Ushauri Wizara ya Elimu: Nyadhifa zitolewe kwa kuzingatia Kiwango cha Elimu, kipaumbele kikiwa kwenye elimu ya juu zaidi

Mtu kuwa na elimu kubwa, inatafsiri wewe ni mtu wa kimataifa; ukishakuwa na hiyo elimu hutakiwi kufikiria mishahara wala posho; we fanya machapisho yenye tija kimataifa, utakuwa unaitwa kwenye presentation huko nje na kupiga hela.

Kusoma huku ukitegemea mshahara au vyeo; unakuwa na elimu ya karatasi lakini kichwani unakuwa hamna kitu.

Unatakiwa u- act kisomi; Dunia ikutambua wewe ni nani; tunategemea siku moja utaitwa pale Harvard au Oxford ukafanye 'presentation'.​
 
Wenye elimu ya chini huwaogopa wenye elimu kubwa kwamba watanyang'anya vyeo vyao hivyo huwafanyia firigisu
 
Mshikaji alienda kusoma apewe madaraka. Imekula kwake ameamua kulalamika.

Sent from my Infinix X688B using JamiiForums mobile app
Wewe ndiye asili ya watanzania tulionao kwa sasa. Akili zako ndipo zilipofikia ,fikiria kama msomi acha uzamani.Wenzetu hata KENYA wasomi ni wengi kwasababu wanadhaminiwa. Kwa akili yako ndogo ulitaka aende kusoma ilikuongeza maarifa kwa ngazi ya uzamili na uzamivu?
 
Tatizo wenye Elimu ya juu, ndo wanaongoza kwa uzombi. 🤢🤢
 
Unajaribu kumfundisha mbuzi kuandika? Huoni unapoteza muda? Bila CCM kuondoka kwenye madaraka hakuna kitu kitakachobadilika. Sana sana mambo yatazidi kuwa mabaya. Huu muda unaotumia kuipa CCM ushauri unaupoteza bure. Bora uelemishe watu hata wawili umuhimu wa kupigana ili CCM iondoke.
 
Nakuhakikishia inakuwa hivyo kwa sababu ya uongozi tulio nao. Kama rais ni zombi na hataki kuondoka unadhani wasomi watafanya nini?
Nikweli, kwa Sasa Aliye ishia Darasa la tatu B, aliye ishia Darasa la saba, aliye ishia kidato cha nne, aliye ishia Kidato cha sita, Mpaka sijui PhD huko = wote akili zinafanana.

Nina Imani kabisa hata asiye soma, hii Tanganyika anaiongoza vizuri kabisa.
 
Hata rais tuliye naye sasa huwezi kumweka kwenye kundi la wasomi. Ana elimu ya kuungaunga tu hivyo hili la kuweza kuongozwa na rais ambaye hajasoma ni kama limeshatokea.
 
Upo sahihi kabisa
 
Ila na wewe bwana...mbona unamawazo takataka hvi kwahyo kufanya presentation Harvard au Oxford ndo unakuwa mtu wa kimataifa 🤣
 
Nina mchepuko huko Mkuranga ni mwalimu mkuu,yaani mpaka aibu naona mimi jinsi asivyo na uwezo wala uelewa wa nini anatakiwa kufanya kwenye kutimiza majukumu yake.
Na huyu ni wa diploma ya kujiendeleza.

Anavyopiga madongo wenzake wenye shahada moja ama mbili sasa, ni hatari tupu.
 
Nyie watu nyie, magufuli alikuwa na PhD maksema hana akili sasa hao wenye PhD waende wapi tena nanyi mliisha sema PhD siyo maarifa?
 
Mimi nataka hiyo ya kugawa uvungu, unagawaje gawaje jamani🤣🤣🤣 Nimechoka Yani kuchukiwa bila sababu kisa Kibachelor uchwara🤣, wangejua Kibachelor chenyewe nimekipata Kwa tabu bodi wananikausha damu🤣
 
Ni vizuri ila kuna wakati mwingine hao wenye elimu kubwa wanaweza kuwa na uwezo mdogo kiutendaji. Kwa nchi yetu ninavyoona kadri mtu anavyozidi kuwa na elimu kubwa ndivyo ufanisi wake kazini unapungua au anakuwa anafanya maamuzi ambayo hata mlioko chini mnashanga.
 
huu ujinga wa kwenda kusoma ukiwa unapigia mahesabu vyeo ni ujinga. hiyo hela ya kusoma masters au PhD ungefuga mbuzi tuu mwalimu ungekuwa mbali sana. acha umbulula.
 
Wewee...
Watu wanaendesha boda.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…