Ushauri wa bure kwa mchezaji Feisal Salum baada ya mchezo wa marudio kati ya Taifa Stars na Uganda The Cranes

Ushauri wa bure kwa mchezaji Feisal Salum baada ya mchezo wa marudio kati ya Taifa Stars na Uganda The Cranes

Tate Mkuu

JF-Expert Member
Joined
Jan 24, 2019
Posts
33,092
Reaction score
96,127
Kwanza nichukue nafasi hii kuipongeza timu yetu ya Tanzania (Taifa Stars) kwa kupata ushindi wa goli 1-0 dhidi ya wapinzani wao wa jadi Uganda. Hakika ushindi wa leo, umefufua matumaini ya kufuzu AFCON kwa mara nyingine tena.

Nije sasa kwa mchezaji Feisal Salum (Fei Toto). Kwanza nampongeza kuitwa kwenye timu ya Taifa, huku akiwa hata hajulikani alipo kwa takribani miezi 3 sasa, kwa kweli anatakiwa ajione kama mtu aliyepewa heshima kubwa ambayo hata hakustahili!

Maana kuna wenzake wengi tu wameachwa huku wakiwa wamefanya vizuri kwenye vilabu vyao, tofauti na yeye ambaye mpaka sasa klabu yake ya Yanga inamtambua kama mchezaji mtoro!

Ushauri wangu kwake nikiwa kama mdau wa michezo, mara tu baada ya hiyo mechi ya marudio kumalizika; namshauri aitishe mkutano na vyombo vya habari. Halafu ajitokeze hadharani kuomba radhi kwa klabu yake ya Yanga, wanachama, mashabiki, na wadau wote wa mpira wa miguu kwa sintofahamu iliyojotokeza, ili maisha yaendelee.

Kama msamaha ukipokelewa, arudi kwenye kikosi, na kucheza kwa bidii mpaka mkataba wake utakapokwisha hapo mwakani na kama ataona kuna umuhimu wa kuongeza, ataongeza, kama ataona anahijitaji changamoto mpya, basi ataondoka kwa heshima kama free agent.

Angalizo; Iwapo hiyo mechi ya marudio itapita, halafu dogo atapotelea tena mafichoni, basi nitamuona kama ni kijana ambaye siyo muungwana, mkaidi, na asiye na busara, na nitashangaa sana kama TFF watamuita kwa mara nyingine tena mchezaji asiye na timu, asiyejitambua, na aliyekosa nidhamu kama Fei Toto.

Huyu mtoto anatakiwa kutambua ya kwamba, maisha yake kwa sasa yanategemea mpira. Hivyo kama mpira kwa upande wake ni kazi, basi anatakiwa pia auheshimu, na aweke pembeni mahaba yake na timu nyingine.

Ajifunze kwa maelfu ya wafanyakazi nchini na duniani kwa ujumla, ambao wanafanya kazi mbalimbali kwa moyo huku baadhi yao wakiwa hawana hata mahaba na hizo kazi. Maana kinacho angaliwa ni ule mshahara ambao mfanyakazi akiupata, anautumia kwenye mahitaji yake ya kila siku na wala siyo mahaba na hiyo kazi.
 
Nakazia..
Japo sijui mlimfanya nini huyu kijana yani hataki hata kuwasikia..ni kama kuna kitu kilifanyika ambacho kwake ni ngumu kusamehe...au unasemaje Tate Mkuu
Yaani hana namna. Anatakiwa avumilie. Mwakani hata siyo mbali. Ataondoka akiwa ni mchezaji huru. Sina uhakika kama ataitwa yena kwenye timu ya Taifa, iwapo tu ataendelea na huu msimamo wake.

Lakini pia naamini kwa wakati huu huko kambini, atapata ushauri wa kila aina kutoka kwa wachezaji wenzake waliomzidi kila kitu.

Binafsi namuombea agundue ya kwamba njia aliyochagua kwa sasa, siyo sahihi.
 
Me Mwana yanga lakini binafsi navomuona kijana ni muungwana sana sema najaribu kufikiria yaweza kua yanga walimvuruga sana kijana pengne maelewano Yao hayakua kama talivo sasa had kuleta mtafaruku yeye akazie nyaya hapohapo.

Kwani ajira ni moja tu, timu ni moja tu.
Ikatokea ameomba msamaha napenyewe mtazungumza kua na mpumbavu huyu kijana.

Bora akaze hapohapo.
 
Mimi nadhani yule aliyempa dogo zile hela ndiye Mafia namba moja.
Kama kuna mtu alimpa Feisal zile pesa basi yule ndio muungwana

Alikuja kuwakumbusha Yanga kuhusu thamani ya mchezaji na namna wanavyochezea shilingi chooni

Mwanzo Yanga waliamini pesa ndio kikwazo cha kumpelekesha Feisal watakavyo, pengine walijua hawezi kuwa na uwezo wa kumudu kulipa kiwango kile na ndio maana hata alipowafata kuhusu kuboreshewa maslahi walimpuuza.

Since ile pesa imerudishwa kuna kitu wamejifunza hata kama sio kwa Feisal badi kwa wachezaji wengine waliobakia watakuwa makini
 
Career ya football kwa mchezaji ni fupi sana...Mchezaji asiposimama kidete kudai stahiki zake basi ajue kuwa muda wake wa kustaafu ukifika ajue hana chake na hatathaminiwa tena tofauti na mwajiriwa wa serikali ambaye muda wake wa kustaafu ni miaka 55.Mchezaji mpira hustaafu akiwa na miaka 35 tu. Mfanyakazi wa serikali baada ya kustaatu ana uhakika wa kupata kiinua mgongo na pensheni zake tofauti na mchezaji mpira ambae akimaliza muda wake hapewi hata thumni.

Namsapoti Fei toto aendelee kusimama na msimamo wake huohuo. Wanayanga wanataka waje kukucheka pindi utakapokuwa unauza urojo pale Forodhani waseme kuwa ulifuja pesa ilihali ulikuwa unalishwa ugali kwa sukari
 
Acha akaendelee kuvua huko, kama anadhani kila siku ataitwa national team bila kucheza.

Hakuna mchezaji huwa anavunja mkataba kienyeji enyeji hivyo hasa wa mpira na tofautisha nakazi zingine bold Mpira
National team wachezaji wengi hawaipi uzito

Hata humu kulikuwa kuna mijadala kwanini Samatta haonekani kujituma akiwa national team wakati akiwa kwenye Club yake anacheza kwa intensity kubwa

Watu wengi wali suggest kuwa anafanya hivyo kukwepa injuries ambazo zitamfanya akae kando kwa muda asiweze kucheza kwenye Club yake ambayo inamlipa mtonyo mrefu kuliko kile anachokipata kwenye National team

Hata leo wengi wameshangazwa na performance ya Taifa stars kuwa ya juu, wengi wameihusisha kutokana na ile ahadi ya pesa walioahidiwa.
 
Kama kuna mtu alimpa Feisal zile pesa basi yule ndio muungwana

Alikuja kuwakumbusha Yanga kuhusu thamani ya mchezaji na namna wanavyochezea shilingi chooni

Mwanzo Yanga waliamini pesa ndio kikwazo cha kumpelekesha Feisal watakavyo, pengine walijua hawezi kuwa na uwezo wa kumudu kulipa kiwango kile na ndio maana hata alipowafata kuhusu kuboreshewa maslahi walimpuuza.

Since ile pesa imerudishwa kuna kitu wamejifunza hata kama sio kwa Feisal badi kwa wachezaji wengine waliobakia watakuwa makini
Uko sahihi kabisa. Kama viongozi wa Yanga nao walikiwa wanamdhulumu bwana mdogo, watakuwa nao wamepata funzo.

All in all, bado wadau wengi wa michezo tulitamani kuuona mwisho mwema wa huyu kijana.
 
Back
Top Bottom