USHAURI: Tubadili mfumo wa viti maalum, vifutwe!

USHAURI: Tubadili mfumo wa viti maalum, vifutwe!

Miongoni mwa mambo yanayo ifilisi nchi hii, ni kuendekeza mifumo inayobuniwa kukidhi matakwa ya kisiasa. Jambo hilo limepelekea tuwa na serilikali kubwa mno, inayokula rasilimali yote ambayo vinginevyo ingeliwekezwa katika mipango ya maendeleo. Hii ni pamoja na kuwa na bunge kubwa lisilo na tija; kuwa na wilaya ambazo kwa kiwango kikubwa kazi zake zingeliweza kufanywa na halmashauri za wilaya; kuwa na msululu wa mawaziri na manaibu waziri wasiokuwa na kazi n.k. Itakuwa vema iwapo katiba mpya inayotarajiwa itaweka utaratibu mzuri wa kudhibiti mambo hayo.

Nashukuru mkuu kwa mawazo, kwenye hiyo katiba mpya ungependa hili jambo lisomeke vipi mkuu ili kufanikisha ushauri wako?
 
wabunge wa viti maalum ni ubadhirifu wa hela tu. Waliochaguliwa na wananchi wanatosha. Ni kuliongezea taifa mzigo wa matumizi yasiyo na maana

Lakini mkuu kuna idadi kubwa ya waliochaguliwa na wananchi ambao ufanisi wao bungeni ni finyu kuliko wabunge wa viti maalumu. Kwenye hoja yangu ya msingi nimeomba tuchangie mawazo ni namna gani ya kuwajibisha wabunge waliochaguliwa ambao hawana tija wala ufanisi. Wengi wakishachaguliwa basi, wanajua hata kama wakiboronga namna gani ni mpaka uchaguzi ujao. Na sisi wote tunajua uchaguzi ni kanga na t-shirt ndiyo maana tunao wabunge waliochaguliwa kwa kishindo siyo kwa uwezo wao kiuongozi bali uwezo wao kifedha

hebu tusaidie mawazo mkuu
 
Kama Ubunge wa viti maalumu ni ubadirifu vipi ule wa kuchaguliwa?

Naamini katika utaratibu huu wa kuwapatia wanawake sauti ili hatimaye na wao watoe mchango kwa taifa lao kwani kutokana na mfumo dume ambao umetawala conscious na subconscious mind yetu basi bila huu utaratibu pengine bunge lingekuwa na more than 80% wanaume na hali ya maisha ya mtanzania ingekuwa mbaya zaidi ya sasa.

Lakini napenda nikosoe utaratibu unaotumika kuwapata hawa wabunge wanawake na pia concept nzima ya gender katika siasa za Tanzania, kwani unafuata mfumo ule ule dume wa kupata hao wabunge; japo kuwa ni wanawake lakini wengi wao ni wanaume kimtazamo na hivyo kuendeleza mfumo ule ule dume ambao tunapingana nao.

Kwanini na sema hivyo kwa sababu hali inajionyesha kama hao hawana fikra dume basi maisha ya mwanamke na mtoto (kundi kandamizwa) wa tanzania yasinge kuwa kama yalivyo sasa kwani hali ni mbaya mahospitalini kwa wanawake wanaojifungua; watoto wanaokufa wakiwa wachanga; mimba za watoto wakike shule za msingi etc

Napenda niweke wazi kuwa tunapoongelea gender haina maana mwanamke tu, no na hii ni misconception ya concept hii ndiyo maana wanawake wenye mawazo ya mfume dume wamefanikiwa kuuteka na kuutumia kwa manufaa binafsi na hivyo ku abuse this precious opportunity ya kumkomboa mwanamke kama kundi moja wapo la jamii lililokandamizwa na mfumo dume.....

Ili kutoa ufafanuzi wa haya ninayo yaongea naomba wana JF walio na access na vyombo vya habari hasa star TV kwenye kipindi chake cha Asubuhi; ITV kwenye kipima joto wa waalike TGNP kuweka vizuri hii dhana na kuelimisha umma wa watanzania kuhusu nini maana ya Gender and Development (GAD) tofauti na concept za zamani I mean the whole process of how it came into existence and how has it evolved over time na vipi huu mfumo wa kisiasa unavyo fanikisha wanawake wenye mawazo ya kimfumo dume ku dominate hizo nafasi hivyo kusababisha lengo la hii affirmative measures kutofikiwa

Mimi ni activist wa Gender na kwa usongo basi nikiwa undergraduate was the best University student in DS mwaka wa pili; swali la gender ndo lilinipa maksi ya kupita wote na hatimae kupewa award ya Bank kuu....acha niji promote kidogo au siyo! Kwa hiyo kwa theory sihaba naifahamu Gender japo simzidi mama Usu Mallya ambaye pia ni mwalimu wangu wa Gender. I know for sure she can put this concept right kama hata ogopa siasa za Tanzania!

Tatizo ni kwamba wabunge wengi wa viti maalum ni vigogo na hivyo hawajui matatizo ya wanawake watz. Pengine tatizo ni mchakato wa kuwapata hawa wabunge wa viti maalum. Lakini tunahitaji wengi hivyo kweli kutetea mambo ya wanawake? Mbona yule mbunge mwanamke mlemavu wa ngozi ametetea sana albino bungeni na yuko peke yake? mbona yule mama mlemavu, alitetea sana mambo ya walemavu bungeni na sheria nyingi sasa zina mtazamo chanya kwa walemavu, na yuko peke yake?
 
Lakini mkuu kuna idadi kubwa ya waliochaguliwa na wananchi ambao ufanisi wao bungeni ni finyu kuliko wabunge wa viti maalumu. Kwenye hoja yangu ya msingi nimeomba tuchangie mawazo ni namna gani ya kuwajibisha wabunge waliochaguliwa ambao hawana tija wala ufanisi. Wengi wakishachaguliwa basi, wanajua hata kama wakiboronga namna gani ni mpaka uchaguzi ujao. Na sisi wote tunajua uchaguzi ni kanga na t-shirt ndiyo maana tunao wabunge waliochaguliwa kwa kishindo siyo kwa uwezo wao kiuongozi bali uwezo wao kifedha

hebu tusaidie mawazo mkuu

Njia moja muhimu na ya kwanza ni kuondoa incentive ya pesa katika cheo cha ubunge maana ubunge si profession ni siasa, mbona madiwani hawapewi package kama ya wabunge na bado wanachapa kazi? Ku attach cash value kwenye cheo cha ubunge kimefanya ubunge uingiliwe na watu ambao kimsingi si wanasiasa bali ni sehemu ya kuondoa poverty kwa haraka kwani inalipa kuwa mbunge kuliko kuwa professional; pia rushwa ni sababu ya pili ya wafanya biashara kukimbilia wote bungeni kwani cost ya kufanya biashara na ku break even ni kubwa kwa mfanya biashara ambaye si mwanasiasa na speicifically mbunge.....maana biashara kubwa Tanzania ni Tender za serikali na zinapatikana kwa urahisi ukiwa mbunge kuliko mfanya biashara wa kawaida as one factor lakini pia kusumbuliwa na TRA plus system in general kunapungua ukiwa katika domain hiyo ya siasa kuliko vingine....One important factor ya ku punguza ni kuangalia leagal enforcement ambayo ndiyo italeta equity katika production function ya uchumi wa nchi

In general muundo wetu mzima unaathiriwa na UFISADI; Poverty and poor governance kama means ya ku combat the two.
 
According to ccm wanataka wananchi waamini hii formula:
C = M + U + D + C + H + L
Details:
C = Bunge la Tanzania
U = uganga wa kienyeji
C = Deals za mafisadi
H = Hongo ya ccm
L = Lazima uhakikishe unatumia hii pesa kuchaguliwa tena kumlinda Rostam
 
Wana JF

Ndio kuna wabunge wachache wa viti maalumu waliofanya mambo makubwa ya kuwatetea wanawake. Ninasema wachache, lakini wengi wamekuwa mzigo mkubwa kwa sisi walipa kodi. Wabunge hao wa viti maalumu hata ukisikia michango yao bungeni kusema kweli hata kujenga hoja hawawezi kabisa. Hivyo basi hao wengi ambao ni unproductive wanawameza wachache ambao ni productive hivyo kama ni ku strick the balance wabunge wa viti maalumu ni mzigo mkubwa kwa mlipa kodi coz wengi wanawajibika kwa chama na wananchi hatuna njia ya kuwa wajibisha.

Katika katiba mpya tutakayojiwekea sipendi kabisa vyeo vifuatavyo viwemo
  1. Wambunge wa viti maalumu
  2. Wabunge wa kuteuliwa na Rais
  3. Wakuu wa mikoa
  4. Wakuu wa wilaya
  5. Waziri mkuu (kwasababu tunafuata president system. (Rais na VP wanatosha)
  6. Wabunge kuwa Mawaziri
  7. Mameya/Wenyeviti wa halmashauri kuchaguliwa na madiwani (Tufanye direct election)
  8. Muundo wa Wizara za serikali uainishwe kabisa kwenye katiba (sio rais kujiundia wizara zake)
Samahani ninaanza kutoka kwenye maada wabunge wa viti maalumu plus wa kuteuliwa is a wastage of resources. Jamani nchi yetu hii bado ni masikini hatuna hizo resources za kuwakirimu hawa wa viti maalumu na kuteuliwa
 
...basi nikiwa undergraduate was the best University student in DS mwaka wa pili; swali la gender ndo lilinipa maksi ya kupita wote na hatimae kupewa award ya Bank kuu....... kwa theory sihaba naifahamu Gender japo simzidi mama Usu Mallya ambaye pia ni mwalimu wangu wa Gender.
what's the point?
 
Wakuu
nimejaribu kufuatulia kwa karibu sana juu ya umuhomu wa viti maalumu mbele ya matumizi yake yapasayo kwa watanzania.
nilichokuja kugundua ni kwamba hivi viti ni mzigo mkubwa kwa Taifa kwani wanawake hawa wanalipwa mabilion ya pesa kila mwezi bila kuzalisha kitu chochote.
mfano kwa sasa kila mmoja amepewa milioni 90 kwa ajili ya kununa gari la kifahari, wabunge hawa wapo zaidi ya 100 hivyo kufanya hela pekee waliyochota wao ni zaidi ya bilion 9 ambazo wanafunzi wa vyuo vikuu wanazidai wapatiwe BOOM la kumi elfu kila siku...
najua wanaonufahika na hivi viti hawatanielewa lakini huo ndio ukweli na sitajali ni mchungu au mtamu kiasi gani.

BAADA YA DOWANS JANGA LINGINE LA TAIFA NI VITI MAALUM
 
Tulishajadili hili swala hapa JF,search hiyo thread alianzisha Msando Alberto.....nakubaliana na wewe viti maalum ni mzigo kwa taifa ila vina umuhimu wake katika harakati za kumuinua mwanamke na kumfanya ashiriki katika maamuzi...tatizo lipo kwenye idadi na namna wanavyopatikana hao wabunge.....swali langu ni je hao wabunge wasio wa viti maalum wanafanya lipi la maana sana??? tuchukue mfano wa Halima Mdee akiwa bado viti maalum na Idd Azan akiwa mbunge wa kuchaguliwa wa Kinondoni??

Kuna haja ya kupunguza idadi na kurekebisha namna wanavyopatikana kikatiba,ila kwenye suala la kuzalisha chochote hata hao waliochaguliwa wengi ni useless tu.soma maoni yetu zaidi kwa hiyo thread ukiipata.....
 
Tulishajadili hili swala hapa JF,search hiyo thread alianzisha Msando Alberto.....nakubaliana na wewe viti maalum ni mzigo kwa taifa ila vina umuhimu wake katika harakati za kumuinua mwanamke na kumfanya ashiriki katika maamuzi...tatizo lipo kwenye idadi na namna wanavyopatikana hao wabunge.....swali langu ni je hao wabunge wasio wa viti maalum wanafanya lipi la maana sana??? tuchukue mfano wa Halima Mdee akiwa bado viti maalum na Idd Azan akiwa mbunge wa kuchaguliwa wa Kinondoni??

Kuna haja ya kupunguza idadi na kurekebisha namna wanavyopatikana kikatiba,ila kwenye suala la kuzalisha chochote hata hao waliochaguliwa wengi ni useless tu.soma maoni yetu zaidi kwa hiyo thread ukiipata.....

Maoni yangu viti maalumu viwepo tu ngazi ya madiwani tuu na halmashauri ziimarisha zifanye kazi zake kwa ufanisi kama yalivyo majimbo ya Marekani
 
Maoni yangu viti maalumu viwepo tu ngazi ya madiwani tuu na halmashauri ziimarisha zifanye kazi zake kwa ufanisi kama yalivyo majimbo ya Marekani

kwanini viwepo ngazi ya udiwani na halmashauri na si bunge na executive?? is it because ni wanawake walio kwa viti maalum?give us your reasons.....:A S 13:
 
Swala cio viti maalum tatizo ni ufanisi wa mbunge yoyote mi naona idadi ya wabunge ipungue 360 too much,chukulia wengine wapo kwa ajiri ya kuzomea wenzao kama majuha na wengine kazi kusinzia kama yule ko....ba
 
Back
Top Bottom