Ushawahi kufedheheka (kupata dharura) ukiwa safarini kwenye usafiri wa umma?

Ushawahi kufedheheka (kupata dharura) ukiwa safarini kwenye usafiri wa umma?

Ilikuwa mwaka 2009 nikirudi St John Dodona Chuoni, nikiwa katika basi la Scandinavia, baada ya kuimaliza Morogoro kwa mbele, tumbo likaanza kuuma, nikahisi kuharisha. Nikamuomba konda wa basi, akaniruhusu, nikaenda polini maana ilikuwa polini na sikuwa na namna, akanipa maji, nikakaa huko kama dakika 1, najua wajua tumbo la kuhara, unahisi kama mzigo bado upo. Nikamaliza nikarudi kwenye gari. Gali ilinidubiri, kutembea kidogo nikabanwa tena, nikasema na konda, gari ikasimama, kwenye siti nilikaa na Classmate wangu wa kike.

Dah safari haikuwa rahisi ila mwisho wa siku tukafika Dom kwa taabu sana. Sitasahau. Sababu ya madhira yote hayo ilikuwa kula kuku katika harusi ya baba yangu mdogo, wale kuku walikuwa kama wameharibika.
POLE SANA MKUU
 
Mkiwa na safari jitahidini msile msile hovyo ,kuleni biscuit tu kwa watu wasio na sukari.
Mwaka 2012/3 nilikuwa nasafiri sana. Kutokana na safari nyingi nikawa naepuka kula kula nikawa natumia biscuit sana na maji. Asee nilikuja kupata constipation ya hatari. Yani kimba halitoki nzutu inauma hatari ikabidi nijisalimishe hospital nikapewa dawa mzigo ukamwagika. Nikaapa sirudii tena kula biscuit sana. Bora nisile njiani kuliko kushindia biscuit...
 
2013 Dar- Mwanza, nilikula mayai ya kuchemsha moro iyo shida nilipata sijawahi ona
 
Miaka ya nyuma kidogo, nilikua natoka shule Kigoma Sec kurudi home Sumbawanga, kuna sehemu inaitwa Mishamo, nilikula nyama za kuku nyingi sana za buku 10, hii ilikua ni hasira baada ya kademu fln siti yangu kuninyima namba. Baada ya kama nusu saa, tumbo likachachamaa, mhuni najikaza tu, ikafika muda shuzi linataka kutoka ila kana lina dalili ya tumavi, daah, nikaomba gari isimame niende chaka, gari haijasimama vzr nipo nje. Nilikaa kama dkk 25 Waha wanawaka kinoma matusi , dereva ananipigia honi, mm ndo kwanza najisaidia, ilikua fedheha aisee. Nikamaliza, nikarudi, kila mtu macho kwangu.
 
Miaka ya nyuma kidogo, nilikua natoka shule Kigoma Sec kurudi home Sumbawanga, kuna sehemu inaitwa Mishamo, nilikula nyama za kuku nyingi sana za buku 10, hii ilikua ni hasira baada ya kademu fln siti yangu kuninyima namba. Baada ya kama nusu saa, tumbo likachachamaa, mhuni najikaza tu, ikafika muda shuzi linataka kutoka ila kana lina dalili ya tumavi, daah, nikaomba gari isimame niende chaka, gari haijasimama vzr nipo nje. Nilikaa kama dkk 25 Waha wanawaka kinoma matusi , dereva ananipigia honi, mm ndo kwanza najisaidia, ilikua fedheha aisee. Nikamaliza, nikarudi, kila mtu macho kwangu.
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwaka 2012/3 nilikuwa nasafiri sana. Kutokana na safari nyingi nikawa naepuka kula kula nikawa natumia biscuit sana na maji. Asee nilikuja kupata constipation ya hatari. Yani kimba halitoki nzutu inauma hatari ikabidi nijisalimishe hospital nikapewa dawa mzigo ukamwagika. Nikaapa sirudii tena kula biscuit sana. Bora nisile njiani kuliko kushindia biscuit...

Ni kweli kama ni mtu wa kusafiri sana haishuriwi kutumia biscuit sana,biscuit ni safari zile moja moja kwa mwaka....wewe hapo inabidi safarini usile kitu ,ukifika ndio unakula vyakula vya fibre kwa sana.
 
Mimi wakati tunatoka SA nilipanda bus moja ya wazambia ililala pale Chirundu mpaka wa Zimbabwe na Zambia miaka ya 2004 gari iliwasha taa Simba wakalifata lile bus na kuzunguka nje tulikua tunawaangalia tuu na wakaondoka walikua dume mbili baadae baada ya abiria wote kupata usingizi mimi niliota kama wale Simba wananitoa kwenye dirisha la bus nilipiga kelele ambazo sijawahi toa sauti vile dereva akawasha taa ya ndani na kuniuliza nikawaambia nilikua naota wale Simba wanaondoka na mimi walicheka sana mziki ukawa asubuhi tulipopanga foleni wakawa wanaongea kikwao " huyo wamene akunda mairo" wakimaanisha aliepiga kelele jana nilioneka sio jasiri kabisa ikawa ndio hadith ya Chirundu mpaka Lusaka tulipofika..
 
Mimi wakati tunatoka SA nilipanda bus moja ya wazambia ililala pale Chirundu mpaka wa Zimbabwe na Zambia miaka ya 2004 gari iliwasha taa Simba wakalifata lile bus na kuzunguka nje tulikua tunawaangalia tuu na wakaondoka walikua dume mbili baadae baada ya abiria wote kupata usingizi mimi niliota kama wale Simba wananitoa kwenye dirisha la bus nilipiga kelele ambazo sijawahi toa sauti vile dereva akawasha taa ya ndani na kuniuliza nikawaambia nilikua naota wale Simba wanaondoka na mimi walicheka sana mziki ukawa asubuhi tulipopanga foleni wakawa wanaongea kikwao " huyo wamene akunda mairo" wakimaanisha aliepiga kelele jana nilioneka sio jasiri kabisa ikawa ndio hadith ya Chirundu mpaka Lusaka tulipofika..
Mzee baba uliwaamsha wenzako woote kwa ndoto yako. inaonekana kabla ya hapo ulikuwa huwashuhudia simba live
 
Safari ngumu sana kwangu,ilikuwa natokea mjini Sumbawanga naelekea Mpanda,nilipanda basi mida ya asubuhi mapema,baada ya kilo mita chache tumbo la kuhara likaanza namshukuru MUNGU watu wote walilielewa tatizo lililonisibu,basi lilisimama mara sita njiani ili niende kwenye vichaka vya jirani kujisaidia,halafu kuna maeneo ni mbuga ya wanyama inaitwa Katavi,uoga wa simba na nyati nikiuweka pembeni ili jukamilisha haja,sitaisahau safari ile.
 
Nilibanwa na tumbo la kuhara halafu tupo eneo la jeshi halafu nimekaa karibu na dereva wa basi hilo, namweleza ananiambia hili eneo la jeshi hawaruhusu kusimama. Huku mimi mzigo umeshaanza kureport kwenye boxer mdogo, aisee nilimgonga ngumi ya mgongoni nikamwambia mjomba leo nakunyea kabisa.. alisimama bila kupenda nilienda kuhara akanipa na maji ila boxer niliiacha hukohuko porini
Nimecheka mpaka machozi😂😂😂
 
Mi natoka zangu arusha naenda mbeya si nikakaa siti moja na mama ana mtoto mtundu huyo sasa mara adondoshe pochi naambiwa niikote,mara simu imedondoka kaka naomba uniokotee.sasa kikubwa akapanda hadi kifuani anarukaruka nikamfinya akalia akatulia
😀 😀 😀 😀 😀 😀 huyo anaitwa JUNIA
 
Safari ngumu sana kwangu,ilikuwa natokea mjini Sumbawanga naelekea Mpanda,nilipanda basi mida ya asubuhi mapema,baada ya kilo mita chache tumbo la kuhara likaanza namshukuru MUNGU watu wote walilielewa tatizo lililonisibu,basi lilisimama mara sita njiani ili niende kwenye vichaka vya jirani kujisaidia,halafu kuna maeneo ni mbuga ya wanyama inaitwa Katavi,uoga wa simba na nyati nikiuweka pembeni ili jukamilisha haja,sitaisahau safari ile.
Pole sana mkuu wanasemaga SAFARI HATUA
 
Natoka zangu buza naenda kawe ndani wkt naingia kwenye basi siti ya nyuma nikakuta mtoto mkareee katulia tuliii ninja nikaona isiwe tabu nikaenda kukaa nae

Baada ya vituo viwili nikaona ngoja nimsaundishe sista duu akawa anielewi baadae alivoona na mkomalia kwa msauti mkubwaaa akabwatuka we "we kaka mbona hunielewi" basi wote wakageuka nyuma na kutuangalia na basi lote lilikuwa kimya

Da mchizi nikaona hili soo na Mimi muda huo nikaamua kupiga counter attack kwa msauti mkubwaaa " hunielewi nn kama umejamba nisikwambie"

Da yule manzi aliona aibu na watu wote walianza kucheka ndani ya gari ilibaki kidogo dereva apindue gari .......dadeki sitaki mchezo na vi sistaduu uchwaraaa


Sent from my HUAWEI LUA-U22 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom