Ushauri wa bure kwa mchezaji Feisal Salum baada ya mchezo wa marudio kati ya Taifa Stars na Uganda The Cranes

Ushauri wa bure kwa mchezaji Feisal Salum baada ya mchezo wa marudio kati ya Taifa Stars na Uganda The Cranes

Kwanza nichukue nafasi hii kuipongeza timu yetu ya Tanzania (Taifa Stars) kwa kupata ushindi wa goli 1-0 dhidi ya wapinzani wao wa jadi Uganda. Hakika ushindi wa leo, umefufua matumaini ya kufuzu AFCON kwa mara nyingine tena.

Nije sasa kwa mchezaji Feisal Salum (Fei Toto). Kwanza nampongeza kuitwa kwenye timu ya Taifa, huku akiwa hata hajulikani alipo kwa takribani miezi 3 sasa! Na kwa kweli anatakiwa ajione kama mtu aliyepewa heshima kubwa ambayo hata hakustahili! Maana kuna wenzake wengi tu wameachwa huku wakiwa wamefanya vizuri kwenye vilabu vyao, tofauti na yeye ambaye mpaka sasa klabu yake ya Yanga inamtambua kama mchezaji mtoro!

Ushauri wangu kwake nikiwa kama mdau wa michezo, mara tu baada ya hiyo mechi ya marudio kumalizika; namshauri aitishe mkutano na vyombo vya habari. Halafu ajitokeze hadharani kuomba radhi kwa klabu yake ya Yanga, wanachama, mashabiki, na wadau wote wa mpira wa miguu kwa sintofahamu iliyojotokeza, ili maisha yaendelee.
Na msamaha ukipokelewa, arudi kwenye kikosi , na kucheza kwa bidii mpaka mkataba wake utakapokwisha hapo mwakani. Na kama ataona kuna umuhimu wa kuongeza, ataongeza. Na kama ataona anahijitaji changamoto mpya, basi ataondoka kwa heshima kama free agent.

Angalizo; Iwapo hiyo mechi ya marudio itapita, halafu dogo atapotelea tena mafichoni! Basi nitamuona kama ni kijana ambaye siyo muungwana, mkaidi, na asiye na busara. Na nitashangaa sana kama TFF watamuita kwa mara nyingine tena mchezaji asiye na timu! asiyejitambua, na aliyekosa nidhamu kama Fei Toto.

Na huyu mtoto anatakiwa kutambua ya kwamba, maisha yake kwa sasa yanategemea mpira. Hivyo kama mpira kwa upande wake ni kazi, basi anatakiwa pia auheshimu, na aweke pembeni mahaba yake na timu nyingine.

Ajifunze kwa maelfu ya wafanyakazi nchini na duniani kwa ujumla, ambao wanafanya kazi mbalimbali kwa moyo huku baadhi yao wakiwa hawana hata mahaba na hizo kazi. Maana kinacho angaliwa ni ule mshahara ambao mfanyakazi akiupata, anautumia kwenye mahitaji yake ya kila siku. Na wala siyo mahaba na hiyo kazi.
Yanga mnapenda sana kuabudiwa
 
Kijana ana msimo wa hovyo, katika maisha flexibility ni muhimu sana. Angekuwa na akili sawa sawa baada ya hukumu tu angerudi aeleze tu kuwa alitafsiri mkataba vibaya, mambo yangeisha na angeondoka Yanga kama mchezaji huru na hapo ndipo angepiga hela ya maana. Wachezaji wengi wakubwa tunao waona kwenye TV decision making katika masuala yao inafanywa na majopo ya wabobezi katika masuala ya biashara, mpira, sheria, afya etc. Feisal nina wasiwasi uamuzi wake kashauriwa na mama yake na wachambuzi uchwara.
 
Yaani hana namna. Anatakiwa avumilie. Mwakani hata siyo mbali. Ataondoka akiwa ni mchezaji huru. Sina uhakika kama ataitwa yena kwenye timu ya Taifa, iwapo tu ataendelea na huu msimamo wake.

Lakini pia naamini kwa wakati huu huko kambini, atapata ushauri wa kila aina kutoka kwa wachezaji wenzake waliomzidi kila kitu.

Binafsi namuombea agundue ya kwamba njia aliyochagua kwa sasa, siyo sahihi.
huko timu ya taifa hakuna faida yoyote hata asipokwenda ni sawa..
 
Nakazia..
Japo sijui mlimfanya nini huyu kijana yani hataki hata kuwasikia..ni kama kuna kitu kilifanyika ambacho kwake ni ngumu kusamehe...au unasemaje Tate Mkuu
SHIDA NI ILE PESA ALIYOPEWA WAKATI ANASHAWISHIWA KUVUNJA MKATABA...AMEKULA IMEISHA..KURUDISHA NI NGUMU...Hapo chacha...huyo aliyemdanganya hatomsahau daima...

Feisal was the greatest Tanzanian player...from nowhere...from HERO to ZERO...
 
Yaani hana namna. Anatakiwa avumilie. Mwakani hata siyo mbali. Ataondoka akiwa ni mchezaji huru. Sina uhakika kama ataitwa yena kwenye timu ya Taifa, iwapo tu ataendelea na huu msimamo wake.

Lakini pia naamini kwa wakati huu huko kambini, atapata ushauri wa kila aina kutoka kwa wachezaji wenzake waliomzidi kila kitu.

Binafsi namuombea agundue ya kwamba njia aliyochagua kwa sasa, siyo sahihi.
Yanga mnaona mmedharirishwa sana na dogo. Mnajiona ni watu muhimu sana, mngetamani dogo atokee huku analia akiomba radhi ili nafsi zenu ziridhike. Hovyo kabisa.
 
Yanga mnaona mmedharirishwa sana na dogo. Mnajiona ni watu muhimu sana, mngetamani dogo atokee huku analia akiomba radhi ili nafsi zenu ziridhike. Hovyo kabisa.
Ungekuwa umeajiriwa, ungeielewa kwa haraka sana mantiki yangu.
 
Back
Top Bottom