Usidanganywe na stori za vijiweni, ijue Sheria ya Ndoa na Talaka

Usidanganywe na stori za vijiweni, ijue Sheria ya Ndoa na Talaka

Chini ya umri huo, unaweza kuomba kibali cha mahakama na wazazi ili kupata ruhusa ya kuolewa. Lakini wanaharakati wa haki za watoto (hasa wa kike) pamoja na Umoja wa Mataifa wamekuwa wakipambana kuhakikisha umri huu wa wanawake kuolewa unaongezwa na kuwa miaka 18, rejea hukumu hii Attorney General vs Rebeca Z. Gyumi (Civil Appeal 204 of 2017) [2019] TZCA 348 (23 October 2019); | Tanzlii ya mwanaharakati REBECCA GYUMI (2019) iliyoeleza kuwa vifungu vya umri wa ndoa (Kifungu Na. 13 na 17) ni batili kwani vinakandamiza mabinti na vinatakiwa kurekebishwa na Serikali ndani ya mwaka 1 kutoka 2019. Japo mpaka sasa, bado Serikali haijarekebisha vifungu hivyo, hivyo vipo lakini ni kama visivyo na maana yoyote kisheria.
Mkuu kwenye swala la kuolewa chini ya miaka 18 mbona kama sheria zimebadilishwa ndio maana huyu jamaa amepandishwa kizimbani.
Rejea habari hii
 
Mkuu kwenye swala la kuolewa chini ya miaka 18 mbona kama sheria zimebadilishwa ndio maana huyu jamaa amepandishwa kizimbani.
Rejea habari hii
Ahsante sana mkuu kwa umakini wako. Huyo ndugu yetu ameshtakiwa kwa kosa la kuishi na mtoto wa shule (mwanafunzi) ambapo sheria ya elimu pamoja na Sheria ya mambo ya kingono (SOSPA) ilimtambua mwanafunzi kuwa mtu aliyefaulu shule na kuwepo katika elimu ya msingi au sekondari hata kama atakuwa amepita miaka 18. Ndio maana huwa unaona mtu akikamatwa na mwanafunzi hata kama ana miaka 19, anafunguliwa mashtaka ya ubakaji chini ya Sheria ya Kanuni ya Adhabu (penal code)nk

Kwa hiyo sheria ya ndoa ilimzungumzia mwanamke asiye masomoni, yaani aliyepo nyumbani baada ya kufeli shule ya msingi au ambaye hajasoma kabisa ila ana umri chini ya miaka 18.
 
O: DHANA YA NDOA (Presumption of Marriage)
Je, Nini maana ya dhana ya ndoa?

Dhana ya Ndoa ni ile hali ambayo watu huitwa wanandoa kwa kuwa wameishi pamoja kama mume na mke kwa kipindi cha miaka miwili na kuendelea;

Wanawake wengi wamekuwa wakiaminishwa vibaya kuwa akikaa na mwanaume kwa miezi 6 tu basi hapo mwanamke anatambulika kama mke halali wa huyo mwanaume, jambo hili si sahihi, sababu Sheria inatambua kipindi cha miaka miwili (2) mfululizo kuishi kama mke na mume, hapo ndipo dhana ya ndoa hutambulika.

Dhana ya Ndoa humalizikaje? Je nayo huombewa talaka?
HAPANA
, dhana ya ndoa huvunjwa na mahakama kwa kutolewa kwa amri ya kubatilisha dhana hiyo (decree of annulment) na sio talaka. Talaka hutolewa kwa wanandoa rasmi tu.

Vipi kuhusu mali na mgawanyo wa watoto waliopatikana katika dhana ya ndoa?
Mgawanyo wa mali, na uangalizi wa watoto pamoja na matunzo yao hufanyika kwa kuzingatia mambo yaleyale yanayozingatiwa wakati wa utoaji wa talaka.

P: UANGALIZI WA WATOTO NA MATUNZO YAO:
Wakati wa kutoa talaka au utengano Mahakama ina uwezo wa kuamuru mtoto akae chini ya uangalizi wa baba au wa mama na ikiona mazingira hayaruhusu kwa mtoto kukaa kwa baba au mama yake mzazi, basi inaweza kuamua mtoto akakae kwa ndugu yeyote wa mtoto au kwenye kituo cha kijamii kinacholea watoto;

Mahakama katika kuamua ukaaji wa watoto huzingatia maslahi ya mtoto kwa kuangalia;
  • Maombi ya wazazi wenyewe;
  • Maombi ya mtoto ikiwa ana umri wa kuweza kujielezea;
  • Mila na desturi za mahali wanapoishi wanandoa;
Mtoto wa umri chini ya miaka saba hudhaniwa kuwa ni vyema akikaa kwa mama yake, ingawa sio lazima akae huko kulingana na mazingira yatakavyokuwa;

Sambamba na hilo, mahakama itaangalia:
  • Haki za kimasomo za mtoto, kama kumhamisha kutaharibu masomo yake au la;
  • Itaweka utaratibu wa mzazi aliyenyimwa uangalizi kumtembelea mtoto huyo;
  • kuweka zuio la mtu aliyepewa uangalizi wa mtoto kutoka naye nje ya Tanzania bila ruhusa ya mzazi mwenza na pia ya Mahakama.


Q: DHANA YA KIFO (Presumption of death):
Wakati mwingine watu hupotea na kutopatikana waliko au habari zao, jamii hufikia kuamua kuwa mtu huyo alishakufa huko alikopotelea na baadhi ya jamii hufanya ibada ya mazishi kana kwamba wana mwili wa huyo mtu (marehemu). Hii fikra ndio inayoitwa dhana ya kifo

Kisheria, mtu asipowasiliana na mtu yeyote ambaye kwa kawaida wangepaswa kuwasiliana mfano baba, mke, kaka nk kwa kipindi cha miaka 5 na zaidi, basi kutakuwa na dhana kuwa mtu huyo alikwishafariki dunia.


R: MAKOSA YA JINAI YAHUSIANAYO MAMBO YA NDOA
  • Ukizuia isivyo kisheria kufungwa kwa ndoa ambayo wanandoa tarajiwa wamepitia hatua zote na wana sifa za kufunga ndoa, ama ukienda kufanya vituko kwenye sherehe ya harusi ya wanandoa kwa lengo la kuwadhalilisha au kuwafedhehesha unakuwa umefanya kosa la jinai na likithibitishwa unaweza kuapata adhabu ya kifungo cha miezi 3 jela.

  • Kuolewa na mtu ambaye uhusiano wake umekatazwa kisheria;

S: Sheria za Kimila za mwaka 1963 – Tangazo la Serikali (GN.) Na. 279 la 1963
Hizi zilipangwa kutumika katika wilaya za Handeni, Kahama, Kondoa, Lushoto, Musoma, Ngara na Pangani – Lakini kwa sasa zinachukuliwa kutumika kwa jamii yote Tanzania.

Vipi sasa watu wakikaa pamoja bila ndoa na kuamua kutengana kabla miaka 2 haijafika?
Ikiwa watu watakua na mahusiano ya kimapenzi yenye muelekeo wa kindoa, wakakaa pamoja na kuvunja mahusiano yao kabla ya miaka 2 ambayo wangetambulika kuwa wanandoa ksheria (kwa dhana ya ndoa) basi mali walizochuma pamoja hutambulika kama mali za ushirika ( partnership properties).

Mali hizi za ushirika hugawanywa na Baraza la Kata kwa kuzingatia taratibu za kijamii za mahali husika. Kwa kuwa sheria ya kimila iliyorasimishwa ni hili tangazo la Serikali namba 279 la 1963, basi ndio linalozingatiwa wakati wa ugawaji. Mgao huwa ifuatavyo:

[emoji1542]
Mifugo, vyakula vilivyomo ghalani, mazao ya biashara, mazao ambayo hayajavunjwa, hugawanywa sawa sawa kwa hao watu wawili.
[emoji1542]
Nyumba hupewa mwanamume na mwanamke huchukua vyombo vya jikoni.
[emoji1542]
Baada ya mavuno, shamba huwa mali ya mume.
[emoji1542]
Kila mtu atachukua vitu vyake binafsi anavyovimiliki kama vile nguo mapambo n.k. pamoja na zawadi alizopokea toka kwa mwenziwe.

[emoji3502]
Kama mwanamke amemfuata mwanamume katika nyumba yake na wakaishi pamoja na kama wote wawili wameshirikiana kuendesha kazi hapo kwao na kupata mali, ama kama wote walikuwa na kazi rasmi, basi mwanamke ana haki ya kupata robo ya vitu vyote au mali zote zilizopatikana kwa msaada wake isipokuwa vitu vyake mwenyewe (mali binafsi)
[emoji3502]
Kama mwanaume amemfuata mwanamke katika nyumba yake na wakachuma mali pamoja, ana haki ya kupata robo ya vitu vyote vilivyopatikana kwa msaada wake isipokuwa vitu vyake binafsi.


T: MIRATHI

Hili ni somo pana ambalo litahitaji siku nyingine kulizungumza, ila hapa nitazungumza kwa ufupi sana kuhusu mirathi ya mali za marehemu kwa wajane na watoto.

Je, ikiwa anayefariki ni mume, kina nani wanastahili kuwa warithi wake?
Sheria inasema kuwa warithi ni wale watu walioandikwa katika wosia wa marehemu. Ikiwa marehemu hajaacha wosia, basi watu wa karibu ya marehemu (ndugu) wanaweza kuwa warithi wake. Watu hao ni mke, watoto, wazazi na wengine ikiwa ni pamoja na wale waliomuuguza kipindi cha mwisho cha uhai wake.

Je, ni kila mke anayeweza kurithi mali za marehemu (mume)?
Hapana
. Sio kila mke atakuwa na uhalali wa kurithi mali za marehemu, bali ni mke halali tu wa marehemu ndiye atayeweza kurithi.

Ikiwa wamejitokeza wake wawili wa marehemu na wote wana vyeti vya ndoa, yupi atakuwa ni mke halali?
Ikiwa ndoa ilikuwa ni ya mke mmoja, mke aliyeolewa kwanza ndio atakua halali na ndiye atakastahili kurithi. Huyu mwingine hatahesabika kama mke wa marehemu bali kama hawara tu. Ikiwa walichuma pamoja na marehemu basi atapata mali hizo kwa mtindo wa ushirika (partnership) na sio kwa mtindo wa mirathi.

Je, watoto waliozaliwa hapo kwenye ndoa inayoonekana kuwa ni haramu, watahesabiwa urithi?
Kwa mujibu wa Sheria ya Mtoto ya mwaka 2009 (The Law of the Child Act, CAP 13 R.E 2019) , watoto hawa wataweza kutumia na kufurahia mali za baba yao, sheria hiyo haijawekwa wazi kama wataweza kurithi (kumiliki) pindi baba atakapokufa. Maamuzi ya karibuni ya mahakama kuu ya Tanzania chini ya Jaji Mlyambina yalionesha kuwa watoto hawa (maarufu kama haramu) wanaruhusiwa kurithi mali za marehemu baba yao.

Hata hivyo maamuzi haya bado yanaendelea kufanyiwa tathmini ya kisheria kwa kuwa tayari kulikuwa na maamuzi ya Mahakama ya Rufaa ambayo yalitamka wazi kuwa mtoto wa nje ya ndoa hawezi kurithi isipokuwa tu kama baba wa mtoto huyo alimkomboa huko kwao na kumtambulisha kwenye ukoo wake kwa tamaduni za ukoo husika, na kwamba mtoto huyo alikuwa akihusika na shughuli za kijamii kwa ukoo wa baba yake.

Mahakama ya Rufaa kupitia kesi ya VIOLET ISHENGOMA KAHANGWA AND JOVIN MUTABUZI v THE ADMINISTRATOR GENERAL AND MRS. EUDOKIA KAHANGWA 1990 TLR 72 (CA) - (KISANGA JJA, MAKAME JJA na MFALILA JJA) iliamua kuwa mtoto haramu anaishia kufurahia mali za baba yake mpaka pale baba yake atakapofariki dunia na hataweza kugusa mali hizo mara baada ya kifo cha baba yake. Wazee wa Mahaka ya Rufaa wakasema kama baba anapenda mwanae wa nje ya ndoa asisumbuliwe pindi yeye baba atakapokufa, basi amfanyie mwanae mambo yote akiwa hai, maana hakuna mtu anayeweza kumzuia baba kufanya vitu kwa mwanawe. Hukumu hiyo mpaka leo hii haijabatilishwa, hivyo ndio msimamo wa Sheria Tanzania.

Ahsanteni sana ninaishia hapa.
Ninakaribisha maoni, mjadala, maswali, ufafanuzi, nyongeza nk ruksa kuja DM na Whatsapp
Mkuuvipi kama watu walikutana, wakaanza kuishi pamoja Kisha mwanaume akapeleka mahari though watu (washenga) baada ya makubaliano ikapokelewa, ila kukawa na migogoro mingi katika maisha ya hao wawili (mwanamke na mwanaume) ei baadhi ya ndugu Wa mwanamke kutotaka Binti yao Aishi na huyo mwanaume. Ikafikia hatua mwanamke kujifungua mtoto ila babaye na mwanamke akamfuata na kumchukua na kukaa naye huko miezi kadhaa. Zingatia hakukuwa na maandishi yoyote katika kulipana mahari, Wala hakukuwa na ndoa iliyofungwa kisheria ila hao wawili wamekaa pamoja karibu mwaka mzima. Je, mwanaume afanyaje ili walau apate haki yake?
Ahsante
 
Mkuuvipi kama watu walikutana, wakaanza kuishi pamoja Kisha mwanaume akapeleka mahari though watu (washenga) baada ya makubaliano ikapokelewa, ila kukawa na migogoro mingi katika maisha ya hao wawili (mwanamke na mwanaume) ei baadhi ya ndugu Wa mwanamke kutotaka Binti yao Aishi na huyo mwanaume. Ikafikia hatua mwanamke kujifungua mtoto ila babaye na mwanamke akamfuata na kumchukua na kukaa naye huko miezi kadhaa. Zingatia hakukuwa na maandishi yoyote katika kulipana mahari, Wala hakukuwa na ndoa iliyofungwa kisheria ila hao wawili wamekaa pamoja karibu mwaka mzima. Je, mwanaume afanyaje ili walau apate haki yake?
Ahsante
Haki gani mkuu?
 
Kesi za Talaka ni kesi za madai na hivyo sheria ya mwenendo wa madai (The Civil Procedure Code Cap 33 R.E 2019 hutumika. Mdai au mdaiwa anapokufa, kesi husimama kwa muda ili apatikane msimamizi wa mirathi wa marehemu ndiye aendelee na kesi. Kwa hiyo, vivyo hivyo, mali walizochuma ikitokea mahamaka imezigawa, basi marehemu atabaki nazo ila kwa uangalizi wa msimamizi wake wa mirathi.
Kesi ya talaka huratibiwa na sheria ya ndoa na Matrimonial proceedings rules pekee...application ya CPC ni kwa mazingira ambayo rules zimeruhusu.

Lakìni huwezi kufungua fresh matrimonial suit na ukabase kwenye CPC kama muongozo wako.

Nadhani maswali ya jamaa yanaenda mbali zaidi...effect ya death kwa parties ktk matrimonial proceedings. Death of one spouse renders any marriage as dissolved.

Sasa ikiwa kifo cha mwenza mmoja kinaua ndoa....je kesi yao kama ilikuwa pending mahakamani itakuwa na umuhimu upi tena? Maana to pronounce judgment as if one spouse yuko hai will be of no legal effect.

My opinion ni kuwa where one party to divorce proceedings dies before judgment is pronounced...the suit abates and does not survive to any legal representative of the deceased...

Everything will have to be dealt in probate and administration of estate laws.
 
Kesi ya talaka huratibiwa na sheria ya ndoa na Matrimonial proceedings rules pekee...application ya CPC ni kwa mazingira ambayo rules zimeruhusu.
Ahsante kwa mchango wako mkuu. Ni kweli kuwa the matrimonial proceedings rules ndio inayoratibu mambo ya talaka, lakini pale inaporuhusu CPC kutumika, sitaweza kusema kuwa,
kwa mujibu wa amri/kanuni ya .... the Matrimonial proceedings iliyoruhusu CPC kutumika basi hapa utafanya hivi na hivi,
badala yake nitaenda moja kwa moja kueleza nini CPC imesema juu ya jambo hilo.

Sasa ukisoma Kanuni/ Amri ya 29 (2) ya the Matrimonial Proceedings Rules inaeleza kuwa wakati wa kusikiliza maombi ya talaka na mali za machumo ya pamoja ( PETITION) mahakama itafanya kama ambavyo ingefanya kwa kesi iliyofunguliwa chini ya the Civil Procedure Code (CPC). Mambo kama namna ya kutoa ushahidi, vielelezo, madhara ya mashahidi kutofika mahakamani nk yataangaliwa kama yalivyoelekezwa kwenye CPC, na ndio maana nikaeleza jibu kuwa hatua zitazochukuliwa ni hizo kwa mujibu wa CPC. Neno nililosema CPC hutumika, nilimaanisha ni pale panapokuwa na lacuna kwenye Matrimonial Proceedings Rules.
 
Death of one spouse renders any marriage as dissolved.

Sasa ikiwa kifo cha mwenza mmoja kinaua ndoa....je kesi yao kama ilikuwa pending mahakamani itakuwa na umuhimu upi tena? Maana to pronounce judgment as if one spouse yuko hai will be of no legal effect.

My opinion ni kuwa where one party to divorce proceedings dies before judgment is pronounced...the suit abates and does not survive to any legal representative of the deceased...

Everything will have to be dealt in probate and administration of estate laws.
Hili jambo halijawekwa katika sheria yetu ya ndoa na wala Amri/kanuni za uendeshaji wa mashauri ya ndoa. Rule 29 (2) ya matrimonial proceedings imeeleza kuwa mahakama iendeshe kesi kama kesi iliyofunguliwa chini ya CPC, sasa kwa kesi iliyofunguliwa chini ya CPC nini hutokea pale mtu anapokufa kabla ya kesi?

imeelezwa chini ya Amri ya 22 (Order XXII) ya CPC kuwa mtu akifa ikiwa tayari usikilizwaji ulifanyika, basi ni kutolewa hukumu bila ya kujali kuwa mmoja ameshakufa. Ikiwa usikilizwaji haukuwa umekamilika, basi atatafutwa msimamizi wa mirathi ili aendeleze kesi. Ni kweli kuwa kifo kinahitimisha ndoa, sasa msimamizi wa mirathi aingie kufanya nini wakati ndoa imeisha yenyewe moja kwa moja? Jibu linakuja kuwa, ni kwa ajili ya mali zilizoombwa kugawanywa (my opinion).

Msingi wa kufanya hivyo ni kwa kuwa orodha ya mali bishaniwa inakuwa tayari ipo katika pleadings, hivyo yoyote anayerithi kesi anaweza kuiendeleza kwa kueleza juu ya mali hizo. Mtazamo wa UK nimeona wanasema kuwa mali zote zitahamia kwa mwanadoa aliyebaki hai ikiwa hakukuwa na wosia (anakuwa mrithi automatically), mtazamo wa jimbo la Pennsylvania USA, wanasema kuwa ikiwa misingi ya kuachana ilishathibitishwa mahakamani basi mahamaka ianendela kugawa mali hata kama mwanandoa mmoja amekufa.

Hakutakuwa na talaka kwa kuwa kifo tayari kitakuwa kimeamua chenyewe ila mali zilizochumwa pamoja na zile za binafsi zitatakiwa kujadiliwa katika suala hilohilo la ndoa na sio kwa mirathi, na haya ili yafanyike italazimu kuwa na msimamizi wa mirathi kwa mujibu wa CPC.
 
Haki gani mkuu?
Shukrani sana mkuu sajo kwa darsa hili muhimu. Nimejifunza mengi ambao nilikuwa siyajui. Kwenye maelezo yako umeonyesha kuwa ndoa inaweza kufungwa wakati mwenza mmoja hayupo physically? Ni sawa au nimeelewa vibaya? Kwa mfano mume yuko masomoni nje ya nchi, akaja Tanzania kwa likizo na kukutana na mwanamke, wakafanya urafiki lakini kwa sababu ya muda, akaondoka kabla hawajafunga ndoa. Je, anaweza kuondoka na kuomba mtu/ndugu, amuwakilishe kwenye ufungaji ndoa eg kiserikali, ili yule mwanamke atambulike kama mke wake?
 
sajo Mbona watu ya dini ya kislamu wanaenda andika talaka na kutengana kwa waliowafungisha ndoa (huko msikitini)
 
Namaanisha mwanaume anaweza kufunga ndoa na mwanamke mwingine na kusiwe na shida kisheria katika mazingira kama hayo?
Suala hilo kidogo lina changamoto kama ifuatavyo.

Mahari hutolewa kwa misingi ya kimila na kitamaduni, kwa makabila mengi ukishatoa mahari ni kama umekwisha kuoa ingawa msimamo wa sheria ni kuwa bado itatakiwa kufanyika harusi baada ya mahari. Na kwa maelezo yako ni kama ulianza kuishi na mwanamke na mpaka kuzaa nae baada ya kutoa mahari, kama hamkufanya sherehe ya harusi basi hamkufunga ndoa (ingawa kiafrika makabila mengi huhesabu hii kama ndoa tayari)

Changamoto ya pili, haieleweki uliwezaje kutoa mahari na ikapokelewa na watu wasiotaka ukae na binti yao. Hiyo mahari walipokeaje na uliitoa kwa watu sahihi? Baba alimchukua binti kwa sababu zipi?

Tatu, ujaeleza mwanamke wako anatakaje? Maana yeye ndiye mpingaji sahihi wa kwanza kwa ndoa nyingine, amekubaliana na matakwa ya wazazi wake au la. Pia hujaeleza kuwa sasa umeamua kuachana na huyo mwanamke au unaoa ila huyo pia uanendelea nae

Kwa ujumla, Kwa kuwa ukaaji wenu ulichukuliwa kama ndoa ya kimila, jibu ni ndio mwanaume anaweza kufunga ndoa na mwanamke mwingine, ila itakuwa ni ndoa ya wake wengi.
 
sajo Mbona watu ya dini ya kislamu wanaenda andika talaka na kutengana kwa waliowafungisha ndoa (huko msikitini)
Kwa imani ya uislamu, ndoa huweza kuisha kwa talaka au kwa makubaliano (khula au mubarat- Khula - mwanamke kurudisha mahari na kuanzisha mchakato wa kuachana; Mubarat - pande zote mbili kutotaka kuendelea na ndoa). Sasa huko misikitini na BAKWATA watu huenda ili kuthibitisha kuachana kwao lakini talaka rasmi ni ile inayotolewa mahakamani, kwa Zanzibar wao wana mahakama ya Kadhi, kwa hiyo baada ya mume kutamka talaka mbele ya mashahidi 2, huenda kwa Kadhi ili kuweza kupata cheti cha Talaka na kuwapa waliokuwa wanandoa. Huku Tanganyika, Mahakama pekee ndio inayotoa talaka, mume akimwacha mkewe bado atalazimika kwenda mahakamani ili kuthibitisha talaka hiyo.
 
Hili jambo halijawekwa katika sheria yetu ya ndoa na wala Amri/kanuni za uendeshaji wa mashauri ya ndoa. Rule 29 (2) ya matrimonial proceedings imeeleza kuwa mahakama iendeshe kesi kama kesi iliyofunguliwa chini ya CPC, sasa kwa kesi iliyofunguliwa chini ya CPC nini hutokea pale mtu anapokufa kabla ya kesi?

imeelezwa chini ya Amri ya 22 (Order XXII) ya CPC kuwa mtu akifa ikiwa tayari usikilizwaji ulifanyika, basi ni kutolewa hukumu bila ya kujali kuwa mmoja ameshakufa. Ikiwa usikilizwaji haukuwa umekamilika, basi atatafutwa msimamizi wa mirathi ili aendeleze kesi. Ni kweli kuwa kifo kinahitimisha ndoa, sasa msimamizi wa mirathi aingie kufanya nini wakati ndoa imeisha yenyewe moja kwa moja? Jibu linakuja kuwa, ni kwa ajili ya mali zilizoombwa kugawanywa (my opinion).

Msingi wa kufanya hivyo ni kwa kuwa orodha ya mali bishaniwa inakuwa tayari ipo katika pleadings, hivyo yoyote anayerithi kesi anaweza kuiendeleza kwa kueleza juu ya mali hizo. Mtazamo wa UK nimeona wanasema kuwa mali zote zitahamia kwa mwanadoa aliyebaki hai ikiwa hakukuwa na wosia (anakuwa mrithi automatically), mtazamo wa jimbo la Pennsylvania USA, wanasema kuwa ikiwa misingi ya kuachana ilishathibitishwa mahakamani basi mahamaka ianendela kugawa mali hata kama mwanandoa mmoja amekufa.

Hakutakuwa na talaka kwa kuwa kifo tayari kitakuwa kimeamua chenyewe ila mali zilizochumwa pamoja na zile za binafsi zitatakiwa kujadiliwa katika suala hilohilo la ndoa na sio kwa mirathi, na haya ili yafanyike italazimu kuwa na msimamizi wa mirathi kwa mujibu wa CPC.
kuna kesi moja ya Mahakama ya Rufani ambapo administrator alifungua matrimonial case akidai mali za the deceased spouse. Mahakama ikaeleza kuwa kwa kuwa sasa hakuna ndoa...msimamizi wa mirathi hawezi kuvaa viatu vya marehemu kufungua shauri la ndoa kwa niaba yake.

Akashauriwa kuwa angetumia kesi za mirathi kudai mali alizoacha marehemu ndani ya ndoa yake pindi alipokuwa hai.

Hii iko sawa na hii situation kifo cha mwenzi kinamaliza ndoa automatically...ikiwa ni hivyo na wanandoa walikuwa na shauri mahakamani juu ya ndoa hiyo na mmoja akafariki kabla ya hukumu...ile ndoa nayo inakuwa imekufa automatically...hatuwezi tena kwenye shauri lile lile la ndoa ambayo kwa waka huo itakuwa haipo, tukamteua msimamizi aje amalizie kipengele cha ugawaji wa mali za ndoa.

My opinion ni kuwa ile order 22 ya CPC inayozungumzia abatement of suits inakuja pale tu kama the suit survives after death. My opinion ni kuwa in matrimonial proceedings akifa mmoja wa wadaawa...shauri linakufa automatically pia. Hali survive. Maana right to sue does not survive in such circumstances.

kwa nini? ni kwa vile wadaawa walienda kuomba ndoa yao ivunjwe na wagawane mali kama zipo...sasa kabla hukumu haijatoka..ndoa ikavunjika automatically kwa kifo.....kesi ikiendelea itakuwa ni academic exercise. Hizo mali za marehemu, msimamizi wa mirathi akazidai kwenye mirathi ya huyo marehemu na si matrimonial proceedings.

it still remains my humble opinion.
 
Shukrani sana mkuu sajo kwa darsa hili muhimu. Nimejifunza mengi ambao nilikuwa siyajui. Kwenye maelezo yako umeonyesha kuwa ndoa inaweza kufungwa wakati mwenza mmoja hayupo physically? Ni sawa au nimeelewa vibaya? Kwa mfano mume yuko masomoni nje ya nchi, akaja Tanzania kwa likizo na kukutana na mwanamke, wakafanya urafiki lakini kwa sababu ya muda, akaondoka kabla hawajafunga ndoa. Je, anaweza kuondoka na kuomba mtu/ndugu, amuwakilishe kwenye ufungaji ndoa eg kiserikali, ili yule mwanamke atambulike kama mke wake?
Umeelewa vyema, ni sawa ndoa inaweza kufungwa bila uwepo wa mwenza mmoja, ili mradi tu mashuhuda wa huyo mwenza asiyekuwepo waliothibitisha uhiyari wake wa kuoa au kuolewa wakiwapo. Mfano halisi ni wa ndoa za waislamu, nyingi hufungwa kwa uwakilishi, unakuta baba au kaka anasimama kwa niaba ya muoaji, na ndoa hii inakuwa halali.

Na kwa huo mfano uliousema, jibu ni NDIYO inawezekana, ili mradi tu wawepo mashahidi wa mume ambao wanathibitisha kuwa mume alitoa hiyari (consent) yake kumuoa huyo mke.
 
Umeelewa vyema, ni sawa ndoa inaweza kufungwa bila uwepo wa mwenza mmoja, ili mradi tu mashuhuda wa huyo mwenza asiyekuwepo waliothibitisha uhiyari wake wa kuoa au kuolewa wakiwapo. Mfano halisi ni wa ndoa za waislamu, nyingi hufungwa kwa uwakilishi, unakuta baba au kaka anasimama kwa niaba ya muoaji, na ndoa hii inakuwa halali.

Na kwa huo mfano uliousema, jibu ni NDIYO inawezekana, ili mradi tu wawepo mashahidi wa mume ambao wanathibitisha kuwa mume alitoa hiyari (consent) yake kumuoa huyo mke.
Asante sana!
 
Kwa imani ya uislamu, ndoa huweza kuisha kwa talaka au kwa makubaliano (khula au mubarat- Khula - mwanamke kurudisha mahari na kuanzisha mchakato wa kuachana; Mubarat - pande zote mbili kutotaka kuendelea na ndoa). Sasa huko misikitini na BAKWATA watu huenda ili kuthibitisha kuachana kwao lakini talaka rasmi ni ile inayotolewa mahakamani, kwa Zanzibar wao wana mahakama ya Kadhi, kwa hiyo baada ya mume kutamka talaka mbele ya mashahidi 2, huenda kwa Kadhi ili kuweza kupata cheti cha Talaka na kuwapa waliokuwa wanandoa. Huku Tanganyika, Mahakama pekee ndio inayotoa talaka, mume akimwacha mkewe bado atalazimika kwenda mahakamani ili kuthibitisha talaka hiyo.
Mkuu sajo narudi tena na swali kama unaweza naomba jibu: Kuna jamaa mmoja alifunga ndoa na mwanamke na alifungia kwa mkuu wa wilaya, mkoani huko. Wakati anafunga ndoa, jamaa hakuwa na mtoto lakini mwanamke alikuwa tayari ana mtoto, wa miaka kumi kutoka kwa mwanaume mwingine ambaye hawakuwafunga ndoa. Yaani walizaa tu. Pamoja na hilo la mwanamke kuwa na mtoto, lakini jamaa alimkubali mwanamke. Alhamudulilah, ndoa ikawapitia watoto wawili na walikuwa wanaishi bila matatizo. Fast forward, baada ya kupita miaka kumi, jamaa akagundua kuwa kumbe huyo mke wake, alikuwa na mtoto mwingine aliyemzaa na mwanaume mwingine tena, kabla hawajafunga ndoa, lakini akadanganya kuwa anaye mmoja tu. Yaani kumbe manzi alidanganya ana mtoto mmoja, kumbe alikuwa tena na mwingine aliyemzaa na mwanaume mwingine (baba tofauti na yule mtoto wa kwanza) lakini akamficha. Je, ndoa kama hiyo inaweza kutengulia kwa kigezo cha mwanamke kudanganya status yake kabla ndoa haijafungwa?
 
Mkuu sajo narudi tena na swali kama unaweza naomba jibu: Kuna jamaa mmoja alifunga ndoa na mwanamke na alifungia kwa mkuu wa wilaya, mkoani huko. Wakati anafunga ndoa, jamaa hakuwa na mtoto lakini mwanamke alikuwa tayari ana mtoto, wa miaka kumi kutoka kwa mwanaume mwingine ambaye hawakuwafunga ndoa. Yaani walizaa tu. Pamoja na hilo la mwanamke kuwa na mtoto, lakini jamaa alimkubali mwanamke. Alhamudulilah, ndoa ikawapitia watoto wawili na walikuwa wanaishi bila matatizo. Fast forward, baada ya kupita miaka kumi, jamaa akagundua kuwa kumbe huyo mke wake, alikuwa na mtoto mwingine aliyemzaa na mwanaume mwingine tena, kabla hawajafunga ndoa, lakini akadanganya kuwa anaye mmoja tu. Yaani kumbe manzi alidanganya ana mtoto mmoja, kumbe alikuwa tena na mwingine aliyemzaa na mwanaume mwingine (baba tofauti na yule mtoto wa kwanza) lakini akamficha. Je, ndoa kama hiyo inaweza kutengulia kwa kigezo cha mwanamke kudanganya status yake kabla ndoa haijafungwa?
Ahsante kwa swali zuri. Ndoa hiyo haiwezi kutenguliwa kwa sababu tajwa ya mwanamke kudanganya status kwa kuwa status ya kuzaa au kutozaa sio kigezo cha kisheria cha kuzingatiwa mtu anapotaka kufunga ndoa, pili status inayozingatiwa kisheria ni ile kama mtu yupo kwenye ndoa tayari lakini akadanganya kuwa hana ndoa.

Hata hivyo, ukidanganywa bado itaonekana ni uzembe wako kwa kuwa sheria imeruhusu kufanya ukaguzi wa hali za ndoa za watu ili muoaji/muolewaji ajiridhishe na ajue anaoana na mtu mwenye hali gani ya ndoa. Ni muhimu kufanya search ofisi za RITA na hata sio gharama kubwa, ni shilingi elfu 20 tu.

Ila ukigundua kuwa ulidanganywa kwa hali ya ndoa, na ndoa hairuhusu nyongeza ya wake au ni mwanamke aliyedanganya, basi ile ndoa inakufa automatically mara baada ya kugundua, utakwenda baraza la kata kuomba mgawanyo wa mali za pamoja (kama zipo) ila sio kwenda mahakamani kuvunja ndoa ama dhana ya ndoa, maana hapo kulikuwa hakuna ndoa wala dhana.
 
Ahsante kwa swali zuri. Ndoa hiyo haiwezi kutenguliwa kwa sababu tajwa ya mwanamke kudanganya status kwa kuwa status ya kuzaa au kutozaa sio kigezo cha kisheria cha kuzingatiwa mtu anapotaka kufunga ndoa, pili status inayozingatiwa kisheria ni ile kama mtu yupo kwenye ndoa tayari lakini akadanganya kuwa hana ndoa.

Hata hivyo, ukidanganywa bado itaonekana ni uzembe wako kwa kuwa sheria imeruhusu kufanya ukaguzi wa hali za ndoa za watu ili muoaji/muolewaji ajiridhishe na ajue anaoana na mtu mwenye hali gani ya ndoa. Ni muhimu kufanya search ofisi za RITA na hata sio gharama kubwa, ni shilingi elfu 20 tu.

Ila ukigundua kuwa ulidanganywa kwa hali ya ndoa, na ndoa hairuhusu nyongeza ya wake au ni mwanamke aliyedanganya, basi ile ndoa inakufa automatically mara baada ya kugundua, utakwenda baraza la kata kuomba mgawanyo wa mali za pamoja (kama zipo) ila sio kwenda mahakamani kuvunja ndoa ama dhana ya ndoa, maana hapo kulikuwa hakuna ndoa wala dhana.
Asante sana mkuu kwa majibu na muda wako.
 
Mkuu kuna mahali umesema "Ndoa za kimila ili iwe ndoa kisheria, zinahitaji ifanyike harusi baada ya kulipa mahari". Naomba tafsiri ya hilo neno HARUSI kwenye hio sentensi. (ulimaanisha tafrija pekee?)

Infact nahitaji kufahamu tafsiri ya KUOA, ni hatua ipi kisheria itafanya uwe umeoa?

Nauliza kutokana na dhana za mitaani kuwa ukilipa mahari umeoa, wengine hudai ukitoa posa umeshaoa, wengine husema ukifunga ndoa(ukiwa na CHETI) wewe ndio umeoa.

Na kuna tofauti kati ya kuoa na kufunga Ndoa?
 
Back
Top Bottom