USHAURI: Tubadili mfumo wa viti maalum, vifutwe!

USHAURI: Tubadili mfumo wa viti maalum, vifutwe!

Wabunge wa viti maalum bungeni wanamwakilisha nani? Na wanawajibika kwa nani ? Kuna muongozo wowote unaoeleza majukumu yao ili tuweze kuwapima ?
 
hata mimi huwa najiuliza sipati jibu kwani wao huwa tunawaona bungeni wakiuza nyago tu wachache sana hurudi kwa wanawake tena wanaorudi ni chama cha mafisadi wa upinzani hauwaoni kabisa . lazima katiba mpya iweke bayana shughuli zao kwani wanalipwa masurufu marefu kwa kodi zetu wanaishia kuyatumia na familia zao
 
Humu jamvini kumbe majority ni mamen hawaoni sababu ya kuchangia masuala ya kuwainua wanawake , nashukuru kwa mchango japo huwa clipendi jina lako
 
Sioni sababu ya msingi ya kuwa na viti maalumu kama wanania ya kweli kwanini kwny cabinet hakuna? kwenye vyama vya siasa hakuna? Kinachonisikitisha zaidi ni mchango wao mdogo kwenye bunge na jamii zaidi ya kuuza sura na kupeana ulaji. Haiini akilini eti kwa miaka 15 bado ni mbunge via viti maalumu mbona basi walemavu hawana? Wazee hawana? wanafunzi hawana? etc
 
hawa wanamwakilisha huyo mtu wao aliyewahonga hivyo viti maalum. Kwa sababu hawa wanawake wanachaguliwa bila vigezo vyovyote vinavyoeleweka. Na hata ukifatilia vyama vya upinzani nako wanawachagua kiupendeleo ndo maana kipindi kile chadema mzozo ulitokea.....

na hata wanachokifanya hakieleweki zaidi ya kugonga meza tu maana wengine hata uelewa hawana ..
 
Mh!.. Kwa upeo wangu Nadhan ni njia tuu ya kugawana fedha kati ya matajiri kwa matajiri... Kwa sababu sinai kumbukumbu ya kuchaguliwa/kuteuliwa kwa mwanamke toka kijijini au hata kutoka mjini ambambaye ni masikini!.. Wote wachaguliwao ni watu wenyewe nafasi zao tayari!...
 
Jina la viti maalumu lina walakini hasa kwa vile linametumiwa kuwatambulisha wabunge wakina mama walioingia kwa upendeleo. Ningeomba kwa wanajua kiswahili fasaha watafute jina muuafaka ambalo halitawakwaza wengine. Kunawengine wana behave kama wanakazi kusudiwa ya kiti.
 
Ndugu zangu,

Niweke bayana kabisa hapa mwanzo kwamba nia ya hoja hii siyo kushambulia viti maalumu bungeni bali ni entry point yangu kuchokoza mjadala wa wajibu na tija wa wabunge wetu. Ieleweke kwamba kuna wabunge wa viti maalumu ambao hoja zao zina mshiko kuliko za wabunge wengi waliochaguliwa. Lakini pia kuna wabunge wa viti maalumu ambao ni mzigo kwa walipa kodi. Hali kadhalika kwa wabunge wa kuchaguliwa majimboni.

Bunge la sasa linatakiwa kuwa na jumla ya Wabunge 357 iwapo rais atamalizia uteuzi wa wabunge wake waliobakia. Wabunge wa viti maalumu ndani ya bunge la sasa ni 102 ambao ni asilimia 29 ya wabunge wote.

Katiba ya JMT haijaweka bayana kazi za mbunge wa viti maalumu lakini nataka nichukulie kwamba anawakilisha wanawake bungeni hasa kwa sababu wote wameteuliwa na vyombo vya wanawake vya vyama vyao vya siasa. Kuna wabunge wa kuteuliwa (na wengine viti maalum) wanaowakilisha makundi yenye mahitaji maalumu kama walemavu. Sina tatizo ha hawa, ingawa pia kuna wabunge wa kuchaguliwa walemavu!

Kwa mujibu wa uchambuzi wa taasisi inayoitwa TWAWEZA, kuna wanawake wa viti maalumu ambao walikuwa na utendaji mkubwa bungeni kuliko wanaume wa kuchaguliwa majimboni. Naomba ninukuu taarifa ya TWAWEZA kutaja wabunge kumi bora wa viti maalumu wa bunge lililopita (overall ranking yao kwenye mabano, kati ya wabunge 267);

Diana Mkumbo Chilolo (6)
Susan Anselm Lymo (10)
Magdalena Hamis Sakaya (17)
Lucy Fidelis Owenya (20)
Stella Martin Manyanya (23)
Mhonga Said Ruhwanya (29)
Esther Kabadi Nyawazwa (30)
Savelina Silvanus Mwijage (40)
Martha Mosses Mlata (42)
Halima James Mdee (47)

Tahadhari kwenye hii ranking ni kwamba kuna ambao hawakuchangia mara nyingi sana lakini michango yao michache inaweza kuwa ya muhimu kuliko ya waliochangia mara nyingi. Kinyume chake pia kinaweza kuwa sahihi.

Pia kuna wabunge wanaoamini bila shaka yoyote kwamba wanachokisema au kufanya kina maana na umuhimu kwa sababu tu wao wamechaguliwa na wananchi (hata kama ni kinyume na maslahi ya wananchi). Kutokana na imani hii hudhani kwamba mawazo yao ni matukufu na hayastahili kukosolewa. Kwamba mawazo mengine yoyote ni hafifu kama yametolewa na mbunge ambaye siyo wa chaguliwa jimboni.

Sasa naomba msaada wenu kujibu maswali yafuatayo;

1. Kama kuna wabunge wanawake wa viti maalumu ambao kazi zao katika bunge zina tija kuliko waliopigiwa kura ina maana gani?

2. Kwa kuwa wabunge wa viti maalumu wanawakilisha wanawake katika bunge, je wamefanikiwa kiasi gani kumkomboa mwanamke wa tanzania kupitia bunge?

3. Je, wananchi wanawezaje kuwajibisha wabunge wa kuchaguliwa na wa viti maalumu ambao hawana tija kwao kupitia bunge?

4. Ni matumizi mazuri ya rasilimali zetu kuweka wabunge 357 kazini kwa miaka mitano kila mmoja akilipwa mshahara na marupurupu yanayokadiriwa kufikia milioni 6.9 kwa mwezi, wakiwa wanachangia tu hoja bila kuwajibisha serikali kikamilifu? Wengi wanarudia walichosema siku za nyuma na wengine wanarudia ambayo yameshasemwa na wenzao, au na wananchi?

5. Je, wabunge wawe wanalipwa kutokana na utendaji wao? Yaani wawekewe malengo na walipwe kutokana na kiwango walichotimiza malengo waliyowekewa.

6. Je, wabunge 357 wana tija ya kufanya maamuzi sahihi kuliko wabunge wachache zaidi?

7. Je, tuendelee na huu mfumo wa kuwa na wabunge wa kuchaguliwa na wa viti maalumu?

Naomba tujadili bila kuegemea ushabiki wetu wa vyama please,

Nawasilisha
 
Miongoni mwa mambo yanayo ifilisi nchi hii, ni kuendekeza mifumo inayobuniwa kukidhi matakwa ya kisiasa. Jambo hilo limepelekea tuwa na serilikali kubwa mno, inayokula rasilimali yote ambayo vinginevyo ingeliwekezwa katika mipango ya maendeleo. Hii ni pamoja na kuwa na bunge kubwa lisilo na tija; kuwa na wilaya ambazo kwa kiwango kikubwa kazi zake zingeliweza kufanywa na halmashauri za wilaya; kuwa na msululu wa mawaziri na manaibu waziri wasiokuwa na kazi n.k. Itakuwa vema iwapo katiba mpya inayotarajiwa itaweka utaratibu mzuri wa kudhibiti mambo hayo.
 
matumizi mabaya ya pesa za umma wabunge hawa wafutike period..katiba mpya iondoe kabisa
 
wabunge wa viti maalum ni ubadhirifu wa hela tu. Waliochaguliwa na wananchi wanatosha. Ni kuliongezea taifa mzigo wa matumizi yasiyo na maana

Kama Ubunge wa viti maalumu ni ubadirifu vipi ule wa kuchaguliwa?

Naamini katika utaratibu huu wa kuwapatia wanawake sauti ili hatimaye na wao watoe mchango kwa taifa lao kwani kutokana na mfumo dume ambao umetawala conscious na subconscious mind yetu basi bila huu utaratibu pengine bunge lingekuwa na more than 80% wanaume na hali ya maisha ya mtanzania ingekuwa mbaya zaidi ya sasa.

Lakini napenda nikosoe utaratibu unaotumika kuwapata hawa wabunge wanawake na pia concept nzima ya gender katika siasa za Tanzania, kwani unafuata mfumo ule ule dume wa kupata hao wabunge; japo kuwa ni wanawake lakini wengi wao ni wanaume kimtazamo na hivyo kuendeleza mfumo ule ule dume ambao tunapingana nao.

Kwanini na sema hivyo kwa sababu hali inajionyesha kama hao hawana fikra dume basi maisha ya mwanamke na mtoto (kundi kandamizwa) wa tanzania yasinge kuwa kama yalivyo sasa kwani hali ni mbaya mahospitalini kwa wanawake wanaojifungua; watoto wanaokufa wakiwa wachanga; mimba za watoto wakike shule za msingi etc

Napenda niweke wazi kuwa tunapoongelea gender haina maana mwanamke tu, no na hii ni misconception ya concept hii ndiyo maana wanawake wenye mawazo ya mfume dume wamefanikiwa kuuteka na kuutumia kwa manufaa binafsi na hivyo ku abuse this precious opportunity ya kumkomboa mwanamke kama kundi moja wapo la jamii lililokandamizwa na mfumo dume.....

Ili kutoa ufafanuzi wa haya ninayo yaongea naomba wana JF walio na access na vyombo vya habari hasa star TV kwenye kipindi chake cha Asubuhi; ITV kwenye kipima joto wa waalike TGNP kuweka vizuri hii dhana na kuelimisha umma wa watanzania kuhusu nini maana ya Gender and Development (GAD) tofauti na concept za zamani I mean the whole process of how it came into existence and how has it evolved over time na vipi huu mfumo wa kisiasa unavyo fanikisha wanawake wenye mawazo ya kimfumo dume ku dominate hizo nafasi hivyo kusababisha lengo la hii affirmative measures kutofikiwa

Mimi ni activist wa Gender na kwa usongo basi nikiwa undergraduate was the best University student in DS mwaka wa pili; swali la gender ndo lilinipa maksi ya kupita wote na hatimae kupewa award ya Bank kuu....acha niji promote kidogo au siyo! Kwa hiyo kwa theory sihaba naifahamu Gender japo simzidi mama Usu Mallya ambaye pia ni mwalimu wangu wa Gender. I know for sure she can put this concept right kama hata ogopa siasa za Tanzania!
 
Kama Ubunge wa viti maalumu ni ubadirifu vipi ule wa kuchaguliwa?

Naamini katika utaratibu huu wa kuwapatia wanawake sauti ili hatimaye na wao watoe mchango kwa taifa lao kwani kutokana na mfumo dume ambao umetawala conscious na subconscious mind yetu basi bila huu utaratibu pengine bunge lingekuwa na more than 80% wanaume na hali ya maisha ya mtanzania ingekuwa mbaya zaidi ya sasa.

Lakini napenda nikosoe utaratibu unaotumika kuwapata hawa wabunge wanawake na pia concept nzima ya gender katika siasa za Tanzania, kwani unafuata mfumo ule ule dume wa kupata hao wabunge; japo kuwa ni wanawake lakini wengi wao ni wanaume kimtazamo na hivyo kuendeleza mfumo ule ule dume ambao tunapingana nao.

Kwanini na sema hivyo kwa sababu hali inajionyesha kama hao hawana fikra dume basi maisha ya mwanamke na mtoto (kundi kandamizwa) wa tanzania yasinge kuwa kama yalivyo sasa kwani hali ni mbaya mahospitalini kwa wanawake wanaojifungua; watoto wanaokufa wakiwa wachanga; mimba za watoto wakike shule za msingi etc

Napenda niweke wazi kuwa tunapoongelea gender haina maana mwanamke tu, no na hii ni misconception ya concept hii ndiyo maana wanawake wenye mawazo ya mfume dume wamefanikiwa kuuteka na kuutumia kwa manufaa binafsi na hivyo ku abuse this precious opportunity ya kumkomboa mwanamke kama kundi moja wapo la jamii lililokandamizwa na mfumo dume.....

Ili kutoa ufafanuzi wa haya ninayo yaongea naomba wana JF walio na access na vyombo vya habari hasa star TV kwenye kipindi chake cha Asubuhi; ITV kwenye kipima joto wa waalike TGNP kuweka vizuri hii dhana na kuelimisha umma wa watanzania kuhusu nini maana ya Gender and Development (GAD) tofauti na concept za zamani I mean the whole process of how it came into existence and how has it evolved over time na vipi huu mfumo wa kisiasa unavyo fanikisha wanawake wenye mawazo ya kimfumo dume ku dominate hizo nafasi hivyo kusababisha lengo la hii affirmative measures kutofikiwa

Mimi ni activist wa Gender na kwa usongo basi nikiwa undergraduate was the best University student in DS mwaka wa pili; swali la gender ndo lilinipa maksi ya kupita wote na hatimae kupewa award ya Bank kuu....acha niji promote kidogo au siyo! Kwa hiyo kwa theory sihaba naifahamu Gender japo simzidi mama Usu Mallya ambaye pia ni mwalimu wangu wa Gender. I know for sure she can put this concept right kama hata ogopa siasa za Tanzania!

Wabunge wa viti maalum ni ubadhirifu wa pesa za serikali. Waliochaguliwa wanatosha. Kama issue ni gender balance in the congress/perliament, basi inakuwaje tunapata wabunge wa kuchaguliwa na wananchi huko majimboni? Tunao akina Anna kilango, Halima Mdee, nk.ambao wamechaguliwa na wananchi huko mjimboni kwao kutokana na juhudi zao. Kama wao wameweza then kuna haja gani ya kuteua akina CHITANDA? Ni unnecessary waste of time, money and resources.
Kulazimisha gender issues bila kuangalia merits ndio one of the things vimetufanya tupatiwe the WORST SPEAKER IN THE HISTORY OF THE BUNGE IN ANNA MAKINDA. Kulazimisha hiyo gender representation ndio inatupatia vichwa butu na visivyokuwa na manufaa kwenye maendeleo ya Tanzania kama akina MARY CHITANDA na wenzake
Kuhusu DS pale mlimani, yes, nimesoma DS lakini I'm of the opinion that DS and its entire department be scrapped asap! kwasababu ni waste of time and resources.
 
Miongoni mwa mambo yanayo ifilisi nchi hii, ni kuendekeza mifumo inayobuniwa kukidhi matakwa ya kisiasa. Jambo hilo limepelekea tuwa na serilikali kubwa mno, inayokula rasilimali yote ambayo vinginevyo ingeliwekezwa katika mipango ya maendeleo. Hii ni pamoja na kuwa na bunge kubwa lisilo na tija; kuwa na wilaya ambazo kwa kiwango kikubwa kazi zake zingeliweza kufanywa na halmashauri za wilaya; kuwa na msululu wa mawaziri na manaibu waziri wasiokuwa na kazi n.k. Itakuwa vema iwapo katiba mpya inayotarajiwa itaweka utaratibu mzuri wa kudhibiti mambo hayo.

We have a very big government!!
 
Kwanza kabisa naungana na wote wanaolaani matumizi mabaya ya fedha chache za walipa kodi kugharamia wabunge wa kuteuliwa.
Mimi ninaamini kwa dhati kabisa kuwa mwananke anauwezo sawa na mwanaume.
Mambo ya 30% uwakilishi ni dhana iliyojengwa Nordic countries na Europe kwasababu mfumo dume uliwatenga akina mama hata kama walikuwa na sifa za kielimu. Ndiyo maana wabunge wao wa kuteuliwa wengi ni PhD holder.
Waafrika kwa akili zetu chafu za kuiga tukakubali kama tulivyokubali uzazi wa mpango ambao huko ulaya sasa ni historia. Tumesahau kuwa tatizo la mwanamke wa Tanzania ni elimu na kuwezeshwa. Watoto wa kike wanapata mimba hovyo, wanaozeshwa mapema, hawapewi kipaumbele hata na wazazi wao n.k.
Ili kuwakomboa wanawake jambo la muhimu ni kuwapa elimu na si kuwapa wabunge ambao wengi hawajui ndoo ya maji inawekwa vipi kichwani kwasbabu wamezaliwa Oysterbay na wanaona nyoka kweye maonyesho ya sabasaba.
Uteuzi wa wanawake hauzingatii mahitaji ya mwanamke bali kujaza idadi ili kupata support ya kisiasa. Pesa za wabunge 102 zingeweza kusomesha wanawake wengi sana.
Kama Halima anaweza kupambana Kawe, Regia anapambana Kilombero, Anna Kilango, Tibaijuka n.k hivi kuna sababu gani ya kuteua mvivu mmoja kuwa mbunge kwasababu ya umbile la kike!
Hata hao wanaoteuliwa kazi yao kubwa ni kusikiliza chama kinasema nini, hata kama Chama kikipeleka mswada wa wanawake marufuku shule, hawa wakuteliwa watapiga makofi.Hawana say, wameteuliwa hawajui wanawajibika kwa nani zaidi ya Makamba!(sorry)

Tatizo la Tanzania sio gauni au suruali, ni kupata kiongozi atakayetuvusha katika umasikini huu bila kujali jinsia. Kwa mwendo huu wa kuchaguana kwa vigezo vya jinsia hatulitendei haki taifa. Kama kipo kitu cha kubadilisha katika katiba mpya hiki ni kimojwapo, futilia mbali nafasi za kuteuliwa, tunataka viongozi wa kulisaidia taifa.
Nitafurahi sana kama wabunge wa kuchaguliwa 200 ni wanawake. Lakini sikubaliani hata kidogo na huu utaratibu wa kugharamia mtu tusiyejua anawajibika kwa nani eti kwasbabu tu amevaa gauni!
Hata wabunge wa kuteuliwa na Rais ni uchafu mwingine tunaopaswa kuundoa ndai ya katiba mpya.
 
ubunge wa kuteuliwa umeshapitwa na wakati. Raisi anapomteua MP wa viti maalum, do u think huyo mbunge atampinga aliemgaia ubunge?
 
Mimi naungana na wale wanaosema ni matumizi mabaya ya fedha za serikali. Hivi mbunge kama Mama mchungaji Lwakatare, anamchango gani kwa taifa hili? hata ukiangalia shule zake ni za gharama za juu kwelikweli.
 
Kama Ubunge wa viti maalumu ni ubadirifu vipi ule wa kuchaguliwa?

Kwanini na sema hivyo kwa sababu hali inajionyesha kama hao hawana fikra dume basi maisha ya mwanamke na mtoto (kundi kandamizwa) wa tanzania yasinge kuwa kama yalivyo sasa kwani hali ni mbaya mahospitalini kwa wanawake wanaojifungua; watoto wanaokufa wakiwa wachanga; mimba za watoto wakike shule za msingi etc
!

Hapo umenikuna kabisa. Kama mleta mada alivyosema kwamba hawa wabunge wa viti maalumu wote ni wanawake na jukumu lake ni kutetea maslahi ya wanawake katika utunzi wa sheria na upitishaji wa bajeti huko bungeni. Labda atokee mtu achambue kila mbunge wa viti maalum katika bunge lililopita alifanya nini bungeni kutekeleza jukumu lake. Pia tufanye documentation ya wabunge wa viti maalum wa bunge hili ni namna gani kila mmoja anatekeleza wajibu wake.

Kuna wachache sana nakumbuka kwenye bunge lililopita walitetea sana wanawake kisera na kibajeti lakini sauti yao haikutosha. Mfano, Martha Mlata, Susan Lyimo, na Magdalena sakaya. Wengine wote walikuwa wanapiga bla bla tu hawakuwa na mshiko kisera wala bajeti.

Lakini pia kama ulivyouliza kwanza na kama mleta mada alivyotahadharisha. Kuna wabunge wa kuchaguliwa ni bogus kuliko wabunge wachache wa viti maalum.
 
matumizi mabaya ya pesa za umma wabunge hawa wafutike period..katiba mpya iondoe kabisa

Naunga mkono hoja hii, kwa sababu nchi yet ni maskini. Sambamba na hilo, jazia hoja hizi.
1. Tupunguze idadi ya majimbo ya uchaguzi
2. Tuondoe kabisa wabunge wa kuteuliwa na raisi
3. Wabunge waiwe wakuu wa mikoa
4. Ubunge uwekewe ukomo, mf. miaka 15 tu.
 
Back
Top Bottom