Ushauri wa bure kwa mchezaji Feisal Salum baada ya mchezo wa marudio kati ya Taifa Stars na Uganda The Cranes

Ushauri wa bure kwa mchezaji Feisal Salum baada ya mchezo wa marudio kati ya Taifa Stars na Uganda The Cranes

Kijana ana msimo wa hovyo, katika maisha flexibility ni muhimu sana. Angekuwa na akili sawa sawa baada ya hukumu tu angerudi aeleze tu kuwa alitafsiri mkataba vibaya, mambo yangeisha na angeondoka Yanga kama mchezaji huru na hapo ndipo angepiga hela ya maana. Wachezaji wengi wakubwa tunao waona kwenye TV decision making katika masuala yao inafanywa na majopo ya wabobezi katika masuala ya biashara, mpira, sheria, afya etc. Feisal nina wasiwasi uamuzi wake kashauriwa na mama yake na wachambuzi uchwara.
Dogo anazingua. Mbaya zaidi mama yake naye siyo msaada kwake. Maana hata yale mahojiano yake alijikita zaidi kwenye kuongelea mabaya, kana kwamba mtoto wake hakuwahi kutendewa wema wa aina yoyote ile na Yanga; jambo ambalo siyo sahihi hata kidogo.
 
Amekaririwa akisema huko unguja..kwamba akirudi yanga na afe..yanga kuna kitu wamemkwaza huyu kijana
Kama kingekuwepo, Yanga wangemkubalia kwa urahisi hilo ombi lake la kutaka kuondoka. Inawezekana hasira zake zote zimetokana na kukoda hilo dau alilo ahidiwa na hiyo timu iliyokuwa ikimtaka.

Na kwa bahati mbaya, alishindwa kutafsiri mkataba wake, na sasa ameamua kuchagua maisha ya popo! Anatambulika kama mchezaji wa Yanga, na wakati ukweli hauko hivyo.

Wakati mwingine nitashangaa sana kama ataitwa tena kwenye timu ya Taifa, na kutambulika kama mchezaji wa Yanga, asiyo ichezea kwa sababu zake binafsi.
 
Muda si mrefu ataikumbuka hata ile M4 aliyokuwa analipwa! Kwa kiwango kile cha jana hata Namungo hapati namba!
 
Kwani kafanya kosa gani?
Kwa mtazamo wangu, na kwa umri na akili zake; naona kosa lake kubwa ni utoto.

Hivyo kuomba radhi hadharani, ni uungwana kwa mchezaji wa kiwango chake. Na uzuri akifanya hivyo, hatapungukiwa na chochote.
 
Dogo anazingua. Mbaya zaidi mama yake naye siyo msaada kwake. Maana hata yale mahojiano yake alijikita zaidi kwenye kuongelea mabaya, kana kwamba mtoto wake hakuwahi kutendewa wema wa aina yoyote ile na Yanga; jambo ambalo siyo sahihi hata kidogo.
Sisi waswahili professionalism huwa tunaweka pembeni katika masuala mengi tu ya Msingi. Michezo inahitaji sana nidhamu pengine kushinda nyanja nyingine kwasababu jambo dogo linalo onekana la kawaida linaweza kumpotezea mwekekeo mchezaji. Kwa hiyo ukisha tanguliza mambo ya kiswahili huwezi fika popote. Angalia Samata ambaye ndiye icon ya mpira wetu kwa sasa, ana nidhamu ya hali ya juu nje na ndani ya uwanjani toka yupo Simba. Asingekuwa na nidhamu angeishia tu TP Mazembe.
 
Muda si mrefu ataikumbuka hata ile M4 aliyokuwa analipwa! Kwa kiwango kile cha jana hata Namungo hapati namba!
Uko sahihi kabisa. Jana alikuwa ni yule Fei Toto wa JKU! Athari za kutokuwepo klabuni na wenzake, zimeshaanza kumuathiri. Bila shaka itamchukua muda kurejea kwenye kiwango chake cha awali.
 
Na thamani yake inapotea slowly..!!! Jana kwanza utadhani hakuwepo uwanjani.
Nina uhakika angekuwa ametokea kwenye klabu yake, angeanza kwenye kikosi cha kwanza. Ila ndiyo hivyo tena, hata alipopewa nafasi, hakuwa Fei yule tuliyemzoea.
 
Sisi waswahili professionalism huwa tunaweka pembeni katika masuala mengi tu ya Msingi. Michezo inahitaji sana nidhamu pengine kushinda nyanja nyingine kwasababu jambo dogo linalo onekana la kawaida linaweza kumpotezea mwekekeo mchezaji. Kwa hiyo ukisha tanguliza mambo ya kiswahili huwezi fika popote. Angalia Samata ambaye ndiye icon ya mpira wetu kwa sasa, ana nidhamu ya hali ya juu nje na ndani ya uwanjani toka yupo Simba. Asingekuwa na nidhamu angeishia tu TP Mazembe.
Nakumbuka Samatta kuondoka Mazembe haikua rahisi Katumbi alikataa kumuachia ikabidi avumilie mkataba uishe aondoke bure baadae waka zungumza biashara ikafanyika
 
Ulichosema ni kweli kuna mda inabidi ujishushe ila mambo yaende,umemaliza kila kitu
 
Uko sahihi kabisa. Jana alikuwa ni yule Fei Toto wa JKU! Athari za kutokuwepo klabuni na wenzake, zimeshaanza kumuathiri. Bila shaka itamchukua muda kurejea kwenye kiwango chake cha awali.
Kwanza hapo ashukuru kuitwa. Ningekuwa mimi kocha🤣 angeangalia wenzie kwenye TV
 
Kuomba radhi ni kitendo tu cha uungwana, ili wakati fulani kupisha mambo mengine yaendelee. Na wala hakuna uhusiano na kuabudiwa.
Kwa nini mnakesha mkiomba aje kuwaomba radhi kwani amekiri kuwakosea? Acheni mambo zenu.
 
Ungekuwa umeajiriwa, ungeielewa kwa haraka sana mantiki yangu.
Kwani kawaambia anaishi kwa shida? Mnatumia geresha ya kumuonea huruma wakati yeye hana hata habari na nyie. Kama mnamuonea huruma, ongezeni mshahara wake maana ameshawaambia ana majukumu mengi ya kifamilia na mshahara mnaomlipa hautoshi. Kama hamuwezi, kaeni kimya.
 
Kwanza nichukue nafasi hii kuipongeza timu yetu ya Tanzania (Taifa Stars) kwa kupata ushindi wa goli 1-0 dhidi ya wapinzani wao wa jadi Uganda. Hakika ushindi wa leo, umefufua matumaini ya kufuzu AFCON kwa mara nyingine tena.

Nije sasa kwa mchezaji Feisal Salum (Fei Toto). Kwanza nampongeza kuitwa kwenye timu ya Taifa, huku akiwa hata hajulikani alipo kwa takribani miezi 3 sasa, kwa kweli anatakiwa ajione kama mtu aliyepewa heshima kubwa ambayo hata hakustahili!

Maana kuna wenzake wengi tu wameachwa huku wakiwa wamefanya vizuri kwenye vilabu vyao, tofauti na yeye ambaye mpaka sasa klabu yake ya Yanga inamtambua kama mchezaji mtoro!

Ushauri wangu kwake nikiwa kama mdau wa michezo, mara tu baada ya hiyo mechi ya marudio kumalizika; namshauri aitishe mkutano na vyombo vya habari. Halafu ajitokeze hadharani kuomba radhi kwa klabu yake ya Yanga, wanachama, mashabiki, na wadau wote wa mpira wa miguu kwa sintofahamu iliyojotokeza, ili maisha yaendelee.

Kama msamaha ukipokelewa, arudi kwenye kikosi, na kucheza kwa bidii mpaka mkataba wake utakapokwisha hapo mwakani na kama ataona kuna umuhimu wa kuongeza, ataongeza, kama ataona anahijitaji changamoto mpya, basi ataondoka kwa heshima kama free agent.

Angalizo; Iwapo hiyo mechi ya marudio itapita, halafu dogo atapotelea tena mafichoni, basi nitamuona kama ni kijana ambaye siyo muungwana, mkaidi, na asiye na busara, na nitashangaa sana kama TFF watamuita kwa mara nyingine tena mchezaji asiye na timu, asiyejitambua, na aliyekosa nidhamu kama Fei Toto.

Huyu mtoto anatakiwa kutambua ya kwamba, maisha yake kwa sasa yanategemea mpira. Hivyo kama mpira kwa upande wake ni kazi, basi anatakiwa pia auheshimu, na aweke pembeni mahaba yake na timu nyingine.

Ajifunze kwa maelfu ya wafanyakazi nchini na duniani kwa ujumla, ambao wanafanya kazi mbalimbali kwa moyo huku baadhi yao wakiwa hawana hata mahaba na hizo kazi. Maana kinacho angaliwa ni ule mshahara ambao mfanyakazi akiupata, anautumia kwenye mahitaji yake ya kila siku na wala siyo mahaba na hiyo kazi.
kukubali kuichezea taifa stars jana kwa kutambulika kama mchezaji wa yanga amedhihirisha kwamba dogo hajitambui,ni dhahiri kabisa vishawishi vyenye nguvu ya pesa ndivyo vilivyomfanya awasingizie yanga mambo ya kipuuzi ili jamii imuone anaonewa aondoke kirahisi ni kama vile alivyofanya demu wa greenwood...SHAME ON HIM
 
Back
Top Bottom