USHAURI: Tubadili mfumo wa viti maalum, vifutwe!

USHAURI: Tubadili mfumo wa viti maalum, vifutwe!

Ninaendelea kufanya utafiti kujua nchi ngapi za africa zina ubunge wa dezo kama huu ambao ni mzigo kwa walipa kodi
 
Wataalamu wa sheria wanisaidie kufafanua kipengele hiki cha katiba yetu hasa kwenye mstari wa pili
"NA KWA KUWA
misingi hiyo yaweza tu kutekelezwa katika jamii yenye demokrasia ambayo serikali yake husimamiwa na Bunge lenye wajumbe waliochaguliwa na linalowawakilisha wananchi, na pia yenye Mahakama huru zinazotekeleza wajibu wa kutoa haki bila woga wala upendeleo wowote, na hivyo
kuhakikisha kwamba haki zote za binadamu zinadumishwa na kulindwa, na wajibu wa kila mtu unatekelezwa kwa uaminifu"

 
Naomba mwenye kufahamu anijuze, NEC wanapigaje hesabu za kupata viti Maalum bunge la 2010? Kwa hiyo baada ya uchaguzi mdogo uliomalizika hesabu inkuwaje?
 
Hii ni ya 2005 sijui mwaka huu mahesabu yakoje

PartiesVotes%DirectAdditionalTotalseatsWomenseats seats Chama Cha Mapinduzi (Revolutionary Party)7,579,8977020658264Civic United Front (Chama Cha Wananchi)1,551,24314.3191130Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Party for Democracy and Progress)888,1338.25611Tanzania Labour Party297,2302.71—1National Convention for Construction and Reform–Mageuzi239,4522.2———United Democratic Party155,8871.41—1Others117,6711.2———Members nominated by the Union president10Representatives of the Zanzibar House of Representatives5Ex officio members223275324
 
Tanzania ni nchi masikini lakini ina wabunge wengi sana na imefikia wakati wa kufuta viti maalumu!. Imefikia wakati ambao kila mtanzania wa rangi yeyote, jinsia yeyote anaweza kupata kura na kuwa mbunge sasa ni kwanini tunatumia pesa nyingi kwa wabunge. Wabunge ambao kwa kiasi kikubwa hawasaidii lolote kwa nchi yetu rushwa ipo palepale, gharama za kuwatunza ni za juu sana, na pesa ingeweza kutumika kuleta umeme, maji, kujenga shule na kudumisha afya kitu ambacho bunge limeshidwa kufanya. Bunge la Tanzania limekuwa sehemu ya kula bure pesa ya walala hoi na ni wakati wa kusema hakuna haja ya viti maalumu. Mfano mzuri hata kwa upinzania Chadema imeshinda viti 23 na wabunge maalumu 25!!. Je CCM ina wabunge maalumu wangapi na wana fanya nini hasa tofauti na wabunge wa kawaida!!
 
Naunga hoja. Hebu angalia idadi ya wabunge Zanzibar na baraza la wawakilishi. Watu wenyewe hata milioni moja hawafiki bado unaongeza viti maalum. Kuna mawaziri 25. Bado hujahesabu masheha. Kila mtu kule anakula kweye siasa. Kila mtaa kuna mbunge au waziri au mjumbe wa baraza la wawakilishi. Tutafika kweli jamani? Ukiangalia na huko mawizarani, wizara inaweza kuwa na magari matano, lakini madereva walioajiriiwa wako kama kumi hivi, wanacheza bao na kusubiri mshahara. Kweli iko kazi bado mnauliza kwa nini waafrika tunaendelea kuwa maskini wakati majibu yapo.
 
Hivi jamani viongozi wetu bila kuzingatia itikadi zao kisiasa hawalioni hili kuwa wabunge ni wengi sana hasa wanaoingia ki uraini kama wanawake....na viti maalum.
Kuna wagonjwa wangapi Muhimbili, Mwananyamala, Amana na Temeke wanakosa vitanda? Hiyo pesa wanayolipwa naamini ingeokoa maisha ya mamilioni ya watanzania....
 
Naunga mkono hii hoja. Ni ukweli usio pingika kwamba hakuna sababu ya msingi kuwa na wabunge wa viti maalumu. Kwanza kazi yao kubwa ni ipi? Jee wanawakilisha jimbo gani? Nadhani walioanzisha huu mfumo walikuwa na lengo zuri kabisa ambayo ilikuwa kutrain baadhi ya wanawake ili warudi majimboni wakashindane kwani tayari walikuwa na ujuzi, lakini kuanzia miaka ya 2000 hivi viti vimekuwa ni sehemu za ahadi za vigogo kwa nyumba ndogo zao (kwa asilimia kubwa). Huu ulikuwa mradi wa muda mfupi kama uanzilishi wa zile shule za special.

Nadhani ile hoja inayosema wapi tutapata pesa za kusomesha vijana bure kuanzia std 1 mpaka form 6 nadhani tunaweza kuanzia hapa. Tuweke tuu namba ya kawaida kwamba wabunge hawa wako 100. Mishahara yao ya 12,000,000/month kwa mwaka ni 14.4 Billion shilling au 10.2 Million USD. Then Jumlisha pesa ya dereva na retirement accumulation per year hapo utakuta tunasave 5 million USD. So, wabunge hawa 100 watasave serikali kiasi cha 15 million ( hii ni salary na retirement annually).

Kiasi cha 15 Million USD tunaweza kusomesha wanafunzi wangapi? Assume mwanafunzi mmoja analipiwa 400,000 kwa mwaka tungeweza kusomesha wanafunzi 52,447 kwa mwaka. Sasa tukiongeza yale marupu rupu na vikao vya chai, mafuta, per diem na vingenevyo basi tungeweza kuongeza uwiano wa walimu.

Nilishasema na nitasema hawa wabunge ni 0. I don't care wanatoka CCM au NCCR we do not need wabunge wa viti maalum.
 
Ni hoja nzuri sana

Wangeweza kutumia kigezo walichotumia kumpata speaker mwanamke kama haja ni kuongeza uwakilishi. Yaani kuna kuwa na maazimio kabisa kuwa jimbo fulani msimu huu lisimamishe wagombea wanawake tu kwa vyama vyote na kuwa na circulation kila baada ya miaka mitano. Vinginevyo kama wanataka kuku democrasia basi wote bila kujali jinsia wala rangi wakapigane majimboni. Mbunge ni mwakilishi wa wananchi sasa wabunge wa viti maalum na kuteuliwa ni wawakilishi wa kina nani?. Yaani bunge linaonekana sasa ni sehemu ya kugawana ulaji zaidi badalaa ya kutumikia wananchi. Gharama za serikali zimekuwa kubwa zaidi ya matokeo ya kuwa na msululu wa watu wanaosubiri posho tu.
 
Ni hoja nzuri sana

Wangeweza kutumia kigezo walichotumia kumpata speaker mwanamke kama haja ni kuongeza uwakilishi. Yaani kuna kuwa na maazimio kabisa kuwa jimbo fulani msimu huu lisimamishe wagombea wanawake tu kwa vyama vyote na kuwa na circulation kila baada ya miaka mitano. Vinginevyo kama wanataka kuku democrasia basi wote bila kujali jinsia wala rangi wakapigane majimboni. Mbunge ni mwakilishi wa wananchi sasa wabunge wa viti maalum na kuteuliwa ni wawakilishi wa kina nani?. Yaani bunge linaonekana sasa ni sehemu ya kugawana ulaji zaidi badalaa ya kutumikia wananchi. Gharama za serikali zimekuwa kubwa zaidi ya matokeo ya kuwa na msululu wa watu wanaosubiri posho tu.

Kwa nini tutumie muundo huo hapo juu? Wanawake wangapi wamemaliza vyuo na wanaujuzi wa kutosha kushindana na wanaume. Sidhani kabisa kwamba swala ni elimu au nini. Nadhani swala ni dhana potofu ya kwamba wanawake hawawezi kusimama majimboni. Ukweli ni kwamba Wanawake wa Tanzania ni washupavu ambao wanaweza kuleta mabadiliko wakipewa chance, tuwapeni chance kwa kuwaacha washindane na wanaume. Halima Mdee kashindaje? Spika Kashindaje? Mama Anna Kilango? Mama Tibaijuka? Hawa wote wamewashinda wanaume tena wengine wenye majina ya juu kabisa. Nadhani ni muda muafaka wa kukomesha hii siasa baguzi.
 
Badala yake lianzishwe baraza la SENATE ambalo kila mkoa utoe senator wawili na Zanzibar itoe sita tu. Yaani Pemba Watatu na Unguja watatu. Baraza hili litatathmini nmaamuzi yote ya bunge, to confirm all appointment of Ministers and Judges. Hapo tutakuwa tumeula kabisa. Maana Rais wanamuonea sana, majukumu mengi, shughuli nyingi yote hayo mtu mmoja tu.
 
  • Hivi ni lazima viti maalum wawe ni wanawake tuuuu! (logic please)
  • Kuna tofauti gani kati ya wabunge wa viti maalumu na wabunge wa kuteuliwa na rais?
  • Ni nini kazi ya wabunge wa viti maalumu na je ni muhimu wao kuwepo?
Jengo la bunge letu limejengwa muda si mrefu na kufanya bunge lihame toka chimwaga na kwenda pale Jengo jipya maarufu kama Mjengoni. Jengo hili limejengwa kwa gharama kubwa sana mabilioni ya shilingi yametumika pale. Wasiwasi wangu ni kwamba baada ya muda mchache tu tutalazimika kutumia mamilioni mengine kujenga lingine au kulitanua kwa kilekinachoonekana kushindwa kuhimili uwingi wa wabunge. Tunabahati nzuri moja tu kuwa wabunge wetu wengi ni wavivu hawahudurii vikao laiti ingekuwa kinyume basi hili la kuongeza ukubwa au kujenga lingine basi lingeshajitokeza muda mrefu uliopita
 
Kwa nini tutumie muundo huo hapo juu? Wanawake wangapi wamemaliza vyuo na wanaujuzi wa kutosha kushindana na wanaume. Sidhani kabisa kwamba swala ni elimu au nini. Nadhani swala ni dhana potofu ya kwamba wanawake hawawezi kusimama majimboni. Ukweli ni kwamba Wanawake wa Tanzania ni washupavu ambao wanaweza kuleta mabadiliko wakipewa chance, tuwapeni chance kwa kuwaacha washindane na wanaume. Halima Mdee kashindaje? Spika Kashindaje? Mama Anna Kilango? Mama Tibaijuka? Hawa wote wamewashinda wanaume tena wengine wenye majina ya juu kabisa. Nadhani ni muda muafaka wa kukomesha hii siasa baguzi.

Kumbe na wewe umeona eeenh! kuwa kitendo cha kusema wagombee upika wanawake watupu miongoni mwa chama chenye wabnge wengi ni siasa za ubaguzi, hata viti maalum si tu ubaguzi bali ni udhalilishaji wa wanawake kuwa ni disabled wanahitaji kusiadiwa kitu ambacho kimepitwa na wakati. Ukweli mambo ya kuwa na wabunge wasio tokana na majimbo ni upuuzi ulioanzishwa na watu wenye mawazo ya kuona kuwa uongozi ni ulaji badala ya kuhudumia.
 
Excellent, tulishapendekeza hapa JF hawa Viti maalum ni hasara tupu, yaani wafutwe mara moja, tangia wameanza nani anaweza kusema hata wana faida gani? wengi wao ni vihiyo, kulala bungeni, fuata upepo na kuunga hoja hata hawazijui, na nyumba ndogo kibao na vikuku miguu usiseme, na wanatutia gharama kubwa sisi walipa kodi, kazi yao in general hawana, na sijui nani alianzisha hii system, umaskini wanatuongezea sana hawa, isitoshe if is about gender equality si hoja tena most women wamemaliza varsities & can compete with men in constituencies, LAZIMA KATIBA MPYA IFUTE HII, HATUTAKI HAWA KUPE, PARASITES WANATUNYONYA
 
Back
Top Bottom