Mwanasayansi Kalivubha
JF-Expert Member
- Feb 4, 2024
- 344
- 926
Usifanye kosa la kupuuza historia yake kwa muonekano wake mpya wa leo, wengine ni maji tu yaliyopoa yamerudi ubaridi ila kwenye moto yatarudia hali yake ya umoto.
Usijifanye kipofu kupuuza historia yake bali hakikisha kuwa unajua kipi kilikuwa nyuma ya historia yake hiyo na je kuna namna ya muendelezo endapo mazingira yaliyopelekea historia yake hiyo yatajirudia tena leo? Usiogope kujiridhisha na hayo kabla hujatoa kibali cha kuendelea naye kwenye hatua ya mbele.
Matokeo ya kupuuza historia ni matukio ya kushangaza tunayoona leo na ukifuatilia historia ya muhusika unakuta aliwahi kuwa hivyo miaka kadhaa nyuma au alikuwa na viashiria hivyo lakini harakati za maisha zikamfanya apoe kwa muda ila uhalisia wake ni ule ule.
Changamoto za maisha zinafanya wengi waigize maisha kwa kujipa taswira zisizo na hatia ila ukiingia tu kwenye mfumo taswira inavuliwa na kurudissha uhalisia wake sasa yawezekana utakuja kugundua hilo tayari muda umeenda na kakuharibia mambo mengi.
Sio wote ila kwenye majumba ya ibada huko pia wapo ambao Changamoto zimewapa taswira ya kimaigizo ili tu wanase ambaye atafuta Changamoto zao na kisha warudi kwenye uhalisia wao ,Hivyo usione umekutana naye Kanisani/ Msikitini ukadhani historia yake haina nguvu tena la hasha fuatllia kwa kina ujue nini kilikuwa nyuma yake na je si endelevu endapo mazingira yatajirudia?
#Mwanasayansi Saul kalivubha
#Fikia Ndoto Zako.
Usijifanye kipofu kupuuza historia yake bali hakikisha kuwa unajua kipi kilikuwa nyuma ya historia yake hiyo na je kuna namna ya muendelezo endapo mazingira yaliyopelekea historia yake hiyo yatajirudia tena leo? Usiogope kujiridhisha na hayo kabla hujatoa kibali cha kuendelea naye kwenye hatua ya mbele.
Matokeo ya kupuuza historia ni matukio ya kushangaza tunayoona leo na ukifuatilia historia ya muhusika unakuta aliwahi kuwa hivyo miaka kadhaa nyuma au alikuwa na viashiria hivyo lakini harakati za maisha zikamfanya apoe kwa muda ila uhalisia wake ni ule ule.
Changamoto za maisha zinafanya wengi waigize maisha kwa kujipa taswira zisizo na hatia ila ukiingia tu kwenye mfumo taswira inavuliwa na kurudissha uhalisia wake sasa yawezekana utakuja kugundua hilo tayari muda umeenda na kakuharibia mambo mengi.
Sio wote ila kwenye majumba ya ibada huko pia wapo ambao Changamoto zimewapa taswira ya kimaigizo ili tu wanase ambaye atafuta Changamoto zao na kisha warudi kwenye uhalisia wao ,Hivyo usione umekutana naye Kanisani/ Msikitini ukadhani historia yake haina nguvu tena la hasha fuatllia kwa kina ujue nini kilikuwa nyuma yake na je si endelevu endapo mazingira yatajirudia?
#Mwanasayansi Saul kalivubha
#Fikia Ndoto Zako.