Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Weee nawe kwahiyo ambao hawajajenga hawapaswi kwenda (mliani city) mlimani city kununua simu ya laki Tisa? Watu wana vitu zaidi ya hivyo wanaishi vizuri kuzidi hata waliojengaWee una akili Sana tunaweza kuwa washkaji
Alfu kingine umepanga alfu unaenda mliani cty kununua simu ya laki Tisa milioni. HV nmtu huna vya kufanya mpk kufanya hvyo
Elon musk Hana nyumba amepanga. Nadhani Kila mtu anaishi maisha anayopendaKujenga wakati mwingine ni uoga wa maisha tu, ukiwa na pesa waweza ishi popote isipokuwa mbinguni tu.
kuna watu hapa bongo hudhan nyumba ukiwa nayo umemaliza kila kitu! Nyumba ukiwa nayo kama huna kijaza kipato shida ziko pale paleee,Nyie ndo wale wenye nyumba mnaotegemea kodi kuishi, mnakuaga wanoko, wambea, wachunguzi,
Mnamchunguza Mpangaji wako kapika nini uombe au kanunua nini upandishe bili ya umeme,
Kama nyumba yako uliyojinyima ni kila kitu anza kula matofali msiwakere wapangaji.
Ujinga mtupu.Ishi vizuri kwako I second you!
Wazee WA ready made misifa[emoji2]Watu wengi hupenda kununua vitu vya thamani na kuishi navyo kwenye nyumba za kupanga (nyumba za wanaume wenzao, waliojinyima na kuweka mijengo).
Kufanya hivyo, kunawafanya watu wengi kuishi muda mrefu kwenye nyumba za kupanga, na kusahau kujenga nyumba zao.
Utakuta mtu ana kipato kizuri; lakini utashangaa atakimbilia kununua gari, music system ya gharama, tv kubwa ya gharama n.k, na hivyo vyote anavipaki kwenye mjengo wa mwanaume aliyejinyima na kutimiza ndoto zake.
Inapotokea kipato kimeyumba, na kushindwa kujikimu kwenye kodi ya pango; wanakosa sehemu ya kwenda kuvipaki vitu walivyovinunua kwenye nyumba ya kupanga; matokeo yake ni kuanza kuviuza kwa bei ya hasara.
Ushauri; kwenye nyumba za kupanga, weka godoro, kitanda na vitendea kazi vya kupikia tu.
Salio linalobaki; nenda katafute kiwanja ujenge