Ushauri: Nimepewa RB kwa kosa la kufanya fujo kanisani

Ushauri: Nimepewa RB kwa kosa la kufanya fujo kanisani

Kwani mjomba wewe ndio mchungaji? Mbona unaonekana una uchungu sana?
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] hata mimi kila nikisoma comment zake nikawa nawaza hivyo hivyo. Atakuwa pia ni muumini kindaki ambae humwambii kitu, au ni mmona wa wachungaji
 
Watoto hulelewa na wazazi wawili baba na mama ok mleta mada kasema maziwa ya kopo yaliisha Kwa Nini asiende kununua ? Hela Hana? Kwa Nini asinunue wakati watoto hunywa maziwa ya kopo? Anasubiri Mkewe arudi kanisani ndio anunue ? Yeye kazi yake Nini kutembeza tu mti ulio katikati ya mapaja au? Majukumu yake ndani ya nyumba kulea hao Watoto ni Nini? Kama hata maziwa ya kopo hawezi nunua Hadi afuate mke kanisani? wanakunywa maziwa ya kopo akaangalia yameisha anabeba watoto kupeleka Kwa Mkewe kanisani Kwa Nini asinunue hayo maziwa ya kopo mpuuzi huyo ? Ina maana yeye lofa anategemea mke tu alete maziwa hata ya kopo lofa huyo?

Kilimshinda nini kununua maziwa ya kopo awape watoto Hadi aende kanisani kufanya fujo mke atoke kanisani? Mwambieni anasubiriwa mahakamani atajua mahakama haitetei wajinga kama yeye na kesi yake atapangiwa hakimu Mwanamke .Ajiandae
Mbona una hasira sana na mtoa mada?? Wewe ni mchungaji nini?? Umesoma vizuri kwamba aliambiwa maziwa yameisha na akatoa hela yakaenda nunuliwa watoto wakanywa lakini bado walikuwa wanalia??

Je ni mwanamke mwenye akili ambae anaacha watoto wa miezi 4 bila maziwa anajua yameisha yeye anakaa masaa 10 kuombea watu ni mama au ni katili??

Je unajua kwamba kwa watoto wadogo chini ya miezi 6 anatakiwa kunyonya ziwa la mama tuu labda kuwe na sababu iliyo nje ya uwezo kiafya?? ( sio sababu ya upuuzi kama ya mke wa mleta mada).

Mwisho kabisa unajua kwamba kwa mtoto mdogo hata we na miezi 7 kuendelea ( ameanza kunywa uji na maziwa ya kopo) hakuna mbadala utakaomaliza kiu yake ya maziwa ya mama yake zaidi ya kunyonya??

Hakuna mama mwenye akili timamu anayeacha watoto wachanga masaa 10+ yeye yupo kanisani, hata makazini kuna break za kunyonyesha pia.
 
Kanisa kama Lina usajil be very careful kesi mbaya sana itakayokuumiza ukajuta maisha Yako yote kitakachokukuta wakikuburuza mahakamani kuwafanyia fujo utakoma sababu mkeo hakupekeleka cheti Cha ndoa kama sharti la kujiunga na Hilo kanisa liwe la kweli au la kitapeli.Jiandae kuumia

Ukibanwa mahakamani waweza umia Bure Kwa mihemuko ya kidini ya kidini chako na hatakuja paroko Wala askofu Wala papa Wala katekista au mchungaji au au sista au shehe atakuja mahakamani kama shahidi itakula kwako hawaji uwe.makini mihemuko.ya kidini Yako iliyopitiliza kuliko mapadre,mashehe,wachungaji nk wa dini Yako utaumia Hadi basi ukome.Maumivu huwezi gawana na papa,askofu, mchungaji shehe au mchungaji

Tuliza kichwa wewe
Makanisa ya halali na ya kitapeli Sasa hivi viongozi wasomi sana Wana madgrii kibao huwababaishi chochote utaumia sheria zote wanajua Tena za mahakamani
Tofauti na zanani watakuummiza
Kwa hiyo kama lina usajili mahakama itarunga vifungu vipya vya sheria? Maana hilo unalosema wewe hata kifungu cha sheria hakipo, bunge halijatunga sheria unayoitaka wewe. Kama hujui usitishe watu, kwanza KUFANYA FUJO ni kosa dogo sana na linasikilizwa mahakama ya mwanzo, hata sio wilaya, na wapi ulisikia mahakama ya mwanzo imemfunga mtu mwaka mmoja?
 
To cut the story short siwezi mwaga Kila kitu humu tukutane mahakamani huyo Mkewe atakuwa na mawakili kibao na hiyo case judgement hata hakimu au jaji akiamua itakuwa quoted kama presedence ya case zingine kama hizo mbeleini

Mwambieni huyo mume tunamsubiri Kwa hamu mahakamani
Mchungaji wa mchongo we muhuni tu kama wahuni wengine
 
Umeeleza vizuri Kwa uelewa wako mdogo wa sheria hapo Kuna kesi nyingi tu Kuna trespass unaenda Kwa jirani kusiko.kwako na kumfanyia vurugu kwake bila kuwa na legal document yeyote una mharass na kumuondolea peace of mind yake akiwa Yuko peacefully Yuko kwake

Angeitiws jambazi wakamuua usingeongea uongeayo haya Sasa ule uvamizi ni wa kijambazi sababu hauna legal document au legal backing hata moja

Kaibuka tu hakushirikisha serikali ya mtaa Wala mjumbe Wala RB ya polisi huyo ni jambazi mia Kwa mia aliyeenda kuvamia kanisa la watu .Sema walimhurumia walitakuwa kuitia jambazi jambazi kavamia kanisa umati uje umpe.kipigo Cha mbwa Koko Hadi akate roho sababu pale hakuna mahakama ya kuthibitisha yeye mumewe alienda na vyeti vya ndoa kuthibitisha yeye ndie mumewe? alimuonyesha nani? Kwa Nini asihukuliwe kama jambazi mteka nyara muumini au
Au kafika pale kisheria Kwa kufuata taratibu za kisheria Hiyo kesi kisheria sio nyepesi kama unavyofikiri
Kwa huu uandishi wako tu ushadhihilisha wewe ni hamnazo
 
-Polisi hawakumkomalia, ndio maana wakampa dhamana maana ni haki ya mtuhumiwa.
-Polisi ni kazi yao kupokea kila taarifa itolewayo kituoni na kuichukulia hatua na ndio maana kwa uzito wa kosa walitumia busara ya wito na sio kwenda kumfuata.
Polisi hakuepo eneo la tukio, kimpasacho ni kupokea taarifa na kuifanyia kazi, yaani kuchunguza namna kosa lilivyo tokea, na kwavile chanzo hapo ni mgogoro wa kifamila, na polisi wanajua kua kosa la shambuli anaetakiwa kulalamika mi mke na sio mchungaji wa kanisa, pia polisi sio wajinga wakapeleke kosa hilo mahakamani wakati wanajua kua ndoa itakua na mpasuko na tabu itakua kwa watoto, na Polisi ndie mlinzi wa watoto kisheria.
Pia kwa kosa la shambulio ni mahakama ya mwanzo na hukumu yake ni faini, na faini ni pesa ya serekali na sio ya alie lalamika, kosa hilo hafungwi.
Kosa la kufanya fujo pia nalo sana, hata kanisa wafanyeje, hawawezi kulifanya kua kubwa, na hukumu itategemea na thamani ya uharibifu wa mali, tofauti na hapo kama hakuna thamani nayo ni kupigwa faini, kwa kwa makosa yote hayo faini haivuki laki 2 hata kama kuna uharibifu wa mali. Hiyo ndio kisheria.
Polisi wanajua fika kua ili udhaminiwe unatakiwa ktk wadhamini kuwe na mwanaume, na kama ni mdhamini ni mmoja basi awe mwanaume, lakini polisi walimdhaminisha kwa mama mkwe yani mwanamke, hio ni dalili kua hapo hakuna kesi.
Pia hapo kanisani mchungaji sio msemaji wa mwisho na iko wazi kabisa kua kanisa ndio linaiharibu hiyo ndoa, mzee wa kanisa hawezi kutia aibu kanisa lake kwa kwenda mahakamani kuaibika kwa kusimamia kukosa haki ya msingi ya watoto wa miezi minne kunyonya. Atakosa waumini.
Na polisi hawataacha kuuliza swali la msingi kwa mchungaji ktk maelezo yake ya kua, je! Huoni kwamba wewe utakua chanzo cha ndoa hii kufa?
Hakuna kosa la UJAMBAZI Tanzania. Wewe unaejua sheria niambie kosa hilo ni CRIME, CIVIL au MINER?
Kila kosa lina vithibitisho vyake ili likamilike kua kosa.
Mfano. WIZI. Ili kosa la wizi likamilike lazima kuwe na vitu 3 vifuatavyo-:
1) Kitu kiwe KINA HAMISHIKA.
2) Kitu kiwe KINA MMILIKI.
3) Kitu kiwe na THAMANI
Hivi kikikamilika ndio kosa linasimama, ndio maana kakuna kesi ya kuiba nyumba wa shamba. Sasa wewe unaambiwa kosa ni KUFANYA FUJO wewe unasema ujambazi. Una akili kweli?
 
Update ya mwisho: Kanisa limefungwa 😂 nitafurah kusikia hvyo sanaa, siyapend hayo makanisa mm bas tuh
 
Wasaalam?
Ipo hivi juzi asubuhi Jumapili niliingia nyumbani nilikuwa SA kwa mambo ya kikazi, kufika nyumbani nilimkuta binti yangu wa kwanza pamoja na dada wa kazi kumuuliza mama yako yuko wapi? Akasema ameenda kanisani, nikamuuliza mbona hajaenda na watoto(watoto ni mapacha wana miezi 4) wakashindwa kunipa jibu nikapiga kimya nikaenda kupumzika kutokana na uchovu.

Imefika saa 7 mchana nikashtushwa na kelele za watoto walikuwa wanalia mno nahisi walikuwa wanataka kunyonya kuangalia makopo ya maziwa yameisha nikatoa pesa wakaenda kununua lakini nilipiga marufuku matumizi ya maziwa ya kopo.

Nimebuy time mpaka saa 10 jioni kimya mtu hajarudi nikipiga simu inaita tu haipokelewi, nikashikwa na gadhabu sana nikachukua watoto nikawatupia kwenye gari safari mpaka kanisani kwa wife.
Nimefika kanisani nimemkuta wife yupo madhabauni anaombea watu nikachukua watoto nikawaweka pale pale madhabauni nikamwambia awanyonyeshe watoto wana njaa, akagoma akasema nimemfanyia vitendo vya aibu!!

Ghafla mchungaji mkuu akaja akauliza kuna nini? Mimi nikamwambia mchungaji hayakuhusu nataka watoto wanyonye niondoke nao nyie endeleeni na ibada zenu,mchungaji akadakia akasema ibada ya leo inahitaji utulivu ndio maana tulitangaza watoto wote wabaki majumbani.

Nikamvuta kinguvu wife nikaondoka nae nikamwambia Leo ndio mwanzo na mwisho kusali katika makanisa ya kiroho kama hauwezi kusali roman Catholic pumzika nyumbani tu.

Nimepigiwa simu sasa hivi natakiwa kituo cha polisi kwa kosa la kufanya fujo kanisani na kufanya shambulio la kimwili dhidi ya wife, niende au nisiende? Kwa sababu kesho asubuhi inabidi niende Bujumbura kikazi.

Asante

MREJESHO: no 1
Nimeripoti police nimewekwa selo kwa dakika 30 mama mkwe amekuja ameniwekea dhamana nimetoka.
Cha ajabu muda huu nimerudi nyumbani nimemkuta dada wa kazi tu.. kuuliza naambiwa ameenda kanisani yeye na watoto wote .

Kusikia kwa kenge mpaka damu zimtoke ngoja niende kwanza Bujumbura.
Asante

MREJESHO no 2
Leo tar 5 nimerudi kutoka Burundi muda huu nimeingia nyumbani nimewakuta na waumini wenzake wanafanya fellowship,sitaki kuanzisha vurugu nasubiri kesho nirudi polisi kwanza kuripoti.
Asante.

MREJESHO no 3
Polisi wamesema tuyamalize kifamilia.
Tumekaa kikao cha familia binafsi nimempiga marufuku kwenda tena katika ilo kanisa na hakuna kufanya tena fellowship nyumbani kwangu ni kheri arudi Roman Catholic, kama hataka basi afanye ulokole wake ndani yangu akiwa na watoto wake lakini sio kwenda tena katika makanisa ya kiroho.
Pia wazazi wake wamempiga marufuku kwenda ktk makanisa ya kiroho.

NB:Tumegundua kanisa halijasajiliwa mimi na rafiki yangu tunalivalia njuga ilo kanisa mpaka lifungwe kwa gharama yoyote.

Mwisho
kwa sisi tunaojua kusoma picha, hakuna chochote kilichotokea hapo, na huna hata uwezo kwenda south. ila umeleta hii mada ili kuponda makanisa ya kiroho kwasababu una chuki nayo na umeweka mkeo iwe kama ndio pambio la kufikisha ujumbe wako. wewe kama unachukia makanisa ya kilokole, ni wewe, Tanzania kuna uhuru wa kuabudu, na mkeo ana uhuru wa kuabudu. pamoja na kwamba, kama ingekuwa kweli, anatakiwa kuwa na hekima, na inategemeana anasali kanisa gani, kama ni hayo ya wauza mafuta, shauriana naye kwa upole na amani, ataelewa, ila kama ni walokole wale wa tangu siku zote, it is just a matter of time hata wewe utakuwa mlokole, inaweza kuwa kwa hiari yako au kwa lazima. kuna watu wengine huwa wanaokoka kwa hiari ila wengine wanaokoka kwa fimbo. kuna mmoja wa aina yako alikuwa anawachukia walokole sana, ila kuna siku dawa zote zilidunda, pesa alipukutisha, waganga alimaliza wote, akajikuta anamwambia wife wake "NAOMBA KANIITIA YULE MCHUNGAJI WAKO ANIOMBEE". baba yangu mzazi alikuwa mbishi na alikuwa hataki twende church, ila alikuja kuugua akaita mchungaji, nashukuru Mungu dakika zake za mwisho alimpokea Yesu, hiyo ndio furaha yangu manake nilikuwa nampenda sana. hata wewe kuna siku ipo utaokoka kwa fimbo na utakuja hapa kutoa ushuhuda. acha kiburi cha uzima.

kuhusiana na mchungaji huyo aliyekuja kuuliza kuna nini, inaonyesha hayo ni yale makanisa ya matapeli, mchungaji wa kilokole, kwa heshima ya yule mama (mkeo) na kulinda ushuhuda mbele ya waumini, wala asingekuja kwa namna hiyo, angekuomba tu kwamba naomba tukayamalize nje. na ni lazima anakufahamu vizuri sana na kanisa lote watakuwa wanakujua na wanajua mshirika mwezaoi yaani mkeo anaishi na mtu msumbufu. hivyo kama alikuja kwa namna hiyo basi ana mapungufu. na hata akiwa na mapungufu haiwafanyi wasiwe wameokoka (kama wapo kanisa sahihi).watakuombea na utaokoka tu. mark my words.
 
kwa sisi tunaojua kusoma picha, hakuna chochote kilichotokea hapo, na huna hata uwezo kwenda south. ila umeleta hii mada ili kuponda makanisa ya kiroho kwasababu una chuki nayo na umeweka mkeo iwe kama ndio pambio la kufikisha ujumbe wako. wewe kama unachukia makanisa ya kilokole, ni wewe, Tanzania kuna uhuru wa kuabudu, na mkeo ana uhuru wa kuabudu. pamoja na kwamba, kama ingekuwa kweli, anatakiwa kuwa na hekima, na inategemeana anasali kanisa gani, kama ni hayo ya wauza mafuta, shauriana naye kwa upole na amani, ataelewa, ila kama ni walokole wale wa tangu siku zote, it is just a matter of time hata wewe utakuwa mlokole, inaweza kuwa kwa hiari yako au kwa lazima. kuna watu wengine huwa wanaokoka kwa hiari ila wengine wanaokoka kwa fimbo. kuna mmoja wa aina yako alikuwa anawachukia walokole sana, ila kuna siku dawa zote zilidunda, pesa alipukutisha, waganga alimaliza wote, akajikuta anamwambia wife wake "NAOMBA KANIITIA YULE MCHUNGAJI WAKO ANIOMBEE". baba yangu mzazi alikuwa mbishi na alikuwa hataki twende church, ila alikuja kuugua akaita mchungaji, nashukuru Mungu dakika zake za mwisho alimpokea Yesu, hiyo ndio furaha yangu manake nilikuwa nampenda sana. hata wewe kuna siku ipo utaokoka kwa fimbo na utakuja hapa kutoa ushuhuda. acha kiburi cha uzima.

kuhusiana na mchungaji huyo aliyekuja kuuliza kuna nini, inaonyesha hayo ni yale makanisa ya matapeli, mchungaji wa kilokole, kwa heshima ya yule mama (mkeo) na kulinda ushuhuda mbele ya waumini, wala asingekuja kwa namna hiyo, angekuomba tu kwamba naomba tukayamalize nje. na ni lazima anakufahamu vizuri sana na kanisa lote watakuwa wanakujua na wanajua mshirika mwezaoi yaani mkeo anaishi na mtu msumbufu. hivyo kama alikuja kwa namna hiyo basi ana mapungufu. na hata akiwa na mapungufu haiwafanyi wasiwe wameokoka (kama wapo kanisa sahihi).watakuombea na utaokoka tu. mark my words.
I'd yako nyingine ni @chapwa24 ?
South Africa ni kitu gani mzee? Unataka nikuwekee tickets za flights nilizoruka nazo US,Canada, Brazil,Russia?
Sibishani na mtu mwenye I'd mbili.
 
Kwa ujinga huu unaoufanya mtatuharibia ndoa zetu sana rudini nyuma mjitafakari visa hivi ni vingi sana hasa kwa makanisa ya mlipuko. Mnajazana ujinga tu na miujiza hamjielewi hata hivyo nawapongeza wachungaji wa taasisi imara. Mimi ni mhanga wa visa kama hivi hivi kwann hamna akili au kwa kuwa wanawake kudanganywa ni rahisi. Harafu makanisa haya wamejaa wanawake sana.
 
Back
Top Bottom