USHAURI: Tubadili mfumo wa viti maalum, vifutwe!

USHAURI: Tubadili mfumo wa viti maalum, vifutwe!

Ni mianya iliyotengenezwa ili kupeana ulaji tu na mfumo unaotuongoza sasa. Tukianza kudai tume huru ya uchaguzi then baadae rasimu ya mabadiriko ya Katiba ya Warioba tutakuwa tumeitendea haki nchi yetu na watanzania kwa ujumla wao.

Mabadiriko ya kweli kimaendeleo yataanzia hapo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
JF Igolya!

Ndugu zangu Ibara ya 66 (1) na Ibara ya 78 ya Katiba ya JMT, 1977 na kifungu Cha 86A Cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura 343, vinatambua uwepo wa Wabunge Wanawake wa Viti Maalum wasiopungua asilimia 30 ya Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hata hivyo, Serikali iliamua kufanya uamzi wa kuongeza idadi hiyo kutoka asilimia 30 hadi kufikia asilimia 40 ya Wabunge wote wa Bunge la JMT.

Ni jambo zuri, kwani linakusudia kuongeza nafasi na fursa kwa wanawake katika vyombo vya maamzi.

Asilimia 40, kwa Sasa ni sawa na Wabunge Wanawake wa Viti Maalum 113, ambapo CCM ina Wabunge 66, CHADEMA 37, CUF 10.

Vyama vingine havikubahatika kupata baada ya kukosa walau asilimia 5 ya kura zote halali kwa mujibu wa ibara 78 (1) ya Katiba ya JMT, 1977.

*Swali langu*

Hivi viti ni kwa ajili kuongeza ufanisi pale bungeni, au just utekelezaji wa dhana ya usawa wa kijinsia?

Hizi hela wanazopewa bure bure hizi haziwezi kusaidia kuwatoa Wanafunzi kuandikia chini, na hatimae wapate madawati?

Kuna mjumbe mmoja humu JF alilalamika kuwa alikuwa anarubuniwa kuwa atapewa nafasi ya Ubunge wa Viti Maalum, kama Chama kitapata fursa hiyo pale atakapokuwa ameondoa chupi yake mwilini? Hapa inaonyesha kuwa Kuna wabunge wanaingia bungeni kwa kutumia mbinu hii!- Siwafahamu lakini pia inawez kuwa ni dhana tu.

Lakn swali langu linabaki palepale, hawa ndugu zetu hawa 113, Wana tija yoyote kwa Taifa, au ndo tunaongeza tu matumizi yasiyokuwa ya lazima kwa Taifa? Kwa nn watu wasichuane majimboni, maana uwanja uko huru, haubagui mwanamke Wala mwanume.

Akisinzia bungeni akahojiwe, lkn huyu kiti Maalum hawajibiki kwa mwananchi yeyote.

Nawasilisha kwa mjadala.

Lugumya.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Najua Tu Kuhusu Wa CCM Ambao Kwanza Wanatakiwa Wawe Na GPA Kubwa, Masters Degree au PhD, Akili ZILIZOTUKUKA, Ushawishi, Wasio Wanafiki Na Wagomaji Bila Kusahau Wawe Na Mvuto Mkubwa Sana Machoni Mwa Watu Huku Bila Kusahau AFYA Zao Zisiwe Na Mgogoro...
Kumbe na wewe ni kada kindakindaki hivi!
 
Ubunge ni kazi ya uwakilishi wa wananchi wa eneo fulani.Watu wa jimbo husika wanakuchagua ukawe sauti yao bungeni, ukazungumze badala yao.Hawa wabunge wa viti maalum na wa kuteuliwa ni sauti ya nani na wanazungumza badala ya nani? Tukipata majibu ya haya maswali tutakubaliana kwamba hatuhitaji tena aina hii ya ubunge.

Kama wananchi wa jinsia zote mbili kutoka majimbo yote ya nchi wameamua kuchagua wanaume wabunge wote au kwa sehemu kubwa kupitia uchaguzi huru na wa haki ni sawa na vyema kabisa, wameona hao ndio wanoafaa kuwa sauti yao na wawakilishi wao. Lazima tuheshimu maamuzi yao hayo ya kidemokrasia.

Kama tunapenda sana usawa wa jinsia kiasi cha kutotaka kuwakosa wanawake bungeni basi vyama vya siasa vinavyojinadi viko kwa ajili ya wananchi wote na vingine vinasema wanawake wanavipenda zaidi wahakikishe wanakuwa na wagombea na hatimaye wabunge kupitia kura za wananchi katika majimbo ya uchaguzi.

Naamini ubunge kupitia viti maalum sio sahihi, ni ufujaji mkubwa wa pesa za walipa kodi ambazo zingeweza kufanya mambo mengine ya muhimu kuboresha maisha ya wananchi na kama ilikuwa lazima kuwa na hawa wabunge basi ilipaswa kuwa project ya muda mfupi sana na ilipaswa kuwa imeisha kufikia sasa.
 
Wabunge kupita bila kupingwa ni lazima wapinzane wawe huru kupeleka malalamikowya umnywaji wa haki. Ma DED kukimbia ofisi wakati wa kuchukua na kurudisha fomu pia liangaliwe sana.
 
Hapo ni kuwa na tume huru ya uchaguzi tu.
Wabunge kupita bila kupingwa ni lazima wapinzane wawe huru kupeleka malalamikowya umnywaji wa haki. Ma DED kukimbia ofisi wakati wa kuchukua na kurudisha fomu pia liangaliwe sana.
 
Kuanza na viti maalumu tutakuwa tunaenda mbali zaidi mkuu. Nashauri Tuanze kutafuta uhalali kuhusu wale wabunge 19 wa binafsi (wasio fungamana na chama chochote) Je si matumizi mabaya ya rasilimali za nchi haya??
 
Ninaona kama sasa after ten or fifteen years tutakuwa na wabunge wa viti maalum Wanaume! Kwa sababu kwa sasa kama vile ninaona hamna haja ya kuwa na wabunge wa viti maalum wanawake!
 
Jamani nauliza hivi wabunge wa viti maalum bado wana umuhimu kuwepo bungeni?

Nashindwa kuelewa hawa wanafanya nini bungeni kwa jinsi wanavyo behave pale mjengoni.

Leo hii mbunge anaanzisha nyimbo za mapambio ya kichama ndani ya jengo la kutungia sheria!

Naomba tujadili jamani.

 
Hivi viti maalum vina umuhimu sana ktk kuleta utulivu kwa wabunge wa kiume.

Ukiviondoa viti hivi wabunge wa kiume watakalia nini?
 
Back
Top Bottom