Usipuuze taarifa yoyote inayohusu kuwa umebambikiziwa Mtoto

Usipuuze taarifa yoyote inayohusu kuwa umebambikiziwa Mtoto

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Joined
Mar 24, 2018
Posts
28,297
Reaction score
68,017
USIPUUZE TAARIFA YOYOTE INAYOHUSU KUWA UMEBAMBIKIZIWA MTOTO.

Anaandika, Robert Heriel

Labda uwe unajua kuwa huyo mtoto sio wako, au labda uwe unajua huna nguvu za Kupata mtoto na huyo kwako ni stara yako.

Lakini ikiwa utamsikia MTU yeyote akikuambia au akisema kuwa huyo mtoto au mtoto Fulani sio wako basi usipuuzie hiyo taarifa. Kila taarifa hasa taarifa nyeti kama hizo zichukulie Kwa uzito kama zenyewe zilivyo.

Usije sema kuwa Kitanda hakizai haramu. Hiyo ni misemo ya Watu wajinga, wenye Giza kichwani, misemo ya Watu ambao aidha wanamatatizo ya kiakili, kimwili na Kiroho.

Ni akheri ujithibitishie yaani upate uhakika kuwa mtoto Fulani ni wako au sio wako.Kisha mengine yaendelee kama utaendelea na malezi Kwa Moyo upendo au utabwaga manyanga.

Kwa kizazi cha sasa ni muhimu kuwa makini Sana na kila kitu unachoambiwa. Usimdharau yeyote.
Usidharau taarifa yoyote hasa taarifa nyeti.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
USIPUUZE TAARIFA YOYOTE INAYOHUSU KUWA UMEBAMBIKIZIWA MTOTO.

Anaandika, Robert Heriel

Labda uwe unajua kuwa huyo mtoto sio wako, au labda uwe unajua huna nguvu za Kupata mtoto na huyo kwako ni stara yako.

Lakini ikiwa utamsikia MTU yeyote akikuambia au akisema kuwa huyo mtoto au mtoto Fulani sio wako basi usipuuzie hiyo taarifa. Kila taarifa hasa taarifa nyeti kama hizo zichukulie Kwa uzito kama zenyewe zilivyo.

Usije sema kuwa Kitanda hakizai haramu. Hiyo ni misemo ya Watu wajinga, wenye Giza kichwani, misemo ya Watu ambao aidha wanamatatizo ya kiakili, kimwili na Kiroho.

Ni akheri ujithibitishie yaani upate uhakika kuwa mtoto Fulani ni wako au sio wako.Kisha mengine yaendelee kama utaendelea na malezi Kwa Moyo upendo au utabwaga manyanga.

Kwa kizazi cha sasa ni muhimu kuwa makini Sana na kila kitu unachoambiwa. Usimdharau yeyote.
Usidharau taarifa yoyote hasa taarifa nyeti.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Pole sana kwakuwa umeathirika na tamaduni za ng'ambo ila huku Africa Mchango ni Poa sana hata likipigwa laana kwenye Ukoo wako mtoto uliyechomekewa haimpati pia kuna kuchanganywa Mitoto yenye akili nyingi linakuja Okoa Ukoo kwa dhiki na Ufukara Faida nyingine tunaepusha kupatwa na hasira baada ya kujua ukweli maana ni Rahisi kusababisha mauji na kumdhuru kiumbe kisicho na hatia Kitu kingine hakuna Mwanaume anayependa taarifa kuwa hana Uwezo wa kuzalisha hivyo hilo jambo litamtesa sana. Hivyo ni bora kubambikiwa Mtoto maana faida ni nyingi kuliko hasara.

Waswahili tunasema Yule jamaa ni fala tu hana hata Mtoto wa kusingiziwa hivyo kwa Wanaume ni bora kusingiziwa kuliko kukosa kabisa maana heshima inakuwa ndogo.

Weka akilini hakuna mwaume ambaye huwa anajisikia fresh juu ya jibu hana nguvu ya kuzalisha Mwanamke.
 
Kitanda akizai haramu, kama mpo ndani ya ndoa ni mtoto wako halali hata kama umebambikiwa ila kama bado haujamuoa mwambie ampeleke kwa Baba yake
 
Pole sana kwakuwa umeathirika na tamaduni za ng'ambo ila huku Africa Mchango ni Poa sana hata likipigwa laana kwenye Ukoo wako mtoto uliyechomekewa haimpati pia kuna kuchanganywa Mitoto yenye akili nyingi linakuja Okoa Ukoo kwa dhiki na Ufukara Faida nyingine tunaepusha kupatwa na hasira baada ya kujua ukweli maana ni Rahisi kusababisha mauji na kumdhuru kiumbe kisicho na hatia Kitu kingine hakuna Mwanaume anayependa taarifa kuwa hana Uwezo wa kuzalisha hivyo hilo jambo litamtesa sana. Hivyo ni bora kubambikiwa Mtoto maana faida ni nyingi kuliko hasara.

Waswahili tunasema Yule jamaa ni fala tu hana hata Mtoto wa kusingiziwa hivyo kwa Wanaume ni bora kusingiziwa kuliko kukosa kabisa maana heshima inakuwa ndogo.

Weka akilini hakuna mwaume ambaye huwa anajisikia fresh juu ya jibu hana nguvu ya kuzalisha Mwanamke.

Bora umesema Kwa waswahili,
Umesema vyema kabisa.
Ila hiyo haitumiki Kwa Sisi Watibeli
 
USIPUUZE TAARIFA YOYOTE INAYOHUSU KUWA UMEBAMBIKIZIWA MTOTO.

Anaandika, Robert Heriel

Labda uwe unajua kuwa huyo mtoto sio wako, au labda uwe unajua huna nguvu za Kupata mtoto na huyo kwako ni stara yako.

Lakini ikiwa utamsikia MTU yeyote akikuambia au akisema kuwa huyo mtoto au mtoto Fulani sio wako basi usipuuzie hiyo taarifa. Kila taarifa hasa taarifa nyeti kama hizo zichukulie Kwa uzito kama zenyewe zilivyo.

Usije sema kuwa Kitanda hakizai haramu. Hiyo ni misemo ya Watu wajinga, wenye Giza kichwani, misemo ya Watu ambao aidha wanamatatizo ya kiakili, kimwili na Kiroho.

Ni akheri ujithibitishie yaani upate uhakika kuwa mtoto Fulani ni wako au sio wako.Kisha mengine yaendelee kama utaendelea na malezi Kwa Moyo upendo au utabwaga manyanga.

Kwa kizazi cha sasa ni muhimu kuwa makini Sana na kila kitu unachoambiwa. Usimdharau yeyote.
Usidharau taarifa yoyote hasa taarifa nyeti.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Upewe maua yako mapema kwa mabandiko yako hapa Jf yanayotufungua wengi
 
Pole sana kwakuwa umeathirika na tamaduni za ng'ambo ila huku Africa Mchango ni Poa sana hata likipigwa laana kwenye Ukoo wako mtoto uliyechomekewa haimpati pia kuna kuchanganywa Mitoto yenye akili nyingi linakuja Okoa Ukoo kwa dhiki na Ufukara Faida nyingine tunaepusha kupatwa na hasira baada ya kujua ukweli maana ni Rahisi kusababisha mauji na kumdhuru kiumbe kisicho na hatia Kitu kingine hakuna Mwanaume anayependa taarifa kuwa hana Uwezo wa kuzalisha hivyo hilo jambo litamtesa sana. Hivyo ni bora kubambikiwa Mtoto maana faida ni nyingi kuliko hasara.

Waswahili tunasema Yule jamaa ni fala tu hana hata Mtoto wa kusingiziwa hivyo kwa Wanaume ni bora kusingiziwa kuliko kukosa kabisa maana heshima inakuwa ndogo.

Weka akilini hakuna mwaume ambaye huwa anajisikia fresh juu ya jibu hana nguvu ya kuzalisha Mwanamke.
Umeongea kwa busara na uzoefu wa hali ya juu sana.

Uliyoyasema nimeyashuhudia kwa macho yangu aisee, kuna mzee mmoja alichomekewa mtoto miaka ya zamani, lakini yule mzee wala hakujali akamlea kama mwanae na alimpenda kuliko watoto wote, na tena mbaya zaidi huyo mwanae muonekano wake tu ni ushahidi tosha maana huyo mzee ni mweusi hasa, halafu huyo mtoto ana muonekano wa kiarabu kuanzia nywele hadi rangi, lakini jamaa hakujali kitu.

Basi mwisho wa siku huyo mtoto alikuwa na uwezo mkubwa sana wa kiakili kuwazidi watoto wengine wote kuanzia shule hadi maisha ya mtaani.
 
Back
Top Bottom