Hii hali wahanga wakubwa ni WANAWAKE NA ZILE NJEMBA ZINAZOISHI KIBISHOO MJINI.
Kwangu imewahi kunitokea mara 2 lkn hapa nitaeleza hii moja ambayo imepelekea kumpata huyu mama wa watoto wangu.
Mwaka fulani nikiwa zangu DASALAMA nilikuwa nina tabia ya kwenda kisuper market fulani kupata bidhaa za hapa na pale, sasa kulikuwa na mhudumu mmoha nilimwelewa saaaaaaana, nikajaribu kumsemesha lkn wapi, na hata uvaaji wangu kwa kweli haurudhishi nywele mtihani kuchana, ndevu kama brash ya chachandu, lkn pia kila nikienda huwa nilikuwa naenda na pikpk yangu Boxer, nilimfukuzia yule manzi kama miezi miwili na nusu na sikupata hata namba yake. Mwisho ikawa nikienda pale namsalimia nanunua vitu niwezavyo kwa 30k yangu ndukiiii. Ukapita mwezi bila mm kutokea pale, nyuma huko ile PISI ikaacha kazi yake nami nilikuwa sijui, ikatokea siku moja yule pisi amekuja kwa ajili ya ishu za biashara yake ofisini kwetu. Lahaulaaaaaaa anayemuona anazunguka kwenye kiti ni mimi na nina mamlaka kidogo ya kumtuma mtu na akatii, ile pisi kwanza ilishtuka mm kuniona pale, mi nkaona isiwe kesi nikateremka chini ili niende zangu pata lunch, ila nimefika mapokezi nikajisahau napiga soga na dadaetu wa pale mapokezi ile ikawa inateremka ngazi ikanikuta pale down, akanisalimia nikaitikia akaniambia samahani kuna kitu nimesahau atarudi ili tuongee, mi nkasema fresh huku nikiondoka nje kabisa ya ofisi na kuwasha gari yangu kaliii, yule dada akaniwahi kuomba lift mi nkampatia na sikutaka kabisa mazoea sijui ya kuulizana ilikuwaje wala nn, sikutaka kumpa hata nafasi hiyo nikambwaga alipotaka mi nkaenda pata BIRIANI fureeeesh. Sasa nilivyorudi yule demu akakoma lazima nimuhudumie mm, akalazimisha mi nkamhudumia akaomba no yangu tangia hapo nimemzalisha watoto 2.