Mohamed Said,
Mkuu Maalim Mohammed Said, kwanza asante kuchangia uzi wangu huu na asante ya pili ni kwa wewe kuwa mchangiaji wa kwanza, umelifanyia jambo kubwa sana bandiko hili bila wewe kujijua.
Baada ya kubandika tuu uzi huu nilikimbilia Kanisani kwenye ibada. Baada ya ibada nimekuja kufungua if baada ya masaa 4, nikakuta bandiko liko page 7!. Kuna mabandiko huwa nachangia na yana hoja muhimu sana ila sio tuu linaishia page 1 tuu, bali inakuta limeishia post hiyo hiyo moja ya the thread starter na halikuchangiwa na mtu hata mmoja, mfano ni bandiko hili
...... Kumchagua Mgombea wa Dini yoyote!. Zikiwa zimebakia siku mbili kabla ya uchaguzi mkuu, Sheikh Mkuu wa Tanzania, Mufti Issa Shaaban Bin Simba, amewataka Watanzania kujitokeza kwa wingi siku ya kupiga kura, na kuitumia haki yao ya kidemokrasia kuwachagua viongozi wanaowataka, bila kujali...
Hivyo kitendo cha wewe Mkuu Maalim kutia mguu humu kama mchangiaji wa kwanza kumelifungulia njia bandiko hili na amini usiamini ujumbe huu utawafikia walengwa, japo jf haitatajwa.
Hii ni kufuatia zile powers ulizonazo, nakuomba tena na tena katika mabandiko ya maslahi ya taifa, tuweke tofauti zetu pembeni tutangulize mbele maswali ya taifa kwa watu kama nyinyi kutumia vipawa vya powers mlizojaaliwa ku push forward ajenda za kitaifa kwa mustakabali mwema wa taifa letu.
Katika hili la serikali za mitaa, ni Chama kimoja tuu CCM ndicho kina ofisi kila kata, wana tawi lila mtaa na wana ujumbe wa shine kila nyumba 10 hivyo wagombea wa CCM wamejaziwa hizo fumu na kuhakikiwa. Vyama vingine havina hata ofisi ya wilaya achilia kata na mitaa hivyo wagombea wao ni kama watoto yatima. Ndio maana hapa nimemuomba rais Magufuli aingilie kati kwa kuruhusu wagombea wote wa vyama vyote bila kujali hizo kanuni ili tuu kuruhusu ushindani wa haki.
Tanzania hatuna utaratibu wa kufanya utafiti wa kisiasa ndio maana ile 2005 tuliandikisha wapigakura milioni 22, waliojitokeza kupiga kura ni milioni 12, JK alishinda kwa kura 9,123,952 ambayo ni zaidi ya asilimia 80%. Watu milioni 8 walijiandikisha lakini hawakujitokeza na nobody cares kujiuliza why!.
Uchaguzi wa 2010 walijiandikisha watu milioni 21
Waliojitokeza kupiga kura ni 8,626,283 – 42.84%
Watu milioni 12 hawakujitokeza, nobody asked anything!.
JK alishinda kwa kura 5,276,827 sawa na asilimia 61%. Kutoka asilimia 80% hadi 61% and nobody asked anything. Hakuna research yoyote iliyofanyika.
Kwa vile wewe ni reacher tufanyie research na utufundishe hiyo law of probability.
Swali moja linabaki, hili nililopendekeza humu lisipo tekelezwa na hao waliosusa wakiendelea kususa, what will happen next?.
P