Ushauri: Uwekezaji katika maeneo ya kambi za Jeshi utazamwe kwa jicho la 3

Ushauri: Uwekezaji katika maeneo ya kambi za Jeshi utazamwe kwa jicho la 3

mwanamichakato

JF-Expert Member
Joined
Mar 20, 2015
Posts
1,188
Reaction score
1,090
Majeshi yetu ya Ulinzi na usalama ni vyombo nyeti mno katika mustakabali wa usalama wa nchi yetu (Kisiasa,Kiuchumi na Kijamii). Maeneo ya kambi za Jeshi ni maeneo adhimu na yanapaswa kutochangamana na maeneo ya kiraia kwa namna moja au nyingine.

Miaka michache iliopita tulipata janga la mabomu kulipuka ktk kambi kadhaa za jeshi na kusababisha maafa na utaabishaji mkubwa.Nadhani yatupasa kujifunza na kuepuka ukaribu na maeneo ya kiraia au kuchangamanisha maeneo haya na mambo ya biashara kwa ujumla.

Kwasasa kumekuwa na wimbi kubwa la wafanyabiashara kuwekeza maduka, yards,ofisi,kumbi, showrooms n.k. Inawezekana kabisa nia na lengo ni zuri (Kwa mujibu wa tathmini) kabisa ila kwa unyenyekevu mkubwa nadhani yatupasa kutazama kwa mapana athali zake kiusalama sasa na baadae.
 
Ni jambo la kushangaza na kusikitisha, kuona kambi ya jeshi inaruhusu kuzungukwa na fremu za biashara km ilivyo hapo Lugalo Baracks, nani ameruhusu jambo la namna hii?? Hivi kambi zingine zote nazo zinaruhusiwa kufanya hivi??? Sisi ni nchi ya namna gani tusioheshimu taratibu tulizojiwekea..kambi za jeshi zinapaswa kuwa mbali na makazi ya watu/raia..kwa maana hii kambi ya Lugalo haina sifa kubaki kuwa kambi ya jeshi, serikali ibadilishe kambi hii itumike kwa mambo mengine km chuo nk na wanajeshi wa kambi hiyo wahamishwe kupelekwa kambi nyingine.
 
Ni jambo la kushangaza na kusikitisha, kuona kambi ya jeshi inaruhusu kuzungukwa na fremu za biashara km ilivyo hapo Lugalo Baracks, nani ameruhusu jambo la namna hii?? Hivi kambi zingine zote nazo zinaruhusiwa kufanya hivi??? Sisi ni nchi ya namna gani tusioheshimu taratibu tulizojiwekea..kambi za jeshi zinapaswa kuwa mbali na makazi ya watu/raia..kwa maana hii kambi ya Lugalo haina sifa kubaki kuwa kambi ya jeshi, serikali ibadilishe kambi hii itumike kwa mambo mengine km chuo nk na wanajeshi wa kambi hiyo wahamishwe kupelekwa kambi nyingine.
Lakini hapo Lugalo pia kunauwekezaji wa hospitali pia mbona hatupingi?
 
Miaka michache iliopita tulipata janga la mabomu kulipuka ktk kambi kadhaa za jeshi na kusababisha maafa na utaabishaji mkubwa.

Kwasasa kumekuwa na wimbi kubwa la wafanyabiashara kuwekeza maduka, yards, showrooms n.k. Inawezekana nia na lengo ni zuri kabisa ila nadhani yatupasa kutazama kwa mapana athali zake kiusalama sasa na baadae.
Kwa kuongezea

Ipo siku Mr. Slim atapenyezea watu wake humohumo kuja kusoma mwenendo wa majeshi yetu kisha awatume M23 watusumbue
 
Jeshi limeamua kusaidia biashara ya mafremu kuuza hasa bidhaa za Kichina. Wenzetu kama Misri jeshi lina makampuni ya ujenzi, makampuni ya kufua umeme, viwanda vya chuma na viwanda vya bidhaa za kijeshi kama armoured vehicles na ammunition. Sisi tumeamua mafremu yauze chupi na juisi za ukwaju.

Jeshi lina mainjinia kibao humo wangeanzisha research facilities wakasaidia vitu kadhaa kwenye uchumi. Mfano haya magari na bajaj za gesi. Tatizo serikali haitaki miradi ya maendeo na utafiti, kazi bajeti ya matumizi ya kawaida.
 
Ni jambo la kushangaza na kusikitisha, kuona kambi ya jeshi inaruhusu kuzungukwa na fremu za biashara km ilivyo hapo Lugalo Baracks, nani ameruhusu jambo la namna hii?? Hivi kambi zingine zote nazo zinaruhusiwa kufanya hivi??? Sisi ni nchi ya namna gani tusioheshimu taratibu tulizojiwekea..kambi za jeshi zinapaswa kuwa mbali na makazi ya watu/raia..kwa maana hii kambi ya Lugalo haina sifa kubaki kuwa kambi ya jeshi, serikali ibadilishe kambi hii itumike kwa mambo mengine km chuo nk na wanajeshi wa kambi hiyo wahamishwe kupelekwa kambi nyingine.
Lugalo ipo hapo miaka dahari Mkuu, na mpaka watu wapo hapo maana yake wameshafanya CBA kama kuna risk jeshi huwa ni amri wanatolewa mara moja.
 
Una hoja,mabibo external kama unaenda kisukuru ile ni ujuha,tatizo wanajeshi wajuaji ukiwashayri kitu wanakuona mjinga eti sio Profession yetu
 
Back
Top Bottom