katikati ya baba kuwa kule na mama kuwa kule. Ongeza na gap ya Shule na nyumbani. Wazazi tujifunze kuvumiliana ikishindikana kabisa basi Watoto wakae kwa mzazi mmoja mwenye uwezo wa kuwalea na Mzazi mwingine awe free kuwatembelea Watoto. Ukweli talaka na kutengana ni majonzi kwa Watoto. Tutafakari hili.
 
Kupekua ndio kumemsaidia kujua, kupekua mabegi ya watoto ni muhimu kuliko unavyofikiri. Yeye ndie baba yake ulitakiwa apekuliwe na nani wakati hakai na mama yake? kwani baba hajui kwamba bintiye huwa na mp?
Mkuu....
Nami pia ni mzazi, na nimekua na binti mwenye umri kama huo pamoja na kupitia hatua hizo.
Wababa hatupaswi kufanya hicho alicho kifanya mleta Uzi.
Kuna umri ambao binti akifikia lazima baba utazame njia m-badala ya mumsaidia, ikiwa baba unaishi bila mke.
Bado nasisitiza kwamba baba hakufanya sahihi kumpekua binti yake.
 
Afu hizi smart phones mnawapa watoto ni balaa, mtoto anamaliza form 4 unampa smart phone anakutana na STUNTER kadhaa wa kitaa utafurahi na roho yako, mtoto anatumiwa picha mtu anayonywa k, afu yuko kwenye balehe utafurahi na roho yako
Ni hatari kwa kweli!
 
Mkuu....
Nami pia ni mzazi, na nimekua na binti mwenye umri kama huo pamoja na kupitia hatua hizo.
Wababa hatupaswi kufanya hicho alicho kifanya mleta Uzi.
Kuna umri ambao binti akifikia lazima baba utazame njia m-badala ya mumsaidia, ikiwa baba unaishi bila mke.
Bado nasisitiza kwamba baba hakufanya sahihi kumpekua binti yake.
UNasisitiza alifanya vema sana na imemsaidia kujua kwamba kuna adui anatakiwa apambane Naye kabla hajammaliza yeye!
 
Back
Top Bottom