Usisomeshe mtoto shule za gharama kwa matarajio kwamba atapata ajira, utaishia kuumia tu

Mtoto akifika darasa la7 anajua kusoma na kuandika hiyo elimu inamtosha sana, muachishe shule, peleka chuo cha ufundi veta ama college yoyote akasomee kwa vitendo, akitoka hapo tyr ana ujuzi na anauwezo wa kuanza maisha yake, mtaftie mtaji na urith mapema, then fanya kunawa mikono maana kazi yako kwake unakuwa umeimaliza kama mzaz.

or otherwise kama unajua una connection ya mwanao kwenda kufanya kaz ktk nchi za kigeni ama biashara basi msome izo english medium mpka form4 then achisha shule mpeke short coz ya ujasiliamali miez3-6 then baada ya hapo mkatie urithi wake na mtaji wa kuanzia maisha..

tusiish kwa kukalil maisha kuwa hii mifumo nikama misaafu kwamba huruhusiw kuibadiri ama kufikil nje ya box.

mim nkifanikiwa kupata mtot bas atasoma kwa bata sana, yaan hata shulen atakuwa akienda mara moja kwa wiki, eeh mara moja maana sitaki aende kusomea ajira, bal akasomee kujua kuandika na kusoma tu chazaid akachangamshe akili na watoto wenzake huko, hata mtian wa darasa la7 sitotaka aufanye, maana nikumpotezea muda.

Tuish kiuhalisia jmn maisha ni mafupi why tuteseke?
View attachment 2015279
 
Kuna kijana mmoja tulipata kusoma naye miaka ya nyuma huko 2006 wazazi wa Kijana yule walipeleka shule si kusoma tu .

Weekend na likizo jamaa alikuwa bega kwa bega na Baba yake Mzazi katika Biashara na Magari na Hardware.

Sijui waliwezaje lakini jamaa alikuwa smart sana kichwani ...Mama yake alikuwa mkali zaidi ya Pilipili.

Akiwa na 22 Years jamaa tayari ana maisha yake si ya Baba yake na mishe nyingi sana.

Hii familia pia ilibadili sana maisha yangu ,nawashukuru popote walipo.

Kuna namna sisi tunawaza kulea watoto ila kuna watu wanalea watoto wao kwa akili kubwa sana.
Ukiwa na uwezo leo mtoto kielimu na kijamii pia...kusoma shule za gharama au hata za kawaida ni sawa lakini ni wajibu upi wazazi tunaufanya kwa watoto wetu.

Tuache kelele connection nzuri sio shule ghari wala shule za maskini ni Mzazi uwe na pesa na ujue kuzielekeza na kuwekeza kwa Watoto wako ili ikifika mapema sana waweze kujitegemea.

Pesa sio lazima ziwe kibao ni kile unachoweza fanya na uwezo wako.

Tunahitahitaji Lugha ya kimataifa English itusaidie kufanya mambo mengi sana lakini mwongezee mtoto madini ya kujitegemea kimaisha.

Leo hii watu wanamaliza vyuo na miaka 22-25 ,,lakini wakikosa ajira tu biasha imeisha hivyo.
Aim ya wazazi japo si wote ni umalize upate kazi ili uje usaidie nduguzo na wao wenyewe.

Tuache kuwafanya watoto zetu kuwa vitega uchumi.Haya mambo ni uchawi huo.

Mambo ni mengi muda ni mchache.Lea mtoto wako kwa akili ..sio upumbavu.
 


Comment ya Kimaskini sana hii kama roho yako, unamfatilia wa nini Mpaka unajua siku anayosimamishwa Ada kama sio uchawi huo
 
Pia Kuna swala la urahisi wa kupata visa .Kuna shule ukisoma hata ukienda balozi za Marekani au Ulaya hawahoji hata maswali wanakwambia tu njoo siku Fulani uchukue passy yako .Kuna zingine ukisoma hata uwe na ajira ukatwangwa maswali wanajua lofa huyu anataka kuzamia tu utasumbuliwa Sana kalete bank statement na makorokoro kibao sababu shule ulizosoma mmmmmm hata balozi lazima ashtuke kuwa hapa pana mtoto wa lofa na lofa anataka kuja Ulaya au Marekani atarudi huyu?

Mashule mengine Hadi watoto wa mabalozi wanasoma connection inakuwa pana Sana toka local Hadi international
 
Home schoiling sio nzuri kiukweli, inamfanya mtoto awe socially awkard asipoyajua maisba halisi ya kuchangamana na wenzake.

Labda kama ni mdogo sana miaka 3 au 4
Define socially awkward. Kuna familia Nazi follow insta wanao homeschool na huwa wanakataa hiyo myth kuwa mtoto atashindwa ku socialize.

Me nimesoma shule and I'm a loner by nature, hakuna nikichokuwa nachukia kama group work na kuongea darasani na sports.

Mtoto atapata tu chance ya ku socialize, kuna majirani, kumpeleka sehemu za michezo za watoto, Kwa extended family etc.

Me naona wanao homeschool ndo wenye uwezo (matajiri). Ni kama kijiajiri badala ya kuajiriwa. Kwanza Kila kitu Kiko online bure siku hizi. Elon Musk alisema kusoma chuo kikuu ni kuthibitisha tu kuwa una uwezo kufanya majukumu unayopewa, otherwise not very necessary in today's world.
 


Shule ipi ya gharama umesoma ? St.Mary’s ? 🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Feza ya milioni sita inayotumia mtaala wa necta unaanzaje kuilinganisha na Braeburn ya milioni 50 inayotumia mtaala wa cambridge??

1.IST
2. Braeburn Dar Es salaam International
3. Haven of Peace Academy
4. Feza International Schools

Hizo ndio the most expensive schools in Tanzania
 


True Mkuu My first born goes to IST and my second born goes to Braeburn dar my Niece goes to Feza

huo mzunguko wa shule wanazosoma umefanya nifahamiane na viongozi wengi wa serikali na wafanyabiashara wenzangu wakubwa kwa sababu Ya watoto
 
Ila hakuna kesi mkuu, mpeleke mtoto wako huko umwambie awe anajikomba kwa watoto wa vigogo, ujiandae kumnunulia pampaz
Yani hii point ya kutengeneza connection ili upate kazi it's very disturbing. Mnawapa wenye Mali zao tabu, kila mtu anamfuata kumlilia connection.
 
Yani hii point ya kutengeneza connection ili upate kazi it's very disturbing. Mnawapa wenye Mali zao tabu, kila mtu anamfuata kumlilia connection.
View attachment 2015348


Sio connection kwa sababu ya kupewa kazi au kupewa pesa . Just for the child to be sorrounded with the best na pia apate International education standard ambayo itakuja kumsaidia mtoto kwenye soko la ajira/biashara kimataifa na kitaifa

Local schools mtoto anakua competent kitaifa tu

Unamjengea mtoto ushindani chanya wa Maisha yake
 
Nimesoma maoni mengi ya wadau.

Mimi kwa mtazamo wangu naona kwamba wakati sahihi wa kumsomesha mtoto shule kali ni eidha 5&6 au O Level.

Kwa sababu wakati huu watoto wanakua wamekua na urafiki wa kweli hujengeka hapo kwa maana kama kuna watoto wa wakubwa wa kufanya nao connection basi inakuwa ni rahisi sana.

Kuliko mwanao yuko nasary huko alafu mtu anategemea apate connection ukubwani,ni ngumu sana kwq sababu kuna maisha baada ya nasari na shule ya msingi wanaweza wakatengana na hao watoto wa wakubwa lengo likapotea.

Lakini pia mtoto ni muhimu sana acheze michezo ya kwenda huku na kule na kukimbia na michezo mingine ya akili akiwa na watoto wenzie katika mtaa,hii ni muhimu sana.

Lakini pia wazazi wakae na watoto wao waweke mada mezani wajenge hoja,weka mada inayoendana na akili ya mtoto kisha na wewe unaijadili nae kwa mujibu wa ufahamu wake,hii inamjengea iwezo wa kufikiri na kujenga hoja na kujieleza pia mpaka akija kuwa mkubwa ataona kwamba yeye ni mtu wa kipekee kabisa
 
Yani hii point ya kutengeneza connection ili upate kazi it's very disturbing. Mnawapa wenye Mali zao tabu, kila mtu anamfuata kumlilia connection.
View attachment 2015348
Hoja ya connection inaweza ikamata ila ni upuuzi sana kwa sababu inakuwaje unasomesha mtoto shule ada 5M kwa mwaka alafu bado unatafuta connection ya mwanao ?

Kama ada sio ishu kwako sidhani kama mtu connection itakuwa ishu kwake,japokuwa ni kweli connection zipo wakati mwingine ila haipaswi kuwa hoja ya msingi ya kuipoteza milioni kadhaa kila mwaka kwa muda wa miaka kadhaa
 
Yaani nna Hela alafu nimpeleke mtoto wangu Shule ambayo aina walimu wa kutosha, Mtoto anabeba fagio na kidumu cha maji ya kumwagilia maua na anasoma na watoto ambao Baba zao makapuku no future connections. Acha hizo boss Tafuta Hela
Ndio maana mitoto yenu inakua mivivu mivivu na kuishia kwenye ujames Delicious.

Shule ni sehemu ya kujifunza kazi na stadi za maisha sio masomo tu
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
I agree with all that but tangu mwanzo comments zinarudiarudia tu hiyo point ya connection, mtoto aende shule ya gharama ili ajuane na huyu na yule. Me napata ukakasi. I guess kuna maisha fulani mtu anataka na hawezi kuwa nayo mpaka ajisogezesogeze kwa watu fulani (wenye power/influence), which is the disturbing part.
 
Peleka private ya kawaida shule ya msingi

Kisha mkazanie sekondari asome government
 
True Mkuu My first born goes to IST and my second born goes to Braeburn dar my Niece goes to Feza

huo mzunguko wa shule wanazosoma umefanya nifahamiane na viongozi wengi wa serikali na wafanyabiashara wenzangu wakubwa kwa sababu Ya watoto
Unaongelea hizo shule kudhani ni kwapa kila mtu analo!! hizo shule ni 50 Millions huko na kwa mtu anaetengeneza hizo pesa yupo busy kukagua bank statement na financial statements mda huu, sip kuperuzi jf 😂

Happ ist tu kiwakuta watoto wa tz ni kwa manati
 
nimesoma shule za kawaida na shule za kulipia, nimeona tofauti kubwa kati ya shule hizo mbili. Sio lazima kupeleka mtoto katika shule za kulipia na mchepuo wa Kiingereza ila kuna faida kubwa. Cha msingi kuepuka gharama zisizo za msingi, ila ikinipendeza na uchumi ukiruhusu, ntafanya juu chini mwanangu asije soma bongo shule ya msingi wala sekondari aje apambanae huku chuo Kikuu tu.
 
Maisha connection Ni lazima haikwepeki mfano ukiwa na duka la jumla connection kwenye business world lazima ukiwa na hotel watu uliosoma nao Wenye power kifedha etc wakiwa na shughuli yao waweza kuja kutumia ukumbi wako nk

Umesoma na watoto wa Bakhresa ukajenga urafiki una kituo Cha mafuta waweza pata tenda ya ku supply mafuta kwenye magari na meli zake kupitia hap ulisoma nao

Dunia nzima ziko elite schools na universities ambazo elites watoto wao husoma Bei zake sio za kitoto lakini waweza build network ya kuaga umaskini for good

Mfano umesoma na mtoto wa Mo Dewji mwanae kampa u director of marketing wewe uliyesoma naye Kama ulijenga urafiki aweza kukuteua kuwa sole agent wa kuuza bidhaa zao mkoa wako bila kununua bidhaa cash ukapewa mzigo ukauza ukaulipa sababu anakujua toka mko shule Huna connection hata biashara tu itakusumbua Sana Na sio any connection Ni connection with the right people kwa muda mrefu na muda huo sehemu nzuri ya kupata Ni shuleni mkisoma pamoja

Life is not a lonely planet you need somebody to be somebody

Mzazi utake usitake hiyo kazi na Zigo la kujua mwanao anatakiwa kuwa connected na watoto wa aina gani kwa future yake Ni lako mzazi .Sio la mtoto wewe ndie director wa maisha ya Mtoto.Na kwenye elimu ndio starting point
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…