Ushawahi kuchukuliwa poa na mtu halafu akakuta sivyo kama alivyokudhania?

Ushawahi kuchukuliwa poa na mtu halafu akakuta sivyo kama alivyokudhania?

Juzi tu NMB Dodoma:

Jamaa flan kavaavaa tu afu na midevudevu hivi

Kaenda NMB ATM kakuta na wadada wa benki wameweka meza ya kutoa huduma kwa wateja pemben hapo. Akafika tu kauliza (bila hata kusalimia).....kwanini kadi yangu inakataa kuniunganisha NMB mkononi

Dada kamjia juu...."kwanza salimia;...vipi habari za huko,...haya tukusaidie nini??"

Jamaa hakupokea. Mie nawaangalia tu.

Dada karudia tena ...."vipi mzima mwenzetu?? Za ulikotoka??!.....mbona umekuja kasi sana??!"....

Jamaa anaeaangalia tu. Mara akauliza...."ivi ni lazima kusalimia/ au kupokea salam ya mhudumu ili nipewe huduma NMB???...

Wakaanza kumshangaa ..."unatokea wapi wewe, yani unakuja kuvamia tu bila kusalimia..." ....wamamzodoa flan.

Jamaa akaingia Benki ndani. Straight kwa Meneja. Nafkiri hakueleza shida aliyopata nje. Alimueleza tu kama kutaka kusaidiwa shida yake. Sijui ndani waliongea nini??

Wametoka na meneja...hadi pale ATM kwenye meza ya wale wadada....meneja akiwa kashika mkononi kadi ya yule mshua....akawambia wale wadada mmoja wao (sikumbuki jina)...

Meneja: .....hebu msaidie Katibu Mkuu hapa kumuunganisha na NMB Mkononi...(Meneja akaongeza:....mkuu hapa utahudumiwa)...mara meneja katuomba wote wa kwenye foleni ya ATM..."naomba ndugu tumpishe kiongozi anajambo kidogo kwenye ATM ...samahani"...wakaingia ATM meneja, mshua na yule dada.

Wakafanya mambo humo ...kidogo wakatoka. Tukaendelea.

Meneja akamsindikiza yule mshua hadi kwenye gari akaondoka meneja anapunga mkono.

Niliwaangalia wale akina dada mavi yalivyowagonga chupi. Walitoa macho sana wakawa na wasiwasi mkubwa....

Walimchukulia poa
Kilambimkwidu [emoji23][emoji23][emoji23]upo?
 
Kuna manager wa hotel fulani kubwa tu. Alitusimulia kuwa siku moja akiwa ndio manager wa zamu akaitwa na muhudumu wa mapokezi shida ikiwa kuna mgeni kachoka choka hivi lakini anahitaji room ya bei mbaya pale hotelini.
Sasa muhudumu wa mapokezi akamwambia mgeni mchovu angoje kidogo akamuonyesha na pa kupumzikia ili amuandalie hiyo room uku ikiwa ni kupata muda ili amwambie manager kuhusu kumpa chumba cha bei mbaya jamaa.
Manager kumuona mgeni alivyo ikabidi aende kuongea nae.mshtuko ukampata baada ya mager kujitambulisha jamaa nae akajitambulisha jina ndipo akajuwa jamaa ni footballer mkubwa tu duniani na jezi aliyovaa juu ni ya timu yake ya taifa.mara moja akapewa room bila hata maswali mengi.
Duh.
 
Mbona awamu hizi za karibuni ni kawaida tu kwa wateuliwa au mmeshasahau visa vya waziri Ngereja na Mlinzi wa ATM?


tps://www.jamiiforums.com/threads/kisa-cha-waziri-ngeleja-na-mlinzi-kwenye-atm.49162/page-3
Itume Tena
 
Kuna siku nipo nilikuwa sina kazi nyingi ofisini nikatoka nje hivi nikamweleza PA wangu nipo nje nachukua Juice Fresh kutoka nje kuna gari limeingia Parking kwa speed kidogo liniingie miguuni jamaa hawakuwa na hekima walinitusi Mpuuzi wewe...nimerudi Ofisini naambiwa na PA wangu Meneja kuna wageni wako nikawaruhusu waingie nakuta wale jamaa walionitusi nikawakaribisha na sentensi fupi 'Karibu ABSA' wanageuzageuza nyuso zao hawajui waanze vipi.
ikawaje mwisho wake?
 
Wale house mates walivogundua sikujali nilienda nao poa tu walijua huwa sijali mambo madogo na kuna jamaa mmoja nilimchukuaga kama sales officer maana nafasi hizo nilikua naajiri mwenyewe 1 year contract renewable na hakuniangusha akawa anafanya vizuri tu mpaka akagrow kuwa relationship officer
yule dada wa reception aliyekujibu nyodo vipi??[emoji2][emoji2][emoji2][emoji2]
 
Mwaka juzi natoka kijijini nkafika himo pale nikakuta nyomi ya abiria, nkapanga nichukue vichwa au la maana kuna siku nilichukua abiria aisee alinitesa sanaa, yaani gari ikifika speed 100 ni anaongea adi napunguza mwendo afu alikua mmama, na abiria wenzie wakawa wanamsapoti na mi napenda speed kali,

Nkapaki gari nkaenda kuzurura kuangalia mazingira nikinunua na mahitaji mbalimbali, nkaona mabinti wa3 wamekaa kinyonge baada ya kukosa usafiri na ni saa sita mchana, nkaenda kuwasalimu huku nawahoji vimaswali vya hapa na pale wa2 wakadharau ila yule mmoja akawa ananipa ushirikiano kiasi lkn mwenzie akamwambia kwa kilugha "achana na hilo limtu njoo tuongee mambo ya maana" (nilikua nmevaa ovyo tu na nguo chafu kidogo maana nilitoka porini) hapo wanalaumiana kwanini hawakwenda kupandia gari moshi mjini...

Nkamaliza kununua mahitaji yangu nkaenda washa gari nkawafuata nkamwita yule mmoja alieonyesha ushirikiano akaja nkamwambia mna sh ngapi niwapeleke dar, akasema wana elfu15, nkawaambia ungeni iwe 50 tuende wakafanya hivyo japo kwa aibu na shikamoo wakanipa[emoji23][emoji23][emoji23].

Njiani wanaongea kilugha japo sio cha kwetu kabisa ila nawaelewa sana, hapo wananiteta kiana huku wakilaumiana pengine ningewapunguzia kama wasingenidharau... Waliuliza kabla kama najua kilugha nkawadanganya mi mchaga lakini sijakulia wala kujua hiyo lugha zaidi ya salamu tu

Nkafanya makusudi nkapiga simu kwa jamaa ninaemwazima gari "oyaa mshua vipi, nipo njiani saa 3 ntakua dar nakuletea gari yako" kuskia ivo ndio wakaanza kuniteta tena nawachora tu.

Pale segera nkadakwa na trafiki kwa speed, wakati nawabembeleza nkawaambia sina kitu hii gari ilikua mkoani imeharibika mwenye nayo kaniomba niirudishe dar akaomba kadi ya gari kusoma na leseni akasema unadanganya? Au na leseni ya mwenye gari? Hayo yote walikua wanaskia, nkamalizana nae nkampoza elfu 5 akauliza hao kwenye gari ndugu zako nkamwambia hapana, akasema aliekaa mbele nimemuelewa, akaniambia zuga kidogo nichukue namba akaenda kaongea nae kachukua namba nkarudi kuendelea na safari.

Nkaskia wanaambiana "kumbe ikari li la kajamaa ka, keusani nalo hata ku" mmoja akajibu "tra isarau vandu utevaishi" alimaaninisha kumbe hili gari la haka kajamaa, wala hafanani nalo, mwenzie akamjibu, acha kudharau watu usiowajua.

Kufika dar heshima debe, kumbe walikua wanachuo niliwapeka adi UDSM,

Pisi moja niliielewa kesho yake nkala mzigo baada ya hapo anataka kunifanya kitega uchumi kanijazia mzigo wa shida zake nkampotezea.
 
Hii mambo iliwah nitokea nimetoka chuo na piga kaz na fundi mtaani.
Tuko na fundi mtaan tunapiga kaz kwenye nyumba ya mshua mmoja hv wa mambo ya ujenzi.
Asubuhi hiyo nagonga nyundo sana juu ya dari, fundi mkuu yuko chini na mama mwenye nyumba wanaongea kwa kilugha huku mimi nasikia baadhi ya maongezi yao kuwa "mwangalie fundi wako huko juu asije akaniunguzia nyumba yangu" na fundi akamjibu "haina shida ntaenda kuangalia",
Nilijisikia vibaya kwani kaz ninaijua vizur tu, pia fundi ananikubali kwenye kaz zenye utata lkn huyu mama alinidhalau sana na umbo langu dogo.
Kazi iliisha tukatimua na fundi wangu na ujira wetu mkononi, fundi mkuu alinieleza tulipo toka kuwa yule mama hakuamini kabsa kwenye kazi nikamjibu nilisikia alichoongea nikiwa juu.
Jion sasa yule mama alimwakia fundi kuwa kijana wako kaharibu kule juu anataka kumwunguzia nyumba yake, fundi mkuu akamwahidi kesho atakuja kurekebisha mwenye mama wa watu akapoa. Fundi alinipigia na kunijulisha hiyo inshu na tukakubaliana kwenda kesho.
Siku iliyofuata asb kama kawaida tukakutana fundi, ila fundi siku hiyo mtoto wake alikuwa mgonja hivyo alikuwa anafanya maandalizi ya kumpeleka hospital mtoto wake na hivyo mm kwenda eneo la tukio ila fundi aliniambia nimpe matumaini kuwa atakuja si muda kukangua kazi.
Nimefika site mama wa watu ananiangalia hovyohovyo tu, fundi yuko wapi? Yuko njian atakuja.
Nikaingia mzigoni sasa wala hata sikupanda juu ya dari yaani ni palepale kwenye main switch mchezo ukaisha , namwambia angalia vitu vyako vinafanya kazi? Akajibu ndio. Nikajua imemkaba hiyo na dhalau zke akidhani palipoharibika ni juu ya dari nipokuwa nagongagonga.
Nikawa zangu pale nje namsubili fundi aje maana hatukuwa na mawasiliano ya simu mpaka alipofika akamweleza nn kutokufika kwa wakat kwa kilugha, hao tukaendelea na shughuli zetu.
Nikamwacha anashangaa tu màana na fundi hakuangaika kukagua !
ndo shida za kuwa na boss mwanamke [emoji2][emoji2]
 
ishanitokea zaidi ya mara moja nahisi ni sababu ya mwili mdogo na wembamba pia sio mtu wa kuvunja kabati navaa kawida sana, ndevu hakuna na ki baby face japo nimekula chumvi.

Kuna siku ilikua fiesta wasanii na team ya clouds ilikua imefikia hoteli ambayo na mimi nilikuepo kuhudhuria sherehe ya ufunguzu wa kampuni fulani ya bima ambayo ni wateja wangu nawapa huduma fulani. Nilitoka mida ya saa 3 usiku kabla event kuisha, wakati nashuka chini naenda Launge kuongea na simu nawakuta ma chekibobu wa clouds akina Bdozen, Mchomvu na wengine wengi tu watoto wa mjini pale launge. nikawasalimia na kukaa ila hawakujibu na waliniona kama sio type yao.

Lahaula, kabla sijamaliza kuongea na simu naona binti kanirukia kwa nyuma na bonge la hug na mabusu ya shavuni na kulalamika nimemtupa simtafuti tena. Wale machekibobu wakashtuka macho yakawatoka, wakamuuliza yule dada vipi upo sawa akawajibu "am very happy nahisi hata show leo nitaperform vizuri". Kwa ufupi yule dada ni katika hawa wasanii wa kike wanaosumbua mjini kwa sasa na nyimbo zao na siku ile ndio alikua kati ya wasanii wa kutegemewa katika show. Kanakumbuka mchango wangu tangia kadogo kananifata kuniimbia akapela, nakakosoa na kumpa ushauri sasa am happy kanaishi ndoto yake.
mimi shobo na watu nisiowajua ndo siwezagi kabisa[emoji2][emoji2][emoji2]
 
Kuna dogo mmoja mchafu tu hivi kimuonekano anauza karanga mbichi zile zilizokobolewa na kitenga anatembeza kkoo kuanzia asubuhi na jioni ana kijiwe cha kahawa,
Siku nimekutana nae kule mbagala saku ana nyumba kubwa afu kali kinyama, na nje pana fremu 4 kuna duka kubwa tu anauza mke wake, aliniambia kwake lkn kiukweli sikuamini adi nilienda kuuliza maana nilikokua nimeenda ni karibu.

Kesho yake kaja kuniuzia karanga ilibidi nimuulize kujua labda alikua na maisha mazuri kabla, ndio akaniambia yale yote niliyoyaona yamechangiwa kwa 90% na kuuza karanga, yaani ananunua gunia zima mbichi zilizokobolewa akaomaa akitembeza na zingine anakaangia kashata adi analimaliza kwa mwezi mmoja na akikosa sana faida ni laki 7.
Aisee usidharau usiemjua
 
Kuna jamaa yangu mmoja miaka hiyo anauza duka la ndugu yake pale kawe akatoke dada mmoja mdogo tu akamuelewa sana yaani zaidi ya sana na jamaa umri umeenda na alikua bado hajaoa, yule dada akamtaka amuoe jamaa hataki, nia yake anataka aoe wa kabila lake pia akawa ananiambia huyu dada mzuri sana atakuja kutesa, demu hakua mzuri wa sura kiviile ila hiyo shepu weka mbali na watoto, jamaa akamtosa kaenda kuoa kwao.

Akajajua yule dada ni mjeda pale lugalo na alikua na nyota 3 lkn alikua anamficha na nyumba waliokua wanaenda kufanya yao goba ilikua ya kwake yeye alihisi kapanga,
Jamaa hadi leo anajilaumu na kujitukana kabisa mana yule dada alikuja kuolewa na jamaa anaemfahamu na ndoa kubwa tu kamfungulia mme wake biashara kubwa tu kwenye fremu zake huko goba wanakula maisha tu.
 
Hii hali wahanga wakubwa ni WANAWAKE NA ZILE NJEMBA ZINAZOISHI KIBISHOO MJINI.
Kwangu imewahi kunitokea mara 2 lkn hapa nitaeleza hii moja ambayo imepelekea kumpata huyu mama wa watoto wangu.
Mwaka fulani nikiwa zangu DASALAMA nilikuwa nina tabia ya kwenda kisuper market fulani kupata bidhaa za hapa na pale, sasa kulikuwa na mhudumu mmoha nilimwelewa saaaaaaana, nikajaribu kumsemesha lkn wapi, na hata uvaaji wangu kwa kweli haurudhishi nywele mtihani kuchana, ndevu kama brash ya chachandu, lkn pia kila nikienda huwa nilikuwa naenda na pikpk yangu Boxer, nilimfukuzia yule manzi kama miezi miwili na nusu na sikupata hata namba yake. Mwisho ikawa nikienda pale namsalimia nanunua vitu niwezavyo kwa 30k yangu ndukiiii. Ukapita mwezi bila mm kutokea pale, nyuma huko ile PISI ikaacha kazi yake nami nilikuwa sijui, ikatokea siku moja yule pisi amekuja kwa ajili ya ishu za biashara yake ofisini kwetu. Lahaulaaaaaaa anayemuona anazunguka kwenye kiti ni mimi na nina mamlaka kidogo ya kumtuma mtu na akatii, ile pisi kwanza ilishtuka mm kuniona pale, mi nkaona isiwe kesi nikateremka chini ili niende zangu pata lunch, ila nimefika mapokezi nikajisahau napiga soga na dadaetu wa pale mapokezi ile ikawa inateremka ngazi ikanikuta pale down, akanisalimia nikaitikia akaniambia samahani kuna kitu nimesahau atarudi ili tuongee, mi nkasema fresh huku nikiondoka nje kabisa ya ofisi na kuwasha gari yangu kaliii, yule dada akaniwahi kuomba lift mi nkampatia na sikutaka kabisa mazoea sijui ya kuulizana ilikuwaje wala nn, sikutaka kumpa hata nafasi hiyo nikambwaga alipotaka mi nkaenda pata BIRIANI fureeeesh. Sasa nilivyorudi yule demu akakoma lazima nimuhudumie mm, akalazimisha mi nkamhudumia akaomba no yangu tangia hapo nimemzalisha watoto 2.
 
Back
Top Bottom