Usiku wa kwanza katika ardhi ya Tanzania, Junior alilala mahabusu Keko

Usiku wa kwanza katika ardhi ya Tanzania, Junior alilala mahabusu Keko

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
Junior ni Mholanzi mwenye asili ya Tanzania. Wazazi wake walihamia Uholanzi wakiwa bado vijana. Maisha yake yote Junior ameishi Amsterdam. Alikuja Tanzania kwa mara ya kwanza akiwa na miaka mitano.

Baada ya sherehe yake ya kuzaliwa akifikisha miaka 18, babu na bibi walimnunulia tiketi aje awaone. Junior alibeba misikoto kama mitatu ya bangi, jambo ambalo huko kwao ni sawa kabisa kama si ya kuuza ni kwa matumizi binafsi.

Junior alipotua Tanzania aligundulika kuwa na misokoto. Alipoulizwa alisema ni kwa matumizi yake binafsi. Aliwekwa chini ya ulinzi. Usiku wa kwanza babu hakufanikiwa kumtoa na alilala Keko.

Tuwaeleze vijana wetu wanaozaliwa Ughaibuni sheria za Tanzania kuepusha matatizo kama haya.

1622169933923.jpeg
 
Ubalozi wa Uholanzi ulikaa kimya na wenyewe?
 
Siku ya kwanza haikuwezekana lakini alifanikiwa kutoka asubuhi ya siku ya pili baada ya babu kuhangaika sana.
Kwa utaratibu wa kidiplomasia balozi alitakiwa amtoe raia wake hapo ni uzembe wa ubalozi wake
 
Sawaa una mawasiliano yake nimfanyie delivery?? Asikae mpweke akatusema vibaya akilud kwako
Alipotoka Keko babu alimchapa na bakora za kutosha. Hakutegemea yule mjukuu wake Junior kuwa ni mvuta bangi wakati kwa Junior hii ilikua swaga.
 
Alipotoka Keko babu alimchapa na bakora za kutosha. Hakutegemea yule mjukuu wake Junior kuwa ni mvuta bangi wakati kwa Junior hii ilikua swaga.
Kheeh wakati kwenye dunia yetu tulioumba sie (Holland maana tunadai Mungu aliumba Netherlands sisi tukaumba Holland) Tuna hadi vibanda vya kahawa special kwa kuvuta hiyo kitu
 
Kheeh wakati kwenye dunia yetu tulioumba sie (Holland maana tunadai Mungu aliumba Netherlands sisi tukaumba Holland) Tuna hadi vibanda vya kahawa special kwa kuvuta hiyo kitu
Ulaya unaruhusiwa kuwa na kiasi kidogo kwa matumizi yako lakini hairuhusiwi kuuza. Sasa wananunua wapi sifahamu.
 
Siku ya kwanza haikuwezekana lakini alifanikiwa kutoka asubuhi ya siku ya pili baada ya babu kuhangaika sana.
Hapo UK tu walikuwa hawaruhusu bangi, miaka kadhaa nyuma kuna familia walikuwa wana mtoto ana tatizo la nervous system, ambapo ilikuwa imependekezwa bangi kuwa inaweza kumsaidia.

Ilibidi wahame kwenda nchi inayoruhusu bang ili waweze kuitumia kama tiba.
Jr alipaswa kufanya research kabla. Ila sijui kwanini serikali hairuhusu kilimo cha bang watu wakalima na kuexport.
 
Hapo UK tu walikuwa hawaruhusu bangi, miaka kadhaa nyuma kuna familia walikuwa wana mtoto ana tatizo la nervous system, ambapo ilikuwa imependekezwa bangi kuwa inaweza kumsaidia.
Ilibidi wahame kwenda nchi inayoruhusu bang ili waweze kuitumia kama tiba.
Jr alipaswa kufanya research kabla. Ila sijui kwanini serikali hairuhusu kilimo cha bang watu wakalima na kuexport.
Kuna uzi alipost mkuu Extrovert kwamba imeruhusiwa...
 
Hapo UK tu walikuwa hawaruhusu bangi, miaka kadhaa nyuma kuna familia walikuwa wana mtoto ana tatizo la nervous system, ambapo ilikuwa imependekezwa bangi kuwa inaweza kumsaidia.
Ilibidi wahame kwenda nchi inayoruhusu bang ili waweze kuitumia kama tiba.
Jr alipaswa kufanya research kabla. Ila sijui kwanini serikali hairuhusu kilimo cha bang watu wakalima na kuexport.
Kuhusu Junior si ajabu hata wazazi wake hawafahamu kuwa anavuta bangi hivyo hawakuweza kumpa tahadhari.
 
Kuhusu Junior si ajabu hata wazazi wake hawafahamu kuwa anavuta bangi hivyo hawakuweza kumpa tahadhari.
Hiyo ni kweli, maana watu wana siri nyingi. Halafu kisa cha huyo mtoto nimekisoma tena nadhani shida siyo bangi, ila matibabu ya kutumia bangi kama dawa mbadara yalikuwa hayajawa approved U.K.
Sema bangi mmea makini sana.
 
Back
Top Bottom