Usijichanganye ukachukua “Simu za mkopo”

Hawa jamaa sio wazuri sumsung A03 sijui A14 hahaha et kwa siku 2000 kuanzio 50k.

Kwa mwaka inakuja kama laki 7 na elf 70.

No huu ni unyonyaji.
Hivi wewe umpe mtu simu ya laki 4 halafu akupe 2k kwa siku utakubali? Hiyo 2k hata utajua umefanyia nini?miki hata unilipe hiyo 2k kwa miaka 10 sikukopeshi.., buku mbili nafanyia nini sasa? Maana ni sawa na kuflush choo kwa kudondosha tone moja moja, hata mwaka mzima kimba haliendi.., ni useless
 
Unajua wanao kopa wangap? Tambua hizo simu zinakopwa na maelf ya watu. Tanua akili yako japo kidogo.
 
Mkuu unafuu unaupima kwa kupiga mahesabu ya gharama za kuwekeza vs gharama za mkopo. Gharama za mkopo ushaona ni laki tatu je gharama za kuwekeza mwenyewe ifike laki nne ni kiasi gani?
Nilimaanisha kuwekeza kwa wanaouza simu. Wengine wanaruhusu mteja kuweka kiasi chochote cha pesa kwenye akaunti ya muuzaji hadi hapo utakapokamilisha malipo yako kulingana na aina ya simu uliyochagua ndipo unapewa simu yako.
Hata hivyo kupanga ni kuchagua. Ni vizuri mhusika akachagua njia atakayoona inamfaa
 
Mimi hata sielewi mnachololamika hapo nini, unataka mkopo wa mwaka mzima wakupe simu kwa riba ya 10%?

Kuna options nyingi,
•Save 2000 kila siku hadi ifike 400k ununue cash.
•Chukua mshahara wako ununue mpya chap tu.

Hii 2k per day ina walengwa wake, wenye vipato vidogo na wanahitaji simu yenye ubora mzuri kiasi.
 
Unataka kuanzia sh ngapi mkuu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…