Usipoamua kufanya mazoezi utaendelea kuwa msukule wa hawa wanaharakati wa afya.

Usipoamua kufanya mazoezi utaendelea kuwa msukule wa hawa wanaharakati wa afya.

Matongee

JF-Expert Member
Joined
Jun 17, 2023
Posts
1,056
Reaction score
2,729
Wakuu lazima tukubaliane kuwa maisha yamebadilika sana kuanzia vijijini hadi mijini. Na mabadiliko yametokea ghafla. Ujio wa bodaboda na mabadiliko makubwa ya teknolojia kama uwepo wa mitandao ya kijamii na mobile money umepunguza ugumu wa kazi nyingi. Urahisi wa kufanya kazi nyingi pia nao umekuja na changamoto za kiafya hasa unene na magonjwa yasiyoambukiza hali inayofanya tujikite kwenye mazoezi.

Zamani kutokana na kutokuwepo usafiri ilikuwa kawaida mtu wa Karatu mjini kutembea kwa mguu hadi kijiji cha Geykrum Lambo kufanya jambo lake kisha kurudi tena town. Hapo ni zaidi ya 10km. Mtu kama huyu hata ale chapati 8 kwa siku ilikuwa ngumu kunenepa kirahisi. Hata Arusha mtu alikuwa anatoka Kwa Mromboo hadi Mkonoo kwa mguu kutokana na kutokuwepo kwa usafiri. Kimsingi shuguli nyingi za siku zilikuwa sawa na kufanya mazoezi tena makali. Vibonge walikuwa wachache mno.

Kutokana na urahisi uliopo ninawasihi ndugu zangu tufanye sana mazoezi kutunza afya zetu. Vinginevyo tutakuwa misukule ya hawa wanaharakati uchwara mitandaoni wanaosema tusile ugali, wali, asali, matunda, wala kunywa maji ya bomba. Mazoezi ya kukimbia na gym ni muhimu sana ili uwe huru na maisha yako. Zoezi litalinda mwili wako na kukuweka fit pia mwonekano mzuri.
 
Wakuu lazima tukubaliane kuwa maisha yamebadilika sana kuanzia vijijini hadi mijini. Na mabadiliko yametokea ghafla. Ujio wa bodaboda na mabadiliko makubwa ya teknolojia kama uwepo wa mitandao ya kijamii na mobile money umepunguza ugumu wa kazi nyingi. Urahisi wa kufanya kazi nyingi pia nao umekuja na changamoto za kiafya hasa unene na magonjwa yasiyoambukiza hali inayofanya tujikite kwenye mazoezi.

Zamani kutokana na kutokuwepo usafiri ilikuwa kawaida mtu wa Karatu mjini kutembea kwa mguu hadi kijiji cha Geykrum Lambo kufanya jambo lake kisha kurudi tena town. Hapo ni zaidi ya 10km. Mtu kama huyu hata ale chapati 8 kwa siku ilikuwa ngumu kunenepa kirahisi. Hata Arusha mtu alikuwa anatoka Kwa Mromboo hadi Mkonoo kwa mguu kutokana na kutokuwepo kwa usafiri. Kimsingi shuguli nyingi za siku zilikuwa sawa na kufanya mazoezi tena makali. Vibonge walikuwa wachache mno.

Kutokana na urahisi uliopo ninawasihi ndugu zangu tufanye sana mazoezi kutunza afya zetu. Vinginevyo tutakuwa misukule ya hawa wanaharakati uchwara mitandaoni wanaosema tusile ugali, wali, asali, matunda, wala kunywa maji ya bomba. Mazoezi ya kukimbia na gym ni muhimu sana ili uwe huru na maisha yako. Zoezi litalinda mwili wako na kukuweka fit pia mwonekano mzuri.
Nimeipenda hii:,Mimi nimekulia kwa Babu na Bibi na kusoma Huko Hayo yote uliyoshauri ni Muhimu na lazima kwa anajali afya yake,tuwaache wanaosema nitakufa tuu siku ikifika,Unskufaje kizembe kwa kukosa mazoezi tuu!Mimi kila siku nafanya kazi za kuushughulisha mwili,kulima bustani,pushups, kuchimba mashimo ya kupania miti na migomba,kutembea km2,Siku zingine na bila kusahau kula matunda,Nina miaka 54,Vijana wa 2000 Hawaniamkii kwani hawaamini wananiona kama,tko Rika sawa.
Mazoezi Muhimu, mazoezi ni tiba, mazoezi ni Afya,tufanye mazoezi.
 
Kulikuwa na misemo kuwa Mtu mnene ndiye mwenye afya nzuri au maisha mazuri. Bila shaka Imani hii enzi ilitokana na kwamba wanene walikuwa wachache.

Ila enzi hii Hali ni tofauti. Ni rahisi sana kunenepa kuliko kuwa na slim body!
Hasa hizi buffer zimetuharibu sana!Unakula kwenye maharusi,unapiga bia usiku wa manane,unaamka hoi!Bado asubuhi unaanza na supu ,bia.Hatari sana
 
Uko sahihi mkurugenzi... Watu wengi tumekuwa wavivu kutembea kwa mguu.... Nikiwa darasa la saba nilihamiaga shule ya Kijiji Cha jirani na Kijijini kwetu... Nilikuwa natembea zaidi ya km 8 Kila siku... Kwenda na kurudi nyumbani.... Sasa hivi kutembea km 2 tu nahema kwelikweli 🤣 🤣 🤣....
 
Watu wamefika mbali hadi kiberiti cha kufata dukani anamtuma bodaboda
Mkuu,hii sio Hadithi kuna Jamaa yangu Mmoja ni dogo kiumri ila tumeshibana sana.Akawa analalamika Kuwa anawashwa na miguu kwenye unyayo na kututusika,Tukawa tuko na Dr mmoja yeye ni mtaalamu wa viungo vya Binadamu kwa ujumla,akamuuliza jamaa historia yake Kwa ufupi jamaa hajawahi kukanyaga chini Toka azaliwe, yeye ni ndala na viatu!Dr akamshauri awe anatembea peku kwa kunyoosha barabara na aanze mazoezi nyumbani,Hiyo ikawa imeisha na hakutumia dawa na ndoa yake Iko vizuri kuliko mwanzo,anawalaumu sana wazazi wake kumlea kimayai sana.Hivi ni Kwa ufupi tuu,nitakuwa nimeeleweka.
 
Nimeipenda hii:,Mimi nimekulia kwa Babu na Bibi na kusoma Huko Hayo yote uliyoshauri ni Muhimu na lazima kwa anajali afya yake,tuwaache wanaosema nitakufa tuu siku ikifika,Unskufaje kizembe kwa kukosa mazoezi tuu!Mimi kila siku nafanya kazi za kuushughulisha mwili,kulima bustani,pushups, kuchimba mashimo ya kupania miti na migomba,kutembea km2,Siku zingine na bila kusahau kula matunda,Nina miaka 54,Vijana wa 2000 Hawaniamkii kwani hawaamini wananiona kama,tko Rika sawa.
Mazoezi Muhimu, mazoezi ni tiba, mazoezi ni Afya,tufanye mazoezi.
54?
 
Mkuu,hii sio Hadithi kuna Jamaa yangu Mmoja ni dogo kiumri ila tumeshibana sana.Akawa analalamika Kuwa anawashwa na miguu kwenye unyayo na kututusika,Tukawa tuko na Dr mmoja yeye ni mtaalamu wa viungo vya Binadamu kwa ujumla,akamuuliza jamaa historia yake Kwa ufupi jamaa hajawahi kukanyaga chini Toka azaliwe, yeye ni ndala na viatu!Dr akamshauri awe anatembea peku kwa kunyoosha barabara na aanze mazoezi nyumbani,Hiyo ikawa imeisha na hakutumia dawa na ndoa yake Iko vizuri kuliko mwanzo,anawalaumu sana wazazi wake kumlea kimayai sana.Hivi ni Kwa ufupi tuu,nitakuwa nimeeleweka.
Hongera sana
 
Kulikuwa na misemo kuwa Mtu mnene ndiye mwenye afya nzuri au maisha mazuri. Bila shaka Imani hii enzi ilitokana na kwamba wanene walikuwa wachache.

Ila enzi hii Hali ni tofauti. Ni rahisi sana kunenepa kuliko kuwa na slim body!
Sure
 
Mkuu,hii sio Hadithi kuna Jamaa yangu Mmoja ni dogo kiumri ila tumeshibana sana.Akawa analalamika Kuwa anawashwa na miguu kwenye unyayo na kututusika,Tukawa tuko na Dr mmoja yeye ni mtaalamu wa viungo vya Binadamu kwa ujumla,akamuuliza jamaa historia yake Kwa ufupi jamaa hajawahi kukanyaga chini Toka azaliwe, yeye ni ndala na viatu!Dr akamshauri awe anatembea peku kwa kunyoosha barabara na aanze mazoezi nyumbani,Hiyo ikawa imeisha na hakutumia dawa na ndoa yake Iko vizuri kuliko mwanzo,anawalaumu sana wazazi wake kumlea kimayai sana.Hivi ni Kwa ufupi tuu,nitakuwa nimeeleweka.
Asante Kwa kunikumbusha swala la kutembea peku
 
Uzi mzuri sana...asante kwa kutukumbusha...ila sasa wengine kama mm leo naanza mazoezi kesho naacha basi shida tupu..sijui nitafanyaje ili niwe na muendelezo
 
Back
Top Bottom