USHAURI: Nini cha kufanya kama mwenza wako alikuficha kuwa ana mtoto, Ukaja kujua baada ya miaka zaidi ya 10 baadaye?

USHAURI: Nini cha kufanya kama mwenza wako alikuficha kuwa ana mtoto, Ukaja kujua baada ya miaka zaidi ya 10 baadaye?

Habari wana JF.
Kuna Ndoa imevunjika hapa ndoa ya miaka 15.
Mke alizaa kabla ya ndoa, sasa mama huyu alimficha mtoto,
Huyu mtoto alikuwa anaishi na Baba yake.
Mume alijua kwa mawasiliano ya simu.
Mama alipokuwa anaongea na mwanae.
Na mtoto anaumri wa miaka 20.
Mume wa ndoa kazaa nae watoto 4.

Dawati la suruhisho walijaribu kuweka sawa ili wasiachana ila ilishindika. Hata wachungaji walishauri kuwa asamee tuu kwani hata mtoto kashakuwa mkubwa hakuna shida yoyote lkn ndo hivyo ndoa imevunjwa jana na mahakama.

Huyu mama alizaa kipindi anaumri wa miaka 21.

Sasa wanajamii hivi vitu vinatokana na nini mpk mmoja anaamua kuficha mtoto?

NI NINI CHA KUFANYA BAADA YA KUJUA HATA KWA MUME KAMA ALIFICHA KUWA ALIKUWA ANAMTOTO.
Mume alikua anatafuta sababu! Na kashaipata
 
Umeishi na mtu kwa miaka 15, mmezaa watoto 4, unakuja kumuacha kisa hakukwambia kua aliwahi kuzaa kabla!!?

Ukisikia kutafutiana sababu ndio huko sasa.
Unaona ni kosa dogo?
Kosa sio tu kuzaa, kosa kubwa ni uwazi.

Hili jambo hufufua mambo mengi.

Huenda kuna nyakati alikuwa akiomba ruhusa asafiri aende mahali akidanganya kwa ndg....jamaa anakuja kuunga dots anagundua huenda alikuwa anaenda onana na mume wa awali.

Jambo moja hufufua mengi uliyoyasamehe....waza vizuri usikomenti kirahisi kama hujui umuhimu la hili
 
Huyo jamaa itakuwa Kuna viashiria alikuwa anaviona kwa huyo mke ila alivumilia muda wote akiamini ni mke mwema.....sasa huenda kwenye hivyo viashiria kulikuwa Kuna ukweli....huenda alishakutana hata na baba wa mtoto akiongea na mkewe ila alidanganywa.....MIMI NAMPA KINGOLE HUYO JAMAA,ACHANA NAE MWANAMKE WA NAMNA HIYO
 
Ndani ya hizi ndoa wengi tunaowaita mashemeji mara nyingi huwa ni watoto wa wake zetu.

Unakuta katoto unatambulishwa kama mdogo wa mwisho au mtoto wa dada/kaka kumbe ni mtoto wa mkeo.

Ni nadra kwa wanaume kuficha watoto waliopatikana kabla ya mahusiano ila wanawake mara nyingi wanahusisha kuwa na mtoto kabla na kushuka kwao kwa thamani kupelekea kuficha watoto wao wa kabla ya ndoa/mahusiano.
Bora huyo alimficha, wengine wanawaua kabisa, hii Dunia Ina mengi!! Ila Kwa kumzalia watoto wanne, ajihakiki kama ni wake then asamehe saba Mara sabini, Kwa uzoefu looser mwisho WA game atakuwa baba
 
Unaona ni kosa dogo?
Kosa sio tu kuzaa, kosa kubwa ni uwazi.

Hili jambo hufufua mambo mengi.

Huenda kuna nyakati alikuwa akiomba ruhusa asafiri aende mahali akidanganya kwa ndg....jamaa anakuja kuunga dots anagundua huenda alikuwa anaenda onana na mume wa awali.

Jambo moja hufufua mengi uliyoyasamehe....waza vizuri usikomenti kirahisi kama hujui umuhimu la hili
Kwa mtu mwenye akili timamu, rijali, aliyepitia malezi bora ya wazazi wote wawili hawezi kuacha mke aliyeishi nae miaka 15 na kuzaa nae watoto wanne kisa alimficha kua alizaa kabla, hilo ni kosa dogo sana na linazungumzika.....

Na kama mtu hayupo tayari kuzungumza ya nyuma kwanini alazimishwe??? Kila binaadam ana siri yake na maamuzi yake yanapaswa kuheshimiwa, huwezi jua hilo tukio lilimuumiza vipi akaamua kulifukia na kuanza upya.
 
Sawa mkuu..
Lakini ebu tufikiri katika namna ya kawaida kabisa kama bin adam, je ungeendelea kumuamini??
Kwanini nisimuamini?
Jamani kila Mtu ana siri yake kama ameamua kuitunza as long as haikuwahi kuniletea madhara yoyote si basiiiii,

Tena haya mambo ya Mwanamke kuondoka mahali na kuacha mtoto kisha akaja kuolewa sehemu nyingine na kuzaa, mara nyingi huwasahau wale watoto wa mwanzo na kufocus na family mpya, hadi mtoto aje amtafute na hii sio kwa Mwanamke tu hata kwa Wanaume hutokea,

Mimi naona mnakuza vitu ambavyo kimsingi havina mashiko.
 
Soma tena uzi, nahisi umecomment kwa kisirani sana
Umeanza mihemko isiyo na sababu.
Pili tusijadili mambo kimazoea ya kiswahili.

Mwanzo wa mahusiano una mambo mengi.

Kuna mwanamke mkianza mahusiano anakutaka uwe wazi kwake kama umewahi kuoa au kuzaa nje.

Kwa moyo mkunjufu unamweleza ukweli.

Naye anakwambia hajawahi kuolewa wala kuzaa, baada ya miska 15 ukagundua alizaa na alikuficha kwanini udimwache?

Mwanzoni ukiniambia hata una watoto wawili kwa uwazi huo mimi nitakuoa.

Napendezwa na mwanamke muwazi, makosa kila mtu hufanya.

Lakini kitendo cha kumficha binadamu aliyetoka kiunoni mwako, si unaweza kumficha mmeo jambo lingine kubwa?
Ongea uhalisia uache hasira
 
Lazima kuwe na sababu ya yeye kutokusema,

Kuna Mama alipokonywa mtoto na Mwanaume aliyezaa nae, mtoto alikua ana miezi 11, yule Mama alihangaika kuanzia Ustawi wa jamii hadi Mahakamani, kote aligonga mwamba basi akamuachia Mungu na kurudi kwao (Mikoa ilikua tofauti) baada ya miaka kupita, akaja akapata Mwanaume akamuoa hakumwambia kuhusu tukio lile yeye anasema alijaribu kulisahau hakuona sababu ya kulizungumzia tena, Mtoto alikuja kumtafuta Mama yake ameshakua mtu mzima na wajukuu akamletea, Mume ndio kujua hilo sakata lakini hakureact tofauti zaidi ya furaha familia imeungana tena.
Kama aliamua kusahau, family reunion ilitokea wapi?

Huyo mwanaume aliyemsamehe amepungukiwa busara.

Dawa ya mwanamke muongo ni kuachana naye.
 
Back
Top Bottom