Ushauri: Wilaya za Kibaha na Bagamoyo zihamishiwe Dar es Salaam, Mbagala na Kigamboni zipelekwe mkoa wa Pwani

Ushauri: Wilaya za Kibaha na Bagamoyo zihamishiwe Dar es Salaam, Mbagala na Kigamboni zipelekwe mkoa wa Pwani

Umepangilia vizuri hoja yako na unaijua jiografia vizuri. Hoja ya kudhibiti ongezeko la watu hapa si mahala pake. By the way tuna mapori mengi sana hatuyafanyii chochote Tanzania haina dalili ya over population.
Nchi yetu ya Tanzania suffers from different challenges, but overpopulation is not one of them. This country has a land area larger than California, Michigan, Arizona, and Virginia combined, lakini idadi ya watu ni sawa na size of California's and Virginia's combined.

In a nutshell, data zipo pia.
Kuhusu ukubwa kwamba Tanzania ina eneo kubwa kuliko hayo majimbo ya USA combined nadhani umeoverestimate. Tanzania ina 947,303 sq km wakati hayo yote yana 1,079,989 s km. Ungeondoa Jimbo la Virginia at least bado yana eneo kubwa kuliko Tanzania by 21,901 sq km.
 
Mimi ningekua na uwezo ningehamisha mkoa mzima wa pwani na morogoro na kuuleta Dar ili kutengeneza mkoa mmoja, service delivery ingekua ndio msingi sio utitiri wa hii kitu,nchi nzima mikoa 12 tu.
Kwahio Morogoro iwe Dar? Hapana aisee sifa ya Dar ni kichanga safi😅😅😅 we kama unapoishi hakuna mchanga jua unaishi mkoani tu😂
 
Kwahio Morogoro iwe Dar? Hapana aisee sifa ya Dar ni kichanga safi😅😅😅 we kama unapoishi hakuna mchanga jua unaishi mkoani tu😂
Dar na matope au udongo mwekundu wapi na wapi
 
Mbagala ni Tarafa, ni jimbo ina Mbunge, ina Hospitali, ina mabenki, soko, makanisa na misikiti,ina stendi za mwendokasi daladala; Mbagala imekosa mkuu wa Wilaya tu.
Mbagala inazidi singida mjini
 
Suluhisho hapa ni kuanzisha mkoa mpyaaa utakaojumuisha wilaya za rufiji, mkuranga , kibiti, mafia hapo ndipo binafsi naona ni solution ila sio.kuichukua kigamboni kuipeleka pwani
Naboresha wazo lako kwa kupendekeza kuwa mkoa wa Pwani ubakie na wilaya za Rufiji, Mkuranga, Kibiti na Mafia. Bagamoyo na Kibaha ziende Dar.

Naona tatizo kubwa ni hizi wilaya mbili za Bagamoyo na Kibaha kuwa karibu zaidi na Dar kuliko wilaya washirika za mkoa wa Pwani
 
Naboresha wazo lako kwa kupendekeza kuwa mkoa wa Pwani ubakie na wilaya za Rufiji, Mkuranga, Kibiti na Mafia. Bagamoyo na Kibaha ziende Dar.

Naona tatizo kubwa ni hizi wilaya mbili za Bagamoyo na Kibaha kuwa karibu zaidi na Dar kuliko wilaya washirika za mkoa wa Pwani
Ukifanya hivyo mkoa wa pwani utakuwa mkoa masikini duniani,bagamoyo na kibaha ndio zinaubeba mkoa wa pwani kiuchumi,so pwani ikipewa hata mbagala tu na sehemu ya kigamboni atleast kutakuwa na maendeleo,watu wa pwani hawataenda kariakoo ,wataishia mbagala
 
Ukifanya hivyo mkoa wa pwani utakuwa mkoa masikini duniani,bagamoyo na kibaha ndio zinaubeba mkoa wa pwani kiuchumi,so pwani ikipewa hata mbagala tu na sehemu ya kigamboni atleast kutakuwa na maendeleo,watu wa pwani hawataenda kariakoo ,wataishia mbagala
Ok kweli mkuu
 
Eti
Kipindi nakua mji ulikuwa mwisho ubungo, pale lilipo jengo la Tanesco ndio ulikuwa mzani wa kupima malori ambao sasa uko mkoa wa Pwani, Dar inakuwa kuelekea kaskazini,npaka wa Dar na kibaha unafutika, mpaka wa Dar, Bagamoyo unafutika kwa kasi sababu ya ujenzi unaokuwa kwa kasi ya ajabu.

Jiografia ya mkoa wa Pwani inashangaza sana, mtu wa Bagamoyo akitaka kwenda Rufijii au mafia lazima apitie Dar au apande chombo cha baharini. Ushauri wangu

Hizi wilaya mbili Kibaha na Bagamoyo zije Dar, ili kubalance mapato na uchumi wa mkoa wa Pwani Kigamboni na Mbagala yote iende Pwani,waungane na Mkuranga,Kisarawe, Mafia Kibiti na Rufiji.

Faida zake:

Jiji la Dar eS Salaam litapumua kwa kupata ardhi ya kutosha na kukua kwa kasi ya ajabu kibaha itakuwa kama urusi kwa technology na viwanda na Bagamoyo zitakuwa kama ukraine kwa utalii, pata picha chalinze iwe ni sehemu ya Dar es Salaam.

Tuje Pwani sasa.

Pwani kwa kupewa Kigamboni na Mbagala itachangamka sana, tatizo la Pwani ni kukosa amsha amsha. Mbagala itakuwa Dubai mpya kwa biashara mpaka sasa Mbagala inazidi baadhi ya mikoa kwa idadi ya watu na amsha amsha ya kibiashara njoo Mbagala kuanzia saa kumi jioni mpaka saa nne usiku hutaamini macho yako kila aina ya biashara utaikuta .pata picha Mbagala iko Pwani na na sehemu ya Kigamboni itakuwa Paris au Spain sehemu za kula bata kwenye fukwe.

Bandari ibaki Dar.Wakazi wengi wa Mbagala wana asili ya Pwani au Kusini mwa Tanzania, watafurahi kurudi nyumbani kwa style nyingine.
Chawa wa mama mfikishieni hii
Eti kibaha itakuwa kama Urusi,hivi wewe pita maduka 100 yaliyokaribu na wewe unionyeshe bidhaa ambayo ni made in Urusi kama utaikuta,vitu vingine mnajisemea tu.
 
Eti

Eti kibaha itakuwa kama Urusi,hivi wewe pita maduka 100 yaliyokaribu na wewe unionyeshe bidhaa ambayo ni made in Urusi kama utaikuta,vitu vingine mnajisemea tu.
Njoo huku ngerengere nikuonyeshe vifaru vya kirusi na silaha za kirusi,warusi walishapita huko kutengeneza chupa za chai na tooth pick
 
Mara ya Mwisho kuitembelea Mkuranga ilikuwa lini?
Unajua kuna viwanda vingapi vilivyojengwa Mkuranga?
kwa nini kibaha, chalinze na Bagamoyo unalazimisha ziwe sehemu ya Dar es Aalaam na wakati huo huo ukitaka Mbagala itoke?

Hoja yako ilikuwa mto kizinga ndio itumike kuitenganisha Jimbo la Mbagala na maeneo mengine mkoani Dar es Salaam na kukujibu kwa Kutumia kigezo cha Kizinga itakubidi pia Ukate baadhi ya maeneo ya Jimbo la Temeke pia ni wilaya, ukate baadhi ya maeneo ya Jimbo la ukonga ambalo ni sehemu ya jiji la Dar es salaam.

Labda wewe kwa mtazamo wako Dar es salaam inahanzia wapi na inaishia wapi?

unajua Mbagala ni karibu zaidi na kati kati ya jiji kuliko Kimara, kibamba, Gongo la mboto, Bunju na Tegeta huko,
kwa nini sehemu sehemu ya karibu na kati kati ya jiji la Dar es salaam itengwe ila huko mbali kwenye mishokora pajumuishwe.

Unajua umbali uliopo kutoka Rangi tatu mpaka Kilwa kwa kukusaidia tu KM 288 na hii ni kilwa kivinje tu bao kipatimu na maeneo mengine, hivyo na umbali wa kutoka posta mpaka mkuranga ni km50.
Ungekuwa wewe ndio mtoa maamuzi hayo makao makuu mapya ungeyaweka mkuranga? ukiyaweka mkuranga hujawaweka watu kutoka kilwa kipatimu karibia na liwale kwenye shida.

Nini sababu za kiuchumi za kuichukua kibaha, Bagamoyo, chalinze kuiunganisha na Dar zinazozidi za kuiunganisha Mkuranga na KIsarawe.

hivi hamjui Wandereko na wazaramo hawajawahi kuvuka mto rufiji, ukivuka kabila la huko ni wamatumbi yaani namaanisha rufiji, kibiti, mkuranga , kisarawe, kibaha, chalinze na huku mto wami.

kuna mtoa mada mmoja anasema kisa kuna watu wa kusini wengi hivyo anahisi hawastahili au? kwa maeneo yanayokaliwa na wachaga wengi ndio wanastahili?

mtoa mada unaifahamu historia ya MSASANI? unafahamu wenyeji hapo wengi wanatoka wapi? na yenyewe itolewe?

N.B nilikimbia fesibuku na huku nayakuta yaleyale
 
Kuhusu ukubwa kwamba Tanzania ina eneo kubwa kuliko hayo majimbo ya USA combined nadhani umeoverestimate. Tanzania ina 947,303 sq km wakati hayo yote yana 1,079,989 s km. Ungeondoa Jimbo la Virginia at least bado yana eneo kubwa kuliko Tanzania by 21,901 sq km.
Sasa wewe 21,901 sqm ni big deal?
 
Back
Top Bottom