Usinunue kiwanja au shamba lenye mbuyu mkubwa kama huna uwezo wa kukabiliana na changamoto zake

Niliyo kuambia ni ploti yangu mwenyewe, tena iko Pwani.
Sifanyi biashara ya kukata miti.
Ukikubali moyo na roho yako ididimizwe na washirikina, hiyo ni hiyari yko
Mimi ni fundi siyo mwanasiasa! Lete namba ukakate mbuyu mmoja na posho nzuri utapewa! Chamhimu mbuyu utoke! Tusibishane hapa kwa maneno!
 
Mimi ni fundi siyo mwanasiasa! Lete namba ukakate mbuyu mmoja na posho nzuri utapewa! Chamhimu mbuyu utoke! Tusibishane hapa kwa maneno!
Mbuyu wako ni pilipili ya shamba kwangu.
Nia principle ya kutojihusisha na yasiyonihusu.
Nimekueleza pale kwangu nilichofanya.
Acha uoga ukakate kero yako.
 
Basi hamna wacha Mungu humu ndo maana majini tumeingia [emoji1787] [emoji1787] miafrika tunasafari ndefu sana.
I used to think like you kwamba ushirikina ni story za kusadikika.

Mpaka nilipokutana nao kwenye matukio mawili mbele ya macho yangu.

Achana na hii dunia ina mengi sana ambayo hatuyajui.
 
I used to think like you kwamba ushirikina ni story za kusadikika.

Mpaka nilipokutana nao kwenye matukio mawili mbele ya macho yangu.

Achana na hii dunia ina mengi sana ambayo hatuyajui.

Fikiri vizuri Kuna logical explanation ya uliyokutana nayo, you seem like a sharp-witted man sio kama hawa waaminio kama nyumba wakiambiwa ushirikina tu wanaamini Moja kwa moja no reasoning whatsoever.
 
Sahihi.

Wachawi ni magwiji wa UNAFIKI.
 
Bosi kubwa, ulitakiwa utoe na mifano ili tujue changamoto, yaani ungetujuza mfano sehemu fulani mlishindwa kuukata etc
 
Kuna jirani yetu kipindi nipo Mwanza. Alipewa kazi ya kukata mti mkubwa kwenye kiwanja cha mtu. Baada ya kumaliza kukata. Alikaa kama siku 3 naye alikufa.

Labda kulikuwa kuna matambiko ya watu lakini kibangi bangi watu wanaruka nao ukitangaza dau
 
Ulipata shida sana, nunua chumvi kilo kadhaa kutegemea na ukubwa wa mbuyu, uchimbe, weka changanya na oil chafu, njoo wiki tatu utakuta mbuyu umekufa umeoza.. kazi kwisha... nilitumia roughly 120,000/= tu.

Daa!!sijajua ndugu ila ilibidi niendeleze hapo choo na kweli mikapata
 
Mh wakati nipo mdogo shule tukifagia tulikuwa tunakuta mibuyu imeota asa mm nilikuwa naing'oa nikaambiwa ukifanya ivyo hutopata mtot up now no child I don't know that it's true or not

Na ukaamini
 
Sijui kwa nini, ila naukumbuka ule Mbuyu pale Kinondoni Hananasifu (jirani na shule) tangu 1980's. Miaka 10 iliyopita nilifika pale na ulikuwepo.
Kuna mwingine upo kinondoni katikati ya barabara ya kwenda mahakamani sijui ni mbuyu ule!
 
Mbuyu wako ni pilipili ya shamba kwangu.
Nia principle ya kutojihusisha na yasiyonihusu.
Nimekueleza pale kwangu nilichofanya.
Acha uoga ukakate kero yako.
hamna lolote ujuaji mwingi. Si umeambiwa utoe namba kibaru kipo nenda ukakate sasa.
 
hamna lolote ujuaji mwingi. Si umeambiwa utoe namba kibaru kipo nenda ukakate sasa.
Nitakuwa mwendawazimu kwenda kukata mibuyu isiyonihusu kwa sababu ya fedha kiduchu na mabishano mtandaoni.
I've got better things to do.

Ukiwa na imani za kijinga jinga unaumia mwenyewe, ninachoweza kukuambieni, uza hicho kiwanja wajanja zaidi wakinunue.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…