Ushawahi kuchukuliwa poa na mtu halafu akakuta sivyo kama alivyokudhania?

Ushawahi kuchukuliwa poa na mtu halafu akakuta sivyo kama alivyokudhania?

U

Unayemjua ndio unamdharau? Haitakiwi umdharau mja yeyote uwe unamjua au humjui
Over!
Sio kwamba ninaemjua ndio namdharau, hapana namaanisha mara nyingi watu huwa wanawadharau watu wasiowajua since hawajui status zao mwisho anaona sio alivyomdhania refer shuhuda zote humu. Mimi nawaheshimu wote ninaemjua na nisiemjua. Sababu hata unaemjua ukamdharau huwezi jua lini atakuwa msaada kwako.
 
Jamaa limekuja mtaani kujenga kamjengo kake,katukuta wenyeji tuna mwagilia moyo,yupo na mkewe hata salamu yaani kakausha tu,kachukua mafundi akawaelekeza kazi pale,zikaja semi 2 zimekula nondo na cememt, kisa anajenga ki gorofa hahaaa,kilicho tokea kabakia kwenye msingi tu wabane wae kwara kuanzia nondo mpaka cement mpaka tofali yaani,kaja kushuka baada ya wiki,wenyeji wamejenga kupitia jamaa kuja kushtuka hana pakuanzia,tunasiki yowee tu huko jamaa hana wakumuuliza ,ndugu zangu ukifika sehem usi mdharamu mtu,huwezi jua atakusaidia lini na wapi.
 
Miaka fulani nilikuwa na likizo ndefu ya chuo basi nikaona nisikae bure nikafungua kamgahawa katikati ya mji. Nilikuwa nauza bites zote, juice fresh na matunda fresh.

Nilikuwa karibu na ofisi nyingi na banks. Basi nikawa napata oda ya kupeleka bites na maziwa asubuhi pamoja na matunda.

Dada mmoja staff wa pale CRBD aliweka oda ya matunda kila ikifika saa 6 mchana, ikawa siku nyingine ukipeleka anakwambia umechelewa nishakula kwingine, au leo sili basi narudi nayo. Au ukienda siku nyingine anakuangalia tuu hapokei matunda unabaki umesimama kama sanamu na matunda yako.

Siku moja nikaenda nikiwa na shida ya kufungua joint acc, kufika kwake hata sijamsalimia kanijibu leo sitaki matunda. Nikamwambia nina shida nyingine kabla sijaeleza akajibu tena "hapa tunasikiliza za kiofisi tuu hivyo ondoka". Sijui alijua nataka msaada wa hela au vipi.

Ikabidi niwe mpole maana alikuwa peke yake kwa muda ule customer service pale. Nikamweleza nahitaji fomu kufungua joint acc na mama yangu. Akachukua fomu akanipa akaniuliza "utaweza kusoma na kuzijaza kweli na mama yako??" Nikamjibu ndio. Akaniambia viambatanisho vinavyohitajika nikaondoka kesho nirudishe fomu.

Kesho yake nimeenda na mama, kufika pale akamkaribisha akakae kwenye kiti mimi akaniambia kasubiri pale yaani pembeni, ndio mama akamwambia nimekuja na binti yangu tunafungua joint acc, kwanza alistuka akamuuliza ni mwanao kumbe mama sikujua. Akaishiwa pozi.

Basi katika kupiga stori na bimkubwa akamwambia sikujua kama una binti mkubwa, bimkubwa akamwambia mara nyingi hayupo nyumbani kwasasa yupo likizo anasoma masters huko mkoa X. Alishangaa kwa nguvu Masters?? Aliniangalia sana. Miaka hiyo bimkubwa na mzee walikuwa wafanyabiashara wakubwa sana mkoani na chapaa zipo za kutosha wanajulikana kila kona. Bank pale walikuwa wanajulikana sana.
Enzi hizo bimkubwa na mzee CRDB wana zile VisaGold so wanahudumiwa kishua....kwahiyo dada akajua huyu sio kwamba anauza matunda kwa dhiki

Dada alikosa raha sana hadi muda anatoa copies akaniambia dada kakae kwenye kiti [emoji1][emoji1][emoji1][emoji1] toka siku hiyo alianza na kunisalimia na kunichangamkia. Mimi wala sikumwonyesha tofauti nikaendelea kumpelekea matunda.
Hii bank ishanitokea sana, hasa wale walinzi wa suma jkt wanadharau sana

Ninapoondoka huwa na maswali mengi sana na wasinielewe


Sometimes nafanyaga transaction kubwa kwa niaba ya walionipa kazi fulani ya kuwasaidia.
 
Kuna siku niliazima gari nikaenda pale best bite kuchukua zaga.

Sasa nilivyoingia ndani nikakutana na pisi tatu za kwenda zinatoka ndani, nikazipa hi zikachuna full kunipandisha na kunishusha, nikaona POA tu nikafuata kilichonipeleka.

Sasa ile natoka nje nikazikuta ziko bize zinajisnap kwenye gari niliyokua nayo, hiii bagoshaaa, mbona walikoma kunijua.

Nilianzisha zogo la maana makusudi kabisa, nikaita mpaka uongozi wa pale nikawaambia wawaambie wateja wao wafute picha zote walizopiga gari yangu otherwise niite Askari pale Obey waniambie wana lengo gani na picha za mkwaju wangu?
Ulitisha Sana mkuu😂
 
Jamaa limekuja mtaani kujenga kamjengo kake,katukuta wenyeji tuna mwagilia moyo,yupo na mkewe hata salamu yaani kakausha tu,kachukua mafundi akawaelekeza kazi pale,zikaja semi 2 zimekula nondo na cememt, kisa anajenga ki gorofa hahaaa,kilicho tokea kabakia kwenye msingi tu wabane wae kwara kuanzia nondo mpaka cement mpaka tofali yaani,kaja kushuka baada ya wiki,wenyeji wamejenga kupitia jamaa kuja kushtuka hana pakuanzia,tunasiki yowee tu huko jamaa hana wakumuuliza ,ndugu zangu ukifika sehem usi mdharamu mtu,huwezi jua atakusaidia lini na wapi.
Aisee wahuni walibebaa Bidhaaa zotee na nyie mkakaushaaa[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Kwanza naomba 'nidiclee' kwamba mm ni mmoja wa ME ambae si mtu wa fashion, yani mimi sijui kuvaa kabisa na sina hiyo passion ya pamba pamba. Nishawahi kusemwa sana na ma-ex wangu kuhusu uvaaji wangu lakini haikusaidia kitu.

Sasa weekend iliyopita nilienda sehemu moja flani hivi amazing, chimbo la uhakika haswaa, limejitenga na limetulia kweli. Nilipigilia kipensi changu na ka t-shirt flan hivi local nikachagua sehem nikakaa, kutizama vizuri nikaona kuna meza amekaa mdada mmoja hivi and of coz she is gud looking nikaamua kujitosa angalau kumpa hata hi 'coz tulikuwa wateja 2 tu, nikamfata nikamsalimu.

Yule dada kwanza alinishusha kuanzia juu mpaka chini then akaitikia salamu yangu ki-design kama namsumbua flani hivi. Nikaomba kujumuika nae kama asipojali. Jibu lake ndo lilinitoa confidence kabsa, alinambia: "Kwahiyo kaka unadhani kila msichana akikaa peke yake anahitaji kampani? Hapana sihitaji" Dah, mwanamme nikajizoazoa pale nikarudi nilipokaa. Nilikaa kama masaa ma3 hivi nikaamsha zangu. Sasa kilichotokea jana ndo kimenifanya niandike huu uzi.

Nilipokea maagizo kuanzia J3 ya wiki hii kuwa leo watakuja watu wa Taasisi flani ya kifedha kutoa semina kwa sisi wafanyakazi kwa ajili ya kutushawishi kujiunga na huduma za Taasisi yao, hivyo mimi nikapewa jukumu la kuwakaribisha na kuwapeleka sehemu ambapo semina itafanyika.

Asubuhi mida kama ya saa 3 hv ugeni ukafika, walikuwa watu kama 7 hivi, kati yao alikuwepo yule dada nilieonana naye weekend.

Wakaingia ofisini nikawakaribisha, wakati mkubwa wao anatoa introduction macho nikayakaza kwa yule dada, bahati nzuri tukagonganisha macho, akashtuka flani, nikajua kashanikumbuka.

Baada ya semina kuisha ikafika kipindi cha watu kujiunga sasa kwa walioshawishika. Nikamfata yule dada nikamuomba aje anielekeze namna ya ujazaji fomu. Alivyofika tu, nikamuuliza "Unanikumbuka?" Akachekaaa, akaniambia "Yani wewe, sikutarajia kama unaweza kuwa unafanya kazi huku", nikamuuliza ulitarajia niwe nafanya kazi wapi? Akaishia kucheka tu. Mawasiliano yake kanipa; fresh bila shida kabisa.

Sasa naomba kuuliza wadau, mshawahi kukutana na situation ya namna hii?
Miaka flani hivi 1994 nikiwa nasoma college, nilikuwa napiga kazi za taxi bubu hapa Dar. Kijiwe flani mitaa ya mwenge. Hiyo kazi nilipiga miaka yote nikiwa nasoma college. Sasa gari yenyewe nliyokuwa napiga nayo taxi, ilikua gari ya kuungaunga kwa sana. Yani spana mkononi. Kwakua na mimi nlikua najua ufundi kimtindo, nlikua naimudu vizuri kazi yangu.

Sasa kuna mama mmoja alikua anafanya kazi taasisi flani binafsi inatoa huduma ya kupokea na kusafirisha vifurushi. Huyu mama alikua na nyodo balaa, kila akinikodi, nikimfikisha safari yake nikidai hela, lazima aiseme gari yangu vibaya mno, mi nikawa namezea tu, ilimradi pesa yangu alikua ananipa.

Yani yale maneno yalikua yananiuma sana mwanaume mpaka nikaweka nadhiri kwamba nikimaliza kusoma nikipata kazi lazma ninunue mashine moja kali sana.

huku na huku, mwaka 1998 nikapata kazi ya uhasibu kwenye shirika moja la waswisi. Nikaajiriwa kama mhasibu msaidizi, moja wapo ya majukumu yangu yakawa ni kutayarisha malipo ya suppliers na ku issue checks kwa suppliers, pale zikiwa zimeshasainiwa na mkubwa wa kazi.

Lile shirika analofanya kazi yule mama mteja wangu wa taxi mwenye nyodo na maneno ya kejeli nalo likiwemo kwenye list ya suppliers.

Siku ya siku yule mama katinga ofisini kuja kuchukua check, kanikuta mwamba ndio mhusika pale, hakuamini macho yake, kajitahidi kunisalimia kwa kuchangamka na mbwembwe zote, mi sikuongea sana nikamsalimu, nikamkaribisha, nikamwonyesha sehemu ya kusaini, akapiga wino, nikampa check yake akasepa.

Next time weekend, kanikuta maskani, kanikodisha, maneno yote ya kejeli hayakuwepo tena, na akawa mteja wangu mzuri sana, mpaka nlipopiga chini hiyo kazi ya taxi, na kuamua kuweka muda zaidi kwenye ajira yangu na waswiss.

Hayo ndio maisha, people will judge you by your looks or mazingira utakayokuwepo, but all is good, keep hustling, no matter what.
 
Aiseee...!
Umenikumbusha mkasa mzuri tena wa zamani kidogo.

Ni mkasa wa kweli wa umfikiriaye ni mswahili wa low class, kumbe miaka ikipita ndo anakuwa matawi ya juu.

Kulikuwa na dame, mzuri sana , miguu ya kupendeza figure eight na kwa kweli kila nikimuona moyo waenda mbio.
Na alikuwa ni cheusi mangala, super black, akicheka meno meupee ya kuvutia, juu ni afro zuri natural, hadi leo hii.
Wazazi wake nilikuwa nawafahamu, nivyo nikaona itakuwa rahisi kukubalika.
Ndo kwanza miaka hiyo nimemaliza Form six, dame anaelekea kumaliza form IV.

Sasa nikawa nimepata kibarua cha ukarani benki, hivyo vijisenti vya kununua soda sikosi.
Nikamwaga sera kwa dame yule.
Yeye akawa kama ananihurumia tu, maana anaona nampenda sana lakini anashindwa kuwa muwazi.
Miezi ikapita mingi tu, tuna date na kila tukionana naona hakuna maendeleo, hadi dada zangu wakaanza kunihurumia pia, penzi linavyonitesa.

Mwisho yule dame akaniambia wazi, we bwana si saizi yangu, kwanza watoka Uswazi.
Akaniambia nina mchumba mtoto wa balozi fulani, famous hapa mjini.
Na wazazi wa yule dame walilielewa hilo, kulingana na dame mzuri.

Basi sikukata tamaa, nilijahidi kumweleza dame wangu huyu kuwa mimi haipiti miaka miwili nitaingia chuo kikuu na nikimaliza sitakosa noti ndefu kukutunza wewe na familia, nikubalie tu.
Dame akakataa kata kata.

Siku aliyohitimisha maneno ya kunikataa niliugua, tena homa kali na ya kweli kabisa.
Sikujua kuwa penzi literaly ni homa ya moyo!
Nilinyong’onyea na kulala kitandani siku mbili.

Ile homa naikumbuka vizuri sana.
Slowly homa iliondoa na kukausha upendo wote kwa yule dada.
Nilistaajabu hata mimi kwani nikajiuliza , kwa nini niteseke?
Na kwa muda mrefu sikutafuta tena msichana mwingine awe girlfriend wangu wa kudumu, ile homa iliniumiza ifikra.

Miaka ikapita, na kweli nikaenda UDSM, na kukamilisha kadigilii kangu na kazi nzuri nikapata.
Kazi nikaendelea kupata nzuri zaidi, kumbe yule dame, cheusi mangala, ananifuatilia kwa mbaali.

Miaka mingi ikapita, na mambo yangu alhamdulilhi yakawa si mabaya sana.
Wakati huo ikawa nimepata fiancee kwa kweli mzuri sana, tena half caste.


Huku nyuma dame cheusi akajileta, na tukala mzigo.
Aliponiuliza itakuwaje sasa, nikamwambia tu ukweli kuwa naoa miezi michache ijayo, ile chance haikuwa yetu.
Alilia sana yule dame mzuri.

Mbaya zaidi mie kikazi nikawa matawi ya juu sana, kama nilivyomuahidi dame cheusi nilipokuwa namtongoza na akakataa.
Sikumuuliza imekuwaje na yule mtoto wa balozi, maana sikuona kama yananihusu.
Dame cheusi mangala bado ni mzuri na akajaolewa na classmate wangu.

UPDATE:
Tunaandika hadithi ambazo ni za ukweli kabisa.
Cheusi Mngala baadaye niliambiwa mume wake alikuja fariki kwa ugonjwa wa sukari.
Ingawaje wengi tuihisi ni kale kaugonjwa kanako sumbua.
Kilichonishtua majuzi ni kuambiwa Cheusi Mangala naye kafariki, nilivyompenda nililia!
Hii ni update ya hivi karibuni.
Jamani dunia tunapita.
 
Kwanza naomba 'nidiclee' kwamba mm ni mmoja wa ME ambae si mtu wa fashion, yani mimi sijui kuvaa kabisa na sina hiyo passion ya pamba pamba. Nishawahi kusemwa sana na ma-ex wangu kuhusu uvaaji wangu lakini haikusaidia kitu.

Sasa weekend iliyopita nilienda sehemu moja flani hivi amazing, chimbo la uhakika haswaa, limejitenga na limetulia kweli. Nilipigilia kipensi changu na ka t-shirt flan hivi local nikachagua sehem nikakaa, kutizama vizuri nikaona kuna meza amekaa mdada mmoja hivi and of coz she is gud looking nikaamua kujitosa angalau kumpa hata hi 'coz tulikuwa wateja 2 tu, nikamfata nikamsalimu.

Yule dada kwanza alinishusha kuanzia juu mpaka chini then akaitikia salamu yangu ki-design kama namsumbua flani hivi. Nikaomba kujumuika nae kama asipojali. Jibu lake ndo lilinitoa confidence kabsa, alinambia: "Kwahiyo kaka unadhani kila msichana akikaa peke yake anahitaji kampani? Hapana sihitaji" Dah, mwanamme nikajizoazoa pale nikarudi nilipokaa. Nilikaa kama masaa ma3 hivi nikaamsha zangu. Sasa kilichotokea jana ndo kimenifanya niandike huu uzi.

Nilipokea maagizo kuanzia J3 ya wiki hii kuwa leo watakuja watu wa Taasisi flani ya kifedha kutoa semina kwa sisi wafanyakazi kwa ajili ya kutushawishi kujiunga na huduma za Taasisi yao, hivyo mimi nikapewa jukumu la kuwakaribisha na kuwapeleka sehemu ambapo semina itafanyika.

Asubuhi mida kama ya saa 3 hv ugeni ukafika, walikuwa watu kama 7 hivi, kati yao alikuwepo yule dada nilieonana naye weekend.

Wakaingia ofisini nikawakaribisha, wakati mkubwa wao anatoa introduction macho nikayakaza kwa yule dada, bahati nzuri tukagonganisha macho, akashtuka flani, nikajua kashanikumbuka.

Baada ya semina kuisha ikafika kipindi cha watu kujiunga sasa kwa walioshawishika. Nikamfata yule dada nikamuomba aje anielekeze namna ya ujazaji fomu. Alivyofika tu, nikamuuliza "Unanikumbuka?" Akachekaaa, akaniambia "Yani wewe, sikutarajia kama unaweza kuwa unafanya kazi huku", nikamuuliza ulitarajia niwe nafanya kazi wapi? Akaishia kucheka tu. Mawasiliano yake kanipa; fresh bila shida kabisa.

Sasa naomba kuuliza wadau, mshawahi kukutana na situation ya namna hii?
Juzi tarehe 20 Jan 2023 nipo zangu Mwanza nimekuja kupiga mishe 2, 3!
Kuna mdada ni mpangaji kwenye nyumba yangu hapa lkn hatukuwahi onana zaidi ya kutumiana contracts kusign na mawasiliano ya simu.

Basi last week nikampigia simu kuwa nitakuwepo Mwanza kwa ajili ya kazi fulani ya marekebisho hapo nyumbani (kimsingi kuongeza ubora wa nyumba) basi nikafika J2 pale site... nikaanza kazi na mafundi piga kazi hadi jioni nikasepa zangu...J3 nikafika tena site...piga kazi za hapa na pale na mafundi mara pap sister ameingia akanisalimia tu kishikaji nikaitika akaingia ndani baadae akaja kuwapokea watoto wanatoka shule jioni hiyo saa 11 hv... baadae nikamwambia sister sorry niliona simu yako jana lkn late sana nilikuwa nishalala akahamaki; simu nikamwambia ndiyo...nadhani aka recall baadae akasema wewe ndo baba mwenye nyumba nikamwambia yap....ghafla akakunja mikono kama nidhamu fulani akasema sorry sikukutambua nami nikamwambia worry out ... basi akaniletea maji ya kunywa tukapiga story tu kidogo.....

Baadae akafunguka kuwa dah yaani mi naongea na wewe siku zote najua ni bonge la mbaba...nikacheka zangu tu nikamwambia surely ni bonge la mbaba sema nafanya sana mazoezi ndo maana sina nyama zembe wala tumbo la kuwekewa puto....
 
Juzi tarehe 20 Jan 2023 nipo zangu Mwanza nimekuja kupiga mishe 2, 3!
Kuna mdada ni mpangaji kwenye nyumba yangu hapa lkn hatukuwahi onana zaidi ya kutumiana contracts kusign na mawasiliano ya simu.

Basi last week nikampigia simu kuwa nitakuwepo Mwanza kwa ajili ya kazi fulani ya marekebisho hapo nyumbani (kimsingi kuongeza ubora wa nyumba) basi nikafika J2 pale site... nikaanza kazi na mafundi piga kazi hadi jioni nikasepa zangu...J3 nikafika tena site...piga kazi za hapa na pale na mafundi mara pap sister ameingia akanisalimia tu kishikaji nikaitika akaingia ndani baadae akaja kuwapokea watoto wanatoka shule jioni hiyo saa 11 hv... baadae nikamwambia sister sorry niliona simu yako jana lkn late sana nilikuwa nishalala akahamaki simu nikamwambia ndiyo...nadhani aka recall baadae akasema wewe ndo baba mwenye nyumba nikamwambia yap....ghafla akakunja mikono kama nidhamu fulani akasema sorry sikukutambua nami nikamwambia worry out ... basi akaniletea maji ya kunywa tukapiga story tu kidogo.....

Baadae akafunguka kuwa dah yaani mi naongea na wewe siku zote najua ni bonge la mbaba...nikacheka zangu tu nikamwambia surely ni bonge la mbaba sema nafanya sana mazoezi ndo maana sina nyama zembe wala tumbo la kuwekewa puto....
Hukupiga mwanangu??
 
Tokea hii itokee zimepita Kama wiki tatu hivi....

Baada ya kumaliza chuo huku ajira zikiwa ni ndoto za Abunawasi Kama sio Alinacha, mzee wangu aliamua kunipiga tafu ili tusije kulaumiana huko mbele. Alifumba macho akavunja kibubu akanunua trekta jipya "Massey Ferguson 275" likiwa na tela pamoja na majembe yake halafu akanikabidhi funguo na kadi na kuniambia Kama ninataka mali nitazipata shambani.

Katika kusubiri msimu wa kwenda kuzitafuta mali shambani nikaamua kulipeleka trekta kijijini kwetu maana sio mbali ili niwe nawabebea watu mizigo. maisha ni kujiongeza shekhe! Alhamdulillah, kazi inaenda vizuri hasa ukizingatia suka mimi mwenyewe! Sometimes hata mshua mwenyewe akishirikiana na mama huwa wananipiga mzinga, nawatoa kiroho safi. Kimsingi hata zile text za "Baby nikuambie kitu" siziogopi huwa nazijibu pasina shida yoyote!

Last week nilipata dili la kubeba tofali. Wakati wapakiaji wanaendelea na kazi ghafla Kuna jamaa alikuja pale site akiwa na mwanamke! Walikuwa wamependeza wenyewe, wanawaka hatari na jua lile la utosi wananukia marashi tu. Mikogo yao ilitosha kuonyesha wapo kwenye lindi la huba na mahaba yasiyoelezeka.

Wakafika pale huku wanajipukuta vumbi kwa leso, site hapataki utanashati. Basi jamaa akalitazama trekta Kama traffic anayetafuta kosa, halafu bila hata salamu japo sio lazima akaniuliza linabeba gunia ngapi za mahindi, nikamtajia gunia 35. Akatikisa kichwa kuonyesha ni uwezo mdogo sana! Mbulumundu kabisa, wakati Kijiji kizima trekta langu ndio kubwa na linabeba kuliko wengine wote! Kwanza kijiji chote matrekta yapo matatu tu na langu ndio King of the empire! Nilimvumilia maana mteja sio fala ni mfalme.

Basi akajinyonganyonga pale, akajishingondoa paleee, akajimwemwesa kwa pozi za ashuo mbele ya demu wake halafu akauliza gharama za usafiri, nikamtajia. Akasema,

"Eeh... dogo mbona unapiga sana, bosi wako anajua lakini?" Achana kwanza na ishu za bosi, kwanini aniite dogo tena mbele ya demu wake hasa ukizingatia bei niliyomtajia ni very reasonable? Why? Why always me!

Mjinga aliniharibia siku, shubamiti! Akaongeza chumvi kwenye kidonda,

"Kama vipi nipe namba ya mwenye trekta niongee nae maana nyie madereva huwa mnazingua Sana!" Itoshe tu kusema yule jamaa aliondoka kwa dharau huku akisapotiwa na demu wake! Nilipoteza pambano na sikujisikia vizuri.

Wale wanaopakia tofali ndio wakaniambia kuwa jamaa na demu wake wote ni walimu wa shule ya msingi hapo kijijini. Wanavimba sababu wamesoma. Sasa nikashangaa wanalingia elimu au ajira? Diploma ya kumfanya mtu alinge kweli? Kama wanalinga kwa sababu ya ajira, je wangekuwa makatibu wa elimu wizarani ingekuaje? Just imagine jamaa ndio angekuwa Makonda, hapo mjini Daslam mngeishije? Basi siku ikaisha hivyo kinyonge!

Juzi kati mzee aliniambia nisiache ku apply nafasi za ualimu zilizotangazwa na serikali hata Kama uwezekano wa kupata ni 0.000. So siku hiyo sikwenda bush kwenye trekta nikabaki town ili nifanye application! Nikaenda internet cafe ili mambo yaende fasta!

Kama nusu saa hizi nikasikia sauti Kama naifahamu hivi, kugeuza shingo kumbe yule jamaa na demu wake wanaingia wakiwa na jamaa mwingine. Tukagongana macho, wakatoa macho Kama mjusi kapigwa spana! Hawakutarajia kuniona pale! Dereva wa trekta na macomputer wapi na wapi? nikawapotezea!

Kumbe wamekuja kumsaidia kufanya application yule jamaa ni mshkaji wao. Walikuwa hawajui vitu vingi na mhudumu wa pale cafe hakuwa na msaada kwao akawaambia waje kuniuliza Mimi maana kaniona nafanya application. Hawakuamini kabisa! Dereva wa trekta anafanya application? Kivipi yaani?

Ulikuwa mtihani mzito kwao, liliwashuka, sura zao zikasawijika, wakakosa pozi, wakacharara, waliishiwa kwa kweli ila watafanyaje? Wakaja huku wanajichekesha wakanisalimu kwa kunipa mkono bila ajizi na Mimi nikawapa mkono na tabasamu langu la uongo usiojificha mdomoni.

Wakashangaa Sana kuona ninabonyeza sehemu ya TCU badala ya NACTE. Wakaniuliza nimesoma chuo gani, usitake kujua niliwajibu Nini ila unajua tena sisi wa UDSM tunavyojionaga tumeyapatia maisha! Niliwajibu kwa kadri inavyopaswa!

Yule binti akasema, "sio mbaya lakini, umejishikiza kwenye kuendesha trekta" nikamuangalia usoni nikamwambia hapana Lile trekta ni langu nashindwa kumuajiri dereva maana wanakuwaga wasumbufu Sana! Nilihakikisha wanajua hadi kipato changu kuwa wakiunganisha mishahara yao wote Kama mambo yakikaa sawa Mimi naingiza ndani ya wiki mbili tu.

Jamaa mkosa adabu alikosa raha. Kwenye kiti palikuwa hapakaliki mbaya zaidi demu wake aliweza kwenda sawa na upepo ali connect na Mimi vizuri kabisa! Hadi namba ya simu alinipa ili wakiwa vizuri nikawabebee mahindi yao.

Sasa hapa Nina namba ya simu ya demu, tunachati tu WhatsApp kuhusu changamoto za Maisha na fursa za baadae. Ghafla nimekuwa motivation speaker wake! Ananichukulia Kama role model wake! Sijui Kama jamaa nimemsamehe au vipi acha niendelee kuchati na demu wake kwanza!

Inaonekana ww mwanangu ni kichwa san yan hauna papara
 
dah na mim umenifanya nilete kisa changu ambacho hakina hata miezi miwili.
kuna mdada jina yupo katika ofisi fulani ni majirani zetu(home).Ni wale watu wanaoringa kupita kiasi ukimsalimia kama hakuoni vile( hii ishatokea kama mara 3) last time niko zangu na town anafanya kazi pale benjamin mkapa,nmemkuta yupo na wenzake wakati huo nilikuwa niko na kaka yangu mkubwa.

Nikamchangamkia ila mwenzangu kanilia buyu namtambulisha kwa bro kuwa huyu ndo jirani dah mixer mfyonyo juu hakuna siku roho ilikuwa inaniuma kama siku siyo.

sasa week kama 3 nyuma natokea moro nmeingia kama saa 6 hivi nikasema ngoja sku ya leo nikasalie pale upanga maamur ni mskiti ambao waislamu wengi sana wanapenda kuosha maiti pale na kwenda kuzikia makaburi ya kisutu.

Nilivyofika pale pakawa kama na stori za chini kwa chini kuwa muosha maiti amekimbia baada ya kuosha maiti zaidi ya tano kitu ambacho syo cha kawaida, basi kwenye maongezi maongezi ikajulikana kuwa kuna maiti kama 2 zimeshndwa kuoshwa ndugu hawajui na muoshaji kakimbia(hofu ya corona)

Basi tukajitokeza mimi na mwenzangu tukaingia chumba cha maiti tulikuwa kama wa 4,tukaiosha ile ya kwanza,then tukafata ile ya pili zote tukaandaa safi kabisa ila ile ya pili niligundua alikuwa na baba wa yule dada maringo.

wakati tunatoka kuosha ndugu wakatuvuta pembeni wakatupa kama laki 3,wenzangu walichukua ila mimi sikuchukua hata cent sasa kumbe aliyekuwa anatoa hela ni mdogo wa yule(dada maringo) ambae anaishi nairobi kaja kumzika mzee wake but hanijui.

basi tukachukua maiti tukaenda zetu kuzika makaburi ya kisutu, wakati narudi zangu maeneo ya home ndo nakuta msiba sasa huku zogo pembeni likiwa ni muosha maiti kukimbi, basi jamaa akaniona mdogo mtu tukasalimiana pale ile furaha aliyokuwa nayo akanishika mkono mpaka uwani ambako kulikuwa na dada zake na mjane akanitambulisha na jinsi nilivyowasaidia dada mtu(cha maringo) aliangua kilio kupita maeleozo akaniomba namba nkampa.

baada ya kama dakika 30 baada ya kurudi home nikatumiwa mesage kama gazeti ya kuniomba radhi/msamaha mie nka act humble tu japo kila siku anataka tuonane but kila akinipigia namwambia niko moro japo anafosi anitumie hata nauli nikaonane nae au aje yeye but namchomolea.

katika maisha usimdharau mtu kwani huwezi jua nani atakaekufaa kwani unaweza kuwa trilionea but msaada wako ukatoka kwa mwenye kupata sh 500 kwa siku

Yan katika nakala zote hii ni best zaid
 
Mimi huwa ni ngumu mtu kunitambua kama najua kitu au niko interested kwenye jambo fulani kwasababu ni mtu nisiyependa show off (kujionesha). Nitaelezea machache katika engo tofautitofauti


Madrasa
Enzi za udogo (ujana) nikiwa madrasa jamaa katika kusoma Quran akakosea halafu yeye ndo ana jukumu la kutufundisha basi alipotoka tu yule mfundishwaji nikamrekebisha kistaarabu kabisa jamaa alistaajabu sana ilibidi amuite yule aliyekuwa akifundishwa arudie upya. Ebana wee tangu hapo nikawa nimechokoza moto vijana (maustadh) karibia wote wakawa wakitaka kwenda kusoma (kuaridhi) kwa mwalimu lazima waanzie kwangu kwanza ili nikague makosa yao na alhamdulillah kwa uwezo wa Allah nilikuwa sibahatishi ingawa sura hizo sikuwa nimezifikia bado

Cherehani
Mzee alikuwa anapokea tenda fulani ya kushona halafu anampa kaka sasa ikafika kipindi kaka hayupo yule mtoa tenda akaambiwa safari hii ile kazi yule uliyemzoea hayupo utafanya na huyu (yaani Mimi) jamaa akawa haniamini tena akasema kabisa "huyu dogo hivi aisee ataweza?" Mzee akamwambia wewe usijali huku Mzee nae akiwa na mashaka kwenye spidi yangu basi nilikamatia ile kazi kwa ubora wa hali ya juu na ni ndani ya muda. Mbona walinyoosha mikono na mpaka kesho yule jamaa ananiita fundi

Sensa
Nimeitwa nikarekebishe kishikwambi cha karani, maudhui kaniambia niwakute ofisi ya kijiji basi nikachukua boda fasta. Kufika nakuta mtendaji anaongea na yule maudhui nawapa hai makarani wanaitikia, nawasogelea mtendaji nampa salamu akageuka tu kuniangalia kisha akaendelea kuongea mazungumzo yake nikaachana nae maana huwa sirudiagi salamu muda huo maudhui anafanya kama anandoka kunielekea eti yule mtendaji anamzuia "bwana aachana nao hao angalia huku bado sijamaliza mimi unaenda wapi?" (Akili yake akijua mimi na yule bodaboda labda ni wageni wake katika ofisi yake). Basi yule maudhui akamwambia huyu anahitajika kwingine akiondoka ndo basi tena basi akaambiwa huyu ndo IT wetu wa kata (kama unavyojua tena kwenye sensa watu tulibandikwa matitle makubwamakubwa wakati hatuna lolote- tulitambulika kama maafisa wa sensa ambapo karani aliitwa tu kawaida afisa wa sensa maudhui aliitwa afisa maudhui, mtu wa tehama aliitwa IT). Basi yule mdada aliduwaa yaani akapoa hadi nikawa namuonea huruma akiniangalia hanimalizi na Mimi kwa sifa nikashuhulikia kilichonipeleka kisha ndefu najidai nina haraka

Muvi
Imezoeleka wa shule za kata hatujui ung'eng'e sasa bana eti tunaangalia muvi enzi hizo ndo nimetoka form four jamaa akaniambia hii muvi hutaielewa maana haijatafsiriwa kama muvi zenu mlizozoea basi nikamwambia kama wanaandika (subtitles) basi nitajikaza akaniambia hakuna hiyo kitu. Kucheki ati jamaa akaanza kunishereheshea baadhi ya vipande sasa ikawa kamba nyingi ikabidi nimtolee uvivu mara paap! Mimi ndo namsaidia kumtafsiria tena


Misikitini
Kwa wale wanaoenda kuswali misikitini mtanielewa zaidi. Tumehamia sehemu kwahiyo ikabidi nihame hata msikiti niende ulio karibia na kwetu. Sasa kawaida yangu (kawaida yetu vijana wa madrasa) huwa hatujirembirembi katika maswala ya dini basi swala ikikimiwa tu tayari nipo beside ya mkimuji mbele kabisa. Basi siku hiyo ustadh mkimuji akanitoa ananambia nikae nyuma hapo mbele niwaachie mashekhe (wakati kiuhalisia nikiwaangalia ni mashekhe umri yaani wazee na sio mashekhe kwa elimu). Mungu si Athumani bwana siku hiyo tumechelewa swala kidogo na yeye akiwemo basi mmoja akasema Fulani tuswalishe bana (akinitaja Mimi) basi tangu hapo yule jamaa akawa akiniangalia tu hanimalizi

Wakati nipo chuoni tena (ualimu) msikiti mmoja jamaa mmoja nae alichelewa nikamswalisha swala ya sauti basi kutoka akaniambia "mbona mtu akikuangalia hawezi kuamini kama ni wewe uliyeswalisha pale? Yaani uvaaji wako na namna ulivyo me nkadhani wewe ni mkristu."

Huku kazini nimeswali nao karibia mwaka hawajanigundua sasa kilichokuja kuniponza ni somo la Dini. Ikabidi nijidhihirishe tu lakini na wao walidhani ni muislamu jina tu hata majina yangu walidhani ni majina tu ya mchongo
 
Mimi kuna jamaa tumesoma wote form 1&2 tulikuwa washkaji maana ndo tulikuwa tunaongoza class
Nikafukuzwa so 3&4 tulikuwa tunakutana likizo tu
Baada tukapotezana Ila me nilikuwa napata data zake alimaliza degree ya mambo ya afya akaingiza jeshi then akapelekwa mondul kusomea sijui vyeo then akapangwa mikoan huko
2020 sm inaita ni jamaa " Flan vip? Za siku niomeambiwa uliacha kazi ya ualim now unapiga umachinga dar? Tuonane basi ndg" ni kweli niliachaga ualim nikajichanganya kariakoo kabla sijatoboa kibiashara ambayo hakuwa anajua kuwa nilitoboa tena kwa kiwango kikubwa
Basi tukakutana Mliman me ndo nilitangulia pale Grano
Jamaa akaja "agiza chochote ntalipa kaka " mbwembwe nyingi
Me na mwili mdogo halaf kwenye uvaaji me ni 0% so ngumu sana mtu kujua huyu yuko vzr au la!
Tukiwa pale dem wangu akaniambia nimfate kazin kumrudisha home alkkuwa mjamzito nikamwambia mshkaji akajibu " haina shida na usafir kaka twende tutamchukua tu nishanunua gari siku hizi mambo yangu fresh "
Nikakubali tukatoka nikamwambia tupite nichukue langu tuongozane ndo anaanza kushangaa " kwan una gari? Machinga ana gari mura au nimedanganywa!?"
Tumefika mzee anaona BIMA imepaki nafungua namwambia twende na hii tukirud tutapitia yako
Jamaa alikosa aman sikujua why ila alikosa aman kabisa
Tumemaliza kule namrudisha Mliman kumbe ana Swift old mole dah jamaa tangu pale alikata mawasiliano mpk leo tunaview tu status
Hihihihi[emoji23][emoji23]
 
Kitu kingine ambacho sisahau mpaka leo aisee ni wakati nipo mdogo ilikuwa matangazo ya pombe yale mfano Heineken na tusker yalisababisha nikawa napenda sana Heineken. Sasa siku nikaikuta njiani mtu kabakiza ile ya kopo nikaokota namwambia kaka kuwa nataka niinywe. Basi ile nimeinyanyua nataka kupeleka mdomoni jamaa aliniambia acha wewe pombe hiyo! Basinikaitupa. Ebana wee akaipeleka ile hadithi kwa Mzee basi nyumbani wakawa wanaambiana kuwa nikija kuwa mkubwa nitakuwa mlevi mmoja mkubwa na matata sana... Walinitabiria pia kuwa nitakuja kuwa mtukutu sana kutokana na namna nilivyokuwakuwa katika makuzi yangu lakini cha ajabu ni kwamba kufika darasa la 3-4 zile dalili ovu zote zikatoweka nikawa mtoto mwema sana

Tanbihi;
Namshukuru Mola mpaka leo sijawahi kunywa pombe yoyote Wala bangi/sigara/mirungi wala energy wala shampeni. Kisa cha Mimi kuipenda Heineken naomba nitoe fundisho kwa wazazi wenzangu. Tangu nakuwa nimelelewa kwamba pombe ni haramu lakini nguvu ya media (video) ikanifanya niipende kwasababu kwanza hawasemi kwamba ile ni pombe na pia kuipamba pamba kule na maneno mengi basi moyoni nikaamini ile inanifaa na huku nikimchukulia yule wa kwenye tangazo kama ndiye role model wangu. Maana yake nisingekuwa na kaka ningeinywa au hata kaka asingesema ni pombe huenda ningeitafuta kivingine nipoze roho (pombe tulikuwa tunajua za kienyeji tu na bia ilikuwa ni safari na Kilimanjaro). Tuwafuatilie watoto na ma video haya
 
Back
Top Bottom