Ushawahi kufedheheka (kupata dharura) ukiwa safarini kwenye usafiri wa umma?

Ushawahi kufedheheka (kupata dharura) ukiwa safarini kwenye usafiri wa umma?

EINSTEIN112

JF-Expert Member
Joined
Oct 26, 2018
Posts
21,711
Reaction score
35,644
Kuna mambo mengi yanaweza kukutokea ukiwa safarini

1. Kutapika kwenye gari
2. kubanwa na tumbo la kuharisha
3. Kuachwa na gari wakati wa kuanza safari au wakati mmeshuka kupata chakula.
4. Mengineyo

Mwaka flani nilikuwa natoka Morogoro kwenda Dar. kabla ya safari nakumbuka nlikula zile chapati za Azam (ready made) saivi hazipo sokoni kwenye mgahawa wa wahindi flani pale Morogoro.

Safari ikaanza kufika Mlandizi tumbo likaanza kuuma na nimekaa katikati ya basi la Abood, aisee maumivu yale sidhani kama nishawahi kuumwa makali kama yale nilijitahidi sana kuvumilia ila uzalendo ukanishinda nikaomba kushushwa njiani nikaingia choo cha Bar nikaharisha saaana kama nusu saa nipo chooni, nikaenda kununua dawa pharmacy, baadae nikachukua daladala nikaendelea na safari.

Hebu tupe kisa chochote kilichowahi kukukuta ukiwa safarini kwenye Mabasi.

Karibuni wadau.

Nishamaliza!!

12800330_192579067777375_2771212008545494846_n.jpg
 
Nakumbuka mwaka 2006 natoka Iringa nakwenda Moro nilisafiri na kampuni hiyo,nili pata chakula pale aljazera baada ya mwendo kidogo tumbo likapoteza network nili vumiliaaa hadi nika ona kuendelea kuvumilia nita haribu safari ya wengine.

Nlipo amua kuelekea kwa dereva niombe fair daaa MUNGU mkubwa basi lika anza kumiss dereva bila shuruti kaweka kando niliteremka kwa spidi nikazama chaka nika sevu ngoma tartiiibu bahati nilikuwa na kopo la maji nika jiswafi vizuri.

Walipo maliza kukorokocha safari ikaendelea baada muda tena tumbo lika badilika tenaa,na gari ika zingua tenaa hapo tulikuwa kwenye maeneo wanaishi wamasai pale nika omba kwenye nyumba ingawa kuingia mle toilet ilibidi ni cha gue pa kuka nyaga manake watoto walikuwa wame kichafuaa vibayaa nashukuru nika maliza shida zangu pale.

Toka hapo tumbo haliku zingua tena na gari haikusumbua hadi tuna ingia Morogoro, hakuna mtu aliye jua kama nilikuwa na endesha siku ile sipati picha ninge haribu mambo kwenye basi.
 
Mimi nilipanda basi fulani kwenda mwanza 2012 ilikua, ikafika saa sita, saa Sana, njaa imenikung'uta najiuliza tunashuka saa ngapi Kila, saa name, basi likasimama mji flani siujui Kuna pilikapilika hapo nikajua ndo mda wa msosi, nikashuka nikawaona nazunguka nachagua nyama nzuri nikasohea hadi nikawa mbali na basi, basi nimeagiza zangu nyama na ndizi nasubiri ipashwepashwe hamadi kugeuka naona basi liiiileeee linapotelea, aiseee, nilikimbia Kama hatua tano nikakimbuka msosi, nikarudi nikamwambia finga nae alielewa mchezo akaitupia kwenye mfuko mweusi nikadaka bodaboda nikamwambia wahi lile basi chap, aiseee

Kwa Mara ya Kwanza ndio nikajua pikipiki ikikimbia Sana ule mtetemeko unawashwa Sana, bahati yangu Ni kwamba kumbe sehemu ya Kila ilikua kamji kengine Kama kilomita tano ama nane tu kwa mbele, na ile Toyo nisingeikuta, niliwakuta ndio wamepaki wanashuka Kula, aiseee niliwaka!nyie mnaondokaje mnaacha abiria, ilikua Zoho pale ila kiukweli walinizidi hoja, hatukutangaza Ni muda was kushuka kula. Ikaisha ndizi na nyama haijakatwa nikalia kwenye basi mzuka was kushuka ukapotea Hadi mwanza.
Story nyingine.

Natoka Arusha naenda dar 2016 nikawa nimenunua vodka zangu kadhaa nimechanganya na takeaway za stone naendelea kugonga taratibu, yaani asikwambie mtu Kila kituo nilikua nashuka kukojoa, Sasa ikafika mahali hamna kusimama Kama masaa matatu ivi sikumbuki ilikua wapi, mkojo umesimamia mlangoni Mimi nimezuia mlango Kama nasuia mwizi asivunje aiseee, nimetoka kwenye siti yangu nipo kwa dereva pale namsihi japo nikojoe Yani dk 2 tu, mzee baba ananiambia subiri kidogo, inapita nusu saa, nalia Tena, ananiambia subiri kidogo nilimsumbua Hadi akaona keto akasimama akasema haya kuchimba dawa. Aiseee nilifurahi, nilikua wa kwanza kutoka was mwisho kuingia Mana nilifungulia bomba, nikajifunza sitafanya Tena huo upuuzi
 
Nusu saa nzima unaharisha na bus likakusubiri? Me dk 5 tu dereva aliwaka kinyama na hapo nilikuta bus lishasogea linataka kutoka.
Hujaelewa au labda nimeandika vibaya

Ipo hivii, nlishuka gari ikaondoka
 
Nakumbuka mwaka 2006 natoka Iringa nakwenda Moro nilisafiri na kampuni hiyo,nili pata chakula pale aljazera baada ya mwendo kidogo tumbo likapoteza network nili vumiliaaa hadi nika ona kuendelea kuvumilia nita haribu safari ya wengine!

Nlipo amua kuelekea kwa dereva niombe fair daaa MUNGU mkubwa basi lika anza kumiss dereva bila shuruti kaweka kando niliteremka kwa spidi nikazama chaka nika sevu ngoma tartiiibu bahati nilikuwa na kopo la maji nika jiswafi vizuri!

Walipo maliza kukorokocha safari ikaendelea baada muda tena tumbo lika badilika tenaa,na gari ika zingua tenaa hapo tulikuwa kwenye maeneo wanaishi wamasai pale nika omba kwenye nyumba ingawa kuingia mle toilet ilibidi ni cha gue pa kuka nyaga manake watoto walikuwa wame kichafuaa vibayaa nashukuru nika maliza shida zangu pale!

Toka hapo tumbo haliku zingua tena na gari haikusumbua hadi tuna ingia morogoro!!hakuna mtu aliye jua kama nilikuwa na endesha siku ile sipati picha ninge haribu mambo kwenye basi!!
Duh pole mkuu
 
Mimi nilipanda basi fulani kwenda mwanza 2012 ilikua, ikafika saa sita, saa Sana, njaa imenikung'uta najiuliza tunashuka saa ngapi Kila, saa name, basi likasimama mji flani siujui Kuna pilikapilika hapo nikajua ndo mda wa msosi, nikashuka nikawaona nazunguka nachagua nyama nzuri nikasohea hadi nikawa mbali na basi, basi nimeagiza zangu nyama na ndizi nasubiri ipashwepashwe hamadi kugeuka naona basi liiiileeee linapotelea, aiseee, nilikimbia Kama hatua tano nikakimbuka msosi, nikarudi nikamwambia finga nae alielewa mchezo akaitupia kwenye mfuko mweusi nikadaka bodaboda nikamwambia wahi lile basi chap, aiseee

Kwa Mara ya Kwanza ndio nikajua pikipiki ikikimbia Sana ule mtetemeko unawashwa Sana, bahati yangu Ni kwamba kumbe sehemu ya Kila ilikua kamji kengine Kama kilomita tano ama nane tu kwa mbele, na ile Toyo nisingeikuta, niliwakuta ndio wamepaki wanashuka Kula, aiseee niliwaka!nyie mnaondokaje mnaacha abiria, ilikua Zoho pale ila kiukweli walinizidi hoja, hatukutangaza Ni muda was kushuka kula. Ikaisha ndizi na nyama haijakatwa nikalia kwenye basi mzuka was kushuka ukapotea Hadi mwanza.
Story nyingine.

Natoka Arusha naenda dar 2016 nikawa nimenunua vodka zangu kadhaa nimechanganya na takeaway za stone naendelea kugonga taratibu, yaani asikwambie mtu Kila kituo nilikua nashuka kukojoa, Sasa ikafika mahali hamna kusimama Kama masaa matatu ivi sikumbuki ilikua wapi, mkojo umesimamia mlangoni Mimi nimezuia mlango Kama nasuia mwizi asivunje aiseee, nimetoka kwenye siti yangu nipo kwa dereva pale namsihi japo nikojoe Yani dk 2 tu, mzee baba ananiambia subiri kidogo, inapita nusu saa, nalia Tena, ananiambia subiri kidogo nilimsumbua Hadi akaona keto akasimama akasema haya kuchimba dawa. Aiseee nilifurahi, nilikua wa kwanza kutoka was mwisho kuingia Mana nilifungulia bomba, nikajifunza sitafanya Tena huo upuuzi
Bro vodka mbona kama haileti mkojo ni kama Konyagi na K.Vant
 
Nakumbuka mwaka 2006 natoka Iringa nakwenda Moro nilisafiri na kampuni hiyo,nili pata chakula pale aljazera baada ya mwendo kidogo tumbo likapoteza network nili vumiliaaa hadi nika ona kuendelea kuvumilia nita haribu safari ya wengine!

Nlipo amua kuelekea kwa dereva niombe fair daaa MUNGU mkubwa basi lika anza kumiss dereva bila shuruti kaweka kando niliteremka kwa spidi nikazama chaka nika sevu ngoma tartiiibu bahati nilikuwa na kopo la maji nika jiswafi vizuri!

Walipo maliza kukorokocha safari ikaendelea baada muda tena tumbo lika badilika tenaa,na gari ika zingua tenaa hapo tulikuwa kwenye maeneo wanaishi wamasai pale nika omba kwenye nyumba ingawa kuingia mle toilet ilibidi ni cha gue pa kuka nyaga manake watoto walikuwa wame kichafuaa vibayaa nashukuru nika maliza shida zangu pale!

Toka hapo tumbo haliku zingua tena na gari haikusumbua hadi tuna ingia morogoro!!hakuna mtu aliye jua kama nilikuwa na endesha siku ile sipati picha ninge haribu mambo kwenye basi!!
Mnapotaka kusafiri nunueni ant biotic Safari ikianza unameza

Metronidazole,tinidazole ni nzuri sana utakuwa salama hata ukila chakula kichafu njiani
 
Miaka hiyo naishi Wilayani Kilombero ndani ndani huko! Usafiri mkuu ni Treni ya Tazara!! Si nikapanda mzee kitu cha Express kurudi chuo Dar (udsm)

Mzee nimelipa nusu nauli tu kwa kutumia kitambulisho cha chuo!! (Enzi hizo walikuwa wanaruhusu pia wanachuo kulipa nusu nauli) Hivyo nilikuwa na mpunga wa kutosha tu mfukoni! Na usisahau tulikuwa tunalamba mkopo 100% (2500) kwa siku wanachuo wote.

Dah!! Mtaalamu mwenyewe ile kufika Stesheni ya Kisaki, nikakuta kuku wa kutosha wa kienyeji wa kukaanga! Si nikanunua vipande viwili then nikaona ninunue na wali ili nikiingia Mjini mida ya saa 11 hivi jioni, nipitilize tu kwenda hostel!!

Ule wali sijui ndiyo waliweka hamira kweli kama nilivyo kuja kusimuliwa baada!! Ila kiukweli tumbo lilizingua haswa. Nashukuru nilivumilia mpaka nikafika hostel na kupitiliza mpaka ofisi kuu!!! Baada ya hapo, niliahirisha kabisa kutumia njia ya treni.
 
Nilibanwa na tumbo la kuhara halafu tupo eneo la jeshi halafu nimekaa karibu na dereva wa basi hilo, namweleza ananiambia hili eneo la jeshi hawaruhusu kusimama.

Huku mimi mzigo umeshaanza kureport kwenye boxer mdogo, aisee nilimgonga ngumi ya mgongoni nikamwambia mjomba leo nakunyea kabisa, alisimama bila kupenda nilienda kuhara akanipa na maji ila boxer niliiacha hukohuko porini
 
Back
Top Bottom