Umesema sahihi Mkuu, ndiyo maana inashauriwa usifanye maamuzi ukiwa katika hali ya Furaha sana ama Hasira kali.
Huwezi kuja kuvunja ndoa wakati mna watoto wa miaka 20 plus, wameshindwa hata kukaa chini na kuyajenga.
Mie ilishanitokea nika abort mission, kesi yangu ilikua tofauti kidogo na hii. Hata hivyo nafikiri kama hiyo Hali ingetokea Sasa hivi, huenda ningefanya maamuzi tofauti kabisa na niliyofanya wakati ule.
Kesi yangu ilikua hivi, nilikutana na dada tuliyesoma wote tukiwa na urafiki wa kawaida Hadi tunamaliza shule. Sikuwahi kuwa na mpenzi Wala Ile one night stand, ni full Jesus Boy.
Nikaja kukutana na huyu binti wakati huo tayari nipo kazini, of course tukajikuta tumeendeleza urafiki wa kawaida, shida ikaja mwenzangu akawa anatengeneza mazingira ya kwenda mbele zaidi ikiwezekana Hadi ndoa. Nikaona kama Wazo zuri, ila nikataka tujipe muda wa kufahamiana pia sikutaka jambo la " kimasihara" kabla ya ndoa.
Nikagundua alikua na mtoto japo yeye hakuwahi kuniambia. Kuna siku nokamweleza jambo la mtoto nilitaka atoe hofu awe huru na ajue kwamba mtoto haikua shida kwangu.
Nilimpenda sana yule mtoto na Hilo alilifueahia. Shida yangu nikataka kujua mazingira ya baba wa mtoto, nilitaka Hilo likae sawa Kwa sababu lazima tujue mtoto ataishi kwetu au Kwa baba yake.
Hapo Sasa ndio sarakasi zikaanza. Nikapewa taarifa zisizo sahihi, kwamba baada ya ujauzito mambo yalikua si shwari Kwa vile Binti alikua chuo na baada ya hapo hakikuendelea chochote kati Yao.
Sasa kumbe namie nafsi ikawa inakataa, ikabidi nitumie mbinu za mafunzo ya sungusungu ( local FBI training) in intelligence...
Hapo ndio kujua kwamba Hawa watu walikua wakiishi huko kama Mme na Mke na jamaa alikua anamsomesha, walikua nchi nyingine na Binti alikua amekuja nchini kusalimia jamaa na kusherehekea Sikukuu za mwisho wa mwaka.
Nilichokua sana Kwa hizo taarifa, mbaya zaidi jamaa tukawaziliana nae kiroho safi akasema huyu ni Mke wake akanitumia emails zenye taarifa na ushahidi mwingi tu kuthibitisha Masai yake. Wakati huo Binti na Mama yake wamekataa katakata kumtambua huyo jamaa.
Siku hiyo nimeomba tukutane restaurant Moja Mimi, kaka mtu, Binti na Mama yake baada ya chakula nilitoa zile emails, nikaziweka mezani, nikaenda kulipiza bills nikarudi kuwaaga ukimya ukiwa umetawala.
Hapo tayari wazee walishaenda kupeleka posa ilikua tupangiwe kwenda kutoa mahari.
Huo ndio ukawa mwisho wa hiyo project.
Ni jambo lilinivuruga sana, uzuri nilikua likizo vinginevyo ningeharibu kazi za watu.