INTROVERT MAN
JF-Expert Member
- Aug 5, 2019
- 993
- 1,343
Kilambimkwidu [emoji23][emoji23][emoji23]upo?Juzi tu NMB Dodoma:
Jamaa flan kavaavaa tu afu na midevudevu hivi
Kaenda NMB ATM kakuta na wadada wa benki wameweka meza ya kutoa huduma kwa wateja pemben hapo. Akafika tu kauliza (bila hata kusalimia).....kwanini kadi yangu inakataa kuniunganisha NMB mkononi
Dada kamjia juu...."kwanza salimia;...vipi habari za huko,...haya tukusaidie nini??"
Jamaa hakupokea. Mie nawaangalia tu.
Dada karudia tena ...."vipi mzima mwenzetu?? Za ulikotoka??!.....mbona umekuja kasi sana??!"....
Jamaa anaeaangalia tu. Mara akauliza...."ivi ni lazima kusalimia/ au kupokea salam ya mhudumu ili nipewe huduma NMB???...
Wakaanza kumshangaa ..."unatokea wapi wewe, yani unakuja kuvamia tu bila kusalimia..." ....wamamzodoa flan.
Jamaa akaingia Benki ndani. Straight kwa Meneja. Nafkiri hakueleza shida aliyopata nje. Alimueleza tu kama kutaka kusaidiwa shida yake. Sijui ndani waliongea nini??
Wametoka na meneja...hadi pale ATM kwenye meza ya wale wadada....meneja akiwa kashika mkononi kadi ya yule mshua....akawambia wale wadada mmoja wao (sikumbuki jina)...
Meneja: .....hebu msaidie Katibu Mkuu hapa kumuunganisha na NMB Mkononi...(Meneja akaongeza:....mkuu hapa utahudumiwa)...mara meneja katuomba wote wa kwenye foleni ya ATM..."naomba ndugu tumpishe kiongozi anajambo kidogo kwenye ATM ...samahani"...wakaingia ATM meneja, mshua na yule dada.
Wakafanya mambo humo ...kidogo wakatoka. Tukaendelea.
Meneja akamsindikiza yule mshua hadi kwenye gari akaondoka meneja anapunga mkono.
Niliwaangalia wale akina dada mavi yalivyowagonga chupi. Walitoa macho sana wakawa na wasiwasi mkubwa....
Walimchukulia poa
Duh.Kuna manager wa hotel fulani kubwa tu. Alitusimulia kuwa siku moja akiwa ndio manager wa zamu akaitwa na muhudumu wa mapokezi shida ikiwa kuna mgeni kachoka choka hivi lakini anahitaji room ya bei mbaya pale hotelini.
Sasa muhudumu wa mapokezi akamwambia mgeni mchovu angoje kidogo akamuonyesha na pa kupumzikia ili amuandalie hiyo room uku ikiwa ni kupata muda ili amwambie manager kuhusu kumpa chumba cha bei mbaya jamaa.
Manager kumuona mgeni alivyo ikabidi aende kuongea nae.mshtuko ukampata baada ya mager kujitambulisha jamaa nae akajitambulisha jina ndipo akajuwa jamaa ni footballer mkubwa tu duniani na jezi aliyovaa juu ni ya timu yake ya taifa.mara moja akapewa room bila hata maswali mengi.
Itume TenaMbona awamu hizi za karibuni ni kawaida tu kwa wateuliwa au mmeshasahau visa vya waziri Ngereja na Mlinzi wa ATM?
tps://www.jamiiforums.com/threads/kisa-cha-waziri-ngeleja-na-mlinzi-kwenye-atm.49162/page-3
Sure ustaarabu huanza na salamuHakuna anaekulazimisha kusalimia. Lakini ustaarabu wa mtu uanzia hapo kwenye salaam. Ukisalimia utapoteza nini na utatumia masaa mangapi?
ikawaje mwisho wake?Kuna siku nipo nilikuwa sina kazi nyingi ofisini nikatoka nje hivi nikamweleza PA wangu nipo nje nachukua Juice Fresh kutoka nje kuna gari limeingia Parking kwa speed kidogo liniingie miguuni jamaa hawakuwa na hekima walinitusi Mpuuzi wewe...nimerudi Ofisini naambiwa na PA wangu Meneja kuna wageni wako nikawaruhusu waingie nakuta wale jamaa walionitusi nikawakaribisha na sentensi fupi 'Karibu ABSA' wanageuzageuza nyuso zao hawajui waanze vipi.
yule dada wa reception aliyekujibu nyodo vipi??[emoji2][emoji2][emoji2][emoji2]Wale house mates walivogundua sikujali nilienda nao poa tu walijua huwa sijali mambo madogo na kuna jamaa mmoja nilimchukuaga kama sales officer maana nafasi hizo nilikua naajiri mwenyewe 1 year contract renewable na hakuniangusha akawa anafanya vizuri tu mpaka akagrow kuwa relationship officer
wanyakyusa ndo wana hiyo tabia?Usikute hata ni mnyakyusa
vipi yamewahi kukutokea nini?Wanawake walosoma na watumishi wana changamoto sana,wengi wao huachika baada ya kuolewa ndani ya miaka 10 ya ndoa....
ndo shida za kuwa na boss mwanamke [emoji2][emoji2]Hii mambo iliwah nitokea nimetoka chuo na piga kaz na fundi mtaani.
Tuko na fundi mtaan tunapiga kaz kwenye nyumba ya mshua mmoja hv wa mambo ya ujenzi.
Asubuhi hiyo nagonga nyundo sana juu ya dari, fundi mkuu yuko chini na mama mwenye nyumba wanaongea kwa kilugha huku mimi nasikia baadhi ya maongezi yao kuwa "mwangalie fundi wako huko juu asije akaniunguzia nyumba yangu" na fundi akamjibu "haina shida ntaenda kuangalia",
Nilijisikia vibaya kwani kaz ninaijua vizur tu, pia fundi ananikubali kwenye kaz zenye utata lkn huyu mama alinidhalau sana na umbo langu dogo.
Kazi iliisha tukatimua na fundi wangu na ujira wetu mkononi, fundi mkuu alinieleza tulipo toka kuwa yule mama hakuamini kabsa kwenye kazi nikamjibu nilisikia alichoongea nikiwa juu.
Jion sasa yule mama alimwakia fundi kuwa kijana wako kaharibu kule juu anataka kumwunguzia nyumba yake, fundi mkuu akamwahidi kesho atakuja kurekebisha mwenye mama wa watu akapoa. Fundi alinipigia na kunijulisha hiyo inshu na tukakubaliana kwenda kesho.
Siku iliyofuata asb kama kawaida tukakutana fundi, ila fundi siku hiyo mtoto wake alikuwa mgonja hivyo alikuwa anafanya maandalizi ya kumpeleka hospital mtoto wake na hivyo mm kwenda eneo la tukio ila fundi aliniambia nimpe matumaini kuwa atakuja si muda kukangua kazi.
Nimefika site mama wa watu ananiangalia hovyohovyo tu, fundi yuko wapi? Yuko njian atakuja.
Nikaingia mzigoni sasa wala hata sikupanda juu ya dari yaani ni palepale kwenye main switch mchezo ukaisha , namwambia angalia vitu vyako vinafanya kazi? Akajibu ndio. Nikajua imemkaba hiyo na dhalau zke akidhani palipoharibika ni juu ya dari nipokuwa nagongagonga.
Nikawa zangu pale nje namsubili fundi aje maana hatukuwa na mawasiliano ya simu mpaka alipofika akamweleza nn kutokufika kwa wakat kwa kilugha, hao tukaendelea na shughuli zetu.
Nikamwacha anashangaa tu màana na fundi hakuangaika kukagua !
KweliChai hizo mkuu
mimi shobo na watu nisiowajua ndo siwezagi kabisa[emoji2][emoji2][emoji2]ishanitokea zaidi ya mara moja nahisi ni sababu ya mwili mdogo na wembamba pia sio mtu wa kuvunja kabati navaa kawida sana, ndevu hakuna na ki baby face japo nimekula chumvi.
Kuna siku ilikua fiesta wasanii na team ya clouds ilikua imefikia hoteli ambayo na mimi nilikuepo kuhudhuria sherehe ya ufunguzu wa kampuni fulani ya bima ambayo ni wateja wangu nawapa huduma fulani. Nilitoka mida ya saa 3 usiku kabla event kuisha, wakati nashuka chini naenda Launge kuongea na simu nawakuta ma chekibobu wa clouds akina Bdozen, Mchomvu na wengine wengi tu watoto wa mjini pale launge. nikawasalimia na kukaa ila hawakujibu na waliniona kama sio type yao.
Lahaula, kabla sijamaliza kuongea na simu naona binti kanirukia kwa nyuma na bonge la hug na mabusu ya shavuni na kulalamika nimemtupa simtafuti tena. Wale machekibobu wakashtuka macho yakawatoka, wakamuuliza yule dada vipi upo sawa akawajibu "am very happy nahisi hata show leo nitaperform vizuri". Kwa ufupi yule dada ni katika hawa wasanii wa kike wanaosumbua mjini kwa sasa na nyimbo zao na siku ile ndio alikua kati ya wasanii wa kutegemewa katika show. Kanakumbuka mchango wangu tangia kadogo kananifata kuniimbia akapela, nakakosoa na kumpa ushauri sasa am happy kanaishi ndoto yake.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Sawa mzee baba nimekuelewa sanakwenye issue ya salamu sio muhimu sana. mf.
napenda sana nyuzi za Infantry Soldier ila salamu zake kila uzi .salamu paragraph mbili. huwa naboreka sana. Infantry Soldier kaka toa hizo salamu bhn. we tema madini afu tembea