Ukifanya hizo mishe na mbongo kuambiwa bibi kadedi niskilizie tupitishe kwanza arobaini mbona kawaida sana mkuu.Biashara za ahadi ya malipo ya tarehe fulani (Promissory Notes). Kwa wabongo ni sumu usijaribu huwa hawajali muda!
Hii kitu imenisababishia headaches mpaka sasa nimekwama. Kuna watu nimewauzia mali wakalipia Advance ila kumalizia mikia ndio imekuwa shughuli.
Tunasumbuana mpaka nafikiria nikafungue kesi polisi. Wanakera kinoma yani. Mmoja biashara ya 19/5 akaahidi kumalizia 2/6 ila hajafanya hivyo mpaka sasa ni story nyingi tu mara msiba, mara vile mwisho ananiambia nimepambana nimeshindwa labda mpaka mwisho wa mwezi. Ina maana nipoteze mwezi wote wa 6 bure tu!
Mwengine nae wa Tarehe 9/4 akaahidi by tarehe 30/4 anamaliza. Imefika siku ya kulipa hela hana, akanipiga sound mpaka 15/5 hela yenyewe akatoa nusu. Tumesumbuana tarehe 23/5 akatoa tena nusu ya iliobaki. Toka na hapo hela hajamalizia tena kila nikimcheki anapambana mambo magumu.
Yani usumbufu ninaoupata ndio naelewa umuhimu wa biashara za cash in hand. Mnafunguana mashati mapema tu kila mtu anasonga na njaro zake.
Sisi waswahili hatuna uungwana kabisa. Kumbuka nilipe nisepe wa Belle9 jaribu kusikiliza ukufariji mzee.Yani jau sana mwanangu mwenyewe...Sema nn nimejifunza kitu mkuu! Sahivi mikazo ntakayowapa walimwengu Nduli Iddi Amini akasome. Wacha niitwe roho mbaya kmmmk maana roho za kikristo zinaturudisha nyuma sana wabongo.
Ku deal na wapuuzi ni ushwaini!
Hakuna lolote unawaambia ukweli kuwa hataki kukupa hela yako hata police ni waelewa.. Usiogope kitu kwenye Mali yakoje ukifanya hvo afu akakuitia police kwamba umemletea "vurugu " (au umemvamia) kwny eneo lake la biashara?
Watoe pesa ya usumbufu halafu waambie wakusaidie kuwapa presha hawa wahusika ili walipe ama mali zao zitashikiliwa kufidia hayo madeniHawawezi kunisaidia kuharakisha malipo maana naona usumbufu umekuwa mkubwa na hasa muda wangu ndio mali.
Hapana. Haina haja ni jamaa tu kupigwa presha na kesi unaiweka katika sura ya utapeli ambayo itakuwa jinaiUnae mdai atasema ana uwezo wa kukulipa elfu 5 kila mwezi kutokana na hali mbaya ya uchumi. Hivyo atakuwa anapunguza hiyo buku 5 hadi deni liishe.
Hapo unakuta unadai laki 5! Mna andikihsna kituoni na kila mtu anaenda na njia zake. Ndio taratibu za kesi za madai zinavyokuwa polisi.
Hapana. Haina haja ni jamaa tu kupigwa presha na kesi unaiweka katika sura ya utapeli ambayo itakuwa jinai
Kweli mkuu, nmejifunza aisee bora kubaki na mali yako kuliko kumuuzia mtu kwa advance ambaye atasumbua kumalizia malipo.Sisi waswahili hatuna uungwana kabisa. Kumbuka nilipe nisepe wa Belle9 jaribu kusikiliza ukufariji mzee.
Weka mikakati na kanuni ya namna unataka kuendesha biashara yako. Hakikisha hata wewe mwenyewe huzivunji. Mambo yatakuwa shwari baadae. Ila ogopa sana biashara ya mali kauli hasa kipindi hiki cha COVID-19.