Kuna jamaa yangu mmoja alinielekeza namna nzuri ya kuku kutotoa mayai yote bila kuacha. Ni kwamba aliniambia ninunue vile vibeseni vidogo vya kunawia then ndan unaweka mchanga kiasi halafu weka mayai yako tayari kwa kuliwa na kuku. kiukweli njia hii nilitumia na imefanikiwa. kwa wafugaji wenzangu jaribuni muone maajabu yake.
Kitu kingine ni utunzaji wa vifaranga baada ya kutotolewa napo hapa kuna changamoto wakati wa usiku kutokana na barid kwa vifaranga hasa kwa wafugaji wa hali ya chini,mm mwanzo nilihangaika but nikapata njia nyingine bora ya kutunza vifaranga wakati wa usiku,nilitenga sehm ya kuwalaza. Hapa unaweza chukua hata box kubwakubwa la kuwatisha vifaranga then nikatafuta chungu!! Nikaweka majivu ndani kwa hio kila usiku nilikua unaweka mkaa wa moto mle ndani ya chungu na kufunika na majivu!! Nakwambieni ndugu zangu wafugaji vifaranga hawapati barid kabisaaa! Na huo moto ulioko ktk hilo jivu utaukuta mpka asubuhi na utatumia kwa kuwashia moto hapo kwa nyumba yako. jaribuni na njia hii muone mafanikio yake na si kukaa ohhh nitanunua vifaranga 500 nianze hapana anza hata na kuku 2 au 3 baada ya mda utakuja nambia. Yangu ni hayo labda hujaelewa uliza tupeane maujuzi.