Abul Aaliyah
JF-Expert Member
- Nov 8, 2016
- 7,718
- 5,899
Paskali kajificha, huezi muona hapa.Mbona hao Mataga na Praise team wenyewe hawana tofauti na bendera! Wenyewe hufuata tu uelekeo wa upepo. Usije ukashangaa wakija kwa kasi huku wakiunga mkono hicho kitendo. Ndivyo walivyo siku zote! Wapo kama misukule tu.
Hata Rais akijitoa kwenye Chama alichoshindia Urais,Kumbuka bila chama hakuna mbunge.
Mbunge asiyekuwa na chama anatoka wapi?
Wako wanajifukiza (wanapiga nyungu) wakimaliza watajitokeza. Mhimili wa Bunge umedhalilishwa sana awamu hii ya tano.Mbona hao Mataga na Praise team wenyewe hawana tofauti na bendera! Wenyewe hufuata tu uelekeo wa upepo. Usije ukashangaa wakija kwa kasi huku wakiunga mkono hicho kitendo. Ndivyo walivyo siku zote! Wapo kama misukule tu.
Anuani ya mawasiliano na makazi tafadhali, yaani Tanzania au visiwa vya Tonga.AZIMIO LA KUMSHTAKI SPIKA WA BUNGE LA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA MHE. JOB NDUGAI KWA KUKIUKA MISINGI YA KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA BAADA YA KUMRUHUSU BW. CECIL MWAMBE KUENDELEA NA UBUNGE
Ndugu RAIA MWEMA,
Awali ya yote tunakushukuru na kukupongeza kwa kazi kubwa unayoifanya ya kuzuia kuenea kwa maambukizi ya COVID-19 hasa wakati huu ambapo dunia inaendelea kupambana na janga la virusi vya Corona (COVID 19). Sisi kama watetezi wa haki za binadamu tunapenda kukutia moyo uendelee kujilinda wewe pamoja na uwapendao.
Ndugu RAIA MWEMA,
Shirika la Elimu ya Uraia na Msaada wa Sheria (CILAO) limesikitishwa na kitendo cha Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai kufanya maamuzi yanayokiuka misingi ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Itakumbukwa kwamba, Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Vyama vya Siasa vinaongozwa kwa mujibu wa Katiba na sheria zingine za nchi. Ibara ya 71 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaeleza wazi kuhusu ukomo wa mtu kuwa Mbunge. Kwa mujibu wa Ibara ya 71(1)(e) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ni wazi kuwa Mbunge atapoteza nafasi yake ya ubunge ikiwa atapoteza uanachama wa chama chake kilichompatia dhamana ya ubunge wakati wa uchaguzi.
Mnamo tarehe 6 Mei 2020, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Job Ndugai, aliruhusu, aliyekua mbunge wa Ndanda, Bw. Cecil Mwambe ambaye alishajiuzulu nafasi yake ya ubunge aendelee na kazi hiyo. Hata hivyo, Bw. Cecil Mwambe alishaonekana katika vyombo vya habari akitangaza kujivua uanachama wa CHADEMA na kujiunga na Chama cha Mapinduzi (CCM).
Kwa kuwa Bw. Mwambe alishatangaza kijiondoa CHADEMA, basi tunaamini pasipo shaka kwamba alipoteza tayari sifa ya kuendelea kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Ndugu RAIA MWEMA,
Kitendo cha Spika kumruhusu Bw. Cecil Mwambe kuendelea kuwa Mbunge ni ukiukwaji wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kwa kuwa Katiba inatamka wazi katika Ibara ya 26(1) kuwa kila RAIA ana wajibu wa kusimamia na kutetea Katiba na Sheria, sisi kama Taasisi tunaomba kushirikiana nawe na wadau wengine kusaini azimio hili la haraka ili kumtaka SPIKA kubatilisha maamuzi yake. Pia tunaomba tushirikiane haraka iwezekanavyo kufungua kesi katika Mahakama Kuu kuomba ufafanuzi wa Mahakama kuhusu kitendo hiki cha Spika.
#PamojaTulindeKatiba
Azimio hili limeandaliwa na: Civic and Legal Aid Organisation (CILAO)
Sent using Jamii Forums mobile app
Kwani kwenye barua yao si wamesema wanakusudia kwenda mahakamani au hukuisoma?Kama amekiuka Katiba si mchukue hatua kuliko kulalamika tu huku mtandaoni. Jamani inakera. Mahakama si zipo.
Yaani imebidi nicheke msibani eti " ... hiyo ni spika tu chanzo ni redio ..."Haya mambo mwalimu NYERERE, aliyaona sana, ndio maana akasema binadamu anaweza akajifanya MUNGU mtu, na ndio kinachotokea na hiyo ni spika tu chanzo ni radio ipo sehemu nyingine kijijini imetulia, mambo yanaendeshwa kama mpira wa makaratasi?
Kwa Tanzania sahau hili halitokuja kutokea, kuna watu hata hili wanamuunga mkono 100%. Nchi ambayo majority ni vilaza labda itokee kitu kiue 50% ya vilaza wote kitu ambacho ni impossible. Power play itazidi kua hivi Tanzania miaka na miaka. Ukichoka haisaidii huku majority ya nchi nzima wanaunga mkono
Lazima alaumiwe sababu amekaa anasikiliza mambo anajua si ya haki ila anafata tu, yeye si mtu mzima ana elimu anaweza kataa? Kama kiongozi wa muhimili unaojitegemea kukubali kuendeshwa na mtu mwingine lazima tumlaumu, kashikwa map****bu tu anatekenywa anacheka, jinga kabisamnalaumu Spika bure tu....
fuatilia uone Nani kashika microphone
Wewe kwa akili zako unaona yuko sahihi hakukiuka katiba?Hii awamu kusigina katiba imegeuka jambo la kawaida kwa wakubwa na hawajali lolote.
Vipi kuhusu Mheshimiwa Selasini Mbunge wa Rombo aliyetangaza hadharani kujivua uwanachama wa Chadema na kuhamia NCCR-Mageuzi na bado anaendelea na ubunge?.
Yaani Chadema inatangaza kwamba Wabunge wake waliohamia NCCR Mageuzi wataendelea na Ubunge lakini aliyehamia CCM avuliwe, hii ni akili?
Nakumbuka vizuri kwamba, Spika alihitaji Muhtasari wa Kikao cha chama cha CHADEMA kuhusu kumuondolea Mwambe Ubunge. Lakini Chadema waliwasilisha barua pekee pasipo viambatanisho.
Civil Society msitumike kama mawakala wa Mabeberu na Vyama vya upinzani, teteeni Haki za Kiraia zenye tija kwa wananchi na Taifa.
Lengo lenu ni kuikomoa CCM, Kumkomoa mbunge au Wananchi wa Rombo wasipate mwakilishi katika bunge la bajeti?.
Ikumbukwe kwamba, Mheshimiwa Zitto, wakati amezuliwa uwanacha na Chadema, bado aliendelea na ubunge, Mbona hamkuazimia kumshtaki spika wala mahakama?.
Mbunge ni mwakilishi wa wananchi sio chama, hivyo tulieni
Hizi nazo ni mahakama?Kama amekiuka Katiba si mchukue hatua kuliko kulalamika tu huku mtandaoni. Jamani inakera. Mahakama si zipo.