Ushuhuda: Leo nimekutana na kipanga jeuri wa darasani. Kweli hakuna uhusiano wa uwezo darasani na wa maisha halisi

Ushuhuda: Leo nimekutana na kipanga jeuri wa darasani. Kweli hakuna uhusiano wa uwezo darasani na wa maisha halisi

Mimi nilikuwa kipanga pale pugu sekondari combination ya PCB mwisho wa siku nikajikuta mlimani BSc Education. Wenzangu wengine vilaza wenye connection pamoja na kupata division III walienda Algeria na China kusoma medicine, wengine wazazi wao wenye uelewa wakawaambia wakasome wildlife sasa hivi wako TANAPA.

Hawa jamaa hawakuamini kwamba yule mtabe wa organic, cytology na simple harmonic motion kawa ticha.

Nilifundisha miaka miwili nikaenda kupiga degree nyingine tofauti. Haya maisha yana mengi ya kujifunza.
Maisha ni Kama gwaride ukisikia nyumaaa! geuka !!!wa Kwanza anakuwa wa mwisho wa mwisho anakuwa wa kwanza
 

Hii kama chai inataka kuzidi sukari, huyo alikuwa kipanga kweli au kishoka?
akikujibu ni-tag.

Maana vipanga wenye alama "B" na "A" kwenye PCM, PCB, PGM ukikutana naye, respect yake lazma umpe.

Maana akikosa hela anaweza kukamata madogo wa A-Level akawapigia Topic Moja ya "Advanced Physics" au "Pure Mathematics" kwa Tsh. 20,000/- hapo akiwa na wanafunzi 20 tu anaweza kula mpaka Tsh. 400,000/- zake fasta kwa Topic moja tu tena bila makato ya kodi.
Tena Topic yenyewe unakuta anaimaliza kwa siku 12 tu.

Mimi li-kipanga lolote lile lenye "A" au "B" zake za A-Level kwenye combination za PCM, PCB, PGM, CBG na EGM.
Likipanga la hivyo huwa hata nilikute limechoka vipi huwa bado naliheshimu sanaaaa.
 
Mara nyingi stori kama hizi huwa zinatoka kwa watu waliofeli masomo yao darasani au waliokuwa hazichaji kichwani na huwa faraja yao pekee ni kusubiri kipanga mmoja apigwe na maisha warudi kusema 'yako wapi sasa'! Lakini wanasahau kwamba ukiwa na cheti au akili, hela bado una nafasi ya kuitafuta. Lakini hata kama una hela, kama hazichaji kichwani bado haziwezi kuja na hauwezi kuzitafuta akili kwa hela zako
Jua kuna akili za shuleni na akili za kwako mwenyewe sisi sote tunatumia akili binafsi katika kufanya vizuri katika maisha ,hapa ndipo tunatofautiana akili.
Wengi waliokua na akili darasani waliona wana akili ya kuwin maisha pale ni class kuna x toa y sawa na 2 ,maishani akuna izo mambo huku kuna kutafuta pesa haijalishi shuleni ulikuaje.

Na akili sio kupata pesa akili ni kutumia pensa kufanikisha malengo ulio jiwekea.


Sent from my TECNO KB7j using JamiiForums mobile app
 
Man down, I repeat man down
Mara nyingi stori kama hizi huwa zinatoka kwa watu waliofeli masomo yao darasani au waliokuwa hazichaji kichwani na huwa faraja yao pekee ni kusubiri kipanga mmoja apigwe na maisha warudi kusema 'yako wapi sasa'! Lakini wanasahau kwamba ukiwa na cheti au akili, hela bado una nafasi ya kuitafuta. Lakini hata kama una hela, kama hazichaji kichwani bado haziwezi kuja na hauwezi kuzitafuta akili kwa hela zako
 
Vilaza bana basi roho yako kwatu [emoji3][emoji3]
 
Mchawi sio lazima aruke na ungo.Kitendo cha kufurahia mwingine kuwa na maisha magumu kisa alikuwa anakuzidi kitaaluma ni uchawi tosha. Ukisikia huyo jamaa kafukuzwa hapo utafurahi, ukisikia jamaa anaumwa utafurahi,kiufupi wewe ni mchawi.
 
Wewe ni mjinga hata kudanganya hujui!

IQ yako ndogo sana! Mtu mliyesoma naye darasa moja obviously atakuwa age mate wako!

Sasa ulivyom-address na huyo rafiki yako alivyom- address kijana wake wa kazi kwako obviously hakuna uhalisia wowote! Hizi ni story za vil.aza kutungia vil.aza wenzao.
wewe ndio hujui. ukiajiriwa na mtu hata kama unamzidi au unalingana nae Umri huyo mtu anabaki kua kijana wako tu. Ndio maana wenye Peasa wanaitwa wazee tena na watu Wazee.
 
Bora hata usingemtumia msg maana anahisi unamsanifu,ila tusiwe na tabia ya kukufuru,maisha siku zote ni kupanda na kushuka,kutokuwa na akili ya darasani sio kutokufaulu maisha,binadamu katika swala la kufanikwa kila mtu huwa na karama zake alizopewa na Mungu...
 
Kila shule na kila faculty vyuoni ina hawa viumbe wanaitwa vipanga; ni watu ambao wanafanya vizuri sana darasani aidha kwa kutumia jitihada kubwa ama uwezo mkubwa wa akili waliojaaliwa.

Tatizo sio kuwa kipanga, tatizo ni kuwa kipanga jeuri, ni wale watu wanaofanya vizuri darasani na kuona kwao tayari washapita mtihani wa maisha, yaani ni wale type za kuringa, zenye kujitenga pamoja na vipanga wenzao, wanaonyima watu chabo kwenye mitihani n.k

Sasa navyosoma zamani kulikuwa kuna huyu bwana alikuwa na tabia hizi na kiukweli kwake namba yake ilikuwa ni moja tu, yani alikuwa na tabia kama hizo nilizotaja, Chuoni assignment zake, notes zake za summary, n.k alikuwa anatunyima na hata kuwaita wazi wazi wasio na uwezi darasani ni vilaza.

Nimekodisha frem sehemu flani nimeweka binti awe anauza maana mimi muda mwingi nipo kazini, sasa kuna rafiki yangu tunaefanya nae kazi akavutiwa kufungua biashara ya kipati cha ziada, nikamshauri achukue fremu eneo lile nililopo maana ni pazuri, basi taratibu zikafanyika na rafiki yangu akafungua stationery kubwa tu.

Leo nlipotoka kazini nilienda dukani kwangu kuhesabu mzigo lakini pia lengo kuu nilikuwa na shauku kubwa ya kuona mradi wa huyu rafiki yangu maana leo ndio rasmi alianza kuuza.

Kufika pale nikapigwa na butwaa, nikaona kijana wa kazi pale ni yule kipanga, kiukweli nilihisi nmechanganya sura maana nilijua jamaa atakuwa huko kwenye vitengo vya juu au kufundisha vyuoni.

Nlimwita jina akaitikia nikajua hapa sijakosea ni yeye, basi ndio nikamkumbusha ndo akanijua akaniambia kafungua steshonari yeye, mimi nikawa namchora tu mbona ananidanganya, rafiki yangu akafika akamtambulisha huyo ndio kijana wake wa kazi, dah basi kwa kipanga ikawa aibu tupu.

Wakati wanafunga tukaagana na yule rafki yangu na mimi nikafunga maana dada wa kazi alikuwa kaniacha, nikamkuta njiani kipanga nikamwambia apande kama anajitaji lifti yeye akasema anasubiri mtu.

Usiku huu namcheki WhatsApp, nmemtumia message hadi sasa kaisoma ila hajajibu

Japo hiyo hali ipo ila kwa hii story yako ni TANGO PORI.
 
Kila shule na kila faculty vyuoni ina hawa viumbe wanaitwa vipanga; ni watu ambao wanafanya vizuri sana darasani aidha kwa kutumia jitihada kubwa ama uwezo mkubwa wa akili waliojaaliwa.

Tatizo sio kuwa kipanga, tatizo ni kuwa kipanga jeuri, ni wale watu wanaofanya vizuri darasani na kuona kwao tayari washapita mtihani wa maisha, yaani ni wale type za kuringa, zenye kujitenga pamoja na vipanga wenzao, wanaonyima watu chabo kwenye mitihani n.k

Sasa navyosoma zamani kulikuwa kuna huyu bwana alikuwa na tabia hizi na kiukweli kwake namba yake ilikuwa ni moja tu, yani alikuwa na tabia kama hizo nilizotaja, Chuoni assignment zake, notes zake za summary, n.k alikuwa anatunyima na hata kuwaita wazi wazi wasio na uwezi darasani ni vilaza.

Nimekodisha frem sehemu flani nimeweka binti awe anauza maana mimi muda mwingi nipo kazini, sasa kuna rafiki yangu tunaefanya nae kazi akavutiwa kufungua biashara ya kipati cha ziada, nikamshauri achukue fremu eneo lile nililopo maana ni pazuri, basi taratibu zikafanyika na rafiki yangu akafungua stationery kubwa tu.

Leo nlipotoka kazini nilienda dukani kwangu kuhesabu mzigo lakini pia lengo kuu nilikuwa na shauku kubwa ya kuona mradi wa huyu rafiki yangu maana leo ndio rasmi alianza kuuza.

Kufika pale nikapigwa na butwaa, nikaona kijana wa kazi pale ni yule kipanga, kiukweli nilihisi nmechanganya sura maana nilijua jamaa atakuwa huko kwenye vitengo vya juu au kufundisha vyuoni.

Nlimwita jina akaitikia nikajua hapa sijakosea ni yeye, basi ndio nikamkumbusha ndo akanijua akaniambia kafungua steshonari yeye, mimi nikawa namchora tu mbona ananidanganya, rafiki yangu akafika akamtambulisha huyo ndio kijana wake wa kazi, dah basi kwa kipanga ikawa aibu tupu.

Wakati wanafunga tukaagana na yule rafki yangu na mimi nikafunga maana dada wa kazi alikuwa kaniacha, nikamkuta njiani kipanga nikamwambia apande kama anajitaji lifti yeye akasema anasubiri mtu.

Usiku huu namcheki WhatsApp, nmemtumia message hadi sasa kaisoma ila hajajibu
[emoji1787] [emoji1787] [emoji1787] [emoji1787] Nimecheka lakini man sio poa, usijaji watu hivyo [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] unaweza kuta jamaa alikua vizuri darasani sema mtaani akakosa connections na wengi wao wanaokua darasani vizuri ni wale unakuta kwao maisha yao ni magumu kimtindo, wapo wengi sana mbona mjini, ila usicheke mzee [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Ndio maana huko niliko kwenye group moja ya secondary huwa na mute kimyaaaa kwasababu ya vichuki chuki vya kijinga kama hivi watu kukupiga majungu kisa ulikua unawakimbiza darasani ila maisha hamtofautiani kivilee mtaani wanaona kama ulikua una ringa hata kama walikua washkaji zako .Wivu mbaya sana. 😂😂😂
Kumbe na wewe ulikuwa kipanga bro hahaaaaa
 
Hakuna maisha nayapenda Kama kujishusha mbele ya jamii, wale kazi zao zinazodharaulika ndio huwa nawafanya marafiki nawasalimu kwa ukarimu, Basi najisikia amani sana.

Una nyodo na jeuri ya shibe, ukishiba leo kumbuka kuna aliyekosa hata ngumi moja ya hicho chakula, kesho giza rafiki yangu usije kuona aibu tu.

Huyo mate wako ni kiburi, ingekuwa Ni Mimi ningechangamka na ningepanda lift ili tu kukuonyesha kuwa najikubali na hali yangu.
Unajikubali na hali yako imemshinda hiyo maana shuleni pia alikua na na dharau kama mdau alivyosema kuwaita wenzake vilaza, kama asingekua na dharau shuleni siajabu angeweza hata kumuomba jamaa connection za kazi, life imepinda halafu unajifanya imenyoka, ila pia huwezi kuchagua kazi kuna baadhi ya kazi ni daraja kwenda kufikia kwenye lengo
 
Mara nyingi stori kama hizi huwa zinatoka kwa watu waliofeli masomo yao darasani au waliokuwa hazichaji kichwani na huwa faraja yao pekee ni kusubiri kipanga mmoja apigwe na maisha warudi kusema 'yako wapi sasa'!

Lakini wanasahau kwamba ukiwa na cheti au akili, hela bado una nafasi ya kuitafuta. Lakini hata kama una hela, kama hazichaji kichwani bado haziwezi kuja na hauwezi kuzitafuta akili kwa hela zako

moja ya comment BORA kabisaa..
Wengi wanadhani wakipata pesa wataonekana bora zaidi na kuondoa udhaifu wao kumbe watu wanakaa kimya na kuwafurahisha ili wavune pesa zao. Ila kiuhalisia bado wanayaona madhaifu yao clearly na wakiona hawana faida tena bhasi wanatumia hayo hayo madhaifu kuwatelekeza
 
Mara nyingi stori kama hizi huwa zinatoka kwa watu waliofeli masomo yao darasani au waliokuwa hazichaji kichwani na huwa faraja yao pekee ni kusubiri kipanga mmoja apigwe na maisha warudi kusema 'yako wapi sasa'!

Lakini wanasahau kwamba ukiwa na cheti au akili, hela bado una nafasi ya kuitafuta. Lakini hata kama una hela, kama hazichaji kichwani bado haziwezi kuja na hauwezi kuzitafuta akili kwa hela zako
Maneno yako yanayo faraja ambayo haina tija saaana.

kwanza Elimu na Akili ni vitu viwili tofauti ambavyo kwa namna mmoja ama nyingine vinaweza kuingiliana au kukanganywa katika kuvielewa.
Iwapo tunazungumzia Elimu/Cheti basi tuihusishe na ujuzi na iwapo tunazungumzia Akili/Ujanja basi tubainishe za wapi Darasani ama Mtaani/Duniani/Kimaisha.

Wapo watu na Elimu zao lakini wanafeli maisha bila ya kujali kipato walichonacho na pengine kufulia kabisa pamoja na kwamba wanavyo vyeti vyao (Kutokuweza kuitumia Elimu waliyonayo kujiendesha au kujipa misha yenye unafuu machoni mwa wanaowazunguusha)

Kwa upande mwingine, wapo wasio na Elimu kabisa lakini maisha yao ni tambarale kufikia hata hao wenye ma-Phd. kuwa waajiriwa wao.

Kufupisha mada hata uwe na vyeti chumba kizima,
Iwapo havikufanyi uwe na misha bora,mazuri na yenye furaha mpwa umefeli.

Hoja ya kuwa kwakuwa unayo Elimu basi unao uwezekano wa kuyarekebisha hiyo ni kujifariji.

Elimu ni nyenzo yakurahisisha mengi yatakayotawala maisha yako.
Iweje asie na nyenzo atoboe wewe ulie nayo ushindwe kisha usema eti, kwakuwa unayo nyenzo basi ipo siku,lini?
Faraja!
 
moja ya comment BORA kabisaa..
Wengi wanadhani wakipata pesa wataonekana bora zaidi na kuondoa udhaifu wao kumbe watu wanakaa kimya na kuwafurahisha ili wavune pesa zao. Ila kiuhalisia bado wanayaona madhaifu yao clearly na wakiona hawana faida tena bhasi wanatumia hayo hayo madhaifu kuwatelekeza
Mungu kaumba karibia kila kitu kwa upekee wake na ndio maana hakuna
kiumbe anaelingana na yeyote mwingine ingawa wanaweza kuwa wa jamii moja
na wakati mwingine mmoja kufananishwa na mwingine.

Binadamu hata wazaliwe pacha wa kufanana (identical)
bado wanazo tofauti, ziwe zinazoonekana ama nyingine zisizoweza
kuonekana kiurahisi kwa macho.

Kama ilivyo kwa uumbaji ni majaaliwa,
tukubali basi kuwa hata maisha tunajaaliwa na kufanikiwa kwetu kunatofautiana pia.

Ukiikataa kanuni hiyo ni kwakuwa umejaaliwa ujuaji.

Unaweza kujaaliwa Elimu/Ufaulu/Ujuzi nk.,
Mwenzako kajaaliwa kufanikiwa kwa njia nyingine kabisa isiyohitajiElimu kuubwa kama au zaidi yako.
Hivyo ndivyo ilivyo,taka-usitake, kubali au kataa.

Lakini ukweli ulio mchungu na unaouma 'ndani kwa ndani ';
Msomi upo na rundo la mavyeti yako ndani lakini unaishi maisha ya nusu na robo.
-kisha kuna mpumbavu mmoja tena Std 7, au yule Fala uliemburuza sana darasani,
unashuhudia maisha yake ni yale ya;-ananing'inia tu juu kwenye balcony
huku akiawangalia kwa chini wanaze,kwenye swimming pool moja matata
mbele ya mjengo wake babkuubwa,huko nyuma 'wife' wake yupo bustanini
anagida na kunywa Mvinyo lainiiiii, lhali nyumba nzima imezunguukwa na wahudumu
wote wakiwajibika kuitumikia Familia ya yule fala, .
Achilia mbali miradi lukuki inayoingiza 'mafwedha' kwa kwena mbele.

Inauma ee?

Msomi unasubiri kamshahara/pension kako kasikofika hata katikati ya mwezi,

Hujaitusi tu elimu yako bado hapo?

Unasubiri nini kumbe?

Hapana usifanye hivyo,
Ndio maisha hayo.😆

Kisha eti mwingine anajifariji, "Nina Elimu" mwenzake hana.
Kwahivyo?

Sasa kusudio la maisha nini?
Uwe na Elimu utaabike???
 
Back
Top Bottom