Ushauri wa Bure kwa Dkt. Hussein Mwinyi: Mfute Kazi Haraka Othman Masoud Kabla Hajaendelea Kueneza Sumu

Ushauri wa Bure kwa Dkt. Hussein Mwinyi: Mfute Kazi Haraka Othman Masoud Kabla Hajaendelea Kueneza Sumu

Juzi juzi Kiongozi wa huko visiwani imebidi atolee maelezo/ ufafanuzi tuhuma za yule Mzee wa chama aliyepigwa kidogo auwawe.

Kama sio hizo kelele za huyo Mzee wananchi wangejuaje mambo ya kandarasi, viwanja na tuhuma zingine alizozisema?
 
Tatizo GNU yenyewe Ni mkataba wa kimaslahi binafsi. Ni mpango wa CCM kuendelea kuungata upinzani au fikra pinzani kwa style ya panya "kungata na kupuliza".

Gnu haijibu hoja na haja za wazanzibari, Ni mpango tu wa political giant-figures kupeana ulaji.


Mpinzani wa kweli hawezi kuamini katika mfumo huu wa GNU usio address true grievances za watu bali kugawana madaraka viongozi.
 
Ingalikuwa kipindi cha Mwalimu Nyerere huyu bwana angalipata tabu Sana kwa kosa kubwa la kuvunja muungano ulio jengwa kwa gharama kubwa!
 
Wanabodi,

Politics is a game like any other games, that people plays, it has its rules and regulations, ukikiuka unaweka pembeni. Yaani mchezo wa siasa pia ni mchezo kama mchezo mwingine wowote, una sheria zake, taratibu na kanuni, ukikiuka, unapewa kadi nyekundu unawekwa pembeni.

Serikali ya Zanzibar, ni serikali ya mseto, inaendeshwa na vyama viwili, CCM na ACT, ila watu wa ACT ndani ya GNU wanapaswa kutekeleza sera za CCM.

Serikali ya GNU japo ni serikali ya mseto, lakini inaongozwa na Ilani ya uchaguzi ya CCM, hivyo ACT ndani ya GNU ama wanatakiwa kuhubiri ilani ya uchaguzi ya CCM, na sera za CCM ama wanyamaze kimya, halafu wale ACT wengine nje ya GNU ndio wanaweza kuendelea kupiga siasa za ilani ya ACT!.

Ndani ya Serikali, kuna kitu kinaitwa a collective responsibilities, ukiishakuwa ndani ya serikali, huwezi kusema jambo lolote ambalo ni kinyume cha sera na ilani inayotawala ukabaki salama.

Maalim Seif alipokuwa ndani ya GNU, alinyamaza, hivyo Masoud Othman Masoud ama naye anyamaze, ama atoke nje ndio akaendelee kuhubiri kuuvunja huu muungano wetu adhimu!

Mtu aliyemo ndani ya serikali, hawezi kuyasema maneno kama haya

Kwa maoni yangu, huyu mtu anatakiwa awekwe pembeni, apate muda wa kutosha ajishughulishe na siasa, kwasababu ACT ndani ya GNU wanatakiwa kutekeleza Ilani na sera za CCM!

Ushauri kama huu kumhusu mtu huyu huyu niliwahi kuutoa kule nyuma na ukatekelezwa, Dr. Shein Mfute Kazi Haraka, Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Kabla Hajamwaga Sumu Hii

Hili la kila uchao mtu huyu kuuchokoa muungano hakuanza leo, na hakuna ubaya wowote kuuzungumzia muungano kwa jambo lolote alimradi hilo linalozungumzwa ni liwe la ukweli kuna siku aliongopa kuhusu sovereignity Kuhusu Muungano, Makamo wa Kwanza wa Zanzibar, Adai ni Zanzibar Pekee iliyopoteza Sovereignty, Je Yuko Sahihi?

Hata Mama Samia akiwa VP aliwahi kushauri watu waachwe wa vent kuhusu muungano "Watu waachwe Huru kuujadili Muungano"- VP, Samia Suluhu Hassan. Huyu mama anaongea vizuri kwa Unyenyekevu mpaka raha. Huchoki kumsikiliza

Kama watu waachwe huru kuujadili muungano ndiko huku kunakofanywa na huyu, na kunajumuisha kuwa huru kuujadili muungano negatively hara Kwa mtu uliye ndani ya GNU, then I doubt kama huku ni kuujadili muungano kwa nia ya kuuimarisha bali ni kuujadili muungano kwa nia ya kuuvunja.

Paskali
Naunga mkono hoja, OMO ni mnafiki kwanza shavu zake zimejaa kuonesha karidhika ila kuna kitu anataka zaidi. Badala ya kuongelea issue za maendeleo yeye anataka kulete fujo.
 
Kwani kuwa makamu wa kwanza wa Rais Zenji, inaondoa uanachama wa mtu kutoka chama cha upinzani iwe CUF, ACT nk?

Wanabodi,

Politics is a game like any other games, that people plays, it has its rules and regulations, ukikiuka unaweka pembeni. Yaani mchezo wa siasa pia ni mchezo kama mchezo mwingine wowote, una sheria zake, taratibu na kanuni, ukikiuka, unapewa kadi nyekundu unawekwa pembeni.

Serikali ya Zanzibar, ni serikali ya mseto, inaendeshwa na vyama viwili, CCM na ACT, ila watu wa ACT ndani ya GNU wanapaswa kutekeleza sera za CCM.

Serikali ya GNU japo ni serikali ya mseto, lakini inaongozwa na Ilani ya uchaguzi ya CCM, hivyo ACT ndani ya GNU ama wanatakiwa kuhubiri ilani ya uchaguzi ya CCM, na sera za CCM ama wanyamaze kimya, halafu wale ACT wengine nje ya GNU ndio wanaweza kuendelea kupiga siasa za ilani ya ACT!.

Ndani ya Serikali, kuna kitu kinaitwa a collective responsibilities, ukiishakuwa ndani ya serikali, huwezi kusema jambo lolote ambalo ni kinyume cha sera na ilani inayotawala ukabaki salama.

Maalim Seif alipokuwa ndani ya GNU, alinyamaza, hivyo Masoud Othman Masoud ama naye anyamaze, ama atoke nje ndio akaendelee kuhubiri kuuvunja huu muungano wetu adhimu!

Mtu aliyemo ndani ya serikali, hawezi kuyasema maneno kama haya

Kwa maoni yangu, huyu mtu anatakiwa awekwe pembeni, apate muda wa kutosha ajishughulishe na siasa, kwasababu ACT ndani ya GNU wanatakiwa kutekeleza Ilani na sera za CCM!

Ushauri kama huu kumhusu mtu huyu huyu niliwahi kuutoa kule nyuma na ukatekelezwa, Dr. Shein Mfute Kazi Haraka, Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Kabla Hajamwaga Sumu Hii

Hili la kila uchao mtu huyu kuuchokoa muungano hakuanza leo, na hakuna ubaya wowote kuuzungumzia muungano kwa jambo lolote alimradi hilo linalozungumzwa ni liwe la ukweli kuna siku aliongopa kuhusu sovereignity Kuhusu Muungano, Makamo wa Kwanza wa Zanzibar, Adai ni Zanzibar Pekee iliyopoteza Sovereignty, Je Yuko Sahihi?

Hata Mama Samia akiwa VP aliwahi kushauri watu waachwe wa vent kuhusu muungano "Watu waachwe Huru kuujadili Muungano"- VP, Samia Suluhu Hassan. Huyu mama anaongea vizuri kwa Unyenyekevu mpaka raha. Huchoki kumsikiliza

Kama watu waachwe huru kuujadili muungano ndiko huku kunakofanywa na huyu, na kunajumuisha kuwa huru kuujadili muungano negatively hara Kwa mtu uliye ndani ya GNU, then I doubt kama huku ni kuujadili muungano kwa nia ya kuuimarisha bali ni kuujadili muungano kwa nia ya kuuvunja.

Paskali
Walipokubali kuwaunganisha wapinzani walitakiwa kuwa na makubaliano kuhusu watakavotawala na hayo yalitakiwa kuwa na msingi ktk katiba na sheria zao iloruhusu kuwepo kwao. Kama kitu hicho hakipo, ni balaa nyngne. Unakuwa mpinzan unapotofautiana chama tawala. Kuingizwa madarakani haikumanisha umeacha upinzan na ikiwa katiba au sheria zao zinalazmisha hayo, ndo mapungufu yenyewe. Iltakiwe pawepo hicho kipengere ktachotatua masuala yenye utata ktk utawala wa nchi. Suala la collective responsibility ni pale tu mnapokua timu moja na ktokana na ktofautiana kimawazo concensus inapatkana kw kura. Lkn pia inajulkana kuwa sio kila wkt majority wako right ndo sbb ktk masuala makuu kuna knachoitwa minority opinion. Wajue kuwa wapinzani wapo kw sbb hawakuridhika na hizo sera za CCM. Hayo mambo ya collective responsibility ni huku kwetu, otherwise hiyo Ktb itawaletea mattzo, ipitiwe upya
 
Huu ni uchawa,mbna Ruto anampinga Kenyatta ktk baadhi ya mambo???hii nchi itachelewa sana kuendelea
Mkuu Ngali, Ngalikihinja, kwanza naomba kujitanabaisha kuwa mimi ni miongoni mwa watetezi wakuu wa freedom of expression, hivyo ushauri huu usitafasiriwe kuwa ni kuingilia freedom of expression ya OMO, no!.
Kuna baadhi ya nafasi za juu za uongozi kwenye ngazi za maamuzi, kiongozi huwezi kutoa maoni kinzani.

Uongozi wa serikali ni kama ndoa, wana ndoa wanafungwa na kanuni ya a collective responsibility. Hata ikitokea wanandoa wamehitilafiana, watoto hawapaswi kujua, au ikitokea mzee ni hakuna kitu, mama hawezi kutangaza public na kusema no anatoa maoni yake.

Wabunge wa ACT walio ndani ya serikali ya GNU ya Zanzibar, ni wanatekeleza ilani ya uchaguzi ya CCM yenye lengo la kuimarisha muungano.

Hivyo viongozi wote wa GNU wanabanwa na kanuni ya a collective responsibility kudumisha muungano

Hapa ukinipa mifano, nitakushukuru. A collective responsibility inataka kama hukubaliani, unanyamaza kimya, na ukiamua kuongea, ondoka kwanza ndani ya serikali ndipo upinge.

Hapana, tunataka viongozi waadilifu, maadam umekubali kuingia kwenye ndoa, ni lazima utimize masherti ya ndoa ikiwemo kutimiza wajibu wa ndoa.
P.
 
Pascal nadhan una hoja ya msingi..Mimi sielewi kwa wanaotaka kuuvunja muungano wanawafikiriaje wazanzibar wanaoishi bara, ambao wameolewa, wanafanya kazi, wanalima, wanafanya biashara kubwakubwa....wanawafikiraje...????hivi wanajua maana ya kutengana..kutengana hakuna mswalie mtume shekh.....watu nahisi wamechoka amani...
Wale hawataki kujitenga, wanataka cha zaidi. Sisi Watanganyika, ajira za Muungano ndio hizo hizo za Tanganyika, Ardhi ya Muungano ndio hiyo hiyo ya Tanganyika. Wao wana ardhi ya Zanzibar na ardhi ya Tanganyika. Wao kuna ajira za Muungano na Ajira za Zanzibar. Sisi siasa za Muungano ndio hizo hizo za Tanganyika. Wao wana siasa(uongozi na manufaa yake yote) za Zanzibar na za Muungano.
 
Hv mwanamke kama hakutaki kwann ulazimishe penzi?????
Wale hawataki kujitenga, wanataka cha zaidi. Sisi Watanganyika, ajira za Muungano ndio hizo hizo za Tanganyika, Ardhi ya Muungano ndio hiyo hiyo ya Tanganyika. Wao wana ardhi ya Zanzibar na ardhi ya Tanganyika. Wao kuna ajira za Muungano na Ajira za Zanzibar. Sisi siasa za Muungano ndio hizo hizo za Tanganyika. Wao wana siasa(uongozi na manufaa yake yote) za Zanzibar na za Muungano.
 
Nakubaliana kabisa.

Anti Muungano agents wang'olewe at any cost.

Huyo Othman akayaongee anayo ongea akiwa nje ya serikali.

Jitu linakula heka ya Muunano halafu linaunanga, ni ushamba usiovumilika.
Mada ingekuwa Othman ajiuzulu au atakiwe kujiuzulu (kauli ya kumfukuza au kumfuta kazi haina staha and is not politically correct). Huwezi kuwa tofauti na msimamo mkubwa wa serikali katika suala zito kama la muungano halafu ukaendelea kuitumikia serikali hiyo hiyo.

Uhuru wa kuongea anao; hawezi kunyang’anywa. Lakini haikubaliki kuupinga muungano huu jinsi ulivyo ukiwa ndani ya ajira ya serikali ya CCM. Kwanza, mantiki ya kawaida kabisa inadai asingekubali nafasi hiyo ya kazi kabla ya kutoa sharti la marekebisho ya muungano kuwa ajenda muhimu ya SMZ.

Kibatala alipoulizwa kama akiteuliwa kuwa AG atakubali? Alijibu itabidi kwanza marekebisho makubwa yafanyike katika mfumo mzima wa eneo hilo ndipo akubali. Nje ya hapo ni out of question.
 
Back
Top Bottom